Pre GE2025 Tundu Lissu: Tuna upungufu wa kutisha wa fedha kwa ajili ya shughuli za Chama (CHADEMA), msiniulize nimekuta nini, jibu halitakuwa zuri!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kuna dalili za ufisadi, Lissu amekwapua fedha ya chama
 
Mbowe alijitoa Kwa HALI na MALI ,Lissu. anaweza kujitoa Kwa HALI na HARAKATI.
 
Na hiyo nyumba ya oysterbay atoke huko, yeye sio kiongozi wa wapinzani bungeni...
Na aanze kutumia hela zake binafsi kufadhili chama, alidhani kuna hela za kumwaga kwenye uenyekiti......
 
Hao so called wafanya biashara walipiga kura? Lissu si wakuja amekuwepo humo ndani for waaaaay long, ame suffer nusura apoteze uhai halaf unaita wakuja? Have some respect
 
Maji ya shingo....

Ni rahisi sana ukiwa jukwaani kumzodoa mnenguaji kuwa haendi sambamba na miondoko ya ngoma.....
Kwa hiyo ulitaka Mbowe ndo awe tegemeo siku zote? Ujinga wa hali ya juu! Mwanzo mgumu hata mimi nitachangia na niloshachangia pia!
 
Kumbe ndiyo maana Mbowe alikuwa hataki kuachia madaraka akiogopa kufichuliwa maovu yake. Jamaa alikuwa mwizi mno.
 
Kumbe za kuhonga wajumbe zilikuwa zinachotwa kwenye kapu la chama.
 
MBOWE ana kinyongo
Wakongwe kama wewe hawapaswi kuongea hivyo. Uongozi wa Mbowe uliweka wazi kuwa hakuna hela, na hata Mkutano Mkuu wa Uchaguzi, wajumbe wa Kamati Kuu waligawana viwango vya fedha vya kutafuta kwa marafiki zao, hata Lissu aligawiwa ingawa hakuchangisha.

Sasa kama Mkutano wa mwisho tu wa awamu iliyomalizika haukuwa na fedha za chama za maandalizi, Lissu hakutegemea kukuta akaunti haina kitu au na hata kuikuta na madeni?

Unasema Mbowe ana kinyongo, sasa hicho kinyongo ni kipi, hataki kuchangia chama au ni vipi?
 
Chama hakiwezi kumshinda kwa sababu hiki chama kina rasilimali watu wengi sana bado tu hajajipanga akisha jipanga fedha ni nyingi sana CDM.Pia harakati zilizo hazishwa na chama za no reform no election pia zimewatisha kidogo watu ambao tayari walikuwa na mipango yakugombea nafasi mbali mbali ambao asilimia kubwa ndiyo wachangiaji wa chama,Ila akisha weka mikakati tu ya Chama kitapaata fedha, fedha zitamimiminika kwa wingi. Kama ni fedha tu kama fedha hata CCM wapo tayari kuwapa ila kwa masharti kama yaliyokuwa mwanza kuwa wasifanye harakati zozote za kweli kama vilivyo vyama vingine. CDM ya Tundulisi siyo Chama cha kununuliwa kirahisi na asipofanikiwa yeye tujue watanzania tutaendelea kuishi utumwani milele kwanni hakuna mtu mwingine yioyote ambaye atakuwa yupo tayari kujitolea kama Yeye. Fedha siyo tatizo CDM tatizo ni kuwa hizo fedha zinatoka wapii?
 
Alikuwa anaongea na wanachama wa Chadema sasa wapi amekupigia kelele wewe kapuku unayeishi kwa uchawa na kushibia makombo toka mezani kwa unaowasifia kutwa kucha.
 
Lisu naye atoe uthibitisho kama hazikutumika milioni 65 na athibitishe kuwa hakukuta kitu alipoingia uenyekiti

Hizo pesa za retreat alitoa wapi ? Aeleze chanzo cha hizo pesa
Aliuza uñga akapata hizo hela.
 
Watu waelewe kuwa vyama vya upinza vyanzo vyake vikubwa vya fedha ni mifukoni mwa wanachama wake,,, hakuna mtu baki yoyote anaye weza akawapatia hizo fedha. Ndiyo maana inakuwa rahisi kununuliwa. CCM kinaogelea kwenye mabilioni ya walipa kodi kwakujilipa mabilioni ya ruzuku, huku vyama vya upinzani vikihongwa vijisenti ili vififishe mapambono yakudai haki. CDM wasikubali kurubuniwa ili kufifisha harakati,, za kutafuta tume huru na katiba mpya naona vyama vyote vimefyata mkia,vikiwa vinazengea viposho vya kuhongwa.
 
Hii nilishasema CDM hawana fedha mpaka leo wana Tsh 2,450,000
 
Wewe kidampa wa mama Abdul ni hopeless kabisa,ulitaka Lissu adanganye kakuta empty cofers?

Yaani watu tulikataa habari za mtu kukiita chama chake mara sijui kakikopesha ,hicho sio chama ni duka sasa au biashara binafsi.

Ukweli ndio dawa chama kitachangiwa maana ni cha wanachama sio private entity .

Nyerere wakati anaenda UN hakuwa na pesa hata pesa za kumudu tiketi ya daraja la uchumi kwenye ndege achilia mbali malazi na chakula huko alikokwenda ila kupitia wanachama alienda.

Ukiwa kilaza utadhani kuendesha chama ni sawa na kuendesha biashara.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…