Siku Dkt. Bashiru, Prof. Kabudi au Balozi Polepole wakisimama dhidi ya CCM nitaogopa sana lakini Lissu, Lema na Mbowe hawana maajabu

Yaani nimekudharau sana, yaani wewe ni zwazwa tu kama hao unaowataja, yaani nikae namsikiliza Polepole huyu ambae ananiambia sijui utamu wa kupanda V8! Au Kabudi aliyekuwa anamwita Magufuli "mheshimiwa mungu"!🚮🚮💩
 
Kabudi na Bashiru wasitoke, wapambane wakiwa ndani ndo Pana support kubwa kuliko nje.

Wahuni watoke CCM Ili Imani irudi Kwa wananchi.
Kuna watu wajinga sana hii nchi! hivi kuna wahuni zaidi ya hao watu waliotajwa na huyo mleta mada? Nakumbuka hao watu 2013-2015 walikuwa wapinzani wakubwa wa CCM na mifumo yake yote, then akaja Magu sababu ya uoga wake wa kukosolewa akawapa vyeo, wakapiga bonge la UTURN!!! Mmojawapo hapo alikuwa anapinga cheo cha UKUU WA WILAYA, Alipoteuliwa hicho cheo alikipokea kwa mikono miwili!! Hamtokuja kupewa nafasi nyingine kamwe kuiongoza hii nchi, kosa la 2015 halitorudiwa tena, tunaenda na Mama hadi 2030, baada ya hapo tutajua nani atakuwa rais, ila siyo nyinyi wahuni
 
[emoji23]Ni mtazamo wake... yaani mimi kabisa nikae chini niwaamini watu (hovyo) aliowataja wanishawishi kwa hoja? Kundi la watu walio wafu kisiasa na wasio aminika?

Wewe ndio upo hai? Mbona na wewe mfu kisiasa.
 
Ndani ya CCM, hakuna mwanasiasa aliye na nguvu ya kushawishi watu. Kilicho na nguvu ndani ya siasa za nchi hii ni Rais ambaye yupo madarakani. Yeye ndiye huamua nani atangazwe kuwa Rais, nani awe mbunge. Fikiria wagombea asilimia 75% wa CCM hawakupitishwa na wajumbe kuwa wagombea wa ubunge kupitia CCM, lakini Magufuli aliamua wawe wagombea wa CCM na wawe wabunge. Wanachi waliwachagua wagombea wengi wa ungunge toka upinzani, lakini jwa kauli moja ua Magufuli, ushindi wao wote ukafutwa wakatangazwa aluowataka yeye.

Fikiria Kikwete alichofanya 2015. Mshindi kwenye kura za Urais alikuwa Lowasa,na Zanzibar alikuwa Maalimu Seif. Kikwete alipoona dalili zote za Magufuli kushindwa, akatuma watu kwenda kusambaratisha mpaka kituo cha kuhesabia kura za Lowasa, na waliokuwa wanapokea matokeo kuwakamata na kuwasweka ndani. Halafu akaamuru Magufuli na Dr Sheni watangazwe washindi, na hakuna aliyefanya kitu.

Rais kwa kutumia polisi, akitaka hata wewe uwe Rais, utakuwa. Hakuna mwanasiasa hata mmoja, hata apendwe kiasi gani, hata apate kura 80% ya kura zote, atakuwa Rais bila ya Rais aliyepo madarakani kutaka.

Tanzania hatuna uchaguzi, si wananchi wanaomchagua kiongozi bali kikundi kidogo ndani ya CCM ndicho kinachoamua nani awe nani.
 
Hawana chochote hao kazi yao kubwa ilikuwa kununua wapinzani na kuharibu demokrasia na chaguzi.hao wanawekwa kundi moja na wafuasi wa NAZI ambao bado wanaishi wanaweza wakasema nao walikuwa wanashinikizwa ila hawajawahi kuonyesha thamani ya uongozi wao hata kidogo.MAMBO YOTE YA HOVYO YALIYO TOKEA KIPINDI CHAO WAO NDIYO WALIKUWQ WATENDAJI
WAkUU..
 
