Tumetoka mbali sana, tumshukuru Mungu. Wengi hawakujionea kwa macho

Tumetoka mbali sana, tumshukuru Mungu. Wengi hawakujionea kwa macho

Acha tu tulitembea na mdundiko kutoka Tandale mpaka Buguruni tuliporudi home tulichezea stiki na mzee mpaka mjumbe aliingilia kati ndo ikawa pona yetu

View attachment 1989651
Hahaha mkuu umenikumbusha mbali sana, mdundiko ulipita home nje Kijitonyama gafra nikawa katikati ya ule umati nikiufuata na kufurahia mauno na nyimbo za mdundiko. Kuja kushtuka jioni giza linaanza kuingia eneo silijui wala hakuna ninaemfahamu. Nikaanza kulia, wasamalia wema wakanipeleka msikitini kutanganzwa kuwa nimepotea.
Cha kushukuru Mungu nikaulizwa shule ya msingi nasoma wapi? Bila kusita nikiwa nalia nikataja shule yangu ni KITONYAMA PRIMARY SCHOOL so nikachukuliwa mpaka maeneo ya shule nikawaambia hapa ninapajua. Bhas nikangoza njia mpaka nyumbani pamoja na wale wazee wawili (mmoja akiwa ni balozi ) ikiwa ni usiku huku nyumbani nilishatafutwa sana mpaka taarifa polisi ilishatolewa na baba.
Eneo nililopetea ni MBURAHATI, now naijua vizuri tu
 
Umenikumbusha enzi ya ndaga bar magomeni kagera, kibisa friends corner hotel, cinema kwa ngawaiya manzese Argentina yalipokuwa makao makuu ya nccr mageuzi,, ukitaka kwenda kwetu uzaramoni stendi sokoni kariakoo basi isuzu tx nyuma
limeandikwa mchawi na mwizi mzuri nani,, lingine limeandikwa 'dikwembe dibanza ingoma '
 
Enzi ambayo mkila wali nyumbani utahakikisha kwenye chai unanawa mkono mmoja ili mwingine iwe ushahidi kwa masela wanuse hata kidogo viganja vyako
Hahaha uswahilini kulikuwa na vituko sana. Naikumbuka sana hii pamoja mkila kuku hunawi mkono ili masela wakajue dah
 
Yaani wengi watadhani ni as mulizi tu za Jomba Buji, lakini huku ndiko haswa tulikotoka

1. NGOMA YA MDUNDIKO
Zama zile MDUNDIKO ulipita mtaa kwa mtaa jijini, ni mwendo mpwitompwito, nyimbo, ngoma, matusi, mikatiko, yaani kivumbi na jasho, unatoka kwenu Buguruni unajikuta uko Kawe Mzimuni, na nauli huna.

2. JIWE LA FATUMA
Mmelala ndani mnasikia nje watu wanahesabu, moja, mbili taaaaaaaat. Kabla hawajamaliza kuhesabu mnaliona jiwe kubwa sana love naingia ndani, mlango umesambaratishwa, njemba za miraba minne kama Tisa, mapanga yameremetayo yenye makali kuwili yako standby kusambaratisha nyama za miili yenu, MNA music system wanabeba, TV set inaondoka, cheni na vidani vya dhahabu si Mali yenu tena.

Shukrani kwa Augustino Lyatonga Mrema

3. MAGARI KUFUNGWA KWA MAKUFULI NA MAKOMEO
MULTI LOCK kampuni ya ki Israel iliuza sana makufuli na makomeo ya kulinda magari yasiibwe. Mijitu iliiba magari kwa namna mbalimbali, ila kubwa zaidi ilikuwa kwa kutumia fungi Malaya. Multi-lock ikawa changamoto kwa kina Kaka Jambazi

4. KUIFIKIA BAADHI YA MIKOA ILIBIDI UTOKE NJE YA MDUNDIKO TANZANIA NDIPO UFIKE
Mikoa ya kanda ya ziwa hasa Mara, Kagera na Mwanza ilikuwa haifikiki kirahisi hata kidogo, ilibidi ukate passport ya muda ili uvuke Kenya na wakati mwingine Uganda ili uweze kwenda huko.

