Rais Samia: Kuna mtu kakopa benki zetu 5 katoweka

Rais Samia: Kuna mtu kakopa benki zetu 5 katoweka

Magufuli alikuwa anakesha na mafaili hadi chumbani hakuna wanafiki na wachomokea dili fisadi kama wafanyakazi wa umma wakikusoma kuwa huna muda wa kupitia mafaili

wakimjua Raisi kuwa lazier faire watampiga dili atasaini mi dili ya wenzi serikalini hadi akome mwisho wa zigo linamwangua yeye

Kikwete alikuwa lazier faire hajali
.alipigwa na vitu vizito kibao vya kifisadi hadi na waziri mkuu wake Lowasa zikiwemo Dowans,IPTL nk kuamuka anakumbuka shuka kumekucha kashifa zote zinamlenga yeye kuwa yeye Kikwete mwizi na CCM yake

CCM manusura ianguke kama KANU Kenya kutokea Magufuli ndio aliokoa jahazi

Samia ajue watendaji serikalini wanamsoma wanamlia timing tu ya kumwiibia asione wanajitia kuimba wimbo ohh Magufuli alikuwa mbaya ndio nyimbo zao hizo za kuzuga Raisi mpya awape nafasi waited

Kikwete alipooondoka madarakani nyimbo zilihamia kwa Magufuli kuwa wewe uko vizuri kuliko Kikwete,Kikwete alikuwa mwizi mkubwa na maswahiva wake
i
RAISI Samia awe makini na waimba kwaya wa kuponda viongozi waliopita na kumpamba maua kuwa yeye bora laweza kuwa anguko lake kisiasa mbeleni ni ma mafia wa kisiasa

Wanampamba ili awaamini wamwibie tena mno

Asicheke na ngedere atakuja kukuta ngedere wamekula shamba lote

Asione Magufuli alikuwa mjinga kuwa mkali vile hasa kwa Public Servants

Walau katumia neno Stupid kwa hasira kuwa kaanza kuelewa Public servants wanamchezea

Serikalini ukicheka na Public servants jiandae kulia
Unamzungumzia raisi yupi kiongozi kama saa 100 hiyo ni kama myth consipirscy theory .hatuna raisi pale tumepigww na kitu kizito kichwani
 
Ccm ni ileile mkuu, mahakama ni chombo huru hakipaswi kuingilia, sijawahi ona serikaki imemshitaki fisadi au mwizi w mali za umma, mpaka sasa kuna kesi ngapi za mafisadi? Wapo mtaani wanatamba tu
Sasa yule mkwe wake Lowasa,Rugemalira na yule Muhindi walifanywa nini?

CCM ni ile ile na ina matawi yake kama haya.
MMGL0367.jpg

MMGL0885.jpg
 
.........rais Samia kwa sasa anafahanu mengi kuhusu uongozi wa nchi serikali na watendaji Kwa ujumla lakini yeye ni mtu mwenye subira na mvumilivu sana..... ndo maana watu wanaona kama mambo yanaharibika au hachukui hatua, hii sio kweli huyu mama ni menda haki.......na niseme tu zinakuja siku ambazo mama atachukua hatua kali sana Kwa baadhi ya watendaji na watu hawataamini........ni swala la muda tu......
Subira mpaka lini? hatua zichukuliwe kuondoa ndama wanaonyonya bila kushiba hao. Hatuna haja na subira.
 
Ndio maana nakuambia ww unaminyoo kichwa au upo nje ya nchi aliyekuambia 1.5 t ziliibwa ni nani au unakichaa cha mimba unakuja na vitu vya kufikiriak muulize hasadi kama kuna hata 1m liyoibiwa achilia mbali hiyo 1.5t
Ukitaka kujibu hoja za mtu mzima upaswa ujitawaze kwanza hoja yangu ya msingi ni kuweka mazingira ya uwazi kwa serikali kuikubali kuwajibika baada ya kupokea ripoti ya CAG. Kifungu cha 28 cha sheria ya ukaguzi wa umma na 11.ya mwaka 2008 ndicho kinachompa mamlaka CAG kufanya yake. 1.5tr hazikujulikana zilipo licha ya polepole kuja na hesabu zake zisizoleweka. Unachopaswa kujua haya mambo hayataki double standard inapoonekana kuna leakage ya mapato yetu tuwe na maoni ya pamoja sio kutoka mapovu.
 
Ww naona unaminyoo kichwani hasa kwwenye sustial nigra of basalgangalia menmbrane CAG huyo huyo aliyetumbuliwa ni mara ngapi amekuwa akilitolea maelezo kuwa hakukuwa na pesa iliyoibiwa khaa au unaakaa nje ya nchi ni boya
Wewe huna akili unafikili sijui kuwa report inapopelekwa bungeni kujadiliwa ndio hubainishwa kama Kuna wizi au lah pale vyombo husika kama takukuru na kamati za Bunge kufanya uchunguzi wao. Point ni kwamba kwanini report haikwenda bungeni, na kwanini CAG kukejeliwa kwamba alijifanya muhimili na wakati kananu za kimataifa zimebainisha kuwa ukaguzi wa umma ni tathimini huru. Rais hapaswi kujifanya Malaika wewe kenge elewa hata huyu wa sasa kama wananchi tunapaswa kufuatilia ni hatua zipi Zitachukuliwa kwa wahusika baada ya uchunguzi.
 
