Rais Samia: Kuna mtu kakopa benki zetu 5 katoweka

Rais Samia: Kuna mtu kakopa benki zetu 5 katoweka

Mzee baba mwenyewe ripoti kama hizi aliziogopa sana tu rejea kutenguliwa kwa prof Assad, watanzania tunatabia za kinafiki sana si ajap kuona tunamtukuza rais kuliko taifa lenyewe. Rais sio Mungu wala Malaika Kuna muda na wakati anaitaji msaada kisayansi, kimedani na ujuzi kuweza kukabiliana na uvujaji wa mapato ya nchi.
Eti mtu.huu ndi ujinga umelitafuna hili taifa kwa miaka mingi.

Hazizungumziwi taasisii, watu wanataka mtuuu.ujinga.
 
.........rais Samia kwa sasa anafahanu mengi kuhusu uongozi wa nchi serikali na watendaji Kwa ujumla lakini yeye ni mtu mwenye subira na mvumilivu sana..... ndo maana watu wanaona kama mambo yanaharibika au hachukui hatua, hii sio kweli huyu mama ni menda haki.......na niseme tu zinakuja siku ambazo mama atachukua hatua kali sana Kwa baadhi ya watendaji na watu hawataamini........ni swala la muda tu......
Tueendelee kusubili huku kibubu chetu kinaendelea kuisha,wezi hawana huruma lkn Tete kaamua kuwaonea huruma ngoja ieendelee kunyesha.
 
Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan leo wakati akipokea Ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG) Ikulu Jijini Dar es salaam amehoji kuhusu mikopo chechefu na kusema kuna baadhi ya Maafisa wa Benki wanashirikiana na Wateja kupitisha mikopo kinyume na inavyotakiwa kisheria.

“Kuhusu mikopo chechefu na yenyewe unajiuliza why mikopo chechefu?, hivi ingekuwa Benki zinazotoa mikopo ni Benki binafsi kwenye rekodi zao kungekuwa na mikopo chechefu?, kusingekuwa, wetu sisi wa Serikali wanashindwa nini mpaka kunakuwa na mikopo chechefu?, kuna ushirikiano baina ya Maafisa wa Benki na hao wanaoenda kukopa, andika nitakupitishia ukipata chako hiki changu hiki, hailipiki tunasema mikopo chechefu”

“Kuna Mtu, Mfanyabiashara kakopa Benki zetu sita sijui tano Mabilioni kila Benki, kachukua fedha yetu kaitoa nje na yeye kaondoka, leo tunasema mikopo chechefu mlipompa huyu!, dhamana zote alizoweka ni feki, zote feki, kama sio ushirikiano kitu gani?

Lakini Watu wanazunguka tunawatazama, wapo na wanajua walichokifanya, hii mikopo chechefu itachechemea mpaka tujirekebishe na inapochechemea na Nchi inachechemea”

WANAJAMVI HEBU TUJUZANE HUYU ANAYETAJWA HAPA NI NANI?

Sina wazo tofauti na ya wale waloongeza cha juu kwenye manunuzi ya ndege. Hatua ni zilezile zifwatwe. Na hiyo mikopaji ikamatwe irudishe pesa. Hawezi kukimbia asionekane. Tumia polisi ya kimataifa na taifisha mali zote zilizobaki.
 
Hiyo si kweli mama amesinzia mno. Mwamba alikuwa halali si kwa kutaka sifa bali ku detect huu upuuzi wa majizi. Sasa yeye anasubiri tuuuu kazi kucheza mdako
Magufuli alikuwa anakesha na mafaili hadi chumbani hakuna wanafiki na wachomokea dili fisadi kama wafanyakazi wa umma wakikusoma kuwa huna muda wa kupitia mafaili

wakimjua Raisi kuwa lazier faire watampiga dili atasaini mi dili ya wenzi serikalini hadi akome mwisho wa zigo linamwangua yeye

