Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Polisi Nyamongo wameshambulia msafara wetu kwa mabomu ya machozi wakizuia njia kuelekea kwenye mkutano wetu wa kampeni

Yeye anasikiliza porojo za Magu anapodai kasimamishwa njiani ni anadhani kweli. Wakati kiuhalisia kila kitu kinakuwa kimepengwa na ulinzi wa kutosha umesha tayarishwa.

Mahala ambapo ulinzi aujapangwa ata watokee maelfu barabarani Magufuli asimami.

Magufuli akicheza na yeye anacheza jukwaani the guy is obsessed na Magufuli anataka aige kila anachofanya.
 
Kumekucha!

Hata hivyo nilishangaa sana hao polisi kuchelewa kwa muda wote huo kufanya hayo!

Its a shame,sasa wameanza kuwatisha wananchi wanaohudhuria mikutano ya Lissu!Hii nchi ilikabidhiwa kwa washamba na mafedhuli!
 
Anataka nayeye asimamishe magari barabarani kama Magufuli, kwenye kichwa chake yeye kama raia na raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania nyadhifa zao ni sawa.

Mwisho wa siku tutakuja kubaliana jamaa ‘mtambo’.
Sasa kama Magu ni rais anapita kuomba kura za nini?

Polisi wanachofanya ni kuinua zaidi ari ya wapenda mabadiliko na wanampaisha zaidi Lissu kwa watz na dunia nzima kutaka kufuatilia kwa karibu.

Bado watawala wa Tanzania hawajajua bado kwamba tukio la kujaribu kumuua Lissu huko Dodoma ndio limemweka juu kabisa kileleni aliko sasa.

"Haki huinua taifa"
 

..sidhani kama angetumia zaidi ya dakika 10 kuzungumza na kusalimiana na watu hapo barabarani.

..TL amepita maeneo mengi hapa nchini na hakukuwa na matatizo yoyote, tena hata majuzi alianza kuwasifia jeshi la polisi.

..sidhani kama kuna ulazima wa kupiga mabomu kampeni ya chama chochote kile. kwa ujumla wananchi wamekuwa watulivu, wameonyesha uchangamfu, furaha, na hamasa, sidhani kama ni busara kwa jeshi la Polisi kuwapiga mabomu wananchi walio katika hali hiyo.
 
Hongereni Jeshi la polisi, huyo jamaa anajiona yuko juu ya sheria.
 
Habari zinazoanza kushika kasi mtandaoni ni kwamba Msafara wa mgombea Urais kupitia CHADEMA Tundu A. Lissu umevamiwa na polisi waliowatawanya waliokuwa katika msafara huo kwa mambomu ya machozi.

Source:

Hii sio sawa kabisa.
 
Bwana mkubwa kiwewe kimemkumba, siku 30 za mwisho pumzi imekata. Kilichobakia kwake ni matumizi mabaya ya vyombo vya dola. Alianza msajili wa vyama, akaja mkurugenzi wa NEC, sasa polisi nao wameingizwa kazini.

CCM ni sikio la kufa na wala haliwezi kusikia dawa. Wananchi wamewakataa kwa vitendo, sasa mmeamua kuwatisha na kuwapiga mabomu ya machozi, kisa tu wivu wenu kwake kwa mapenzi na hisia wanazo zionyesha kwa Rais wao ajae.

Nasema, ole wenu nyie ambao mnakwenda kinyume na maadili ya kazi na dhamana mliyopewa na umma. Siku ikifika, naam! Nayo imeshafika, mtabaki nyinyi peke yenu na familia zenu. Tambueni ya kwamba uvumilivu una kikomo.
 
Safi sana! ilitakiwa waanze nao tangu zamani.
Ukicheza na kima utavuna mabua
 
Sasa namna hii magufuli atapataje usingizi?
Nahidi igp kila muda anapigiwa simu na kufokewa sn anauliwa.... Hayo mabomu tumewapa ya nini?
IGP RPC OCD wote wanaoshiriki vitendo vya kuwaonea wapinzani kuhatarisha Amani watambue kuwa mara baada ya uchaguzi watafikishwa ICC The Hague kujibu tuhuma zao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…