Wale wakishika maiki lazima ukae kitako kuwasikiliza.

Sio sasa hivi. Walishakula matapishi yao. Kitendo cha kabudi kutetea kupotea kwa Azory gwanda, na Bashiru kutetea matumizi ya dola kubaki madarakani na Polepole kutetea wizi wa Trilioni 1.5 na kuanza kupiga mahesabu kwenye TV, kumewaondoa kwenye viongozi waadilifu.
 
Hao pamoja na wengine wengi wanaungana ndani ya chama kuimarisha chama na kujenga serikali yenye nguvu.

Hawawezi fanana na walioamua kuwa wakimbizi na kwenda kuishi ughaibuni huku wakitaka madaraka Tanzania

Chama chetu Cha Mapinduzi chajenga nchi

Kweli chajenga nchi kwa deni kuongezeka mpaka trilioni 92
 
Unapotaja jina CCM,Kwanza kiuhalisia unakua umeshawaboa raia wengi.itoshe tu kusema MUNGU asante kwa hali ya sasa kisiasa.

Ingependeza ukaambatanisha na kadi yako ya uanachama wa CCM ili upate teuzi kabisa.
 
Upinzani unahitaji watu wenye kariba ya hao niliowataja usonge mbele ,kizazi Cha lema ,lissu na Mbowe kinaurudisha nyuma sana upinzani

Kama haujui, Kabudi alikuwa NCCR na Bashiru CUF, sijui polepole. Magufuli aliwachukua ili kucontain critical minds hasa katiba mpya.
 
Bashiru kwenye mkutano mkuu alikuwa mtu wa kukubali kila kitu na alikuwa dhaifu sana.
Watu wazima huwa hawafanyi vitu kitoto kama unavyowaza wewe. Kipindi issue ya trillion 1.5 ipo hot ,Prof.Assad aliulizwa na Rais kama kweli hazionekani akajibu sio kweli mzee. Je, hapo hakula matapishi yake mwenyewe?

Mtu kama Bashiru, the best political strategist the country has ever had ni mtu anayetumia akili kubwa sana
 
Hakika umesema kweli. Hao ni wa
namapinduzi wa kijamaa wa kweli. Wanabeba fikra na itikadi halisia ya ccm. Itakadi yenye kulinda na kutetea umma wa wananchi. Itikadi inayodai haki na usawa kwenye uchumi.

Na hao sio CCM, Kabudi NCCR na Bashiru CUF.
 
Ndio maana nasema upinzani hauna watu wenye kutazama mbali na wenye kuvumilia hoja. Lazima mtu aelekee upepo unapovuma ili aendelee kusurvive kisiasa.

Mtu kama lukuvi yupo mpaka leo kutakana na kubadilika kutokana na Mazingira
 

Alikula matapishi, hadi makamba anasema wazuri hawafi na yeye anakubali na kupiga makofi.?

Hivi Bashiru ana steategies gani? Za kuzuia mikutano na kuzima internet siku ya kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu, au strategies za kuengua wagombea wa upinzani.

Uchaguzi ungekuwa clean na wakashinda kwa haki hapo ningefikiria kidogo.
 
Hao ndio masalia ya Nyerere chamani,

Nyerere hakuanzisha chama Ili viongozi walambe asali wakati wananchi wanaramba shubiri.

Wavamizi ndani ya chama ndo wafurushwe, hivyo sioni sababu ya Polepole na kabudi Kutoka ndani ya CCM!!!

Tafuta kwanza kujua chama cha kabudi, Bashiru. Pole pole kabla ya chadema kumchukua Lowassa alikuwa anawasupport chadema.
 

Magufuli ndio alitengeneza matabaka CCM. Usikatae.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…