Kikwete alikuwa lazier faire hajali
.alipigwa na vitu vizito kibao vya kifisadi hadi na waziri mkuu wake Lowasa zikiwemo Dowans,IPTL nk kuamuka anakumbuka shuka kumekucha kashifa zote zinamlenga yeye kuwa yeye Kikwete mwizi na CCM yake

CCM manusura ianguke kama KANU Kenya kutokea Magufuli ndio aliokoa jahazi

Samia ajue watendaji serikalini wanamsoma wanamlia timing tu ya kumwiibia asione wanajitia kuimba wimbo ohh Magufuli alikuwa mbaya ndio nyimbo zao hizo za kuzuga Raisi mpya awape nafasi waited

Kikwete alipooondoka madarakani nyimbo zilihamia kwa Magufuli kuwa wewe uko vizuri kuliko Kikwete,Kikwete alikuwa mwizi mkubwa na maswahiva wake
i
RAISI Samia awe makini na waimba kwaya wa kuponda viongozi waliopita na kumpamba maua kuwa yeye bora laweza kuwa anguko lake kisiasa mbeleni ni ma mafia wa kisiasa

Wanampamba ili awaamini wamwibie tena mno

Asicheke na ngedere atakuja kukuta ngedere wamekula shamba lote

Asione Magufuli alikuwa mjinga kuwa mkali vile hasa kwa Public Servants

Walau katumia neno Stupid kwa hasira kuwa kaanza kuelewa Public servants wanamchezea

Serikalini ukicheka na Public servants jiandae kulia
 
Magu kwenye madhimisho ya mahakama (ilikuwa miaka 100 ya mahakama),aliongea mbele ya jaji mkuu kwamba wazipush kesi za mafisadi ambazo kwa kinywa chake alisema kama kesi zingeendeshwa serikali ilikuwa na uwezo wa kuingiza 300+tn.Baadae mawakakili,l,wanaharakati wakiongozwa na wale madada waaojiita mashangazi,wanasiasa na baadhi ya NGO,wakadai rais dikteta anaingili uhuru wa mahakama.

Ndio maana Magu alikuwa anawambia mfisadi watoe hela aondoe kesi mahakamani, watu mkalalamika anapora hela za watu nk.

Sasa ulitaka afanye nini wakati mpaka majaji walimkwamisha.

Hii nchi ukicheka na kima lazima watakurudisha nyuma.
Ccm ni ileile mkuu, mahakama ni chombo huru hakipaswi kuingilia, sijawahi ona serikaki imemshitaki fisadi au mwizi w mali za umma, mpaka sasa kuna kesi ngapi za mafisadi? Wapo mtaani wanatamba tu
 
Madudu hayaishi we unadhani ni kitu kitu gani kilimfanya jpm afoke kila siku hadi afya yake ikatetereka!! Msimsingizie mama wtz ni wezi mno tena mno
Ni kweli hayawezi kuisha ila wananchi tunataka kuona wizi mkubwa unaisha na ubaki wizi mdogo mdogo chini uko Halmashauri.
 
Hasira hukaa kifuani mwa mpumbavu ukiwa kama una akili timamu huwezi kusema 1.5tr haikuwa na ushahidi wakati imetajwa mara kadhaa na CAG na Rais aliepita kujifanya anapiga mikwara mbuzi, hapa hakuna double standard wajinga wachache kama wewe wanataka kumuangushia jumba bovu Rais wa sasa ambae amekubali mapungufu na uwazi kwenye utoaji wa ripoti. Kitu cha aibu siku anaapishwa kichere anachimbwa mkwara kuwa nenda kajifanye muhimili. Acha utoto umeshakua
Ww naona unaminyoo kichwani hasa kwwenye sustial nigra of basalgangalia menmbrane CAG huyo huyo aliyetumbuliwa ni mara ngapi amekuwa akilitolea maelezo kuwa hakukuwa na pesa iliyoibiwa khaa au unaakaa nje ya nchi ni boya
 
