Tukio la Bwana Hamza kuwapiga polisi risasi ni matokeo ya mfumo wa utoaji haki kuoza

Tukio la Bwana Hamza kuwapiga polisi risasi ni matokeo ya mfumo wa utoaji haki kuoza

"amedhurumiwa dhahabu zake na polisi"... hapa tuwe makini kidogo, dhahabu zilifikaje kwenye mikono ya polisi ilihali kuna masoko ya dhahabu na taratibu zake kama leseni ( brokers licence) na ulipaji wa kodi nk.... hivi ni huyu tu anayefanya biashara ya dhahabu Tanzania?.... migodi ya dhahabu tunaambiwa iko chunya, chunya pale na Mbeya kuna masoko ya serikali, ilifikaje Dar es salaam hiyo dhahabu? mbona hakudhurumiwa na polisi Chunya, Mbeya, Iringa, Moro ila imetokea Dar es salaam?...

sitetei polisi wala huyu jamaa, najaribu kuwa na fikra huru kuliko kurusha lawama...
Kwani ishu ya zombe ilifkiaje mpk polisi wakawapiga wale wauza madini risasi Z kichwa??? Na wakayapora
 
katika hili kuna jambo moja la kuchunguza sana.....jamaa yuko very trained kutumia silaha....kuna clip ile alimpiga askari mguuni....AK 47 kwa mkono mmoja na alikuwa analenga vema........amejifunzia wapi.....kuna suala la kujiffunza kutumia silaha na kuna suala la ujasiri.....tuwaachie polisi kwanza...tusihalalishe dhuluma wala ugaidi.....tusubiri yajayo
 
Mbona Mbowe ameshitakiwa kwa kesi ya ugaidi?
Hata huyu angekuwa mpinzani angekuwa gaidi si ndivyo wanaccm
Tokea mwanzo wa taarifa ya tukio hili akili yangu ilikataa kabisa kulihusisha na ugaidi.
Sijui itakavyo kua katika uchunguzi wa polisi, lakini kama ilivyo sema mleta mada msamiati wa haki hapa nchni kwetu umeoza, kuanzia huko serikalini na vyombo vyao vya dola mpaka kwenye dini na hatimae kwa jamii nzima.
 
Stori kwamba huyu jamaa alidhulumiwa ni stupid kabisa.

Kama alizulumiwa, kaua polisi 2 pale mataa, si angerudi tu nyuma kidogo kuna kituo cha polisi Salenda angeenda kuwakuta wengi tu, alikua anafuata nini ubalozi wa ufaransa?

Kama alikua anataka polisi walikuwepo pale stanbic bank, nyuma kidogo ubalozi wa urusi wamejaa, nyuma yake kisogo salenda polisi post, ubalozini alikua anafuata nini?

Ni watu kutaka ku twist hii habari ila ukweli ni kwamba huyu jamaa ni gaidi, ni mfia dini na sasa hivi yuko na mabikra 72 wanamzunguma wanamshika shida anawapiga mashine non stop kama dini inavyosema.
We jamaa ni polisi mwizi
 
Hii family wako poa sana. Kaka yao mkubwa anaitwa mahmood ni mtu poa. Nasikia kweli jamaa ni kweli alidhulumiwa na polisi. Ila kidogo ni mvutaji wa madawa labda siku hiyo alivurugwa akaamua aue polisi. Wanaishi faya. Na watu wanasema familia yote imekamatwa sio kweli
 
Hii family wako poa sana. Kaka yao mkubwa anaitwa mahmood ni mtu poa. Nasikia kweli jamaa ni kweli alidhulumiwa na polisi. Ila kidogo ni mvutaji wa madawa labda siku hiyo alivurugwa akaamua aue polisi. Wanaishi faya. Na watu wanasema familia yote imekamatwa sio kweli
Ahsante kwa taarifa mkuu!
 
Any way Allah amsamehe ndugu yetu....katka mafundisho ya dini ya kiislamu tunafundushwa ya kwamba...

''...yeyote muislamu atakae kufa akipigania Mali yake/haki basi amekufa shahidi..."

Na katika kulipiza kisasi ni kitu ambacho kinaruhusiwa Ila kusamehe ni bora zaidi...

Ndugu Hamza alikuwa anajaribu kutetea Mali/haki yake na bila shaka alikuwa tayari kufa uku akihakikusha kuna watu anaondoka nao hasa hao polisi...

