Rais Samia aagiza kuandaliwe Kanuni za Mikutano ya Vyama vya Siasa Nchini

Rais Samia aagiza kuandaliwe Kanuni za Mikutano ya Vyama vya Siasa Nchini

Ngoja tuone labda kanuni zitakuwa bora kuliko sheria yenyewe ya vyama vya siasa na miongozo yake.

Nachokiona nikama vile mchezaji anajiangusha uwanjani ilikupoteza muda.
 
1647109640957.png
 
Ushauri pekee wa kutolewa kwa sasa ni kuiheshimu na kuifuata katiba iliyopo ambayo inaruhusu shughuli za kisiasa za vyama vya kisiasa.

Hakuna tena haja ya kuandaa kanuni!

Kanuni za nini?

Tunaongozwa na viongozi ama wasioijua katiba au ambao hawaiheshimu kabisa!
Wakati wa jiwe hukuwa mkali hivi kama pilipili kichaa kwenye masuala ya kufuata Katiba!
Umepatwa na nini?
 
Kwani vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara sio haki yao kikatiba?... anyway....wenye kufanya siasa wanaelewa zaidi.
Nadhani hiyo haki kuna watu waliitumia vibaya, sasa ni muda muafaka wa kuangalia hiyo mikutano inafanyika vipi, haiwezekani baada tu ya uchaguzi nchi nzima ianze kampeni kwa uchaguzi ujao
 
Nadhani hiyo haki kuna watu waliitumia vibaya, sasa ni muda muafaka wa kuangalia hiyo mikutano inafanyika vipi, haiwezekani baada tu ya uchaguzi nchi nzima ianze kampeni kwa uchaguzi ujao
Kwani lengo la hiyo mikutano huwa ni kampeni tu...?

Je kama wanatambulisha sera zao ili kuvuna wanachama wapya pia ni kampeni?.... Unadhani bila mkutano wa hadhara wanaweza kupata wanachama wapya kirahisi?
 
Mimi binafsi ninaona kuna mantiki kubwa hapo. Vyama vya siasa viruhusiwe kufanya mikutano yao kisiasa katika muda na siku ambazo maandamano na mikusanyiko yao hayataathiri shughuli nyingine za wananchi. Uwekwe utaratibu shughuli kama hizo zifanyike siku na mida ambayo itakuwa ni rafiki kwa masuala mazima ya kiitifaki katika ulinzi na usalama.

Nashauri kanuni zizingatie siku pendelezwa, pengine ziwe zile za mwisho wa juma, yaani siku ya Jumamosi na Jumapili, ama siku nyingine za mapumziko ya kitaifa. Na muda pendelezwa wa kufanya matukio uwe ni saa tisa alasiri mpaka kumi na mbili jioni.

Shughuli za kisiasa zizingatie kutokubughudhi ama kuwa zenye kuleta kero katika matukio na shughuli za kawaida za wananchi.
 
Waziri wa katiba na sheria ameagizwa atunge kanuni ambazo zitaratibu kufanya mikutano ya hadhara ya vyama. Vya siasa. Hivyo sasa ni ruksa.

===

Rais Samia Suluhu Hassan ametoa agizo kwa Waziri wa Katiba na Sheria, George Simbachawene kuandaa kanuni zitakazoelekeza jinsi ya kufanya mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa.

Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi, Machi 12, 2022 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus imeeleza kuwa Rais Samia ametoa maelekezo hayo leo Jumamosi Machi 12, 2022 baada ya kupokea maazimio ya awali kutoka kikosi kazi alichokiteua cha kufuatilia hoja zilizojitokeza katika mkutano wa wadau wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa uliofanyika Desemba 15-17, 2021 Dodoma.

Rais Samia amemwagiza Waziri huyo kushirikiana na Tanganyika Lawa Society (TLS) pamoja na Zanzibar Law Society (ZLS) kutengeneza kanuni hizo.

“Kikosi kazi hicho chenye wajumbe 24, na ambacho kinawajibika moja kwa moja kwa Mhe. Rais, kiliwasilisha maazimio hayo Ikulu Jijijni Dodoma. Maazimio hayo yamegawanyika katika makundi matatu ya muda wa utekelezaji” imeeleza taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa azimio la muda mfupi ni uandaaji wa kanuni zitakazoelekeza jinsi ya kufanya mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa.