Magu kwenye madhimisho ya mahakama (ilikuwa miaka 100 ya mahakama),aliongea mbele ya jaji mkuu kwamba wazipush kesi za mafisadi ambazo kwa kinywa chake alisema kama kesi zingeendeshwa serikali ilikuwa na uwezo wa kuingiza 300+tn.Baadae mawakakili,l,wanaharakati wakiongozwa na wale madada waaojiita mashangazi,wanasiasa na baadhi ya NGO,wakadai rais dikteta anaingili uhuru wa mahakama.

Ndio maana Magu alikuwa anawambia mfisadi watoe hela aondoe kesi mahakamani, watu mkalalamika anapora hela za watu nk.

Sasa ulitaka afanye nini wakati mpaka majaji walimkwamisha.

Hii nchi ukicheka na kima lazima watakurudisha nyuma.
Zikapelekwa CHINA...
 
Ila Kwa Kwa kweli Mh. Rais kwenye hotuba yake alikerwa wazi wazi. Walioko chini yake kuanzia Makamu wake na Waziri Mkuu wasisubiri mpaka awatume wanatakiwa wachukue hatua fasta.

Yaani mpaka Leo Takukuru walitakiwa wawe wameshakamata watu na wanaotakiwa kutumbuliwa watumbuliwe fasta.

Nakumbuka Kuna Rais mmoja kule Togo aliwahi kusema kuwa kuwa Kuna mtu Fulani ni Msaliti wa nchi na kule Jeshini wakati wa vita wanajua anachotakiwa kufanywa Msaliti.
Kesho yake TU yule mtu alipigwa risasi za kutosha na kuaga nchi Kwa majeraha makubwa.
Sasa Rais wetu Jana alionyesha kukerwa sana na ufisadi jambo ambalo walioko chini yake walitakiwa wakitoka pale watoke na hasira Ile Ile ya Mheshimiwa Rais na kuwatia ndani wahusika wote wa ubadhirifu huo mkubwa sana kuwahi kutokea .
 
Magu kwenye madhimisho ya mahakama (ilikuwa miaka 100 ya mahakama),aliongea mbele ya jaji mkuu kwamba wazipush kesi za mafisadi ambazo kwa kinywa chake alisema kama kesi zingeendeshwa serikali ilikuwa na uwezo wa kuingiza 300+tn.Baadae mawakakili,l,wanaharakati wakiongozwa na wale madada waaojiita mashangazi,wanasiasa na baadhi ya NGO,wakadai rais dikteta anaingili uhuru wa mahakama.

Ndio maana Magu alikuwa anawambia mfisadi watoe hela aondoe kesi mahakamani, watu mkalalamika anapora hela za watu nk.

Sasa ulitaka afanye nini wakati mpaka majaji walimkwamisha.

Hii nchi ukicheka na kima lazima watakurudisha nyuma.
Magufuli alikuwa anatumia njia zinazoleta matokeo ya haraka. Ndio maana wengi hawakumpenda sababu ukifata njia ndefu hufikii lengo maana chenga zinakuwa nyingi. 😀😀😀😀😀 It worked on his favour na ndio maana wengi wamejawa mimba za chuki to date.

Mtu kaiba ila anataka abembelezwe na mahakama we, ahonge honge hela jalada lisiandikwe au kesi ipigwe dana dana mwishowe inazimwa kijanja
 
Hasira hukaa kifuani mwa mpumbavu ukiwa kama una akili timamu huwezi kusema 1.5tr haikuwa na ushahidi wakati imetajwa mara kadhaa na CAG na Rais aliepita kujifanya anapiga mikwara mbuzi, hapa hakuna double standard wajinga wachache kama wewe wanataka kumuangushia jumba bovu Rais wa sasa ambae amekubali mapungufu na uwazi kwenye utoaji wa ripoti. Kitu cha aibu siku anaapishwa kichere anachimbwa mkwara kuwa nenda kajifanye muhimili. Acha utoto umeshakua
Raisi wa sasa anachofanya ni kipi hasa cha maana zaidi ya kukopa hovyo bila kusimamia uwajibikaji na matumizi.

Kukumbatia ufisadi ni udhaifu mkubwa ambao unachefua watu wote wenye akili. Huduma za kijamii hovyo, matozo lukuki, maisha hayaeleweki watu wanaburuzwa buruzwa tu kama wakimbizi yeye kakumbatia wezi na wafanyabiashara wanyonyaji wakwepa kodi. Aisee usitake nikuongeze tusi.

Hio ripoti ambayo imesomwa ikaonesha watu wameiba mabilioni bila kuchukuliwa hatua inanisaidia nini mimi katika haya maisha?
 
Raisi wa sasa anachofanya ni kipi hasa cha maana zaidi ya kukopa hovyo bila kusimamia uwajibikaji na matumizi.

Kukumbatia ufisadi ni udhaifu mkubwa ambao unachefua watu wote wenye akili. Huduma za kijamii hovyo, matozo lukuki, maisha hayaeleweki watu wanaburuzwa buruzwa tu kama wakimbizi yeye kakumbatia wezi na wafanyabiashara wanyonyaji wakwepa kodi. Aisee usitake nikuongeze tusi.
Mi kwa mara ya 1 sijivunii raisi wetu na sijivuniii kuwa mtanzania kwakweli 🤢🤢🤢
 
Back
Top Bottom