Tunduma: Wakuu wa shule wavuliwa nyadhifa kisa wimbo wa Zuchu (Honey)

Tunduma: Wakuu wa shule wavuliwa nyadhifa kisa wimbo wa Zuchu (Honey)

Huo wimbo unapendwa sana kuimbwa na watoto hata wale wachanga ambao hata shule ya awali hawaanza. Kama mnaona huo wimbo hauna maadili upigeni ban. Kuna kigogo mmoja mtu mzito wa hadhi ya juu alikwenda uganda kikazi. Katika mambo ya kuburudisha wageni ukawekwa wimbo uliopigwa marufuku nchini na yeye akaserebuka kisawasawa kana kwamba hajui huo wimbo kuwa ulifungiwa. Ni ule wimbo wenye neno la stendi kuu ya mabasi ya mikoani Mwanza ila sio Buzuruga. Mind kwamba wimbo huo wa honey ni wa mburudishaji wa chama chao katika matukio yao hasa kampeni zao. Ina maana siku kampeni zikianza muimbaji huyo hataimba wimbo huo pendwa na wenye hamasa kubwa kuvutia wananchi kwenye kampeni zao?
 
sexual oriented gyrations haziruhusiwi mashuleni particularly for underage

msg sent to their mind unadhani ikoje? kwa underages.
Kukata viuno ni utamaduni wa pwani na ngoma hizo ni ngona za wakubwa na unahusishwa by 100% na ngono. Kwaheri!
Unafiki tu. Serikali hiyo hiyo kupitia wizara ya sanaa ndo imeruhusu wimbo upigwe maredioni na watoto wanaujua.

Si kweli kuwa walimu wanawafundisha ngono, Kwani umeona walimu wakiwafundisha kukata viuno hapo? Hao watoto wanafurahia tone ya mziki tu wala hawawazi unaloliwaza wewe. Kama wimbo hauna maadili haukupaswa kupigwa kwenye maredio.

Watoto wa zamani wameimba muhogo wa jagombe na hawakujua ni nn wao walifurahia tu wimbo.
 
Kwa hiyo kwa sababu mna sheria nyingi zinazo walinda ndiyo maana mnaona kufanya ujinga wenu ni halali kabisa!!?? Ebu tafakari kama mtu mzima kwanza! Hapa waziri anagusia kuhusu swala zima la malezi kwa watoto wetu!!
Kinachotutesa Watanzania tulio wengi ni hii tabia yetu sugu ya unafiki na kupenda kujikosha. Sasa hao walimu wakuu wamefanya ujinga gani hapo? Kama siyo tu huyo Waziri wenu Kilaza kukurupuka?

Na kama huo wimbo hauna maadili, kwa nini serikali yako kupitia Basata, hawaufungii? Mbona nyimbo zenye mlengo wa kukosoa madudu ya serikali zinafungiwa? Je, umeona hao watoto wanaocheza huo wimbo, wanafahamu maudhui yake?

NB: Ungana na mimi kwenye kusimamia ukweli. Serikali yako inaendekeza sana tabia ya double standard kwenye mambo ya msingi. Huyo Zuchu ni kibaraka wao wakati wa kampeni. Hivyo kama anaimba nyimbi zisizo na maadili, basi wasisite kuzifungia.
 
Siyo kila kinacho chezwa radioni,ni lazima kichezwe mashuleni!!
Unafiki tu. Watoto mziki umepigwa wanajua wimbo woote na wanaufurahia na wanaruka kwa furaha. Kwenye kampeni hapo yatapita magari na nyimbo hizo hizo.

Tuna unafiki sana sisi. Kama lengo ni watoto kuwa na maadili na wimbo hauna maadili kwanini upigwe kila sehemu? Unafiki wa kujifanya hatufanyi ngono ila watoto kila kona wanazaliwa.
 
Kinachotutesa Watanzania tulio wengi ni ni hii tabia yetu sugu ya unafiki na kupenda kujikosha. Sasa hao walimu wakuu wamefanya ujinga gani hapo? Kama siyo tu huyo Waziri wenu Kilaza kukurupuka?

Na kama huo wimbo hauna maafili, kwa nini serikali yako kupitia Basata, hawaufungii? Mbona nyimbo zenye mlengo wa kukosoa madudu ya serikali zinafungiwa? Je, umeona hao watoto wanacheza huo wimbo, wanafahamu maana halisi ya hayo maneno ya huo wimbo?

NB: Ungana na mimi kwenye kusimamia ukweli. Serikali yako inaendekeza sana tabia ya double standard kwenye mambo ya msingi. Huyo Zuchu ni kibaraka wao wakati wa kampeni. Hivyo kama anaimba nyimbi zisizo na maadili, basi wasisite kuzifungia.
Tuna UNAFIKI sana.
 
