Rais Mstaafu Jakaya Kikwete: Msijaribu Kuchanganya Dini na Siasa Hata Kidogo
Eti reasoning ya mstaafu iko low [emoji1787][emoji1787][emoji1787].Okay sitaki kutumia nafasi yake kuonesha how uwezo wake wa reasoning ni mkubwa.

Tuambie mkataba unakasoro gani ili tuverify reasoning capacity yako.
TEC wameverify . Hoja zao zijibiwe watu wasikimbilie kwenye u dini.

Wao TEC hawajalalamikia u dini.
 
"Napenda kuchukua nafasi hii kukumbushana kuhusu tunu nyingine muhimu nayo ni kutokuchanganya dini na siasa. Tukiivunja tunu hii gharama yake tutaiona, na kama kuna viongozi wa dini wanataka kutuelekeza kuitumia dini kwa manufaa ya kisiasa, na kama kuna viongozi wa siasa wanataka kuitumia dini kwa manufa yao ya kisiasa, nawaombeni ndugu zangu tuwanyanyapae.

"Siku ikifika ambapo uwanachama wa chama cha siasa au uumini thabiti wa dini ukawianishwa na chama cha siasa kinachofuata ndio mwisho wa nchi yetu, mtakuwa na vyama vya siasa vya wakristu, waislamu, walokole nk. Kuwafanya Watanzania kuyatazama masuala ya kisiasa, kiserikali, utawala kwa mtazamo wa dini zetu ni jambo hatari, halkadhalika watu kuyatazama masuala ya dini kwa mtazamo wa siasa za vyama vyao si jambo lenye afya kwa taifa letu.

"Yote mawili yataathiri umoja na kutishia amani, usalama na utulivu tunaoufaidi hivi sasa. Mfano Zanzibar walifika mahali waisilamu wanamuona shehe ambaye ni mfuasi wa chama ambacho sio chake sio shehe sawa sawa, kwahiyo wakienda kusali kama shehe ni msuasi wa CUF wanangoja amalize kusalisha, halafu anaingia shehe wa waislamu na wafuasi wake.

"Nawaambia vitu halisi na ndio maana nilipokuwa Rais nilishughulika sana pale na kupata muafaka, niliahidi kwenye hotuba yangu ya kwanza ya Bunge 2005 Dec 30, kwamba nitafanya kila ninaloweza tujenge muafaka Zanzibar, haukuwa rahisi. Mkutano ule tuliufanyia Butiama NEC, ilikuwa moja ya kikao kigumu kwelikweli, lakini nikasema pamoja na ugumu wote lazima hapa tuvuke. Tukafika mahali nilipoona mambo yamekuwa makali, nikasema twendeni kwanza tukale, tulipokuwa tunakula ndio tukawa tunaweka mikakati ya namna gani tunalimaliza hili jambo. Tukajipanga nani ataanza kuzungumza, tukakubaliana kwamba tutakwenda Zanzibar kuwa na Serikali ya Umoja wa Kitaifa, na ndio imetusaidia Zanzibar tuna mazingira ya utulivu mpaka sasa, tungekwenda na utaratibu ule ule wa zamani tusingefika.

"…Tukianza kuchanganya dini na siasa tukageuza mimbari za dini na madhabahu kuwa sehemu ya kuhubiri kwishilia mbali nchi yetu. Lakini baba wa taifa ametuasa juu ya hatari ya kuchanganya dini na siasa. Nawasihi Watanzania wenzangu kuitunza tunu hii kama mboni ya jicho letu. Tukatae kuwasikiliza viongozi wa dini na waumini wao wanaofanya vitendo wa aina hii iwe kwa siri au kwa Dhahiri, vitendo hivi vinaweza kutupeleka kubaya."


Kikwete ameyasema hayo leo 20/8/2023 katika ufunguzi wa jengo Kanisa la Kiadventisti Wasabato Mara.
Msichanganye siasa na dini🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 

Attachments

  • 52CC76E4-F9F8-4A9D-BCB5-F5B0D8AC0DF1.jpeg
    52CC76E4-F9F8-4A9D-BCB5-F5B0D8AC0DF1.jpeg
    30 KB · Views: 1
"Napenda kuchukua nafasi hii kukumbushana kuhusu tunu nyingine muhimu nayo ni kutokuchanganya dini na siasa. Tukiivunja tunu hii gharama yake tutaiona, na kama kuna viongozi wa dini wanataka kutuelekeza kuitumia dini kwa manufaa ya kisiasa, na kama kuna viongozi wa siasa wanataka kuitumia dini kwa manufa yao ya kisiasa, nawaombeni ndugu zangu tuwanyanyapae.

"Siku ikifika ambapo uwanachama wa chama cha siasa au uumini thabiti wa dini ukawianishwa na chama cha siasa kinachofuata ndio mwisho wa nchi yetu, mtakuwa na vyama vya siasa vya wakristu, waislamu, walokole nk. Kuwafanya Watanzania kuyatazama masuala ya kisiasa, kiserikali, utawala kwa mtazamo wa dini zetu ni jambo hatari, halkadhalika watu kuyatazama masuala ya dini kwa mtazamo wa siasa za vyama vyao si jambo lenye afya kwa taifa letu.

