Tumetoka mbali sana, tumshukuru Mungu. Wengi hawakujionea kwa macho

Tumetoka mbali sana, tumshukuru Mungu. Wengi hawakujionea kwa macho

Umenikumbusha mbali Ila nianze na hili la jiwe Fatuma.
Kuna mzee mmoja jirani alikua mlevi mlevi, Kuna siku amerudi home saa sita usiku wakati bado Yuko sebuleni anakula akasikia kwa nje wanahesabu moooojah. Fasta akafungua mlango na kuwaambia wale wezi, msinivunjie mlango wangu, chukueni mnachotaka halafu mzee akarudi mezani akaendelea na msosi wake. Basi wale wahuni wamesimama pale mlangoni tiivii chogo wanaiona, deki na redio lkn mzee anakata matonge ya ugali na kutoweza kwenye mchuzi mzito wa samaki.
Wale wahuni walianza kumtukana mzee kwamba Ni mwanga na kuondoka mmoja baada ya mwingine.
Mzee alipomaliza msosi alifunga mlango na kuingia chumbani.
Kesho yake mzee alipokua anahadithia alisema ujinga ule wa kilevi hatakaa aurudie Tena.
 
Enzi hizo ugonjwa mkubwa ulikuwa malaria na badae ukimwi lakini siku hizi ni mwendo wa sukari, presha, ini , figo, stroke.
Halafu kipindi kile kulikua hakuna swala la kukosa nguvu za kiume. Hata ofisa mzee akiamua anakanyagia kweli kweli.
Siku hizi vumbi la kongo na kwa wsheshimiwa Viagra .
 
umenikumbusha kipindi cha miaka 1994 buguruni kwa mnyamani na kile reli ilipokuwa inapita kulikuwa na nyumba za udongo sana.

miaka 2000 tabata,kisukuru,mabibo nyumba zilikuwa za kuhesabu tena mashamba ya mpunga huko tabata.

kwa wale tuliokulia sinza miaka 90 mnakumbuka ukuta wa posta kabla kuwa stendi ya elfu 2000.

maeneo ya chuo kikuu kulikuwa na mitaro yenye maji safi na unapata samaki wa kufuga.

maisha ukianza kukumbuka nyuma unaanza kulia maisha ya zamani yalivokuwa mazuri
 
Yaani wengi watadhani ni as mulizi tu za Jomba Buji, lakini huku ndiko haswa tulikotoka

1. NGOMA YA MDUNDIKO
Zama zile MDUNDIKO ulipita mtaa kwa mtaa jijini, ni mwendo mpwitompwito, nyimbo, ngoma, matusi, mikatiko, yaani kivumbi na jasho, unatoka kwenu Buguruni unajikuta uko Kawe Mzimuni, na nauli huna.

2. JIWE LA FATUMA
Mmelala ndani mnasikia nje watu wanahesabu, moja, mbili taaaaaaaat. Kabla hawajamaliza kuhesabu mnaliona jiwe kubwa sana love naingia ndani, mlango umesambaratishwa, njemba za miraba minne kama Tisa, mapanga yameremetayo yenye makali kuwili yako standby kusambaratisha nyama za miili yenu, MNA music system wanabeba, TV set inaondoka, cheni na vidani vya dhahabu si Mali yenu tena.

Shukrani kwa Augustino Lyatonga Mrema

3. MAGARI KUFUNGWA KWA MAKUFULI NA MAKOMEO
MULTI LOCK kampuni ya ki Israel iliuza sana makufuli na makomeo ya kulinda magari yasiibwe. Mijitu iliiba magari kwa namna mbalimbali, ila kubwa zaidi ilikuwa kwa kutumia fungi Malaya. Multi-lock ikawa changamoto kwa kina Kaka Jambazi

4. KUIFIKIA BAADHI YA MIKOA ILIBIDI UTOKE NJE YA MDUNDIKO TANZANIA NDIPO UFIKE
Mikoa ya kanda ya ziwa hasa Mara, Kagera na Mwanza ilikuwa haifikiki kirahisi hata kidogo, ilibidi ukate passport ya muda ili uvuke Kenya na wakati mwingine Uganda ili uweze kwenda huko.