Scandinavia Express walipiga sana hela, pia kulikuwa na kampuni ya Akamba wakitoa huduma hizo.

5. YO!! RAP BONANZA
Miaka hiyo ya tisini mwanzoni kurap ndo ilikuwa mpango mzima kwa wajanja. Chris's Phabby, Ras Pomppy Dou na Wengine wengi waliokwenda kuonyesha umahiri wao

6. KUMBI ZA STAREHE
Zama zile muziki wa dansi ukiwa umeshika hatamu, kumbi zetu zilikuwa Bonga Bar, Lang'ata Social Hall, DDC, Ruvuma Mpaka Maputo, Amana Social Hall.
Disco kwa MBOWE.

7. CODRY NA RABA MTONI, SKIPA NA DENGRIZ

Wajanja walienda Greece kwa kuzamia meli walirudi na suruali zao za codry, dengdriz, skipa na raba mtoni.
Enzi hizo madukani vitu vilikuwa adimu mno.

8. MODEL ZA MAGARI
Zama zile kulikuwa na Datsun, Toyota Staut, Isuzu KB, Pajero ambayo ilikuwa inatajwa Hadi kuwa nantv inayoonyesha majeneza na watu wakienda kuzika pale inapokimbizwa Sana. Kulikuwa na gari inaitwa Morris, kulikuwa na Impala, Scania 111, Bedford, Isuzu NKR, Isuzu TX, Land Rover 109 kidume. Zama zile ilikuwa NI marufuku kwa Range Rover kupaki benki.
Disco kwa MBOWE huyuhuyu anaesumbuliwa na kima wa vijijini eti ni gaidi.
 
1.Nyama kwenye pick up ikipelekwa buchani huku na wanunuzi wakiwa wamepanda juu wakiikanyaga hiyo nyama.
2.watu wakivuta sigara ndani ya basi.huku basi likiwa limewekewa ashtray kabisa.hakuna abiria anaelalamika.

Mche wa sigara ulikuwa unavurumishwa hadi hospitalini bila kelele ya mtu!
 
Harbours Club Kurasini near mivinjeni ...Mzee Naido, Bugi service mapikipiki Uwanja wa Barafu kuwaona wakina Rozi Walele na kimini cha netball Mzee Mwishehe Dukani Magorafa ya customer kwakina Antonita bonge la pisi leupeee....haha Salvatory Edward tunacheza mpirapale shule ya vidudu tukiwafunga wanatufukuza na mawee...Bambino relini shimo la udogo bar mziki wa nyako nyako konyaaaa......meli ya Kishitobe bandalini .....Amina mento bonge la pisi kurasini kotaz
 
AHAAAAAAAAAAAA, UMENIKUNA SAANA LEO, MUZIKI WA DANSI, DDC KARIAKOO, MAGOMENI KONDOA , EQUATOR BAR MTONI PALE, UWANJA WA NDANI WA TAIFA, KIGONGO BAR BUGURUNI, HIYO NI SIKINDE BWANA USIPIME. YANGA AU SIMBA ISHINDA MDUNDIKO TOKA UWANJANI HADI MAKAO MAKUU, KURUDI UTAJUA MWENYEWE. MAMA NITILIE NI JIONI SAA MOJA MOJA SAANA UNAUZIWA MAHARAGE
Bila kusahau kumbi za sinema kama Empire,Empress, Drive Inn,New Chox,Star Light,Odeon,Cameo.Kipindi hicho tunamuangalia Angela Mao,Churck Norris,James Bond,Bruce Lee halafu jumatatu tunakwenda kuhadithiana Shuleni[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
Brother umeua! Brother umeua! 😁😁😂

Vichupi vilikuwa vinabana vile,yet wanaume kama wanaume tulikuwa na nguvu za kiume za kutosha.Sijui leo boxer ndo zinafanya watu wakose nguvu?

Zamani zile ukiona paja la mdada ngoma inasimama kinyama.Leo mtu umevaa boxer mdada mzuri anasimama mbele yako kwenye mwendokasi akiwa hajavaa kitu,mmebanana kinoma,ila bado mtambo hausimami.Boxer zilaaniwe!
 
Back
Top Bottom