"Yote mawili yataathiri umoja na kutishia amani, usalama na utulivu tunaoufaidi hivi sasa. Mfano Zanzibar walifika mahali waisilamu wanamuona shehe ambaye ni mfuasi wa chama ambacho sio chake sio shehe sawa sawa, kwahiyo wakienda kusali kama shehe ni msuasi wa CUF wanangoja amalize kusalisha, halafu anaingia shehe wa waislamu na wafuasi wake.

"Nawaambia vitu halisi na ndio maana nilipokuwa Rais nilishughulika sana pale na kupata muafaka, niliahidi kwenye hotuba yangu ya kwanza ya Bunge 2005 Dec 30, kwamba nitafanya kila ninaloweza tujenge muafaka Zanzibar, haukuwa rahisi. Mkutano ule tuliufanyia Butiama NEC, ilikuwa moja ya kikao kigumu kwelikweli, lakini nikasema pamoja na ugumu wote lazima hapa tuvuke. Tukafika mahali nilipoona mambo yamekuwa makali, nikasema twendeni kwanza tukale, tulipokuwa tunakula ndio tukawa tunaweka mikakati ya namna gani tunalimaliza hili jambo. Tukajipanga nani ataanza kuzungumza, tukakubaliana kwamba tutakwenda Zanzibar kuwa na Serikali ya Umoja wa Kitaifa, na ndio imetusaidia Zanzibar tuna mazingira ya utulivu mpaka sasa, tungekwenda na utaratibu ule ule wa zamani tusingefika.

"…Tukianza kuchanganya dini na siasa tukageuza mimbari za dini na madhabahu kuwa sehemu ya kuhubiri kwishilia mbali nchi yetu. Lakini baba wa taifa ametuasa juu ya hatari ya kuchanganya dini na siasa. Nawasihi Watanzania wenzangu kuitunza tunu hii kama mboni ya jicho letu. Tukatae kuwasikiliza viongozi wa dini na waumini wao wanaofanya vitendo wa aina hii iwe kwa siri au kwa Dhahiri, vitendo hivi vinaweza kutupeleka kubaya."


Kikwete ameyasema hayo leo 20/8/2023 katika ufunguzi wa jengo Kanisa la Kiadventisti Wasabato Mara.
Anaandika Baba Askofu Dr. Stephen Munga, Askofu Mstaafu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Mashariki.

ACHENI KUCHEZA KARATA YA UDINI - HOJA IJIBIWE KWA HOJA

Suala la mjadala wa mkataba tata wa bandari sio mchezo wa kamari. Hapo hatufanyi majaribio katika kuhoji na kujibu hoja. Pia hapo tunatazama mambo mapana ya taifa kwa vizazi vingi vijavyo. WATU WENYE AKILI TIMAMU NA NGUVU YA KUFIKIRI HUPAMBANA KWA HOJA. WALIO DHAIFU WA AKILI NDIO HUTUMIA MUSULI NA MIKUKI NA BUNDUKI NA MAHABUSU KUDHIBITI WENYE NGUVU YA HOJA.

Tukumbuke hoja za awali kuanzia maamuzi ya bunge kukubali mkataba huu tulitembea katika barabara mbovu. Kumbukeni wazungumzaji wa awali wakiwemo maprofesa Shivji na Tibaijuka; wakifuatiliwa na jamii ya wanasheria na baadae sehemu ya wenye nchi (wananchi). Tulidhani serikali na bunge wagejibu hoja zile kwa ufasaha na urahisi kumbe sivyo. Pia tulidhani itakuwa safari ya ndugu watembeao katika njia moja ili kufikia mwisho mmoja kumbe sivyo. Kabla safari haijafika mwisho tumegeukana na kuitana wahaini na kutiana minyororo. Sasa limetoka tamko la Baraza la Maaskofu Katoliki lililojipambanua kwamba ni sauti ya watu na hivyo ni sauti ya Mungu. Tungali tunasikilizia.

Jambo lingine la kufadhaisha kabisa ni pale tunaposikia watu wengine wakifanya mjadala wa mkataba tata wa bandari kama mchezo wa karata katika kamari. Katika mchezo huo wanashusha karata ya udini. Wanawaona wanaohoji, na kipekee tamko la Baraza la Maaskofu Katoliki kama mchezo wa kamari ya udini. Hizi ni fikra dhaifu na finyu. Tunapenda kuweka wazi kwamba wapo Watanzania ambao watatetea maslahi ya taifa hili na kamwe hawatakubali kudhoofishwa kwa dhihaka au kuchafuliwa kwa namna yeyote. Penye hoja tujibu kwa hoja. Shutuma sio hoja.

