Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli na Samia, yupi Rais bora kwako?

Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli na Samia, yupi Rais bora kwako?

Kwa vyovyote vile hakuna duniani mtu mwenye uwezo wa kurekebisha Historia. Kwa ivo hawa ndiyo walikuwa marais wetu na Samia ndiye Rais wa Tanzania kwa sasa.

Kwa mtazamo wako hawa ukiwaweka kwenye mizani yupi amekuwa Rais bora kwako na kwa nini ukiangalia changamoto alizokabiliana nazo na jinsi alivyozitatua na unadhani kwamba amecha alama (Legacy) gani kwa watanzania wote.
Inategemea unauliza upate majibu kutoka kizazi kilichozaliwa lini?
 
Wote0 hakuna kitu hapo alichokiacha Nyerere ndoo kinaendelea japo yeye hakuwa mwizi ila ni muasisi wa mfumo wizi na utapeli.
 
Nyerere na Magufuli wanaongoza kutajwa,wenye chuki na Magu kama nawaona walivyo vimba,dadadeki.
 
Maraisi borani
Mwinyi
Kikwete
Wa mwisho ni
Nyerere na Jiwe
 
Kipimo cha Nyerere ni kikubwa sana kwa hao wote waliokuja baada ya yeye kutoka madarakani. Nikupe mfano mmoja.

Mwaka 1998 wakati Frederick Chiluba akiwa ni Rais wa Zambia, alimweka Jela mtangulizi wake Keneth Kaunda kwa siku 28. Lakini Nyerere alikwenda kumwambia amuachie na akamwachia. Miaka 3 baada ya Nyerere kutoka kuwa Raisi wa Tanzania.

Ushawishi wa Mwalimu huwezi kuulinganisha na yeyote kati ya hao wengine. Mwalimu alijenga uchumi kutoka bila ya kuwa na uchumi, ila alikosea katika falsafa yake ya kuuendesha huo uchumi. Kama ulisikia Mkapa kwamba aliuza mashirika ya Umma na benki. Nyingi zilianzishwa wakati wa Mwalimu.
Alijenga uchumi gani alileta sera za ujamaa upumbavu tu
 
Kila mmoja ni bora na ni bora KWA namna yake na KWA Wakati wake , .

Ila siku zote ataanza Mwalimu with facts ...

Ameweza kuniaminisha /kutuaminisha kuhusu Tanzania na tumeliweka hilo kwenye fikra zetu plus passing such belief/imagined reality to our offsprings .. once hakukuwa na Tanzania but he managed to create it ...


Wengine wanaendeleza tuuu...
 
Kwa hitimisho lako , uzito unalalia wapi?
Ukimtoa Nyerere hapo sioni hata mmoja aliyewafanyia au kuwaongoza watanzania nakuwapa maendeleo. Nyerere aliwaza mbali kuwapa watanzania lugha ya kuelewa ya Taifa na kuwatoa katika lugha zao za kikabila. Ilikuwa kazi ngumu Sana lakini alifanikiwa. Akakubali vyama vingi baada yakuona watanzania wanaelewa. Waliofuata wangekuwa waelewa wangeiimarisha katiba imulike watanzania wote bila kujali wapinzani. Kwa uchungu walionao watanzania tungekuwa mbali hata wizi chuki visingekuwepo. Hawajachelewa embu wavitoe.


Naweza kusema kipindi Cha JK na Lowasa walifanya Jambo ambalo mpaka leo linasaidia Sana watanzania, shule za kata. Huyu ndiyo anaweza kuonekana alikuwa na mikakati ya kusaidia watanzania na vizazi vijavyo.

Tatizo la hiki chama cha CCM ni wabinafsi, wafitini, wana michuki, waongo, wapenda sifa n.k.

Nyerere alituachia zawadi kubwa Sana ya lugha. Tusingekuwa na lugha yetu ya kuelewa kipindi Cha mwendazake tungekufa watu wengi Sana na lingeweza kitokea vita Kali baina yetu sisi wenyewe. Huyu alihatarisha amani, kawagombanisha dola na raia na vyama vya upinzani, kajanga chuki ya vyama na vyama, kajenga chuki baina ya Tanzania na mataifa mengine kajifanya ni mrusi wa pili, kajenga chuki kwa Raia kutokana na vyama vyao. Kasumbua familia za watu bila sababu kwa ajili ya kijenga makaravati. Kaondoa ubinadamu kabisa.

Mkapa hakuna alichokifanya zaidi ya kumfilisi mtanzania kamwacha anatembea na ndala badala ya kumtenge ezea ajira kaja kuuza viwanda na kubi afsisha, pamoja na ukali wake. Tunaweza kusema ni afafhali hata mkoloni angebaki.

