RC Adam Malima ashauri Serikali kuwa makini kwenye Mkataba wa DP World, ili tusipigwe kama kwenye Mikataba ya Madini

RC Adam Malima ashauri Serikali kuwa makini kwenye Mkataba wa DP World, ili tusipigwe kama kwenye Mikataba ya Madini

Nimemsikia ila hakuna popote aliposema mkataba wa DPW ni mkataba mbovu!.

Alichosema ni tuwe makini ili tusipigwe, kwasababu huko nyuma, tulipigwa!.

Msimchonganishe Malima na Samia!. Serikali yetu inafanya kazi kwa mtindo wa a collective responsibility, serikali ikiisha sema ndio, Bunge likasema ndio, chama tawala, chama cha Mapinduzi, CCM, kikasema ndio, hawezi tena kuibuka mserikali yeyote akasema sio, huko kutakuwa ni kwenda kinyume cha kanuni ya collective responsibility.

Kwenye kanuni hiyo ya a collective responsibility, ukiamua kutofautiana na uwajibikaji wa pamoja ni unajinyamazia kimya!. Ukijiona huwezi kunyamaza, kwanza ana resigns ndipo unapinga!.

Hivyo mleta mada umepotosha!, usimlishe maneno Adam Malima.

P
mkuu nadhani pia hujamwelewa, mheshimiwa sana Malima kakosoa kwa staha ( in your voice), shida kubwa ya ukosoaji wa kistaha ambao unapendwa sana na (supporters wa DPW), wanaunyumbulisha na kujifanya hawauelewi, ndio maana nawapenda pia wasiotumia staha (against DPW), maana wanaeleweka zaidi maana wako focused na nini.
 
Nimemsikia ila hakuna popote aliposema mkataba wa DPW ni mkataba mbovu!.

Alichosema ni tuwe makini ili tusipigwe, kwasababu huko nyuma, tulipigwa!.

Msimchonganishe Malima na Samia!. Serikali yetu inafanya kazi kwa mtindo wa a collective responsibility, serikali ikiisha sema ndio, Bunge likasema ndio, chama tawala, chama cha Mapinduzi, CCM, kikasema ndio, hawezi tena kuibuka mserikali yeyote akasema sio, huko kutakuwa ni kwenda kinyume cha kanuni ya collective responsibility.

Kwenye kanuni hiyo ya a collective responsibility, ukiamua kutofautiana na uwajibikaji wa pamoja ni unajinyamazia kimya!. Ukijiona huwezi kunyamaza, kwanza ana resigns ndipo unapinga!.

Hivyo mleta mada umepotosha!, usimlishe maneno Adam Malima.

P
Kifupi hofu aliyonayo ndio tulionao wengi, ila sababu ya ugali wake ame balance maneno.
 
Nimemsikia ila hakuna popote aliposema mkataba wa DPW ni mkataba mbovu!.

Alichosema ni tuwe makini ili tusipigwe, kwasababu huko nyuma, tulipigwa!.

Msimchonganishe Malima na Samia!. Serikali yetu inafanya kazi kwa mtindo wa a collective responsibility, serikali ikiisha sema ndio, Bunge likasema ndio, chama tawala, chama cha Mapinduzi, CCM, kikasema ndio, hawezi tena kuibuka mserikali yeyote akasema sio, huko kutakuwa ni kwenda kinyume cha kanuni ya collective responsibility.

Kwenye kanuni hiyo ya a collective responsibility, ukiamua kutofautiana na uwajibikaji wa pamoja ni unajinyamazia kimya!. Ukijiona huwezi kunyamaza, kwanza ana resigns ndipo unapinga!.

Hivyo mleta mada umepotosha!, usimlishe maneno Adam Malima.

P
Vipi Afya yako mkuu nasikia umepata ajali.
 
Mwenyekiti wa CCM mkoa Ruvuma ndugu Oddo K. Mwisho - Maoni ya WaTanzania yazingatiwe ili uwe wa manufaa



Mwenyekiti wa mkoa ndugu Oddo Killini Mwisho pia ni mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa NEC CCM azungumzia maoni mbalimbali kuhusu suala la bandari na ikiwa Mikataba ifuatayo mkataba-mama itarudi bungeni basi jambo sahihi litafanywa kuhusu mikataba ifuatayo ya bandari.. hivyo maoni ya waTanzania yazingatiwe, yaboreshwe na kuwa rafiki kwa Tanzania... waTanzania wasiligeuze suala hili katika sura ya udini na namna hasi ... Watanzania tuendelee kutoa maoni ili mikataba iwe rafiki na ya tija kwa nchi yetu ...
 