Ni hivi: Tunaongelea maslahi ya taifa. Tunaongelea mambo mazito ya uzalendo (patriotism). Hatufanyi sensa ya wakristo na makanisa au waislamu na misikiti. Ninaposimamia mambo ya imani yangu kwa Mungu najua kwamba hayo ni kwangu na wale ninaoshiriki nao imani moja. Katika mkataba wa bandari tunaongelea juu ya heshima na enzi kuu (sovereignty) ya taifa kuu la Tanzania. Katika heshima na enzi kuu ya taifa hili Mungu alilotupa hakuna aliye juu ya katiba na sheria za nchi hii tulizojiwekea. Kwa mtazamo huo, tunapozungumzia juu ya maslahi ya nchi sisi sote tunakalia vigoda vinavyolingana. Ni pale tu mfumo wa utawala unapokuwa kandamizi ndipo uwiano huo wa ushiriki katika kuzungumzia maslahi na heshima ya taifa huvurugika. Kucheza karata ya udini katika mambo mapana ya maslahi ya taifa ni sawa kutaka paka avute mkokoteni uliobeba tembo.

Tukumbushane kwamba katika hoja za wale wanaoona mapungufu katika mkataba tata hakuna anayekataa uwekezaji. Tena ieleweke kwamba sio suala la kuikataa serikali au kumkataa Rais. Nionavyo mimi wanaosaidia serikali na Rais ni wale wanaohoji mambo kwa wazi na kwa nia njema. Maadui wakubwa wa serikali na Rais ni wale wanafiki wanaosema kuna giza kumbe kuna nuru; na kwamba kuna nuru wakati kuna giza. Hili ni jambo la kulinda mambo ya msingi (matters of principle) ili taifa libaki kuwa taifa.

Hoja za msingi ni kwamba tunakubali uwekezaji kwa manufaa mapana ya taifa. Lakini pia kwamba ziwepo juhudi za makusudi za kuwajengea uwezo na nidhamu ya kiwango cha juu wawekezaji wazalendo. Lazima hawa wasaidiwe kufikia kiwango cha kuwa na sifa za ushindani za viwango vya kimataifa. Njia sahihi ya kukabili tatizo sugu la ukosefu wa ajira kwa vijana ni kujengea uwezo na nidhamu taasisi za ndani ili ziwe vitovu vya kukua kwa uchumi na kutengeneza fursa za uhakika za ajira. Kucheza karata ya udini katika fikra pana za maslahi mapana ya kijamii ni kuleta kasumba mbaya. Kama dini yako haikupanui upeo wa kufikiri kwako na kuona maslahi mapana ya jamii basi dini yako haitusaidii. Usipoifuga dini yako vizuri yaweza kuwa sumu kwa maendeleo ya jamii.
 
Alikuwa aliongea Leo huko Mara alikoalikwa kama mgeni Rasmi kwenye sherehe ya ufunguzi wa jengo la ibada la Kanisa.

My Take
Naunga mkono hoja,TEC na wachochezi wengine wakemewe na waonywe.

=====

"Tukianza kuchanganya dini na siasa, tukageuza...madhabahu ndio mahali pa kuhubiri siasa za vyama vya siasa, kwishiria mbali nchi yetu...lakini Baba wa Taifa ametuasa juu ya hatari ya kuchanganya dini na siasa, nawasihi Watanzania wenzangu kuitunza tunu hii kama mboni za jicho letu tukatae kuwasikiliza viongozi wa dini na waumini wao wanaofanya vitendo vya aina hii iwe kwa siri au kwa dhahiri, vitendo hivi vinaweza kutupeleka kubaya" Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Jakaya Kikwete wakati akizindua kanisa la SDA Rorya mkoani Mara, leo Agosti 20, 2023.

View attachment 2722951
Ili ushauri wako uende vizuri , ungewaeleza wanasiasa na viongozi Kwa jumla Yao wasiwahusishe wasanii kwenye vitu vya kitaaluma ni matusi na dhihaka Kwa wananchi ambao miongoni wao ni viongozi wa dini na wanataaluma husika
 
"Napenda kuchukua nafasi hii kukumbushana kuhusu tunu nyingine muhimu nayo ni kutokuchanganya dini na siasa. Tukiivunja tunu hii gharama yake tutaiona, na kama kuna viongozi wa dini wanataka kutuelekeza kuitumia dini kwa manufaa ya kisiasa, na kama kuna viongozi wa siasa wanataka kuitumia dini kwa manufa yao ya kisiasa, nawaombeni ndugu zangu tuwanyanyapae.

"Siku ikifika ambapo uwanachama wa chama cha siasa au uumini thabiti wa dini ukawianishwa na chama cha siasa kinachofuata ndio mwisho wa nchi yetu, mtakuwa na vyama vya siasa vya wakristu, waislamu, walokole nk. Kuwafanya Watanzania kuyatazama masuala ya kisiasa, kiserikali, utawala kwa mtazamo wa dini zetu ni jambo hatari, halkadhalika watu kuyatazama masuala ya dini kwa mtazamo wa siasa za vyama vyao si jambo lenye afya kwa taifa letu.