“Baadhi ya maazimio ya muda wa kati ni pamoja na rushwa na maadili katika uchaguzi, ruzuku, elimu ya uraisa, huku masuala yanayohusu uchaguzi wa katiba mpya vikiwa ni mpango wa muda mrefu”

Mwananchi
minaamini katika kutunga au kubadiri kanuni inamaana zile za mwanzo hazikukidhi au zinamapungufu ,sheria ya vyama vya siasa ipo hivyo kanuni zitungwe kuzingatia sheria zenyewe mfano jeshi la police libakie kwenye ulinzi wa laia na mali zao, wasimamie usalama na sikupanga nani afanye siasa nanani asifanye.
 
Mbona utaratibu wa kufanya hayo upo!

Why are these people reinventing the wheel???

Katiba, hata kama ni pungufu na iliyopitwa na wakati, ipo lakini haifuatwi.

Hiyo mpya ndo itakuwaje sasa?

Huu ni ujuha.
Mteule wa Rais aandae utaratibu wa mikutano ya siasa
 
Mbona utaratibu wa kufanya hayo upo!

Why are these people reinventing the wheel???

Katiba, hata kama ni pungufu na iliyopitwa na wakati, ipo lakini haifuatwi.

Hiyo mpya ndo itakuwaje sasa?

Huu ni ujuha.
Mteule wa Rais aandae utaratibu wa mikutano ya siasa
 
Muongo wewe!
Huyu[emoji116] alikuwa wewe?
 
Bado anatokea mmakonde mmoja na kusema wanawake ni viumbe dhaifu, wakati kila mianaume ya upinzani inaitwa ikulu na huko kwa mabeberu kisha inainamishwa vichwa kwa sauti laini inakuwa miimba mapambio.

Hata Samson na miguvu yake aliwezwa na mwanamke mmoja tu legevu legevu kimuonekano, the same kwa Zitto, Mbowe na Lissu.

Maendeleo hayana chama
Ndugu yangu usitupofushe wakati ramani inasomeka vyema. Mama aliminywa kisawasawa akaambiwa aende kwa Lissu kupata maagizo. Baada ya mkutano wao Lisu aliwahi fasta kutuhabarisha makubaliano ili ulimwengu usikie. Mama akasema "tumesawazisha". Lissu alisema wamekubaliana Mbowe afutiwe mashtaka bila masharti na hili limefanyika, wale 19 watolewe bungeni hili bado ila linakija, kuwepo na mikutano ya hadhara ndo hili linatekelezwa. Ukitaka kuhakiki nenda YouTube uhakiki ndo utaona mama anacheza ngoma ya Lisu.

Licha ya kucheza ngoma ya Lisu mama ameonyesha ukomavu na uvumilivu wa kisiasa kwa hiyo mtu kama huyu kwa nini umsumbue wakati anatekeleza makubaliano?
 
Nikwann wanaccm wengi hili halijawafurahisha na wanalipinga Kwa mgongo wa kuwalaimu mbowe na lissu walitaka lissu na mbowe wamgomee mama ili achafuke wataulu mambo yao waliomuandalia 2025
 
Inavoonekana mwendazake alizifuta kanuni kimya kimya,ndiyo maana haionekani kwenye katiba,vinginevyo Kama ameakiza kanuni zitungwe sasa,inavoonekana vyama vingi ndiyo vinaanzishwa sasa.
Kwenye hizi Kanuni mpya Mapolisi yasitajwe kabisa zaidi ya kutoa ambayo ndio kazi yao.
 
Ukiwa na utapiamlo wa akili ukaona nyuzi kama hizi ambazo zinataja neno 'Rais' kila saa unaweza kufikiri kuwa ni kweli Tanzania ina Rais.
Moja ya michango yako yenye maneno kagumu toka wewe kuingia jf ni hii aseee
Mzee mwenzangu umekutwa na nini tena aseee
 
Huyu[emoji116] alikuwa wewe?
I love it! Haya twende kazi.

Huyu aliyeanzisha hii mada ni baba yako au bwana wako!

 
I love it! Haya twende kazi.

Huyu aliyeanzisha hii mada ni baba yako au bwana wako!

Wewe dimwit ulikuwa unatetea uvunjaji Katiba wa jiwe halafu unaleta kiuzi chako cha kubomoa cha kujibaraguza. Huna akili au ni mshamba usiyejua tofauti ya uvunjaji Katiba na upuuzi mwingine.
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge kwa kushirikiana na Tanganyika Law Society (TLS) pamoja na Zanzibar Law Society (ZLS) ameagizwa kuandaa kanuni zitakazoelekeza namna ya kufanya mikutano ya hadhara ya Vyama vya Siasa...
qRI8Gs7.gif
 
Back
Top Bottom