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya : Unafiki unatutesa hatuzungumzi hadharani sisi viongozi wa chama na serikali



Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mbeya ndugu Dkt. Stephen Mwakajumilo awalaumu viongozi wa serikali ya CCM kushindwa kujitokeza kusema wazi kweupe badala yake wanaongea kwa vificho vichakani .... ajenda kubwa kama hii inatakiwa kiongozi kusimama katika mstari unaouamini siyo kuwa wa msimamo wa kati kwa kunyamaza kimya kwa uonga kuhusu ajenda ya bandari ... semeni kwa uwazi ili tupate jibu kwa manufaa ya nchi kukosea siyo dhambi ila kurudia kosa ndiyo makosa na historia ni mwalimu mzuri hivyo wananchi wanahaki na ni kheri kurekebishana kwa nia nzuri ...
 
Unaelewa maana yake? Kama kuna makosa yarekebishwe? Ina maana raisi alisaini agreement yenye mapungufu, je alikua hajui?
Nilipokuwa mtoto niliamini baba yangu anaweza kila kitu.
Hata hivyo, baadaye nikapata ufahamu kuwa kuna wengine ikiwa ni pamoja na mimi tunaoweza vitu tofauti na yeye.
Tuwe wakweli na kwa haki, viongozi (hasa wa kisiasa) hutegemea wasaidizi kwa asilimia kubwa.
Wanachotakiwa kufanya, ni kutafuta watu wenye weledi na werevu, watumike katika kufanya mambo sahihi kwa wakati sahihi.
Changamoto iliyopo ni kwamba, siasa zina fitina, upendeleo, kujuana, fadhila na yanayofanana na hayo. Hivyo kupata watu sahihi kwa usaidizi wenye tija na usalama ni shughuli pevu.
Kwa hiyo, viongozi wengi wa kisiasa huogelea kufuata uelekeo wa mawimbi na upepo.
 
..mbona serikali nzima, chama, na chawa wa Mama Samia, wameshupaza shingo, na wanasisitiza kwamba mkataba uko sawa?
Hii ndiyo changamoto ya siasa zetu. Yawezekana pia ni uthibitisho wa umasikini wa fikra.
Maoni na mitazamo tofauti juu ya jambo fulani ni kawaida, ila mwisho wa siku mamlaka halali zitatoa muelekeo.
 
Ni wachache walio serikalini na Mteule kusema wazi wazi kama Adam Malima, wengine wanaofia matumbo yao...
 
Kama umemsikiliza hakusema, ni SAWA maana unathibitisha kuwa HAKUSEMA wala watu wasiweke maneno ambayo hayakusemwa.
Swala la collective responsibility hilo achana nalo. Ccm waseme ndiooo, Bunge la wabunge wa ccm majority liseme ndiooona serkali ya ccm iseme ndioooo, haizuiii mtu mmoja wa ccm ndani ya serkali kusema siooooo, hata kama iwe ni kwa gharama ya maisha yake.
Ikifika sehemu eti kwa kuhofu nafasi yako ndani ya serkali husemi kile unaona ndio sahihi ni UOGA na uoga ni Utumwa,
Uhuru wa Maoni ni haki ya kisheria na kikatiba.
Hapa Mayalla naona amechemka..!!
 
Mama ananiambia sisi hatuna ndugu wa kiarabu
Hilo tatizo kubbwa sana.


Pole sana.

Mimi nna ndugu wa takriban kila taifa dunani. Wahindi, Wachina, Waarabu, Wamarekani, Ulaya, Japa.

Tanzania ndiyo usiseme.
 
Akizungumza katika kipindi cha Good morning Wasafi FM, Malima ambae marehemu baba yake aliwahi pia kuwa waziri wa fedha kipindi cha Nyerere, amesema Kinachopingwa sio ufanisi wa bandari bali ni vipengele vya mkataba, na huko nyuma, 1998 Tanzania iliwahi Ingia mikataba mibovu ya madini, na alipokuwa waziri wa nishati miaka kumi baadae wakaikataa .

Akafafanua zaidi amesema kwamba Waarabu sio wajomba zetu na hivyo muhimu ni kuangalia vifungu vyenye shida virekebishwe kwa maslahi ya taifa na si vinginevyo.


Msikilize mwenyewe 👇

View attachment 2684047
Huyu U-RC wake uko shakani. Sisi tunataka tuwape bandari wajomba zetu, waarabu wa dpw , yeye anatoa ushauri feki
 
Akizungumza katika kipindi cha Good morning Wasafi FM, Malima ambae marehemu baba yake aliwahi pia kuwa waziri wa fedha kipindi cha Nyerere, amesema Kinachopingwa sio ufanisi wa bandari bali ni vipengele vya mkataba, na huko nyuma, 1998 Tanzania iliwahi Ingia mikataba mibovu ya madini, na alipokuwa waziri wa nishati miaka kumi baadae wakaikataa .

Akafafanua zaidi amesema kwamba Waarabu sio wajomba zetu na hivyo muhimu ni kuangalia vifungu vyenye shida virekebishwe kwa maslahi ya taifa na si vinginevyo.


Msikilize mwenyewe 👇

View attachment 2684047
2025 inakuja na umri nao unapenda, mengine jiongeze mwenyewe .
 
Back
Top Bottom