"Yote mawili yataathiri umoja na kutishia amani, usalama na utulivu tunaoufaidi hivi sasa. Mfano Zanzibar walifika mahali waisilamu wanamuona shehe ambaye ni mfuasi wa chama ambacho sio chake sio shehe sawa sawa, kwahiyo wakienda kusali kama shehe ni msuasi wa CUF wanangoja amalize kusalisha, halafu anaingia shehe wa waislamu na wafuasi wake.

"Nawaambia vitu halisi na ndio maana nilipokuwa Rais nilishughulika sana pale na kupata muafaka, niliahidi kwenye hotuba yangu ya kwanza ya Bunge 2005 Dec 30, kwamba nitafanya kila ninaloweza tujenge muafaka Zanzibar, haukuwa rahisi. Mkutano ule tuliufanyia Butiama NEC, ilikuwa moja ya kikao kigumu kwelikweli, lakini nikasema pamoja na ugumu wote lazima hapa tuvuke. Tukafika mahali nilipoona mambo yamekuwa makali, nikasema twendeni kwanza tukale, tulipokuwa tunakula ndio tukawa tunaweka mikakati ya namna gani tunalimaliza hili jambo. Tukajipanga nani ataanza kuzungumza, tukakubaliana kwamba tutakwenda Zanzibar kuwa na Serikali ya Umoja wa Kitaifa, na ndio imetusaidia Zanzibar tuna mazingira ya utulivu mpaka sasa, tungekwenda na utaratibu ule ule wa zamani tusingefika.

"…Tukianza kuchanganya dini na siasa tukageuza mimbari za dini na madhabahu kuwa sehemu ya kuhubiri kwishilia mbali nchi yetu. Lakini baba wa taifa ametuasa juu ya hatari ya kuchanganya dini na siasa. Nawasihi Watanzania wenzangu kuitunza tunu hii kama mboni ya jicho letu. Tukatae kuwasikiliza viongozi wa dini na waumini wao wanaofanya vitendo wa aina hii iwe kwa siri au kwa Dhahiri, vitendo hivi vinaweza kutupeleka kubaya."


Kikwete ameyasema hayo leo 20/8/2023 katika ufunguzi wa jengo Kanisa la Kiadventisti Wasabato Mara.
Hatimaye wenye mkataba wamejitokeza
 
HAIWEZEKANI KUWATENGA VIONGOZI WA KANISA NA SIASA ZA NCHI YAO!

Wapendwa Watanzania!
Limekuwa ni jambo la kawaida kwa watawala au watu walio karibu na watawala wa Tanzania wakibanwa na viongozi wa dini hasa maaskofu huanza kutoa maneno ya propaganda dhidi ya viongozi wa dini wakiwaambia 'wasichanganye dini na siasa'. Msemo huu wanautumia kama kichaka cha kujifichia wasiguswe na viongozi wa dini!

Kauli hizo zimeibuka tena kwa kishindo zaidi kuanzia mwezi Juni 2023 baada ya maaskofu kuingilia sakata la Mkataba wa Bandari. Hivi karibuni tuliikemea Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ilipoitisha mkutano wa viongozi wa vyama vya siasa ili kujadili hoja ya viongozi wa dini kuonekana wakiwa na viongozi wa vyama vya siasa.

Tumeona ni wajibu wetu ili kuwaelimisha watu kuhusu suala hili kusudi wasije wakapotoshwa na wanasiasa katika suala zima la kudai haki katika taifa lao. Wanasiasa ni wajanja sana na wanajua nafasi na nguvu ya viongozi wa dini katika jamii ndio maana wanatumia nguvu ili kupotosha ukweli kuhusu nafasi ya viongozi wa dini katika ukombozi wa kifikra katika taifa.

Tunapenda kukiri kuwa hili tunaloliandika ndilo eneo ambalo sisi tuna ubobezi nalo, kwa hiyo hatubahatishi bali tunakiandika tunachokijua, tulichokisomea na kukifundisha katika ngazi za Chuo Kikuu.

Kwa upande wa Wakristo, chimbuko la dini hiyo ni mji wa Yerusalemu, Israeli ya Kale. Lakini, ni vizuri watu wakaelewa kuwa Ukristo una mizizi yake miaka 5000 kabla ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo. Hivyo, msingi mkubwa wa mafundisho ya Ukristo ni Biblia Takatifu yenye sehemu kuu mbili - Agano Jipya na Agano la Kale.

Dini haifanywi kwa wanyama na wala siasa pia haifanywi kwa ndege. Dini ni mfumo mzima wa maisha ambao ndani yake kuna mambo mengi. Tunaposoma au kufundisha kuhusu dini lazima tusome maisha ya jamii nzima ambayo kwanza dini ilifika kwayo. Kwa upande wa Wakristo, sisi tunasoma kuhusu jamii mbalimbali kama Misri, Syria, Ukaldayo (Babeli), Rumi, Wagiriki, Jordan, Waisraeli, Waajemi, Waarabu, Lebanon, nk.

