Tetesi: TEC haifurahishwi na mwenendo wa Serikali kuhusu makubaliano ya bandari na DP World

Tetesi: TEC haifurahishwi na mwenendo wa Serikali kuhusu makubaliano ya bandari na DP World

Nadhani umekosa kitu Fulani kwenye uelewa wako.Kwanza mleta mada hajataja source ya habari.Hivyo ni mambo ya hisia au tetesi.Iweje utukane?.Pili hata wakisema si watakua wameungana na watanzania wengine wanaopinga au kuunga mkono huu mchakatoSikia hoja ndio udadisi hoja yenyewe.Vinginenyo turudi enzi za JPM ambapo kuhoji ilikuwa kosa.
Bwana we nendeni mkasupport ushoga huko
 
Ndio maana kuna Bunge wabunge wakikubali nchi imekubali watu kama nyie kipindi cha kampeni hamsikilizagi sera mnaletaga ligi oooh mbele kwa mbele yakiwafika shingoni mnatuletea zozo tumewachoka
Wabunge wepi hao! Hawa wezi wa kura na waliopewa ubunge wa bure kwa maelezo ya kupita bila kupingwa.😳
 
Duru ndani ya TEC hawafurahishwi na namna Serikali ilivyokubaliana na DP Word kuhusu usimamizi wa bandari yetu/zetu.
Kwani katika uendeshaji wa nchi, hawa TEC ndio nani?. Tusichanganye dini na siasa, Maaskofu waendelee kuwahubiria watu habari Njema za ufalme wa Mungu ili kuwapeleka waumimi wao mbinguni. Bwana Yesu alituhimiza tumpe Mungu yaliyo ya Kimungu na Kaisari yaliyo ya Kaizari.
hata Baba Askofu wake ameshangazwa na makubaliano yale tena akiyaita ya AJABU NA YANAYOWEZA KUKUBALIKA KWA WATU WAJINGA!"
Huu ni uchonganishi!, hupaswi kiandika kila unachosikia!, tanguliza kwanza maslahi ya taifa!, Baba Askofu gani anawaita wale waheshimiwa wetu wajinga?. Hajui kwamba kukubali kule ni maelekezo?. Hii inamaanisha huyo Baba Askofu anamuita hata nanilii ni mjinga?, kwasababu mtu wa kwanza kumkubali Mwarabu wa Dubai ni yeye!.
P
 
TEC mnatupa moyo sana sisi wanyonge. Waraka utoke tu sasa kwa hawa watawala madhalim..
 
Kwani katika uendeshaji wa nchi, hawa TEC ndio nani?. Tusichanganye dini na siasa, Maaskofu waendelee kuwahibiria watu habari Njema za kuwapeleka mbinguni.

Huu ni uchonganishi!, hupaswi kiandika kila unachosikia!, tanguliza kwanza maslahi ya taifa!.
P
Kwani kwenye uendeshaji wa nchi wewe ni nani?
 
Duru ndani ya TEC hawafurahishwi na namna Serikali ilivyokubaliana na DP Word kuhusu usimamizi wa bandari yetu/zetu.

"....Wahashamu wengi hawaungi mkono sintofahamu hiyo na huenda Katibu akaelekezwa aandae Waraka mahsusi kulisemea hilo hivi karibu."

"....nadhani baadhi ya vipengere ndani ya makubaliano yake hata wao yamewaogofya kama ilivyo kwa Watanzania wengi! Na ndiyo maana wao kulitolea tamko hilo jambo ni suala la wakati tu."

"....Mhashamu Rais nadhani bado anapitia madodoso ya safari iliyopita kule Vatican lakini kwa mjibu wa Mkurugenzi wa Miito Padre ( jina kapuni) amealikwa kesho yaani leo kwenye mkutano uhusuo mkataba ule. Nimeongea na Padre ..... hata Baba Askofu wake ameshangazwa na makubaliano yale tena akiyaita ya AJABU NA YANAYOWEZA KUKUBALIKA KWA WATU WAJINGA!"
Hatujawahi kuwa na baraza la kuropoka kabla ya waraka! Utakuwa una kiherehere wewe! Muumini mpuuzi wewe! Au ulitaka ututangazie kwamba unafahamiana na Padre?
 
Kaka ukiacha shekhe ponda na yule padri wa ngara wengine wote waliufyata kipindi kile tuwe wakweli na makanisani akienda kusali wanampa na nafasi atoe hotuba, hawakuwahi kuhoji wala hata hii mikataba haikuwa wazi, yeye ndio alikuwa muamuzi wa mwisho na wote tulibakia kisifia au kukaa kimya
Boganza[emoji2935]
 
Wasilamu walimkana shekhe ponda mchana kweupe hewa kabisa
.
20230324_092143.jpg
 
Duru ndani ya TEC hawafurahishwi na namna Serikali ilivyokubaliana na DP Word kuhusu usimamizi wa bandari yetu/zetu.

"....Wahashamu wengi hawaungi mkono sintofahamu hiyo na huenda Katibu akaelekezwa aandae Waraka mahsusi kulisemea hilo hivi karibu."

"....nadhani baadhi ya vipengere ndani ya makubaliano yake hata wao yamewaogofya kama ilivyo kwa Watanzania wengi! Na ndiyo maana wao kulitolea tamko hilo jambo ni suala la wakati tu."

"....Mhashamu Rais nadhani bado anapitia madodoso ya safari iliyopita kule Vatican lakini kwa mjibu wa Mkurugenzi wa Miito Padre ( jina kapuni) amealikwa kesho yaani leo kwenye mkutano uhusuo mkataba ule. Nimeongea na Padre ..... hata Baba Askofu wake ameshangazwa na makubaliano yale tena akiyaita ya AJABU NA YANAYOWEZA KUKUBALIKA KWA WATU WAJINGA!"
Waache unafiki!

Kwanini wasidai katiba mpya ili owe rahisi kumwajibisha Rais!!?

Wake kwa kutulia acha nchi iserereke mbele kwa mbele hadi Bandarini!!
 
Wao ni wataalamu wa uendeshaji wa bandari na sheria ?
 
Back
Top Bottom