Rais Samia: Kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, lakini mbona mnakula sana mnavimbiwa? Jipimieni!

Rais Samia: Kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, lakini mbona mnakula sana mnavimbiwa? Jipimieni!

Tuhamasishe wananchi wawakatae hata kabla ya uchaguzi?

Tuandamane?

Tugome na kufanya migomo ya nguvu?

" kila waziri anatakiwa ale kulingana na urefu wa kamba yake" Anonymous.

F8B8ABD4-3E8C-4392-BBFF-2439CC24CEA6.jpeg
 
Nimemsikia Rais Mama Samia anasema kila mbuzi hula kutokana na urefu wa kamba yake akiwambia kikao na Mawaziri wake, sijuwi amemaanisha nini kwamba mawaziri sasa wataanza kugawana rasilimali na mapato?

Emu tujielekeze hapa kidogo wale watu wenye taaluma fasihi, Mama kila siku anatoa kamsemo mpya mpya

View attachment 2079590

Natanguliza shukurani
Maanake wao waendelee kula vinono
 
Rais akiwahutubia Mwaziri na makatibu wakuu,, amasema anajua kila mtu anakula na atakula kwa urefu wa kamba yake lakini kwa sasa waanzidi hadi awanagombana. Je, hii si ndiyo maana ya Rais kuruhusu upigaji ila uwe wa kiistarabu?
Na watu wanapiga kweli kweli
 
Siyo kwa viongozi tuu, Mtu yeyote yule anayeongea kabla ya kupanga nini cha kusema, wapi pa kusemea, na namna ya kusema ni mtu mropokaji. Bahati mbaya kwa Tanzania ni kwamba hao ndio viongozi.

Na pia sio lazima Rais aandikiwe nini cha kuongea, hapana! Muhimu ni yeye mwenyewe kujiandalia nini cha kuzungumza. Vladmir Putin anajiandikia hotuba zake yeye mwenyewe, na hajawahi kutoa boko.
Hapa tumeliwa kwa kweli
 
Kwa sasa hivi SSH ana- 'grapple' na 'government coordination'.. Wengi wa Mawaziri wake wanakosa ubunifu hivyo kufanya 'vision' za SSH kutekelezwa kwa mwendo wa kobe au ndivyo sivyo..
Hapa ndipo ilipotakiwa 'robust opposition' kuwaamsha..
Pia asisahau bado mawazo ya baadhi ya Mawaziri wake yapo katika uchaguzi mkuu wa 2025 hivyo bado atapambana nao sana..
 
Acha kujifanya kuwa hamnazo.Wewe ulikuwa unafikiri kuwa ufisadi ni kuiba peke yake na ndiyo maana ukawa unadai kuwa mtu alieiba fedha nyingi kiasi hicho amezificha wapi?Kumbe ufisadi siyo lazima mtu aibe.

Unachopaswa kufanya ni kunishukuru kwa kuwa nimekupa elimu ya ufisadi.Ulikuwa hujui maana ya ufisadi.

Onyesha sehemu niliyo sema nafikiri ufisadi nikuiba pekeake.
Otherwise unalopoka tu kama mlevi.

Ikiwa unawaza kama kunamtu humu kwenye hili jukwaa hajui maana ya ufisadi basi wewe ni mtu wa kupuuzwa.
 
Onyesha sehemu niliyo sema nafikiri ufisafi nikuiba pekeake.
Otherwise unalopoka tu kama mlevi.

Ikiwa unawaza kama kunamtu humu kwenye hili jukwaa hajui maana ya ufisadi basi wewe ni mtu wa kupuuzwa.
Ulichoandika kimeandikwa wala huwezi tena kubadilisha maana yake.

Kitendo chako cha kudai kuwa "Hiyo pesa mtu anaweza kuiiba pekeake alafu isijulikane ilipo, aliiweka kwenye account gani ama ipo kwenye mabegi nyumbani kwake?" kinathibitisha bila kutia shaka kuwa ulikuwa unaamini kuwa ufisadi ni wizi peke yake, wakati 1.5 trilioni inaweza kupotea kupitia rushwa,kununua wapinzani,matumizi nje ya budget na kadhalika.

Wenye akili zetu tunajua kusoma na kuelewa vizuri.
16421374254300.jpg
 
Wewe mpumbavu tutajie hata watu watano waliouawa na Magufuli? Hivi unaunga mkono huu ujinga anaousema huyu bibi yako? You are very stupid!
Wewe ndiyo mpumbavu popoma. Pokea orodha hii
1.Ben Saanane
2. Azory Gwanda
3. Lwajabe
4. Diwani wa CDM Hananasif
5. Akwilina
6. Diwani wa Ifakara
7. Wananchi 300 wa MKIRU
8. Kutekwa kwa Roma Mkatoliki
9. Kutekwa kwa MoDewji
10. Kutekwa kwa Masoud Kipanya
11. Kushambuliwa kwa Zakaria Trans Tarime
12. Kushambuliwa kwa Tundu Lissu

Mungu ni wa ajabu, Tundu Lissu yuko hai lakini Magufuli amekuwa chakula cha minyoo huko Chato
 
Nimesikiliza mara kadhaa alichosema siamini nilichosikia! Ule ni uhamasishaji wa rushwa wa kutisha! Kwamba wale kidogo wasivimbiwe! Mbele ya National Television!

CCM haipiti miaka miwili mtapita magumu kiutawala ambayo hamjawahi kupitia toka chama hiki kianzishwe! Tunajua awamu zote kuna wizi/ufisadi ila si kwa kiongozi mkuu kutamka maneno ya namna hii. Shame!
 
Ulichoandika kimeandikwa wala huwezi tena kubadilisha maana yake.

Kitendo chako cha kudai kuwa "Hiyo pesa mtu anaweza kuiiba pekeake alafu isijulikane ilipo, aliiweka kwenye account gani ama ipo kwenye mabegi nyumbani kwake?" kinathibitisha bila kutia shaka kuwa ulikuwa unaamini kuwa ufisadi ni wizi peke yake, wakati 1.5 trilioni inaweza kupotea kupitia rushwa,kununua wapinzani,matumizi nje ya budget na kadhalika.

Wenye akili zetu tunajua kusoma na kuelewa vizuri.
View attachment 2080194

Nilicho andika kimeeleweka jinsi kilivyo, we endelea kudhibitisha lamli zako.
 
Back
Top Bottom