Wengi huwaita waislamu ni magaidi Ila ukweli ni kwamba waislamu hawapendi dhulma wapo tayari wafe wakitetea haki/Mali yao.....na ni watu wa visasi ni kama wa wakurya (vita ni vita mura) omba sana usiingie Kwenye anga zao.

Polisi uku mtaani wapigaji wa Dili vibaya...
Huo ni upumbavu sababu aliowauwa siyo waliomzulumu, hili ni tukio la kigaidi
 
Huo ni upumbavu sababu aliowauwa siyo waliomzulumu, hili ni tukio la kigaidi
Ni kuvurugwa mkuu,usiombe kudhulumiwa mali ambayo ulikuwa unaitegemea ikutoe kimaisha akili hugeuka na unakuwa tayari kwa lolote maana unahisi duniani bila hiyo mali wewe si lolote.
 
Ni kuvurugwa mkuu,usiombe kudhulumiwa mali ambayo ulikuwa unaitegemea ikutoe kimaisha akili hugeuka na unakuwa tayari kwa lolote maana unahisi duniani bila hiyo mali wewe si lolote.
Ni kuomba Mungu yasikukute ya kudhulumiwa.Ni balaa!
 
Mpaka leo, kumbukumbu zilizopo, ni kwa Polisi kuua na kuwatesa mara kadhaa viongozi, wanachama na waungaji mkono wa vyama vya upinzani.

Wapenzi na wanachama wa CUF wamewahi kuuawa na Polisi huko Zanzibar.

Wapenzi na wanachama wa CHADEMA wamewahi kuuawa a Polisi huko Morogoro na Arusha.

Wapenzi na wanachama wa ACT wamewahi kuuawa na Polisi huko Zanzibar.

Na hivyo vya vyote, wanachama, wapenzi na viongozi wake wamewahi kuteswa, kuwekwa mahabusu, hata kutekwa na kufungwa.

Lakini haijawahi kutokea hata mara moja, kiongozi, mwanachama au mpenzi wa CCM kuteswa au kuuawa na Polisi wakati akiwa kwenye harakati za kufanya siasa.

Mara zote Polisi hawajawahi kuviacha vyama vya upinzani vishindane na CCM, na hasa pale itakapoonekana CCM kuelemewa. Polisi wakiona kuna uelekeo wa CCM kuzidiwa na vyama vya siasa kwenye ushindani wa kisiasa, huingilia kati wakitumia nguvu za dola, ili kuilinda CCM. Kwa sasa Polisi, ni taasisi inayotegemewa sana na CCM kuliko taasisi nyingine zote. Jeshi la Polisi limekuwa idara muhimu sana ya CCM katika kuhakikisha CCM haizidiwi katika mashindano ya siasa.

Kijana Hamza alikuwa ni kada kindakinda na kiongozi mfia chama wa CCM. Imekuwaje huyu kada mwaminifu wa CCM hata akaenda kushambulia na kuua Polisi ambao ni makada zaidi ya makada katika kutetea maslahi ya chama? Imekuwaje wafia chama hata wakaanza kuuana wenyewe kwa wenyewe? Ni jambo la kufikirisha sana.

Kuna matukio mengine, yanayoendana na haya. Huko siku za nyuma ilikuwa ni kawaida sana Ndugai kuwafanyia harassment wabunge wa upinzani bungeni. Leo hawapo. Hivi karibuni Ndugai kawaita makada na wabunge wa CCM, Gwajima na Jerry kwenda bungeni kufanyiwa sawa na walivyokuwa wanafanyiwa wapinzani. Imekuwaje wafia chama kuanza kufanyiana harassment wenyewe kwa wenyewe kupitia Bunge? Inafikirisha sana.

Chini chini, ndani ya CCM na nje ya CCM, wapenzi, viongozi na wanachama wa CCM, wanafanyiana fitina za hali ya juu, huku baadhi wakimwunga mkono Rais wa sasa na wengine wakimpinga. Rais ambaye, hapo zamani angepingwa kwa baadhi ya mambo na wapinzani, sasa anapingwa kwa nguvu nyingi na wana-CCM wenzake. Inatikirisha sana.

Wakati nikiyafikiria haya, nikijatibu kuitafuta hekima, nikachukua kitabu changu kitakatiktu. Ndipo macho yangu yakaangukia kwenye kitabu cha Kut 17:8-15

Katika simulizi hii kwenye biblia, wana wa Israel walipoliitia jina la bwana ili kupigana na Waamaleki, Musa alipoinyanyua mikono yake, Waisrael walishinda.