Katika kusoma na kujifunza dini tunafundisha waumini kuishi kwa mifano ya jamii hizo ikiwa ni pamoja na kuiga mema na kuyaacha mabaya na hayo yanawezekana tu kwa kusoma kuhusu maisha yao kupitia viongozi au manabii wao.

Tunaposoma na kujifunza Biblia tunakutana na mambo yafuatayo:
1. Familia (family institutions): familia, ndoa, watoto, wajane, urithi, kifo, maziko, nafasi ya wanawake katika jamii, nk

2. Taasisi za Kiraia (Civili institutions): idadi ya watu, utumwa, taasisi ya kifalme, familia za kifalme, utawala, ajira na uchumi, kilimo, Afya na tiba, sheria na haki, mgawanyo wa muda, vipimo vya uzito, mahakama, nk.

3. Taasisi za Kijeshi (military institutions): majeshi ya Israeli, ngome za kijeshi, mbinu za kivita, siraha za kivita, vita, vita vitakatifu, nk

4. Taasisi za dini (Religious institutions): ibada, madhabahu, nyumba za ibada, uongozi wa taasisi za dini, Ofisi ya Ukuhani, Ofisi ya Walawi, sadaka, imani potofu, uchawi, utaratibu wa ibada, siku za ibada, sherehe na siku za sikukuu, nk.

Watu waliokuwa juu ya yote hayo ni viongozi wa dini na ndio waliopewa majukumu ya kuifundisha na kuionya jamii. Taasisi hizo ziliwekwa kwa ajili ya watu na kilichotofautisha ni ratiba. Wakati wa vita walipigana na wakati wa amani watu hao walifanya sherehe. Wakati wa mambo mazito ikiwemo kujua mustakabari wa nchi walikwenda kutafuta ushauri kwa viongozi wa dini. Alipotokea kiongozi mkorofi au jeuri alikemewa na viongozi wa dini au hata kutangaziwa kuondolewa madarakani na hao viongozi wa dini.

Sisi Askofu Mwamakula tunaitoa kwenu elimu hii ili msiyumbishwe ili muelewe kuwa viongozi wa dini kuingilia kati mtafaruku wa kisiasa au kiutawala ni ishara kuwa jamii yenu iko na afya!
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki
Dar es Salaam, 20 Agosti 2023; 12:35 jioni.

Sent from my TECNO BC1 using JamiiForums mobile app
 
Alikuwa aliongea Leo huko Mara alikoalikwa kama mgeni Rasmi kwenye sherehe ya ufunguzi wa jengo la ibada la Kanisa.

My Take
Naunga mkono hoja,TEC na wachochezi wengine wakemewe na waonywe.

=====

"Tukianza kuchanganya dini na siasa, tukageuza...madhabahu ndio mahali pa kuhubiri siasa za vyama vya siasa, kwishiria mbali nchi yetu...lakini Baba wa Taifa ametuasa juu ya hatari ya kuchanganya dini na siasa, nawasihi Watanzania wenzangu kuitunza tunu hii kama mboni za jicho letu tukatae kuwasikiliza viongozi wa dini na waumini wao wanaofanya vitendo vya aina hii iwe kwa siri au kwa dhahiri, vitendo hivi vinaweza kutupeleka kubaya" Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Jakaya Kikwete wakati akizindua kanisa la SDA Rorya mkoani Mara, leo Agosti 20, 2023.

View attachment 2722951
Naunga mkono hoja
 
"Napenda kuchukua nafasi hii kukumbushana kuhusu tunu nyingine muhimu nayo ni kutokuchanganya dini na siasa. Tukiivunja tunu hii gharama yake tutaiona, na kama kuna viongozi wa dini wanataka kutuelekeza kuitumia dini kwa manufaa ya kisiasa, na kama kuna viongozi wa siasa wanataka kuitumia dini kwa manufa yao ya kisiasa, nawaombeni ndugu zangu tuwanyanyapae.

"Siku ikifika ambapo uwanachama wa chama cha siasa au uumini thabiti wa dini ukawianishwa na chama cha siasa kinachofuata ndio mwisho wa nchi yetu, mtakuwa na vyama vya siasa vya wakristu, waislamu, walokole nk. Kuwafanya Watanzania kuyatazama masuala ya kisiasa, kiserikali, utawala kwa mtazamo wa dini zetu ni jambo hatari, halkadhalika watu kuyatazama masuala ya dini kwa mtazamo wa siasa za vyama vyao si jambo lenye afya kwa taifa letu.

"Yote mawili yataathiri umoja na kutishia amani, usalama na utulivu tunaoufaidi hivi sasa. Mfano Zanzibar walifika mahali waisilamu wanamuona shehe ambaye ni mfuasi wa chama ambacho sio chake sio shehe sawa sawa, kwahiyo wakienda kusali kama shehe ni msuasi wa CUF wanangoja amalize kusalisha, halafu anaingia shehe wa waislamu na wafuasi wake.

