Tundu Lissu: Rais Samia amenilipa stahiki zangu nilizonyimwa na Magufuli

Tundu Lissu: Rais Samia amenilipa stahiki zangu nilizonyimwa na Magufuli

Makamu mwenyekiti wa Chadema Tundu Lissu amesema Rais Samia amemlipa stahiki zake kama mbunge ambazo ni kiinua mgongo Serikali ya Rais Magufuli ilikuwa imekataa kumlipa

Pia serikali ilimuambia aandike barua pamoja na kuambatanisha na nyaraka ili apewe fedha zake za matibabu ambazo serikali ya Rais Magufuli pia ilikataa kumlipa

Tundu Lissu alikutana na Rais Samia alipotembele nchini Ubelgiji ambapo waliongea mambo kadhaa ikiwemo stahiki hizo


I love reconcilliation
 
Kwamba Samia ndio Kamlipa ? Hii nchi itakuwa ya Kifalme kama vile ambavyo tungekasirika uweze wa JPM kuzuia ndio tukasirike uwezo wa Rais kulipa..., Ifike wakati tuwe na Taasisi zinazofuata sheria inasema / inataka nini sio mtawala anaamua nini
 
Ingawa Rais Samia, kama mwanadamu, anaweza kuwa na mapungufu yake, lakini kwa kweli katika utu, hekima, ubinadamu na busara, Mungu amemjalia. Tumshukuru Mungu kwa kutupa nafasi mbili zilizo kinyume:

Alitupatia kiongozi katili asiye na busara, ili tuone umuhimu wa kuwa na kiongozi mwenye busara.

Akatupatia kiongpzi mwenye busara, ili kutuoneshe ilivyo jambo jema na la furaha kuwa na kiongozi mwema.

Rais Samia, kwa hekima yake, ataheshimika na wengi, tofauti na mtangulizi wake ambaye ameendelea kudharaulika kwa ukatili wake, hata wakati akiwa ameondoka Duniani.

Maombi yetu, Mungu azidi kumjalia busara Rais Samia, maana busara ya kiongozi ni faraja kubwa kwa wanaoongozwa.
 
Devoted Muslims have a clear sense and meaning of ''justice'' than the other devoted and pious imitators
Afadhali umesema ni imitators.

Yule mwingine, kwa hakika hakuwahi kuwana dini, labda mizimu.

Hakuna muumini wa dini yeyote awe mkristo, muislam, budha au hindu ambaye anaweza kuwa muuaji,mtekaji na mpotezaji wa binadamu wenzake.

Ndiyo maana, wengine walisema, "tuna shetani"
 
Back
Top Bottom