Profesa Assad: Hakuna bandari inayouzwa, ni uelewa mdogo wa watu

Profesa Assad: Hakuna bandari inayouzwa, ni uelewa mdogo wa watu

Kwanza prof kaamua kutoa mawazo yake. Sasa asiseme tuna uelewa mdogo. Amesema hivyo vitu vitatu, mtaji, watu na mfumo.

Inashindikana nini kuleta watu wenye huo mfumo tukaumiliki wakatrain watu wetu wakafanya?

Mtaji sio shida maana biashara ya bandari inalipa kwa nini tusikopesheke? Mbona zipo kampuni za ndani zikipewa zinamudu? Kwani share zikiuzwa hatutanunua?

Kukataa jambo haimaanishi uelewa ni mdogo.
 
Ona sasa unabishana na aliyekuwa mdhibiti na mkaguzi wa mahesabu ya serikali yaani mashirika yote anajua kwa undani hali ya fedha ya serikali kuliko hata wewe ila sasa unambishia 😂
Akishasema Shivji, Mh. Warioba na kidogo Butiku hiyo itakuwa imekwisha. Yaani kwenye issue za Sheria nimsikilize Prof. Assard badala ya Prof. Shivji? Huo utakuwa uzuzu usio kiwango.
 
Ni kweli kabisa hakuna palipoandikwa inauzwa lakini pia hakuna palipoandikwa inakodishwa wala kupangishwa hivyo basi.

Kama haiuzwi
Kama haikodishwi
Kama haipangishwi

Maana yake ni moja tu inatolewa bure...

Zaidi Assad naye anataka kugeuka mchumia tumbo.

Maana yeye anazungumzia bandari moja tu wakati IGA inasema bandari zote Tanzania na miundombinu yake.

Mwambie kachelewa kidogo

Sent using Jamii Forums mobile app
Naomba kujua qualifications zako za elimu, coz unaonekana umemzid hata huyo professor [emoji23]
 
shida ya profesa wako, bado anawaza kuteuliwa kuwa C.A.G, ndio maana kasoma upepo wa mama na makada mmejaa, hamna kitu humo.

awaachie wakina professa shivji, watueleze kuhusu sheria, yeye ni nani kwenye sheria, ana uelewa wa nini,? na mbaya zaidi maoni ni conclusive ya kutukana waliotoa uchambuzi wa kisheria
Hapa ndugu yangu Profesa Asad ametoka kapa.
 
Profesa Assad husimama kwenye ukweli sio mtu wa kuyumbishwa. Shivji na wenzake hawajawahi kuiunga mkono serikali yoyote ya CCM. Kinachonisikitisha ni nyumbu kuanza kumrushia maneno ya hovyo Profesa Assad.
 
,(1)Unategemea Asad awe kinyume na mkataba wa DP WORLD kivipi, Wakati yeye ni Mzanzibari.

Kwenye huu mkataba hakuna bandari ya Zanzibar hata moja inayobinafsishwa.Ina maana Zanzibar wao hawataki jambo hili kama lina faida?

Lingekuwa na faida lazima wangeshalalamika kwamba kwa nini tuwatenge kwenye huu ubinafsishaji Wakati ZNZIBAR ni sehemu ya Tanzania.

(2) Wananchi wanapolalama kwamba Bandari IMEUZWA,hawana maana kwamba tumewauzia DP WORLD kama vile tunavyouza shamba.HAPANA ! maana yake ni kwamba kwenye huu mkataba kuna vipengele ambavyo Tanzania inakuwa imelaliwa sana na hivyo vipengele hivyo vinatubana mno wakati sisi ndio wenye Mali hivyo virekebishwe.

UKIFUATILIA HAYA MALUMBANO, HAKUNA MWANANCHI HATA MMOJA ANAYEPINGA UBINAFSISHAJI ila wanataka ubinafsishaji WENYE FAIDA, na hata hawa viongozi wetu wanotoa ufafanuzi kwa wananchi wanalijua hili,ila kwa makusudi, either na wao wanatoa ufafanuzi wa kuuzwa au kutokuuzwa kwa Bandari na kuukwepa unwell unaoulizwa wa kurekebisha vipengele vibovu vya kwenye mkataba.

Wafafanuzi wanatoa elimu kwa uoga na unafiki kuelezea kitu ambacho hata nafsi na roho zao binafsi kwa ndani zinawakatalia, Ili kuwaridhisha baadhi ya viongozi wa juu wenye nia OVU waliowatuma na wana maslahi machafu katika vipengele vya kwenye mkataba vilivyokosewa kwa makusudi.