"Nawaambia vitu halisi na ndio maana nilipokuwa Rais nilishughulika sana pale na kupata muafaka, niliahidi kwenye hotuba yangu ya kwanza ya Bunge 2005 Dec 30, kwamba nitafanya kila ninaloweza tujenge muafaka Zanzibar, haukuwa rahisi. Mkutano ule tuliufanyia Butiama NEC, ilikuwa moja ya kikao kigumu kwelikweli, lakini nikasema pamoja na ugumu wote lazima hapa tuvuke. Tukafika mahali nilipoona mambo yamekuwa makali, nikasema twendeni kwanza tukale, tulipokuwa tunakula ndio tukawa tunaweka mikakati ya namna gani tunalimaliza hili jambo. Tukajipanga nani ataanza kuzungumza, tukakubaliana kwamba tutakwenda Zanzibar kuwa na Serikali ya Umoja wa Kitaifa, na ndio imetusaidia Zanzibar tuna mazingira ya utulivu mpaka sasa, tungekwenda na utaratibu ule ule wa zamani tusingefika.

"…Tukianza kuchanganya dini na siasa tukageuza mimbari za dini na madhabahu kuwa sehemu ya kuhubiri kwishilia mbali nchi yetu. Lakini baba wa taifa ametuasa juu ya hatari ya kuchanganya dini na siasa. Nawasihi Watanzania wenzangu kuitunza tunu hii kama mboni ya jicho letu. Tukatae kuwasikiliza viongozi wa dini na waumini wao wanaofanya vitendo wa aina hii iwe kwa siri au kwa Dhahiri, vitendo hivi vinaweza kutupeleka kubaya."


Kikwete ameyasema hayo leo 20/8/2023 katika ufunguzi wa jengo Kanisa la Kiadventisti Wasabato Mara.
Katoka pangoni
Hoja nzito kashibdwa khijibu hata moja.

Naona anatuona sisi wajinga sana. Tunajua sasa nani ni nani kwenye hili
 
JK jikite kwenye Mkataba wa Bandari huko kwenye dini na Siasa ni mawazo yako.
Wajibu waumini kuhusu lile lidude!!
 
Alikuwa aliongea Leo huko Mara alikoalikwa kama mgeni Rasmi kwenye sherehe ya ufunguzi wa jengo la ibada la Kanisa.

My Take
Naunga mkono hoja,TEC na wachochezi wengine wakemewe na waonywe.

=====

"Tukianza kuchanganya dini na siasa, tukageuza...madhabahu ndio mahali pa kuhubiri siasa za vyama vya siasa, kwishiria mbali nchi yetu...lakini Baba wa Taifa ametuasa juu ya hatari ya kuchanganya dini na siasa, nawasihi Watanzania wenzangu kuitunza tunu hii kama mboni za jicho letu tukatae kuwasikiliza viongozi wa dini na waumini wao wanaofanya vitendo vya aina hii iwe kwa siri au kwa dhahiri, vitendo hivi vinaweza kutupeleka kubaya" Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Jakaya Kikwete wakati akizindua kanisa la SDA Rorya mkoani Mara, leo Agosti 20, 2023.

View attachment 2722951
CCM ikibaki madarakani kwa kupora chaguzi za nchi sio tatizo, bali tatizo ni viongozi wa dini wakigomea mikataba ya wizi. Kikwete sio kiongozi muadilifu, hana uadilifu wowote wa kuongelea namna ya kufanya siasa ndani ya nchi hii.

Amani anayoitaka yeye ni yeye na familia yake kupata madaraka kwa ukondoo wa watanzania. Eti huwa anaalikwa kwenda kuwa muangalizi kwenye chaguzi za nchi mbalimbali huku Afrika, cha ajabu hapa nchini chama chake ndio mabingwa wa kunajisi chaguzi. Mke na mtoto wake wako bungeni, sio kwa ushawishi au uwezo wao, bali kwa mifumo iliyojaa upendeleo kwa familia za viongozi. Hapo anaongelea amani itakayoendelea kumfanya yeye na familia yake kufaidi cake ya taifa hili.
 
Mhe. Jakaya akiwa kwenye mkutano wa Kanisa la Adventist (Sabado ) amehutubia kwa kukemea dini kuchanganywa na siasa. Ikumbukwe kwamba ni muda mrefu sana JK hakuwa akipatikana majukwaani na kwenye mikutano ya ndani ya taasisi za kiraia na za dini

Katika hotuba yake anakemea na kuonya kuhusu mgawanyiko wa dini NCHINI. Anakemea akionyesha kwamba wapo watu wanatumia agenda za dini kisiasa na kisiasa kidini. Swali langu kwa mzee wetu huyu; kwanini sasa?

Je anaamini kutetea rasilimali za nchi ni jukumu la kisiasa au ni jukumu la kila mtanzania bila kujali taasisi anayofanya kazi . Je, kusema na kutoa maoni kwa viongozi wa dini ni siasa? Mbona wakati viongozi wa kidini walipofanya mashauriano na serikali awali kuhusu mkataba huu hakuna aliyejitokeza kusema dini na siasa zinachanganywa pamoja?