Scandinavia Express walipiga sana hela, pia kulikuwa na kampuni ya Akamba wakitoa huduma hizo.

5. YO!! RAP BONANZA
Miaka hiyo ya tisini mwanzoni kurap ndo ilikuwa mpango mzima kwa wajanja. Chris's Phabby, Ras Pomppy Dou na Wengine wengi waliokwenda kuonyesha umahiri wao

6. KUMBI ZA STAREHE
Zama zile muziki wa dansi ukiwa umeshika hatamu, kumbi zetu zilikuwa Bonga Bar, Lang'ata Social Hall, DDC, Ruvuma Mpaka Maputo, Amana Social Hall.
Disco kwa MBOWE.

7. CODRY NA RABA MTONI, SKIPA NA DENGRIZ

Wajanja walienda Greece kwa kuzamia meli walirudi na suruali zao za codry, dengdriz, skipa na raba mtoni.
Enzi hizo madukani vitu vilikuwa adimu mno.

8. MODEL ZA MAGARI

Zama zile kulikuwa na Datsun, Toyota Staut, Isuzu KB, Pajero ambayo ilikuwa inatajwa Hadi kuwa nantv inayoonyesha majeneza na watu wakienda kuzika pale inapokimbizwa Sana. Kulikuwa na gari inaitwa Morris, kulikuwa na Impala, Scania 111, Bedford, Isuzu NKR, Isuzu TX, Land Rover 109 kidume. Zama zile ilikuwa NI marufuku kwa Range Rover kupaki benki.
Ila watanzania kwa uwongo na uzushi. Nakumbuka kabisa iyo ya pajero ilivypamba moto eti kuna katv kwenye dashboard jinsi unavyo geza spidi unaona jeneza ukizidi unaona watu wa nabeba jeneza wanaenda kuzika.

Halafu kuhusu popo Bawa yani uzushi tuu hadi tulikuwa tunaogopa kulala. Wakamsingizia hadi mzee ruksa.

Ishu ya wanyonya damu masinga singa walizushiwa
 
Enzi hizo nasoma Olevel Nakuru Kenya, Alevel Kampala international, Chuo Uganda Christian University-Mukono, what ana amazing 27-29 hours dar-kampala, dsm -Nakuru, ukikosa Scandinavia ukipanda zile za wasomali kampala to nairobi wezi kama wote, hifazi mzigo kwenye buti lasivo upakate mzigo.khaa haya maisha. Banzukulu watanielewa, Dembe FM full vituko. My life in Nakuru what an amazing Kenya was, Thank you a lovely flashback in the making.
Usinikumbushe AFRAHA STADIUM, STAGS HEAD HOTEL NA SHULE YANGU MENENGAI . Ulishafika landipanya???
 
1. NGOMA YA MDUNDIKO
Kaka usiache nitoe machozi.
Kuna dogo mmoja mitaa ya Gongo la mboto aliingia chooni kujisaidia. Enzi zile madogo wakiingi chooni wanavua kabisa kaptura na kuiacha nje ya choo. Sasa dogo wakati anamalizia shughuli za chooni mdundiko ukapita. Dogo alipotoka nje alisahau kuvaa kaptura na kufuata mdundiko. Muda umekwenda Sasa mama dogo anamtafuta dogo. Kufika uani anakutana na kaptura ya dogo Ila dogo haonekani. Mama akajua dogo Kwisha tumbukia ndani ya shimo la choo. Muda wote huo dogo Yuko kwenye mdundiko.
Wazee wa mtaa wakaita gari ya faya. Yale makelele ya gari ya faya yakamstua dogo naye ikabidi akaangalie home kulikoni mbona wanavunja choo chetu.
Faya wakavunja choo ndani ya choo hakuna mtu.
Sasa mama mmoja akamuona dogo Hana kaptura akakuambia dogo akavae kaptura. Dogo wakati anaingia kuvaa ndio bi mkubwa akamuona yapata saa kumi na mbili na ushee. Alooh. Dogo alishushiwa kipigo Cha mbwa Koko aka muroto
 
