Suala la Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Vipengele kadhaa vya Kisheria

Ukielewa neno ”Eligible" tu, utajua kwamba hakuna sehemu ya katiba iliyo vunjwa! Hapa maana yake CAG antaserve kwa miaka mitano na anaweza akaongezewa au mitano hiyo hiyo.
Je kama aliteuliwa akiwa na miakatuseme 57? Akitumika kwa miaka 3 akafikisha 60 anaweza akastaafu. Na kwa shera ya bunge 65 years.
 
Mkuu soma historia ya Ma CAG waliopita, hakuna miaka kumi tu? Kwa mfano aliyepita ameongoza muda gani? Vipi yule Wa kwanza.pia kuna umri Wa kustaafu kuanzia miaka 60, kumbuka Assad ana miaka 58.Hawezi staafu maana bado umri huo...Wa kustaafu.
Soma maelezo uelewe, shida tunatumia hisia kujudge ndo shida yetu, wewe umepewa maelezo ya kwanini kaondolewa bado unalazimisha kusoma historia ?

Umeambiwa mamlaka ya uteuzi ndio inayoamua kama aendelee au la sasa umejuaje hao waliomtangulia kama waliona wanafaa kuendelea na madaraka hayo?

Just a simple logic, tatizo tunalazimisha kujiaminisha tunajua kumbe hamna!

Pia unapofanya mijadala kama hii hasa ya kisheria ukumbuke Urais ni taasisi ,kwahiyo kuna wanasheria nguli na washauri ikiwemo hata wazee wa heshima ,sasa watu tunafikia mahali tunajiona kwamba tunajua kuzidi taasisi ya Urais
 
Shall be eligible doesn’t mean shall be reappointed.

Sijui tatizo ni lugha..????
The problem umetumia general English use kwenye masuala ya kisheria!

Katiba yetu Ibara ya 144 (1) inasema wazi kwamba:-
Controller and Auditor-General of the United Republic shall be obliged to vacate office upon attaining the age of sixty or any other age which shall be prescribed by a law enacted by Parliament.
kwamba ATALAZIMIKA kuachia office akishafikisha miaka 60! Je, Profesa Assad aliyezaliwa Oktoba 6, 1961 ameshafikisha miaka 60?!

Na hiyo phrase yako uliyotumia, kutoka Public Audit Act 2008 Ibara ya 6 (1) inasema:-
The Controller and Auditor-General shall hold office for the fixed term of five years and shall be eligible for renewal for one term only.
Hilo neno SHALL umelitafsiri kwa Kiingereza na sio kwa lugha ya kisheria!!

Pasipo na shuruti, katiba na sheria zetu zinatumia neno MAY na sio SHALL kama inavyoelezwa kwenye Interpretation of Laws Act Ibara ya 53 (1&2) kwamba:- Sasa kwa kuangalia tarehe ya kuzaliwa ya Prof Assad, ni kwamba atatimiza miaka 60 Oktoba 6, 2021!

Je, hawezi kuongezewa miaka mingine 5 kwa sababu hadi miaka 5 kwisha atakuwa amevuka miaka 60?! Jibu ni kwamba, katiba imesema wazi kwamba:- "upon attaining the age of sixty or any other age which shall be prescribed by a law enacted by Parliament."

Je, Bunge limetunga sheria yoyote kuhusu hiyo ANY OTHER AGE?!

Jibu ni NDIYO, 2008 Public Audit Act Ibara ya 6(2)(a) inasema:-
Unless the question of removal becomes the subject of investigation in terms of Article 144(3) of the Constitution, the Controller and Auditor-General shall vacate office upon attaining the age of sixty five years;

Summing up, unless kama CAG kafanya jambo la litakalosababisha kuwa under investigation, he shall be eligible for renewal. Na mkataba wake ukiwa renewed, atamaliza miaka 5 mingine mwaka 2024 ambapo atakuwa na umri wa miaka 63!

So, unless kama wameshamtengenezea kesi, jambo ambalo kwa utawala huu hakuna kinachoshindikana, kinyume chake, Rais amevunja sio tu katiba bali pia Sheria ya Ukaguzi wa Hesabu za Umma ya mwaka 2008!
 
Mimi sijui chochote kile,ila nilitaka kufahamu kutoka kwako kama taasisi ya urais inajua kila kitu na haiwezi kukosea,na hakuna taasisi zingine zozote ambazo zinajua zaidi?
 