Simulizi nyingine inasema maadui hata waliuana wenyewe kwa wenyewe. Hii maana yake ni kwamba Mungu anaweza kuwafanya muuane wenyewe kwa wenyewe.

Hiki kilichotokea jana kati ya Polisi ambayo ni taasisi yenye uaminifu mkubwa kwa CCM na kada na kiongosi mtiifu wa CCM, ni friendly fire, ni friendly war, ni friendly calamity, ni fruliendly disaster. Mlinzi wa kampuni binafsi ya ulinzi was caught in fire but was not a target.

Wenye macho ya rohoni, ndani ya CCM, wanatakiwa kutafakari zaidi. Matukio makubwa na mabaya, hutanguliwa na matukio madogo, yanayoonekana ya kawaida.

Wenye kupuuza na wapuuze, maana kuupuuza ukweli hakupunguzi bali huongeza hatari.

Mwalimu aliwahi kunena, "mnasema wao Wazanzibari na sisi Watanganyika kwa sababu ya Muungano, bila Muungano itakuwa sisi wasukuma, sisi wangoni, sisi wachaga, n.k."

Nami ninasema, "Kukiwa na vyama vya siasa vya upinzani, kutakuwa na sisi na wapinzani. Lakini bila upinzani, kutakuwa sisi wana-CCM wa kawaida, CCM Polisi, CCM-wakristo, wana-CCM waislam, wana=CCM wa kanda ya Ziwa, wana-CCM kanda ya Kusini, wana-CCM tunaomwunga mkono Samia, wana-CCM wanaompinga Samia, n.k."

Ujumbe muhimu:

Tuzoee kutenda wema na haki kwa kila mtu hata kama tunatofautiana naye kifikra, kiitikadi, kiimani, kimtazamo au namna nyingine yoyote iwayo. Tukizoea kutenda uovu dhidi ya tunaotofautiana nao, siku wasipokuwepo, roho ya uovu ule ule tutaitumia dhidi yetu wenyewe.

"Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu. Kwa kuwa Mungu Mwenye Nguvu amenifanyia makuu, jina lake ni takatifu. Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi. Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: Amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao; amewashusha wenye nguvu kutoka viti vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.”
 
Stori kwamba huyu jamaa alidhulumiwa ni stupid kabisa.

Kama alizulumiwa, kaua polisi 2 pale mataa, si angerudi tu nyuma kidogo kuna kituo cha polisi Salenda angeenda kuwakuta wengi tu, alikua anafuata nini ubalozi wa ufaransa?

Kama alikua anataka polisi walikuwepo pale stanbic bank, nyuma kidogo ubalozi wa urusi wamejaa, nyuma yake kisogo salenda polisi post, ubalozini alikua anafuata nini?

Ni watu kutaka ku twist hii habari ila ukweli ni kwamba huyu jamaa ni gaidi, ni mfia dini na sasa hivi yuko na mabikra 72 wanamzunguma wanamshika shida anawapiga mashine non stop kama dini inavyosema.
Juha ktk ubora wake
 
Any way Allah amsamehe ndugu yetu....katka mafundisho ya dini ya kiislamu tunafundushwa ya kwamba...

''...yeyote muislamu atakae kufa akipigania Mali yake/haki basi amekufa shahidi..."

Na katika kulipiza kisasi ni kitu ambacho kinaruhusiwa Ila kusamehe ni bora zaidi...

Ndugu Hamza alikuwa anajaribu kutetea Mali/haki yake na bila shaka alikuwa tayari kufa uku akihakikusha kuna watu anaondoka nao hasa hao polisi...

Wengi huwaita waislamu ni magaidi Ila ukweli ni kwamba waislamu hawapendi dhulma wapo tayari wafe wakitetea haki/Mali yao.....na ni watu wa visasi ni kama wa wakurya (vita ni vita mura) omba sana usiingie Kwenye anga zao.

Polisi uku mtaani wapigaji wa Dili vibaya...
Vipengere va kisharia ulivonot ni sawa ila namna ya kuziendea sio ile alotumia
 
Acha kumuhusisha huyo bwana wako (mungu wako) na unafiki wako. Kama ulisikia vizur maneno ya mshambuliaji, basi utapata jibu ni nani aliekuwa nyuma ya lile shambulizi. Inasikitisha kuona kijana kakubali kuuza utu wake, na uhai wake sababu ya laki 6 tu zilizozungumzwa mahakamani. RIP Chacha Wangwe.
 
Usiwashitue boss, sisi wengine tunasubiri na tunawaombea anguko kubwa ili wajifunze kuheshimu utu wa wengine.
 
Back
Top Bottom