Nini maoni yako kuhusu vita ya Palestina na Israel? Bado unaamini Israel ina intelijensia kubwa Duniani?

Nini maoni yako kuhusu vita ya Palestina na Israel? Bado unaamini Israel ina intelijensia kubwa Duniani?

Tunadanganywa sana na documentary zao kuwa wapo makini ki upelelezi na kung'amua jambo linalotaka kutokea, inakuaje watu wanaanda mashambulizi ya vifaa kwa uwingi ule bila kujua na technolojia wanazojisifu nazo
Ukitumia akili utaona waliamua kuliacha ili wapate haki ya kuongeza eneo
 
Hii Dunia sio ya kuiamini wewe fanya maisha yako maisha yaendelee tuu....hujuia walijua wakapiga kimya wafanye wanachotaka au hawakujua

amini hao jamaa na nduguze Marekani wako vizuri sana kwenye ushushu.
Uko sahihi Mossad walikua na taarifa zote waliachwa wachozwe ili wapate uhalali ya kuipiga Hammas, Hesbolah na Gaza na wamefanikiwa Gaza itachazwa vibaya siku 5 mpaka 7 zijazo

Sent from my SM-G950U1 using JamiiForums mobile app
 
Dramatize kuuawa kwa raia wao 600, huku wengine 100+ ikiwemo askari na raia wakuchukuliwa mateka?.....hapana mkuu...

Hii ni intelligence failure kubwa sana itakayowatesa muda mrefu.

Ni vigumu hata kufanya 'rescue operation' kwa idadi kubwa namna hiyo huku ikiwa hujui walipofichwa, Sana Sana Hamas watawatumia kama bargaining chip kupata wanachotaka.

T14 Armata
Sasa wangepata vipi uhalali wa kuichukua Gaza ?
 
Israel imehtukizwa na kupewa kichapo cha 5-1 ndani ya masaa 24. Inshort intelijensia yao haikungamua uwepo wa mashambulizi haya. Hata mataifa makubwa awakutegemea kusikia kilichotokea.

Kwa kichapo kilichotokea maana yake Dunia haipo salama dhidi ya mashambulizi ya kulipiza kisasa. Ni ishara kwamba dola zote duniani zinapaswa kuanza kutathimini hali za amani kwenye maeneo yao.

Ugaidi siyo jambo linalotumia miaka kufanyika ila utumia sekunde kuvuruga nchi. Israel imevamiwa, ofcos watalipa kisasi kwa kuwaua raia lakini lazima wapo watu watawajibishwa kwa kutotimiza wajibu wao.

Kibaya zaidi ni kwamba wanajeshi na Raia wa Israel wamechukuliwa mateka. Kuchukua Raia na wanajeshi mateka kunaihakikishia Palestina ushindi kwani wanaweza kutumia mateka kumfanya Israel arudishe mashambulizi nyuma.

Suala ili lina muunganiko na imani hasa huku Afrika na Tanzania. Je ndani ya Imani unaamini kati ya Israel na Palestina nani achapwe? Katika tafakuri ya wazi unaamini nani mchokozi kati ya mataifa haya mawili?

Mwisho; Tanzania tukawatoe watu wetu kwenye mataifa haya mapema.l
Kuna kila uwezekano hawajashtukizwa bali wamepanga ionekane hivyo ili waifute gaza kwenye ramani ya palestina.

Lakini kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu mipango yao haitafanikiwa.
 
Mkuu ile ilikuwa ni inside Job ya shirika la ujajusi la ndani la Israel inaonekana kupitia mgogoro ule Israel ananufaika sana, kama watu wanaweza kumtoa waziri mkuu kafara unadhani Kuna nini? Israel inajenga makazi mengi sana ya walowez pale, Sasa jiulize kama Yasser Arafat alikubali kwamba kuwe na amani Ina maana kwamba hata wapalestine walishachoka na hali ya kukosa utulivu
Hii ni most complex thing !
 
imefeli pakubwa sana. hata marekani na intelijensia yake yote iliingiliwa na osama ikapigwa nyumbani. lakini mwisho wa siku osama kawa udongo pamoja na watu wake wengi, na ndivyo ilivyo kwa hamas. hadi sasa, unaambiwa wanamgambo mamia wameuawa na wengine wamekamatwa hai kama mateka. huwezi kufanya kitu kama hicho kwa israel ukabaki salama. waliondoka gaza, na kwa jambo hili wanaenda kurudi, hakutakuwa na polisi tena ila waisrael mitaani, hata ramala kule west bank. wamedhamiria wasambae na kupatrol maeneo yote ya wapalestina, na hiyo unajua maana yake? ni kwamba itakuwa rahisi zaidi kwao kufanya expension, sasa ndio watajenga makazi hadi westbank na east jerusalem itaporwa muda si mrefu. kufa kufaana.
Hamas kawaingiza wenzao chaka, sasa watafute sehemu nyingine
 