Huwezi kuelewa mantiki, we endelea kuabudu tu
Nyuzi kama hizi zinaonyesha mlivyo empte.
Mfano hai ibara ya 40 ya katiba ya 1977 ya JMT. Inafanana kabisa na lugha hii ya SHALL BE ELIGIBLE. Soma katiba zote za kiswahili na kizungu upate tafsiri sahihi ya SHALL BE ELIGIBLE. hii ya ibara ya 40 ni ya rais, na mnajua kabisa kwa rais term ya pili anaweza chaguliwa au laa ila ya CAG mnalazimisha ni lazima aendelee eti katiba inasema....
Haihitaji rocket science hapa, assad muda umeisha na hajawa renewed.
 
Kuna watu mmeishia kuzungumzia tu uhalali wa kuenguliwa kwa Assad Ila hili la kuteuliwa mtu ambaye huyo huyo mteuzi alishasema hafai kabisa hamlioni?!?
Mteuzi anafanya kazi ya kumtetea kuwa ngumu sana yani
 
Mimi sijui chochote kile,ila nilitaka kufahamu kutoka kwako kama taasisi ya urais inajua kila kitu na haiwezi kukosea,na hakuna taasisi zingine zozote ambazo zinajua zaidi?
Huwa sipendi kumjibu mpumbavu sawa sawa na upumbavu wake!

Ahsante!
 
Huyo ndiye atamsaidia kutafuna rasilimali za nchi vizuri sana.
Kuna watu mmeishia kuzungumzia tu uhalali wa kuenguliwa kwa Assad Ila hili la kuteuliwa mtu ambaye huyo huyo mteuzi alishasema hafai kabisa hamlioni?!?
Mteuzi anafanya kazi ya kumtetea kuwa ngumu sana yani
 
Tatizo Raisi amefanya haya kwa Mihemko, Kudanganywa na Kujidanganga, Kushauriwa vibaya na Kujishauri vibaya na On top of that Kwa CHUKI binafsi.

Raisi amevunja Katiba ALIYOAPA kuilinda huku akimtaja MUNGU anayedai kumtanguliza mbele'
 
Man, umesoma thread hadi mwisho?! Hiyo "shall" hatuitafsiri sisi bali inatafsriwa na Interpretation of Laws Act Ibara ya 53 (1&2) Kwamba:-
Pale pasipo na SHURUTI, hutumika neno MAY na sio SHALL!!

Fuatilia hata Sheria za US... hata wao hilo neno SHALL iliwabidi wali-replace na MUST kwenye sheria zao kwa sababu wakati kwenye law schools SHALL inafundishwa kwamba ni SHURUTI, kwenye general use of English SHALL sio SHURUTI, na matokeo yake ikawa inaleta mkanganyo!!
 


Hawa jamaa hawana logic wanaendeshwa na emotions, swali zuri hilo, kama ni automatic kwa nini waweke hiyo miaka 5 na wasiseme 10?
 
Man, umesoma thread hadi mwisho?! Hiyo "shall" hatuitafsiri sisi bali inatafsriwa na Interpretation of Laws Act Ibara ya 53 (1&2) Kwamba:-
Kwani nimekataa maana ya shall?

Nimeeleza maana ya shall kabla hujapost thread hii.

Unaelewa objection yangu iko wapi?
 
Mkuu Akishauri Ni Amri Bwana Mwenyekiti Huelewi!!!
 
Kwani nimekataa maana ya shall?

Nimeeleza maana ya shall kabla hujapost thread hii.

Unaelewa objection yangu iko wapi?
Umeeleza maana ya "shall" kwa mujibu wa nini?! Mimi nimeeleza kwa mujibu wa sheria zetu, na nimeweka kifungu! Kwamba kwanini haikutaja miaka 10, kwa sababu suala ukishaweka neno renewable tu, tafsiri yake hiyo contract inaenda kwa terms!
 
Kwa utaratibu huu tusishangae jaji mkuu akitumbuliwa pale mahakama yake itakopoenda kinyume na matarajio yake. Kama kweli anavunja katiba inayompa mamlaka makubwa ya kupiga mpk shangazi wa waziri mkuu alafu aeheshimu ?Hãta vyombo vya ulinzi vinamtii kwa sabab ya katiba sio kwamba yeye ni bondia. Washauri wamshauri umuhim wa kuheshimu katiba what if akaja Rais mwingne akamkamata pmj na katiba kuzuia?Ķuvunja katiba ya nchi a sichukulie kirahisi itakuja kumrudia so far hii ni sign ya dictatorship
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…