Kwanza ukuu wa shule haupunguzi mshahara na ni mzigo, kila mara safari za wilayani haziishi. Bora kuwa mwalimu wa kawaida as long as mshahara wa scale yangu unaingia. Mimi kama mwalimu niko macho na wageni wanaokuja shuleni kwangu no matter ni wakubwa zangu wa kazi wanakuja kufanya nini shuleni, je wataacha positive or negative kwa wanafunzi? Hawa wasiokuwa mabosi zangu ndio kabisa siruhusu wa represent kitu kilichowaleta mpaka nijiridhishe wametoka wapi na wamekubaliwa na mabosi wangu wa ngazi za juu. Hawa watoa misaada wanaokuja na vibe za nyimbo ndio niko macho zaidi kusikiliza nyimbo watakayoiweka. Uzuri ni mwalimu ninayefuatilia miziki kama yote duniani, ukiweka muziki wa wa kihuni/kilevi/kikahaba au muziki tata usiendana na mazingira ya kishule utalazimika kuuzima dakika ileile. Hawa vijana wanaoenda mashuleni kwa wanafunzi kwa shughuli zao huko wawe makini na nyimbo za ku play na hata mitindo ya mavazi wanayovaa. Shuleni ni vituo vya malezi bora
 
Hivi Watanzania akili tumemkopesha nani siku hizi? Huo wimbo una maadili gani ya kumfundisha mtoto? Umeyasilikiliza vizuri hayo maneno yanayotamkwa kwenye huo wimbo? Tunatetea vitu vya kijingaa
Unafiki. Huo wimbo watoto wanaujua mwanzo mwisho kwa kuwezeshwa na serikali kupitia wizara ya sanaa.

Kama hauna maadili kwanini ni wimbo maarufu? Kwamba kwa walimu kuucheza na watoto ndo watoto wameharibika? Watoto ambao wanaujua kuliko walimu? TUACHE UNAFIKI.
 
Mimi kama mwalimu mzoefu nachelea kusema kuwa waziri kakurupuka,shuleni sio mahali pa kujifunza ya darasani tu,kuna extra curriculum ambayo inajumlisha mambo hayo,huo wimbo wa kawaida sana,wasitake kutufanya walimu tuishi kama panya mashinoni

Kama wazirianaona hii comment imemkela na mimi anifukuze kazi,niko shule ya msingi mpigamiti wilaya ya liwale
Hii mpigamiti ifungiwe pia ,jina gani hilo[emoji16]
 

Attachments

  • images.jpeg
    images.jpeg
    40.1 KB · Views: 3
Walimu wana kosa gani? Baada ya nyie(wizara husika),kuona wimbo huo,mlichukua maamuzi gani? Wanajifunzia huko shuleni au mtaani? Kwa nini wazazi wao wasiwe wa kwanza kuwajibishwa kabla ya walimu? Na kwa nini huo wimbo usifungiwe?
 
makosa ya BASATA kutouzuia siyo warrant ya kuimbwa mashuleni. Unatumia common sense kama mwalimu Mkuu na mzazi. Issue ni audience ipi wimbo huo unaimbwa. Yes shulni si swa maana kule kuna mitaala na wale ni watoto wadogo
Kwani target ni nini? Mtoto awe na maadili ya kinafiki anapokuwa shuleni tu?.

Ndo maana wakikua wanakuwa na unafiki wa maadili kumbe ni majizi ya kalamu, mafisadi, mamalaya. Ni kwa sababu ya unafiki waliokuzwa nao. Mtoto anajua wimbo wote badala ya watu kujiuliza kwanini watoto wanajua verse za wimbo wote wanatafuta kiki za kisiasa.
 
Sasa jamani si ilikuwa ni event! Inakuwaje kwenye graduations huko?
 
Kuna ndugu zangu hawapigi nyimbo za kidunia nyumbani kwao, lakini nimeshangaa watoto wao wanaimba hizi nyimbo za kina zuchu mwanzo mwisho loh. Watoto wala hawawazi mnayoyawaza nyie.
Kumdhibiti mtoto kimaadili ni suala mtambuka inahusisha jamii kuanzia wazazi walezi, majirani, madereva, konda, marafiki nk kuwashusha cheo walimu kwasababu hii ni kuwaonea tu,
 
Wamewaonea tu, tuwaache watoto wawe watoto, wauishi utoto wao...
e
Enzi nakua tumeimba sana nyimbo za mdundiko....huku utu uzimani ndo nimejua ujumbe.

Pia wakumbuke kwenye Sanaa kuna fani na maudhui, watoto ni waumini wa fani.....ukute hawaelewi chochote, wao wako na vibe tu.
 
Kumdhibiti mtoto kimaadili ni suala mtambuka inahusisha jamii kuanzia wazazi walezi, majirani, madereva, konda, marafiki nk kuwashusha cheo walimu kwasababu hii ni kuwaonea tu,
Ni kweli, hao wanaosema eti jukumu la kumfunza mtoto ni la wazazi tu wanakosea.
 
Back
Top Bottom