Uchaguzi 2020 Tume ya Uchaguzi yampitisha Tundu Lissu kuwania Urais kupitia CHADEMA

Uchaguzi 2020 Tume ya Uchaguzi yampitisha Tundu Lissu kuwania Urais kupitia CHADEMA

Wandugu;

Huu ucheleweshwaji na ukiukwaji wa ratiba ya wagombea kuwasilisha fomu zao uliofanywa na NEC, hauna afya kwa mustakabali wa taifa letu na uchaguzi wenyewe.

Hivi ikatokea mgombea wa CHADEMA akashambuliwa na wale watu wanaoitwa "wasio julikana" njiani akiwa njiani anarejea kwenye maskani yake baada ya kumalizana na NEC, nani atalaumiwa?

Siombei itokee hivyo lkn nawaza tu kwa sauti!
Hivi haitaonekana kwamba NEC iliujua mpango huo na ikatumiwa na hao "wasio julikana" kuufanikisha?
Ndio, ndivyo itakavyo someka kwa sababu watakuwa wamehusika kwa maksudi kufanya mgombea huyo aondoke NEC usiku.
Ni hayo tu wandugu.
Atakuwa salama tu wakili msomi
Hata sero atalala tu
 
Mgombea Urais Uchwara Tundu Lissu ameanza kupatwa na homa ya kushindwa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, kabla hata kipenga hakijapulizwa baada ya kugundua asilimia kubwa ya Watanzania wanamuunga mkono Dkt. John Pombe Magufuli.

Lissu anajifanya yeye ni msomi wa Sheria lakini nashangaa ni Mwanashera gani wa hovyo huyu ambaye hajui umuhimu wa kufuata taratibu na miongozo iliyowekwa na Tume ya Uchaguzi.

NEC iliweka utaratibu wa Wagombea Urais kurejesha fomu na kila mgombea Urais aliyerudisha ambaye amekidhi vigezo na taratibu amepitishwa kuwa mgombea kwenye Uchaguzi.

Lissu analalama eti Rais Magufuli amependelewa, tukwambie Lissu, Magufuli hapendelewi ila anafuata taratibu zilizowekwa, wewe uliamua kutofuata taratibu ndiyo maana ulianza Kampeni kabla ya wakati sasa tulia dawa iingie.

Kiufupi Lissu wewe ni mtovu wa nidhamu wa kutofuata taratibu na Sheria zilizowekwa, akiondolewa kwenye kugombea Urais atasema Rais Magufuli anapendelewa wakati ni upuuzi wake.

Lissu ukome kumsakama Rais Magufuli fuata taratibu hauko juu ya Sheria
 
Lissu ata teuliwa tu tusubiri NEC watupatie taarifa baada ya kuhakiki makaratasi yake. Hivi huu mfumo wa kutafuta wadhamini na kuhakiki form una maana gani katika mfumo wa vyama vingi? kama mgombea amechaguliwa katika chama chake kuna haja gani aka teuliwa tena na NEC? naona kama NEC wanafanya zoezi ambalo tayari chama imesha lifanya, haya ma longolongo mengi ni ya kuondoa, kuwapotezea watu muda tu.
 
Kama Membe karudisha fomu Sina shida Hata wampitishe Tundu Lisu kugombea Zanzibar Lisu hapati kura kigoma na popote walipo wapemba na waislamu Tanzania bara na visiwani hapati kura

Udini utakumaliza mlamu!
 
Maswali ni mengi saana ya kuuliza bt ngoja niishie hapa
 
Ni Rasmi Sasa!

Tundu Antipass Lissu mwana wa Afrika na mwanademokrasia wa kweli wa Tanzania amepitishwa rasmi na Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC kuwa mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akiitangazia Dunia Mwenyekiti wa NEC Jaji Kaijage amesema Lissu ametimiza vigezo vyote na Masharti ya kuwa mgombea Urais kupitia Chadema.

Kulikuwa na hofu kubwa katika nchi kuanzia asubuhi baada ya Mgombea wa Chadema Kuwasili katika ofisi za Tume tangu asubuhi saa 5 Kama Ratiba ilivyoelekeza lakini Tume haikumteua kwa wakati kwa kile walichodai bado fomu zake kuhakikiwa

Kwa kadiri muda ulivyokuwa unasogea ndivyo Watanzania walivyokuwa na hofu kwa kile walichodhani Kuna hujuma dhidi ya chaguo Lao .

Taarifa kutoka mikoa kadhaa inasema mara baada ya kuteuliwa Shangwe za watu zimesikika kutoka sehemu kadhaa zikiwemo za starehe, masokoni na mashuleni huku kwa jiji la DSM watu kadhaa wamesikika wakipiga honi za magari barabarani kama ishara ya kufurahia kuteuliwa Tundu Lissu ambaye anaonekana ndiye mwenye uwezekano mkubwa wa kushinda nafasi hiyo ya Urais kutokana na kuungwa mkono na Wananchi walio wengi.

Kwa Sasa mpaka kesho saa 10 Jioni ni muda wa mtu yeyote anayestahili kuweka pingamizi Kama hajaridhishwa na maamuzi ya Tume ya kumteua mpigania haki huyu wa watu Tundu Lissu.
 
Back
Top Bottom