Mbona hizi hizi dini wakati wa JPM zilivalishwa mwamvuli wa kamati za amani zikawa zinamlinda JPM na CCM hakuna aliyejitokeza kukemea? Kamati za amani zikatumika kuwakataza wananchi kusema mwisho wake watu wakawa wanapotea, je wakati huo mbona hakuna aliyesema ni Udini?

Mimi ni muislam , alisimama Shekhe Mwaipopo anaongea vibaya sana akidai huo ni msimamo wetu huku mkijua kabisa kwamba yalikuwa mawazo binafsi...mbona hakukuwa na neno kutoka kwetu kukemea alichokuwa anafanya? Juzi hapa amejitokeza mzee wetu kwenye imani ametukana kwa mwamvuli wa kutetea uislamu kwanini hatutoki kutetea?

Wenzetu wameatumia haki yao na wameweka kwenye maandishi hakuna sehemu walipoonesha Udini, hoja yako ya Udini hata kama ina mashiko lakini umekosea wakati sahihi wa kuitoa....inatufanya sisi tuonekane kama tumeshindwa kusimama na mwenzetu kumbe hoja hapa siyo dini ni mkataba wa rasilimali.

Tulitegemea uyaone haya mapema na kulishauri taifa lakini mlipuuza; maneno yakishatoka hatuwezi kuyafuta kwenye nafsi za watu kwa hotuba; TUSIMAMIE HAKI

TANZANIA HAIWEZI KUFA NJAA KWA KUKATAA KUKODISHA BANDARI; WAACHENI WASIOONA FAIDA WAENDELEE KUTAFAKARI HUKU MKIWAPA ELIMU KULIKO KUWAKAMA NA WAKISEMA MNAWAAMBIA NIWADINI. ULIMWENGU UMEBADILIKA ; TUKIKOSEA TUKIRI TUMEKOSEA
Wee nae wale wale tu upuuzi mtupu
Mwaipopo ni Sheikh?
Wee muislam wa wapi aisee?
 
Tusianze kupangiana vya kuongea kwani kuwa kiongozi wa dini ndio usitoe maoni yako juu ya nchi yako
 
Wakati watawala wanavunja amani ya nchi kwa vitisho na kuanza kuwashughulikia wakosoaji wa mkataba wa kipuuzi unaoipeleka nchi yetu kwenye utumwa wa milenia, mzee ulikuwa kimya wala haukutoa neno lolote.

Wakati Shura ya Maimamu walipotoa tamko la kuwasomea Itikaf waislam watakaojitokea kwenye mikutano ya kukosoa mkataba huu wa ajabu ulikaa kimya kabisaa.

Wakati viongozi walipotoa vitisho vya kuwashughulikia wanaoupinga mkataba uliona vyema ukakaa kimya

Sasa umeibuka kwa sababu ya hoja nzito zilizotolewa na wasomi naam weledi wanaojua kujenga hoja ikajengeka. Wameleta hoja mezani na badala ya kuzidadavua hoja hata kuwajibu unakuja na KARIPIO kwamba wanachanganya siasa na dini.

Fahamu kwamba kwenye lile andiko hakuna mahala walipoichanganya dini na siasa bali walisimama kuueleza ukweli ambao serikali na wewe mnatumia gharama kubwa sana kuupindisha.

Hebu onesha weledi maana kila tunapokuangalia usoni unaonekana umepaniki.

Mzee, endelea kukaa kimya maana huko tuendako zama zimeisha na mfalme mpya atawekwa na Mungu, huna la kufanya kuzuia
 
Wakati watawala wanavunja amani ya nchi kwa vitisho na kuanza kuwashughulikia wakosoaji wa mkataba wa kipuuzi unaoipeleka nchi yetu kwenye utumwa wa milenia, mzee ulikuwa kimya wala haukutoa neno lolote.

Wakati Shura ya Maimamu walipotoa tamko la kuwasomea Itikaf waislam watakaojitokea kwenye mikutano ya kukosoa mkataba huu wa ajabu ulikaa kimya kabisaa.

Wakati viongozi walipotoa vitisho vya kuwashughulikia wanaoupinga mkataba uliona vyema ukakaa kimya

Sasa umeibuka kwa sababu ya hoja nzito zilizotolewa na wasomi naam weledi wanaojua kujenga hoja ikajengeka. Wameleta hoja mezani na badala ya kuzidadavua hoja hata kuwajibu unakuja na KARIPIO kwamba wanachanganya siasa na dini.

Fahamu kwamba kwenye lile andiko hakuna mahala walipoichanganya dini na siasa bali walisimama kuueleza ukweli ambao serikali na wewe mnatumia gharama kubwa sana kuupindisha.

Hebu onesha weledi maana kila tunapokuangalia usoni unaonekana umepaniki.

Mzee, endelea kukaa kimya maana huko tuendako zama zimeisha na mfalme mpya atawekwa na Mungu, huna la kufanya kuzuia
HAIWEZEKANI KUWATENGA VIONGOZI WA KANISA NA SIASA ZA NCHI YAO!