6. KUMBI ZA STAREHE
Bonga Bar,

We kijana weeeh. Bonga bar uliijuaje?
Saa kumi na mbili na nusu kagiza kanaanza tu watu tunanawa na koni zinavyonzwa hadharani. Bar Ina mabarmaid wengi kuliko wateja.
Wee mwana wee.
Kumbe umeona mengi mweh.
Siku hizi ukipita Mboka unajichekea kikoyomoyo
 
Yaani wengi watadhani ni as mulizi tu za Jomba Buji, lakini huku ndiko haswa tulikotoka

1. NGOMA YA MDUNDIKO
Zama zile MDUNDIKO ulipita mtaa kwa mtaa jijini, ni mwendo mpwitompwito, nyimbo, ngoma, matusi, mikatiko, yaani kivumbi na jasho, unatoka kwenu Buguruni unajikuta uko Kawe Mzimuni, na nauli huna.

2. JIWE LA FATUMA
Mmelala ndani mnasikia nje watu wanahesabu, moja, mbili taaaaaaaat. Kabla hawajamaliza kuhesabu mnaliona jiwe kubwa sana love naingia ndani, mlango umesambaratishwa, njemba za miraba minne kama Tisa, mapanga yameremetayo yenye makali kuwili yako standby kusambaratisha nyama za miili yenu, MNA music system wanabeba, TV set inaondoka, cheni na vidani vya dhahabu si Mali yenu tena.

Shukrani kwa Augustino Lyatonga Mrema

3. MAGARI KUFUNGWA KWA MAKUFULI NA MAKOMEO
MULTI LOCK kampuni ya ki Israel iliuza sana makufuli na makomeo ya kulinda magari yasiibwe. Mijitu iliiba magari kwa namna mbalimbali, ila kubwa zaidi ilikuwa kwa kutumia fungi Malaya. Multi-lock ikawa changamoto kwa kina Kaka Jambazi

4. KUIFIKIA BAADHI YA MIKOA ILIBIDI UTOKE NJE YA MDUNDIKO TANZANIA NDIPO UFIKE
Mikoa ya kanda ya ziwa hasa Mara, Kagera na Mwanza ilikuwa haifikiki kirahisi hata kidogo, ilibidi ukate passport ya muda ili uvuke Kenya na wakati mwingine Uganda ili uweze kwenda huko.

Scandinavia Express walipiga sana hela, pia kulikuwa na kampuni ya Akamba wakitoa huduma hizo.

5. YO!! RAP BONANZA
Miaka hiyo ya tisini mwanzoni kurap ndo ilikuwa mpango mzima kwa wajanja. Chris's Phabby, Ras Pomppy Dou na Wengine wengi waliokwenda kuonyesha umahiri wao

6. KUMBI ZA STAREHE
Zama zile muziki wa dansi ukiwa umeshika hatamu, kumbi zetu zilikuwa Bonga Bar, Lang'ata Social Hall, DDC, Ruvuma Mpaka Maputo, Amana Social Hall.
Disco kwa MBOWE.

7. CODRY NA RABA MTONI, SKIPA NA DENGRIZ

Wajanja walienda Greece kwa kuzamia meli walirudi na suruali zao za codry, dengdriz, skipa na raba mtoni.
Enzi hizo madukani vitu vilikuwa adimu mno.

8. MODEL ZA MAGARI
Zama zile kulikuwa na Datsun, Toyota Staut, Isuzu KB, Pajero ambayo ilikuwa inatajwa Hadi kuwa nantv inayoonyesha majeneza na watu wakienda kuzika pale inapokimbizwa Sana. Kulikuwa na gari inaitwa Morris, kulikuwa na Impala, Scania 111, Bedford, Isuzu NKR, Isuzu TX, Land Rover 109 kidume. Zama zile ilikuwa NI marufuku kwa Range Rover kupaki benki.
Kitambo mno mkuu
 
Yaani wengi watadhani ni as mulizi tu za Jomba Buji, lakini huku ndiko haswa tulikotoka

1. NGOMA YA MDUNDIKO
Zama zile MDUNDIKO ulipita mtaa kwa mtaa jijini, ni mwendo mpwitompwito, nyimbo, ngoma, matusi, mikatiko, yaani kivumbi na jasho, unatoka kwenu Buguruni unajikuta uko Kawe Mzimuni, na nauli huna.

