Shambulizi la Lissu: Wanaomdhania dereva anahusika sio wajinga, Wana hoja za msingi. Je, anahusika?

Asante sana Pasco Mayalla.
 
Huna hoja ya msingi
 
Leo umekurupuka na umechemka mkuu Pascal Mayalla , umeuliza maswali ambayo Lissu anayahoji...na sasa kwa andiko lako hili uchwara:
  1. Unataka kusema dereva wa Lissu ndo aliyeondoa ulinzi wote wa Site 3 Area D usiwepo siku hiyo kwa kuwa kulikuwa na kazi alikusudia kuifanya
  2. Unataka kusema dereva wa Lissu ndiye aliyeng'oa CCTV Camera kwenye nyumba walimokuwa wakiishi?
  3. Unataka kusema dereva wa Lissu ndiye aliyezuia Bunge lisimtibu Lissu
  4. Unataka kutuaminisha kuwa dereva wa Lissu ndiye ambaye hadi sasa amewazuia polisi kuchunguza jaribio la kumwua Lissu?
  5. Unataka kutuaminisha kuwa dereva wa Lissu ndiye aliyewakataza wabunge wa CCM wasifike Nairobi kumjulia hali mbunge mwenzao?
Kaka Pascal Mayalla, nakuita tena....Ifike mahali tupendane na tuache ushabiki wa kijinga na kujifanya wajuwaji kwenye mambo ambayo wazi mnajua yanawakwaza watu wengi kuliko nguvu ya polisi mnayoitumia kumlinda kiongozi mhalifu.... Lissu amekwambia wakati flan kama wewe ni mtu mwenye akili timamu huhitaji ushahidi ama uchunguzi wa polisi kwa sababu "Jua lenyewe linaliangaza vema tukio lile la mauaji dhidi yake"

Wakati mwingine haya makelele yenu wala hayatusaidii, Mungu mwenyewe atampigania Lissu, na hata sasa amempigania, lakini bado hamwelewi tu....na mhusika wa mpango wa mauaji wenyewe mnamshuhudia anavyoropoka...Mara ajiite Jiwe, mara ajiite Mshenzi Zaidi, Mara ajiite Kichaa...ipo siku ataropoka kuwa ni kweli alijaribu kumwua Lissu, na mtarudi hapa kutaka kufuta nyuzi zenu za kumtetea
 
Kamanda kwahiyo anajidhalikisha kwakuwa kaongea ambayo hupendi kuyasikia?
 
Namba Tisa imefanya nikudharau,
Labda umepoteza umakini sababu umeandika meeeengi,nadhani ukirudia utagundua kitu,
Lkn una hakika hawakuyafanya unayosema?,
Kuhusu dereva km unadhani anahusika alishindwaje kummalizia lisu baada ya kuona hajafa na badala yake akawa wa kwanza kutoa taarifa kwa MBOWE,siyo polic
 
Sidhani kama serikali yetu ina mpango wa kumjua mfyatuaji wa risasi kwa lissu kwani mpango ungekuwa ni huo evidence zipo nyingi bila hata kumhoji Lissu na dereva wake.

Ni kweli usaliti huwa upo but Mayalla usiikimbie hoja ya msingi kwani kufanya hivyo ni kutupotezea muda kujadili au kuitafuta thamani ya kitu ambayo iko wazi. Waliojaribu kufanya umafia ule walipungukiwa ujuzi mwingi mno au MUNGU wetu ELSHAADAI alisimama and not otherwise.
Usituhamishe relini Mayalla kwa post za mkwepo kama hizo simama kwenye uhalisia. Tujadili mengine ya kuumiza vichwa siyo hili. Ndiyo maana wengi wanadai toka uitwe na ile kamati post zako zimeanza kuwa na makengeza. Unaelekea kuwapongeza waovu na uovu wao kwa style ya kutuhamisha kwenye reli tuamini kuwa siyo serikali hii iliyoshiriki shambulio lile bali ni Dereva wa Lissu.