Wapendwa Watanzania!
Limekuwa ni jambo la kawaida kwa watawala au watu walio karibu na watawala wa Tanzania wakibanwa na viongozi wa dini hasa maaskofu huanza kutoa maneno ya propaganda dhidi ya viongozi wa dini wakiwaambia 'wasichanganye dini na siasa'. Msemo huu wanautumia kama kichaka cha kujifichia wasiguswe na viongozi wa dini!

Kauli hizo zimeibuka tena kwa kishindo zaidi kuanzia mwezi Juni 2023 baada ya maaskofu kuingilia sakata la Mkataba wa Bandari. Hivi karibuni tuliikemea Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ilipoitisha mkutano wa viongozi wa vyama vya siasa ili kujadili hoja ya viongozi wa dini kuonekana wakiwa na viongozi wa vyama vya siasa.

Tumeona ni wajibu wetu ili kuwaelimisha watu kuhusu suala hili kusudi wasije wakapotoshwa na wanasiasa katika suala zima la kudai haki katika taifa lao. Wanasiasa ni wajanja sana na wanajua nafasi na nguvu ya viongozi wa dini katika jamii ndio maana wanatumia nguvu ili kupotosha ukweli kuhusu nafasi ya viongozi wa dini katika ukombozi wa kifikra katika taifa.

Tunapenda kukiri kuwa hili tunaloliandika ndilo eneo ambalo sisi tuna ubobezi nalo, kwa hiyo hatubahatishi bali tunakiandika tunachokijua, tulichokisomea na kukifundisha katika ngazi za Chuo Kikuu.

Kwa upande wa Wakristo, chimbuko la dini hiyo ni mji wa Yerusalemu, Israeli ya Kale. Lakini, ni vizuri watu wakaelewa kuwa Ukristo una mizizi yake miaka 5000 kabla ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo. Hivyo, msingi mkubwa wa mafundisho ya Ukristo ni Biblia Takatifu yenye sehemu kuu mbili - Agano Jipya na Agano la Kale.

Dini haifanywi kwa wanyama na wala siasa pia haifanywi kwa ndege. Dini ni mfumo mzima wa maisha ambao ndani yake kuna mambo mengi. Tunaposoma au kufundisha kuhusu dini lazima tusome maisha ya jamii nzima ambayo kwanza dini ilifika kwayo. Kwa upande wa Wakristo, sisi tunasoma kuhusu jamii mbalimbali kama Misri, Syria, Ukaldayo (Babeli), Rumi, Wagiriki, Jordan, Waisraeli, Waajemi, Waarabu, Lebanon, nk.

Katika kusoma na kujifunza dini tunafundisha waumini kuishi kwa mifano ya jamii hizo ikiwa ni pamoja na kuiga mema na kuyaacha mabaya na hayo yanawezekana tu kwa kusoma kuhusu maisha yao kupitia viongozi au manabii wao.

Tunaposoma na kujifunza Biblia tunakutana na mambo yafuatayo:
1. Familia (family institutions): familia, ndoa, watoto, wajane, urithi, kifo, maziko, nafasi ya wanawake katika jamii, nk

2. Taasisi za Kiraia (Civili institutions): idadi ya watu, utumwa, taasisi ya kifalme, familia za kifalme, utawala, ajira na uchumi, kilimo, Afya na tiba, sheria na haki, mgawanyo wa muda, vipimo vya uzito, mahakama, nk.

3. Taasisi za Kijeshi (military institutions): majeshi ya Israeli, ngome za kijeshi, mbinu za kivita, siraha za kivita, vita, vita vitakatifu, nk

4. Taasisi za dini (Religious institutions): ibada, madhabahu, nyumba za ibada, uongozi wa taasisi za dini, Ofisi ya Ukuhani, Ofisi ya Walawi, sadaka, imani potofu, uchawi, utaratibu wa ibada, siku za ibada, sherehe na siku za sikukuu, nk.

Watu waliokuwa juu ya yote hayo ni viongozi wa dini na ndio waliopewa majukumu ya kuifundisha na kuionya jamii. Taasisi hizo ziliwekwa kwa ajili ya watu na kilichotofautisha ni ratiba. Wakati wa vita walipigana na wakati wa amani watu hao walifanya sherehe. Wakati wa mambo mazito ikiwemo kujua mustakabari wa nchi walikwenda kutafuta ushauri kwa viongozi wa dini. Alipotokea kiongozi mkorofi au jeuri alikemewa na viongozi wa dini au hata kutangaziwa kuondolewa madarakani na hao viongozi wa dini.

Sisi Askofu Mwamakula tunaitoa kwenu elimu hii ili msiyumbishwe ili muelewe kuwa viongozi wa dini kuingilia kati mtafaruku wa kisiasa au kiutawala ni ishara kuwa jamii yenu iko na afya!
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki
Dar es Salaam, 20 Agosti 2023; 12:35 jioni.
 
Majibu mazito yenye elimu kubwa kwa kila anayeyasoma
 
Back
Top Bottom