Daaah aseee huyo mbwa kalamba asali ya kwake na vizazi vyake aseee 50B sii mchezo alafu hafanywi kitu sasa daaah mpaka raha [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji16][emoji16][emoji16]

Kweli jpm aliwabinya mapumbu hawa watu

Saivi kila mtu ana jamba kwenye sekta yake na watu wanalamba tu [emoji518][emoji518][emoji518][emoji518] daaah huu ndo muda muafaka mkuuu wakupiga pesa

#Grace period# [emoji16][emoji16][emoji16]
Huyu Raisi alisema hawezi kupola Watu pesa zao kama utawala wa Simba wa Yuda, sasa kama yeye mtenda haki mbona wananchi tunapolwa pesa zetu hataki kuturudishia kama alivyo warudishia matajiri aliyosema waliporwa pesa zao na Magufuli?
 
Wewe ni kilaza wa wapi vyombo vyenye mamlaka kama takukuru na vinginevyo ndio vinaenda kufanya uchunguzi baada ya kuchambua ripoti ya CAG kama kuna harufu ya mis allocation of public funds, kumbuka kangi lugola baada ya kulipuka na kasema CAG ni muongo baada ya wizara take kutajwa akaonywa kuwa ripoti huwa haipigwi kile ni kama Chombo cha usimamizi wa fedha za umma.
Ndio maana nakuambia ww unaminyoo kichwa au upo nje ya nchi aliyekuambia 1.5 t ziliibwa ni nani au unakichaa cha mimba unakuja na vitu vya kufikiriak muulize hasadi kama kuna hata 1m liyoibiwa achilia mbali hiyo 1.5t
 
Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan leo wakati akipokea Ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG) Ikulu Jijini Dar es salaam amehoji kuhusu mikopo chechefu na kusema kuna baadhi ya Maafisa wa Benki wanashirikiana na Wateja kupitisha mikopo kinyume na inavyotakiwa kisheria.

“Kuhusu mikopo chechefu na yenyewe unajiuliza why mikopo chechefu?, hivi ingekuwa Benki zinazotoa mikopo ni Benki binafsi kwenye rekodi zao kungekuwa na mikopo chechefu?, kusingekuwa, wetu sisi wa Serikali wanashindwa nini mpaka kunakuwa na mikopo chechefu?, kuna ushirikiano baina ya Maafisa wa Benki na hao wanaoenda kukopa, andika nitakupitishia ukipata chako hiki changu hiki, hailipiki tunasema mikopo chechefu”

“Kuna Mtu, Mfanyabiashara kakopa Benki zetu sita sijui tano Mabilioni kila Benki, kachukua fedha yetu kaitoa nje na yeye kaondoka, leo tunasema mikopo chechefu mlipompa huyu!, dhamana zote alizoweka ni feki, zote feki, kama sio ushirikiano kitu gani?

Lakini Watu wanazunguka tunawatazama, wapo na wanajua walichokifanya, hii mikopo chechefu itachechemea mpaka tujirekebishe na inapochechemea na Nchi inachechemea”

WANAJAMVI HEBU TUJUZANE HUYU ANAYETAJWA HAPA NI NANI?

Huyu ndio Rais, naye anaongea kama anapigwa stori .

Tumeingizwa chooo Cha kike na Katiba.
 
Kuna sehemu nilimsikia Rais wetu akisema mnaiba fedha zote hizo za nini? Hamtosheki?
Harafu kasema : Kama mmeshindwa kuwatoa hao wabadhirifu wa fedha za umma basi wahamisheni vituo vyao vya kazi muwapeleke kule kwenye sehemu za mapato madogo!
Atoke tu madarakani rais hawezi kuwezi kuwa na kauli kama hiyo aisee hiyo ni fedheha
 
Back
Top Bottom