I stand to be corrected but really you are not normally normal.
 
Kaka mayala naona una umma na kupuliza ebu jipambanue ranging yako andiko uliloandika leo si kwa hadhi yako, nimekufananisha na paramagamba au kitila mkumbo wa leo ambao wanapindisha ukweli ajili ya matumbo yao

Yani baada uhoji serikali imefikia wapi kuhuse uchunguzi wa shambulio la mh tundu lisu ikiwa leo ni mwaka mmoja tangu ashambuliwe

Ajabu tunakuja na hoja dhaifu eti dereva wa lisu
 
Dah huyu jamaa mnaemwita Paskali nashindwa kuelewa credit watu wanazompaga huwa wamedhamiria au huwa wanajikuta tu wamempa bila kujua wamempaje.

Mkuu kwa awamu hii hakika kazana tu na upaze sauti zaidi nafasi haziishi utapata,wachumia tumbo msimu wenu wa neema.Hongereni
Bandiko la hovyo kabisa.
 
Hahaha hivi aliye andika ni huyuhuyu Pascal ninaye mfahamu humu jukwaani?mbona kaandika pumba hata kijana wa Form1 anaweza kujibu na tena asingeweza kuuliza huu uharooo humu.
1.Kwanza tambua wao kufuatwa fuatwa haikuwa Mara yakwanza.Hawakuonyesha kustuka kihivyo,mana kwa mujibu wao haikuwa Mara ya kwanza kufuatwa hivyo na hiyo gari.
2.Pili hatua waliyo chukua ilikuwa nisalama zaidi kama ingekuwa mazingira yapo ktk hali yake ya kila siku.Nikimaanisha waliona mahali salama ni ktk makazi yao ambayo yanalindwa na askari wa serekalini samaa24 na nindani ya uzio.Kwahiyo kwa mawazo yao ulinzi ungelikuwepo .Lakini lakustaajabisha walinzi nao labda walishirikiana na Dereva,sindio!!!!?
3.Lamwisho japo yapo mengi yakukosoa nikuhusu upelelezi kutoka nje ya nchi.Kumbuka hilijambo limetia DOA serekali na vyombo vya Usalama.Mpaka Leo sijajua kama kweli serekali imeshindwa kupeleleza na kama ndio,kigugumizi cha wapelelezi wa nje kinatoka wapi?
 
Yeah! Haya nayo ni maoni tu yenye lengo la kuchangamsha fikra za wasomaji kuhusiana na shambulio dhidi ya TAML; Ni hoja nzuri tu. Hata hivyo, kama lengo ni kuuaminisha umma dereva wake anahusika au aweza kuwa mmoja was "wasiojulikana", basi tuwaachie tu wasomaji wenyewe waamue na tayari tumesoma na kuona wanasemaje!
 

Dereva hakuumia kwanini walimkimbiza Nairobi, Serekali haiendi nchi nyingine kiholela, Dreva kapelkwa Ubelgiji , yote hiyo mko sawa tuu? Mtasema anamsaidia lissu, hiyo ni kazi ya Hospitali, Nairobi Hospital is one of the best in EAst Africa, ninaojua vizuri sana, kuna wagonjwa kweye coma NA wanahudumiwa NA Nurses .

Wana Chadema hampendi kuulizwa maswali , mnapenda watu wale YES man kwenu ama kwa jambo lenu lolote.

Pascal ameuliza very valid questions NA yanahitaji majibu yeye busara, NA LISSU AKISHINDWA KUYAJIBU HAYA VIZURI NA BILA JAZBA ZAKE, BASI ATAKUWA GUILTYBIN CONSIPARANCY NA WALE WALIOMTEDEA MABAYA, kwani anazui ukweli usitoke NA kuitumia hali yake kisiasa.

Which is very cheap and crocked politics
 
Kwahiyo Lisu anajua Dereva kahusika na bado anamsitiri?Hii ndio maana yako?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…