Nenda kasome mgogoro wa Israel na Palestine vizuri, hata Israel anawajua vizuri hamas na kwa taarifa yako huko zamani zilikuwa ni vurugu za mawe , chupa na manati ila mpaka Sasa ivi Hamas amefikia kwenye kurusha rocket na usisahau Palestine ni landlocked kwa hyo kila siku Hamas anakuwa baadala ya kurudi nyuma na kuendeleza harakati zake, mwaka 1995 walifikia hatua nzuri sana katika ya Palestine na Israel ila kwa interest tu za watu mazungumzo ya Oslo I na
Oslo II yalikwama baada ya waziri mkuu wa Israel kuuliwa, hivyo ujue huu mgogoro ni complex sana, utaifa na rasilimari ndo kila kitu kwa Israel na Palestine
Iran kahusika.

Ukiwa na bahari usitegemee kuwa salama sana maana vitu vinaletwa
 
Kuna kila uwezekano hawajashtukizwa bali wamepanga ionekane hivyo ili waifute gaza kwenye ramani ya palestina.

Lakini kwa uwezo wa mwenyezi Mungu mipango yao haitafanikiwa.
Inawezekana kabisa ! Annexation nyingine hiyo !!
 
Dramatize kuuawa kwa raia wao 600, huku wengine 100+ ikiwemo askari na raia wakuchukuliwa mateka?.....hapana mkuu...

Hii ni intelligence failure kubwa sana itakayowatesa muda mrefu.

Ni vigumu hata kufanya 'rescue operation' kwa idadi kubwa namna hiyo huku ikiwa hujui walipofichwa, Sana Sana Hamas watawatumia kama bargaining chip kupata wanachotaka.

T14 Armata
Na mpaka sasa majeshi ya Israel bado haya jaweza kurudisha maeneo yaliyo tekwa na licha ya mapigano makali yanayo endelea kati ya hamas na Israel.
 
Wakungutwe tu watoke kwenye makazi ya watu. Go hezbollah, no matter the outcome ila moto mmeuwasha
Ss ndo kumekucha
Ngoja tuone nani atatoka hwenye ardhi na mwisho nani atakuwa kakung'utwa
 
Na mpaka sasa majeshi ya Israel bado haya jaweza kurudisha maeneo yaliyo tekwa na licha ya mapigano makali yanayo endelea kati ya hamas na Israel.
Mmhh
I don't think so
Mi nasubiri kuona mwisho
 
Tusubili ndani ya saa 72 zijazo, Gaza, will never be the same again. Kama Mbabe Osama aliuliwa, kama kuku, na Arabs mpaka Leo hawajuhi, kabuli lake, subili tuone mtoto wa mama, mkubwa atakavyomfanya mtoto wa mama mdogo.
Acha watu wajitie moyo
Mi neno langu Moja nasubiri nione meisho wake ndo tutaelewa ni mapema sn....
 
MOSSAD na CIA na mbwembwe zooote HAWAKUAMINI kilichotokea...Mae zao.

Kula sana rocket za kitisha aisee Iron Dome imeambulia mikojo ahahahaha. Hii ni aibu ya karne
CIA ina husikaje kwenye hiyo ishu?
 
Sasa wangepata vipi uhalali wa kuichukua Gaza ?
Sio rahisi kiivyo, kwanza kabla ya kuichukua gaza wakomboe kwanza maeneo yaliyo tekwa tangu juzi na Hamas.

Vita sio lele mama.
 
Iran kahusika.

Ukiwa na bahari usitegemee kuwa salama sana maana vitu vinaletwa
Ni kweli Kuna namna hawa watu wamepewa support kubwa kutoka nje, Sasa Israel ana idara tatu imara kbsa za usalama kuanzia mossad , amaan idara ya jeshi na pia Kuna shin bet idara ya ndani, pia ana marafiki ama washirika wake je ni kweli hawa wote walishindwa kupata hata intelligencia na kuzuia hilo mapema kabla ya haya madhara yaliyotokea ?
 
Back
Top Bottom