Team “Kataa ndoa” wapuuzwe, hawana maadili, ndoa iheshimiwe na watu wote

Team “Kataa ndoa” wapuuzwe, hawana maadili, ndoa iheshimiwe na watu wote

Siwezi kuja kuoa kwa ninayoyaona kwenye ndoa za sasa.

Familia nitakuwa nayo.
Watoto nitakuwa nao
Ila ndoa itanisamehe.

KATAA NDOA
Familia utaipataje bila mke?
 
Ndugu mleta mada kabla hujaleta makasiriko hapa ulitakiwa kutulia kwanza uandike fact zinazoeleweka
1. Uongozi bila mke. papa anaongoza maelfu ya wakatoliki na hajawahi kuoa hivyo hoja yako hii haina mashiko
2. Familia. Sisi KATAA NDOA hatukatai familia ila hatutaki kukaa kifungoni na mtu( mwanamke) kwa kivuli cha NDOA. na wengine familia tunazo ila wake hatuna
Kufunga ndoa na mtu ni kukubali kujinyima raha wewe ili mwenzako afurahi ujinga mtupu.
KATAA NDOA, NI UTAPELI NA ULAGHAI, ISHI KWA FURAHA BILA KUFUNGAMANA NA YEYOTE
una housegirl na watoto unaita familia bila mother house? 😂
 
Kumlazimisha MTU kuoa ni kuingilia uhuru wa MTU.


Mimi ntaoa nikifika 35 years
Sababu zangu za kuoa

Nikuweka bond ya watoto na wazazi wao

Japokuwa kuna mambo negative ktk ndoa Ila Mimi ntatafuta mazuri machache ndo ntayamulika .
 
kinachokataliwa ni ndoa tu ila wewe hata ukiweza kuwa na wanawake 10 kuwa na tu sio tatizo.

Mnatakiwa mjue kutofautisha iyo mifumo miwili. Kataa ndoa na kataa ngono ni vitu viwili tofauti kabisa


Wanatumia hoja dhaifu za kusema kataa ndoa ni
Mashoga
Hawana nguvu za kiume
N.k

Hizi hoja dhaifu haziwezi kumfanya MTU aoe.

Ukitaka umfanye MTU aoe mwambie mambo mazuri yanayopatikana katika ndoa na umuhimu wake .
 
wengi kwenye ndoa wamejiegesha tu , sababu ya kuheshimisha jamii, wazazi, ndugu,kanisa, lakin mifumo na haki zote za ndoa wanazipata barabaran/nje.

sijasema msioane,nyie oaneni tu,,mbwaimbwai.
 
Wanatumia hoja dhaifu za kusema kataa ndoa ni
Mashoga
Hawana nguvu za kiume
N.k

Hizi hoja dhaifu haziwezi kumfanya MTU aoe.

Ukitaka umfanye MTU aoe mwambie mambo mazuri yanayopatikana katika ndoa na umuhimu wake .
Kabisa, inatumika nguvu kubwa sana kutulazimisha kuoa ila wao hawataki kuukubali ukweli kuwa mfumo wa ndoa ni mfumo kandamizi kwa mwanaume.
 
Kabisa, inatumika nguvu kubwa sana kutulazimisha kuoa ila wao hawataki kuukubali ukweli kuwa mfumo wa ndoa ni mfumo kandamizi kwa mwanaume.



Kweli nimekuwa nikifatilia hoja zao naona hazina uzito

Kuoa ni muhimu Ila hauwezi kumwambia MTU ambaye hajaoa kuwa Ana tatizo la nguvu za kiume au shoga n.k


Ningefurahia Kama angetokea MTU akachambua kwanini vijana au watu waoe na wakioa watapata nini !


Mfano ukimwambia mtoto wako Kuwa ukisoma utakuwa tajiri utapata pesa nyingi na kuishi maisha mazuri -lazima huyu mtoto ataanza kupenda shule.

Ila ukimwambia mtoto usiposoma utakuwa masikini , utakosa hela maisha yako yatakuwa magumu - lazima huyu mtoto atakupuuza na hazozitangatia masomo.


So Kama ndoa ni kitu bora lazima MTU aseme tukioa tutapata nini na sio kumuita MTU ambaye hajaoa shoga au Hana nguvu.
 
Kwahiyo unataka tuanze kukufundisha types of family??

Tofautisha FAMILIA na NDOA
Nimeuliza swali hilo kwa makusudi, kabla hatujafika huko tutumie familia yenu Kama case study maana waswahili wanasema mtoto wa nyoka ni nyoka!
Baba yako na mama yako wanakaa/walikaa pamoja au umelelewa na singo maza?
 
Back
Top Bottom