TUFANYE JE?

Tuanzie pale kwa Nyerere alipoachia lugha ya Taifa na kupambanua mambo mengine yawe yakitafa zaidi.

Shule tunapambana kila mtu apate elimu.

CCM iondoe chuki na ubinafsi walionao wakubali Tanzania inajengwa na watanzania wote bila kujali kichaa, mpinzani, mgonjwa n.k. Watanye maridhiano ya kurudisha mchakato wa katiba mpya ili kutangeneza mihimili yenye nguvu zaidi. Hata Kama hakutaluwa na serikali ijiendeshe bila usumbufu wa jeshi na kuingia kwenye vita. Mfano kuwe na makatibu amba watachaguliwa na pande mbili za vyama kulingana na katiba mpya itakavyopendekezwa.

Yatengenezwe makundi mawili ya vyama ili kuunganisha huo utitiri wa vyama au vifutwa kuwe na pande mbili za vyama.

Yaani vyama vibaki Kama vilivyosajiliwa viungane viwe upande mmoja ili kuhojiana na upande wa pili wa chama na mihimili itakavyoundwa. Hapa tutapata wabunge.

Ikiewezekana ofisi ya msajili ipigiwe kura na wananchi au ifutwe kabisa kwa sababu inagombanisha vyama.

Hii ndiyo kazi muhimu katika kuleta maendeleo ili kuondoa watu wapenda madaraka na wachochezi wa chuki na wafitini.
 
Nyerere, japo alituachia katiba ambayo yeye mwenyewe alikiri ilikuwa mbovu
 
Kwa mtu yeyote mwenye busara na hekima, hawezi kumlinganisha J.K.Nyerere na marais wote waliomfuatia.

He is by far the best president.
 
Nyerere ndiye rais bora wa wakati wote hadi sasa kwa nchi hii.kwasababu aliweza kuongoza nchi kwakuweka misingi ya kijamii,kitamaduni,kiuchumi na kisiasa nchi nzima wakati kukiwa bado ni zama za giza kitu ambacho viongozi wote waliofuata hakuna ambaye ameweza kufanya hivyo au kufumisha chochote au kuboresha chochote ili kiwe kizuri zaidi wakati wako kwenye dunia ya mwanga na ongezeko la teknolojia kila sehemu.Kua na katiba bora tu kumewashinda wakati mapungufu ya katiba kongwe ya nyerere yanaonekana.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Nyerere.
Huyu aliongoza ujenzi wa Taifa pamoja na waliokuwa nyuma yake.
Aliiacha Tanzania kama Tanzania. Na alitaka kila Mwananchi ajivunie popote Duniani Utanzania wake.
Huyu ndie aliyeongoza kusuka misingi mikubwa ya nchi hii.
Jambo moja kubwa ni kwamba hakuwa na Tamaa binafsi. Aliiona nchi kwanza, maslahi binafsi pembeni.
Alifanikiwa kuacha Taifa la Tanzania ambalo hata majirani hawajui mbinu gani alitumia kuunganisha watu wa kabila na aina tofauti zaidi ya 200.
Alikiri makosa mbele ya safari pale alipoteleza.
Kuhusu vitu vinavyoonekana. Unaweza kutaja hadi ukachoka.
Maksi zao ni kama ifuatavyo:
1.J.K.Nyerere-90
2.B.W Mkapa-50
3.J.M.Kikwete-40
4.J.P.Magufuli-30
5.A.H.Mwinyi-10.
NB:S S.Hassan bado hajamaliza hata awamu moja ya urais,hivyo bado ana incomplete.
 
Kila mtu ana mtizamo wake. Ukisema "Aliyefuata baada ya Mwalimu Nyerere..." ni kama vile unazuia watu kuwa na mawazo yao binafsi.

Kuna watu humu hawajui chochote kuhusu Mwalimu.
Kwahiyo ili swali lako haliwezi kuja kuulizwa miaka 40 ijayo?.Kwasababu miaka hiyo hata hawa tunaowajadili leo wa miaka ya karibuni watakua wameshasahulika.Kiongozi wa nchi hatakiwi kujulikana na watu physicaly bali watu wanatakiwa wamfaham kupitia matendo na vitendo alivyofanya alipokua kwenye hiyo nafasi.Sidhan kama kuna watu walikuwepo ujeruman wakat Adolf Hitler anaongoza ila taarifa zake tunazo hadi uku.Ndo maana kuna historia na legacy.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom