Rais Samia bado anapotoshwa, hajapata washauri wenye weledi

Soma vzr economics baba , mabeberu hawabahatishi wanapotaka lao, umembana kweli kweli amebaki kuongea ongea mambo mepesi
Economics ipi we unaendeaje kukopa pesa ambayo mtu anayekupa anakupangia Cha kufanya wakati anajua umeweka dhamana ya kukopa?

Kama ni wa kupangiwa kwanini ukope?
 
Tatizo ni kuwa wanakijani wapo kila kona, wameshika vitengo vyote muhimu, na tabia yao kubwa ni kumwabudu rais aliyepo madarakani, ndiyo maana nikasema wanaodhani eti 2025 watachukua fomu ya urais CCM na kushindana na Samia wanapoteza muda wao, hamna mwanakijani atakubali hilo!! Njia pekee ya kupata hiyo katiba mnayoipigania ni ni kuBOW DOWN na kushirikiana na chama na serikali bila kejeli wala majigambo ya hovyo, hilo halimaanishi kwamba mtaacha kuikosoa serikali!! UKITAKA KULA LAZIMA NAWE ULIWE, sasa CDM wao wanataka kula tu bila kuliwa!!! COMPROMISES ndizo zinaendesha dunia kwa sasa, unakula kidogo na wewe unaliwa kidogo! Ndicho kinaendelea kwa wataliban na US kwa sasa, ulitegemea hizo pande 2 kuna siku zitakaa meza moja na kufikia makubaliano flani?
 
Wawakilishi Ni bunge lenu la ccm watupu si mlisema upinzani unakwamisha maendeleo? Halafu mnataka wao ndio wawashauri pumbavu nendeni mkashauriwe uo ujinga na wakina mwigulu mtaona matokeo yake !!
Huko ulipo hamna mtu mwenye hadhi hata ya kufunga kamba ya viatu vya Mwigulu
 
Kama unapewa mashariti magumu kwanini ukope? Kukopa Kuna maana gani?

Wewe ndiye mjinga kukopa sio lazima sisi hatuna vita
Hivi nyie mkipewa nchi mtaiongoza kwa hela zipi? Kodi, tozo, mikopo na misaada vyote mnapinga!! Tueleze kidogo source yenu ya income mkipewa nchi itakuwa ni nini?
 
Wewe ndiye kilaza takataka unaleta uvyama kwenye Mambo ya kitaifa isitoshe kusema wewe Ni mpumbavu kabisa
Endeleeni kudai katiba mkiamini eti ndiyo itawapeleka Ikulu, matokeo yake nchi nzima imwewasusia hilo dai lenu la katiba mnabaki kutapatapa
 
Kama umemsikiliza jana NKM wa CDM kwenye press yake basi utajua majukumu ya vyama vya siasa ni nini!! Katika moja ya hoja zake amesema wameomba kuonana na Samia ili KUMSHAURI namna ya kuongoza nchi vizuri bila mikwaruzano! Ingekuwa wabunge ndiyo washauri pekee wa Rais basi Samia asingekubali kuonana na wapinzani kwa sasa maana bunge ni la CCM tupu! Ninachojua kazi ya bunge ni kutunga sheria na kuisimamia serikali, sijawahi sikia mahali eti mbunge kazi yake ni kuishauri serikali, huyo atakuwa ni mbunge asiye na meno!!
Huyo mleta mada kashauri ujinga, kiushabiki, umeshaambiwa huo mkopo una masharti nafuu then yeye anasema kwa nini wanajenga hiki, wananunua hiki, ndiyo masharti ya mkopo hayo!
 
Hayo Ni mawazo yako wewe,na sio lazima tuwaze sawa
 
Mkuu, endelea kupiga mtori. Nyama utazikuta chini
 
Kwaji yeye hana akili hadi apotoshwe? Kama anakubali kupotoshwa na yeye hatumii akili yake basi yeye ndiye tatizo.
 
VIP kununua ndege cash unakubaliana naye?
Unafikiri manunuzi ya ndege yanafanyika kama kununua machungwa sokoni.

Kwahiyo kwa akili yako unadhani order ya hizo ndege imefanyika miezi 6 iliyopita ??
 
Ambacho hujaelewa ni nini?Ndio maana unaona wamesema wameomba kukutana naye ili wamshauri,Rais anaweza akakataa au kukubali!Na chama kinaweza kukaa bila kuishauri serikali na kikaendelea kutambulika na msajili!Sasa hiyo unayosema mshauri mkuu Wa serikali ni vyama vya siasa umeitoa wapi?
Lakini bunge linawajibika moja kwa moja kuishauri/kuikosoa serikali!Ndio maana mapendekezo ya bunge huwa yanachukuliwa na serikali na kufanyiwa kazi,kuna ambayo yanachukuliwa na ambayo yanaachwa!Ndio maana yakaitwa mapendekezo!Hata wabunge wakisimama huwa wanasema wanashauri moja,mbili,tatu hasa kwenye kuchangia bajeti!
Sijasema bunge ndio washauri pekee Wa serikali ila nimepinga kuwa washauri wakuu Wa serikali ni vyama vya siasa!Mshauri mkuu huwezi kuwa na hiari ya kuishauri au kutoishauri serikali!Hapo hakuna uwajibikaji kisheria!
Bunge kuisimamia serikali ni pamoja na kuishauri/kuikosoa!Hili linaeleweka wazi!
Hoja hapa sio mleta mada kashauri jambo LA hovyo au la msingi,hoja hapa ni kuwa ana haki hiyo ya kuishauri serikali,hata kama ushauri wake ni mbovu!Sasa wewe umejikita kumuonesha kuwa Rais anawashauri wake hivyo yeye hana haki ya kuishauri,hapo ndio napingana na wewe!Tu kuisha kuna pia na kuwa anayo haki na wajibu wa kuikosoa serikali basi ndio tunaweza kujadili maudhui ya ushauri wake!
 
Wanao mshauri wanajua kwamba wana mpotosha.

Hao ni kina Mwigulu. Rais wa kwenye mawe. Nae anautaka urais. Hivyo Mama akiboronga ni credit kwa wataka urais.

Mama yeye bado haja soma hiyooo...
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 

Tulia Chief afanye kazi, we nani unampangia?!
 
Kikwetu alisema akili za kuambiwa ongeza na zako. So ifike maali atumie mahamuz yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…