Ushauri wangu ni kwamba, vipengele vibovu virekebishwe,kuwe na uwazi,na Ubinafsishaji uendelee na tuachane kabisa na UBINAFSI WA BAADHI YA HAO WAKUBWA..wanaoendeleza mabishano badala ya kurekebisha hivyo vipengele vibovu,na mkataba uwe bora kwa pande zone mbili ,ili tuendelee na maisha mengine,Badala ya kuendelea kupoteza fedha, muda nk kwa kuandaa mikutano na makongamano yasiyoisha kwa ajili ya ufafanuzi unaozidisha malumbano.
 
hivi profesa kama huyu unaweza kumweka meza moja na shivji? huhu ni kama hajasoma vile. just a good zanzibaris.
 
,(1)Unategemea Asad awe kinyume na mkataba wa DP WORLD kivipi,Wakati yeye ni Mzanzibari.Kwenye huu mkataba isha mengine,Badala ya kuendelea kupoteza fedha,muda nk kwa kuandaa mikutano na makongamano yasiyoisha kwa ajili ya ufafanuzi unaozidisha malumbano.
Asad mzanzibar ashukuru tu Mungu Tanganyika ilimwajiri na amepata ugali tokea Tanganyika, la sivyo angekuwa mvuvi kule nungwi.
 
..sikubaliani na madai yake kwamba Tz haina uwezo au fedha za kuwekezs ktk bandari.

..kama tuliweza kukusanya fedha na kujenga mji mkuu mpya tusiouhitaji, na kununua midege inayotutia hasara, basi hatushindwi kukata shauri kuwekeza bandari.

..Dp / Dubai hawatengenezi cranes au mitambo mikubwa inayotumika bandarini. Mitambo hiyo inaundwa na nchi mbalimbali ambako Tanzania inaweza kwenda kununua.


..Hii habari kwamba hatuna uwezo na ni lazima tusalimishe kila kilichoko ktk bandari zetu kwa Dp World ni udanganyifu.

Kwanza prof kaamua kutoa mawazo yake. Sasa asiseme tuna uelewa mdogo. Amesema hivyo vitu vitatu, mtaji, watu na mfumo.

Inashindikana nini kuleta watu wenye huo mfumo tukaumiliki wakatrain watu wetu wakafanya?

Mtaji sio shida maana biashara ya bandari inalipa kwa nini tusikopesheke? Mbona zipo kampuni za ndani zikipewa zinamudu? Kwani share zikiuzwa hatutanunua?

Kukataa jambo haimaanishi uelewa ni mdogo.
Usishangae akisema kwa sasa Bunge sio dhaifu.
 
Profesa Tibaijuka ambae si Mwanasheria alipoongea kwa kupinga vipengele vya sheria tulimuunga mkono kwa kuwa aliongea tuliyoyapenda kuyasikia

Prof Assad kaongea kwa uzoefu na elimu yake tunapinga asiongelee ya Sheria kwa kuwa si Mwanasheria kwa kuwa tu kaongea tusiyopenda kusikia

Watetezi wengi wa Demokrasia na uhuru wa maoni huwa practically hawaamini hizi falsafa wanazopigania
Bora umesema wewe. Ningesema mimi nimgeambiwa chawa
 
Sio appropriate authority so atulie.

Sisi kugezo 1. Iwe mwanasheria
2. Leta hoja kulingana na andiko lenyewe na si kubuni mambo yako.
 
Ni kweli kabisa hakuna palipoandikwa inauzwa lakini pia hakuna palipoandikwa inakodishwa wala kupangishwa hivyo basi.

Kama haiuzwi
Kama haikodishwi
Kama haipangishwi

Maana yake ni moja tu inatolewa bure...

Zaidi Assad naye anataka kugeuka mchumia tumbo.

Maana yeye anazungumzia bandari moja tu wakati IGA inasema bandari zote Tanzania na miundombinu yake.

Mwambie kachelewa kidogo

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndio kwaheri ya mama?!
Inazidi kudhihirisha labda viatu kweli vilikuwa vikubwa mno...
Hata wam promote kivipi hawezi, hata waanze campaign mapema haisaidii...
LAZIMA KURA ZIIBIWE TU MAMA AENDELEE...
 
Back
Top Bottom