2. JIWE LA FATUMA
Mmelala ndani mnasikia nje watu wanahesabu, moja, mbili taaaaaaaat. Kabla hawajamaliza kuhesabu mnaliona jiwe kubwa sana love naingia ndani, mlango umesambaratishwa, njemba za miraba minne kama Tisa, mapanga yameremetayo yenye makali kuwili yako standby kusambaratisha nyama za miili yenu, MNA music system wanabeba, TV set inaondoka, cheni na vidani vya dhahabu si Mali yenu tena.

Shukrani kwa Augustino Lyatonga Mrema

3. MAGARI KUFUNGWA KWA MAKUFULI NA MAKOMEO
MULTI LOCK kampuni ya ki Israel iliuza sana makufuli na makomeo ya kulinda magari yasiibwe. Mijitu iliiba magari kwa namna mbalimbali, ila kubwa zaidi ilikuwa kwa kutumia fungi Malaya. Multi-lock ikawa changamoto kwa kina Kaka Jambazi

4. KUIFIKIA BAADHI YA MIKOA ILIBIDI UTOKE NJE YA MDUNDIKO TANZANIA NDIPO UFIKE
Mikoa ya kanda ya ziwa hasa Mara, Kagera na Mwanza ilikuwa haifikiki kirahisi hata kidogo, ilibidi ukate passport ya muda ili uvuke Kenya na wakati mwingine Uganda ili uweze kwenda huko.

Scandinavia Express walipiga sana hela, pia kulikuwa na kampuni ya Akamba wakitoa huduma hizo.

5. YO!! RAP BONANZA
Miaka hiyo ya tisini mwanzoni kurap ndo ilikuwa mpango mzima kwa wajanja. Chris's Phabby, Ras Pomppy Dou na Wengine wengi waliokwenda kuonyesha umahiri wao

6. KUMBI ZA STAREHE
Zama zile muziki wa dansi ukiwa umeshika hatamu, kumbi zetu zilikuwa Bonga Bar, Lang'ata Social Hall, DDC, Ruvuma Mpaka Maputo, Amana Social Hall.
Disco kwa MBOWE.

7. CODRY NA RABA MTONI, SKIPA NA DENGRIZ

Wajanja walienda Greece kwa kuzamia meli walirudi na suruali zao za codry, dengdriz, skipa na raba mtoni.
Enzi hizo madukani vitu vilikuwa adimu mno.

8. MODEL ZA MAGARI
Zama zile kulikuwa na Datsun, Toyota Staut, Isuzu KB, Pajero ambayo ilikuwa inatajwa Hadi kuwa nantv inayoonyesha majeneza na watu wakienda kuzika pale inapokimbizwa Sana. Kulikuwa na gari inaitwa Morris, kulikuwa na Impala, Scania 111, Bedford, Isuzu NKR, Isuzu TX, Land Rover 109 kidume. Zama zile ilikuwa NI marufuku kwa Range Rover kupaki benki.
Umenikumbusha ki luxury pugu Kariakoo,ubungo minazi,Kuna watu hawawezi kuelewa ukiwaambia pale ubungo lilipo jengo la Tanesco l,ilikuwa soko kubwa,enzi hizo panaitwa ubungo minazi.
Hivi watu wanajua kabla stend haijaamishiwa makumbusho ilikuwa mwenge!?
Vipi story ya mtu kugeuka chatu!!buguruni!!
Vijana wa leo wakiona mwendo Kasi,wanafikiri ni kitu kigeni kwa baba zao,miaka ya 90,zilikuwepo ikarusi(kumba kumba).
Kipindi hicho,kutoka ubungo kwenda Mbagara ni gari tatu!!
Ubungo buguruni,buguruni Temeke,Temeke Mbagara!!!
Aaaah tumetoka mbali sana.
Kipindi hicho nasoma darasa la tatu external nakaa liver side,natembea kwa miguu,ilipo mabibo hostel,ulikuwa uwanja tunachezea Mpira.
 
Back
Top Bottom