Uwanja wa Ndege Dar: Mapokezi ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu - Julai 27, 2020
Siku zote huwa nasema ukisikia vurugu zimetokea kwenye maandamano au mikutano au shughuli zozote za vyama vya upinzani, jeshi la polisi ndio huwa chanzo cha kuanzisha vurugu hizo! Lakini pasipo jeshi kuanzisha vurugu huwa ni amani na salama salmini na hili limejidhihirisha katika mapokezi ya Lissu, Lait kama jeshi lingeyaingilia kati mapokezi yale kama jinsi lilichimba mkwara basi leo hii tungesikia madhara mengi sana huku mzigo wa lawama na makosa wakitwishwa wanachama wa CHADEMA ili tu waonekane wana hatia mbele ya macho ya sheria! Tusiruhusu utamaduni huu ukaota mizizi, nalipongeza jeshi la polisi utu waliouonyesha siku ya jana japo wengine wanasema ni sababu Bashite hayupo tena pale mbinguni alipokuwa akilitumia jeshi hilo kama mbwa wa kuwafuga nyumbani kwake! Yeye na viongozi wote wa aina yake namuomba Mungu awapotezee mbali kabisa!
 
Asanteni sana @tanpol !!! Tunawapenda SANA!! SISI ni watu wema!!! Tanzania ni YETU SOTE. Tusiruhusu maslahi ya WATU wachache watuvurugie UPENDO wa ASILI wa TAIFA LETU-Halima Mdee
Yawezekana kwa sababu mshauri mkuu na ambaye alikuwa anasikilizwa sana kaenda nchi za mbali kwa speed ya light.
 
Halima Mdee amefanya vyema leo kulipongeza jeshi la polisi, si vibaya chama kikatoa shukran rasmi kwa jeshi la polisi, hata kama ni kwa kinafiki. Pia nashauri sana Tundu Lisu ashauriwe kutokwenda kesho msibani. Kwangu bado Lisu ana hasira na lile shambulio, kwa vyovyote atataka kuionyesha serikali na hasa rais Magufuli kuwa amepona. Na mashabiki wake wanaweza kuonyesha furaha iliyopitiliza ambayo itaipa serekali sababu kuchukua maamuzi hasi dhidi ya cdm.

Kwakuwa wamemstahi leo, ni vyema angeachana na huo msiba, kuna nafasi kubwa ya kushindana na ccm. Na kama itawezekana kuanzia sasa Lisu pia ashauriwe asitumie lugha kali za kupandisha hamasa za chuki, bali apambane na ccm kwa sera. Kuna sehemu nyingi sana za kuwazidi ccm, mfano hii rushwa ya juzi kwenye chaguzi zao, ajira, ugumu wa maisha wa wananchi, demokrasia nk. Ni vyema apange vizuri mashambulizi yake kisiasa, kuliko kuonekana anapambana na mtu binafsi, kwa ajili ya shambulizi lake binafsi. Ni juu yetu wapinzani kutumia kukubalika kwa Lisu kwa njia chanya kuliko kuvutana
Lisu siku zote anaamini ili kuwafurahisha wafuasi wake ni lazima kutumia lugha kali, kejeli, na dhihaka.
 
Walikua wanatamani sana kumkamata na kuzuia huo msafara wa leo, ila walihofia dunia nzima inalitazama hili swala la Lissu kurudi nchini pia wananchi wangechukua sheria mkononi (Wangefanya vurugu kuvunja magari, maduka, wangevunja airport, wangechoma matairi na fujo nyingine).

Tusijidanganye eti polisi wetu wamejifunza kuwa na busara au hekima, hilo halipo, mazingira tu ya leo yamewabana polisi.
Mkuu kwani hao wanachi akili hizo za kufanya hayo kama Lisu angekamatwa hawakuwa nazo siku top ya viingizi wote wa chadema walipotiwa korokoroni?
 
Jana kulikuwa na mafuliko ya mapokezi ya Rais mtarajiwa. Ila cha ajabu magazeti na vyombo vyote vya habari viko bize na maombolezo ya mkapa.
 
Asanteni sana @tanpol !!! Tunawapenda SANA!! SISI ni watu wema!!! Tanzania ni YETU SOTE. Tusiruhusu maslahi ya WATU wachache watuvurugie UPENDO wa ASILI wa TAIFA LETU-Halima Mdee
Walipokea maelekezo wasiwaguse CHADEMA, wangepokea mengineyo wangeyafuata pia, siku hiizi kazi za usalama wa raia hazifanywi kiprofeshno, zinafanywa kwa maelekezo yatokanayo na utashi wa mtu, kile atakacho ndicho kinachofanywa
 
Lisu siku zote anaamini ili kuwafurahisha wafuasi wake ni lazima kutumia lugha kali, kejeli, na dhihaka.

Hizo lugha ziko vyama vyote. Ni juu ya kuelekezana kuwa vijembe na kejeli za hapa na pale ni sehemu ya siasa, ila visivuke mipaka, kwani sio kila mtu ni mvumilivu wa kiwango cha juu. Maana hata mimi ni mfuasi wake, na siafiki lugha kali zinazovuka mipaka.
 
Jana kulikuwa na mafuliko ya mapokezi ya Rais mtarajiwa. Ila cha ajabu magazeti na vyombo vyote vya habari viko bize na maombolezo ya mkapa.

Media nyingi Ni state owned, na zilizobaki Ni biased. Hii Ni hali ya kawaida sana kwenye nchi zenye serikali zinazotawala kwa mabavu.
 
1 JPM

2 LISU


3.MEMBE
Tusitegemee mchuano mkali kabisa kati ya jpm na mgombea mwingine yoyote kutoka vyama vya upinzani kwakuwa tayari sehemu kubwa ya utekelezaji wailani ya uchaguzi ya chama cha mapinduzi umetendeka, kadhalika na yale yaliomo katika ilani ya vyama vingine.
wanao Dhani lisu ataleta ushindani wanaudhaifu katika kumtazama lisu as presidential candidate, kwa sababu hoja nyingi za bwana lisu si zakuinua uchumi bali zakunusuru wapinzani na kiu ya raia si hiyo.

Kila la kheri Tanzania kila la kheri Mtanzania mlinda Amani
Wewe ndie msemaji wa Watanzania?
Kiu ya watanzania ni Haki, Uadilifu,na Nfasi ya kujiendeleza kimaisha.
Tundu lisu atafanya sehemu ya hilo,
na Zito kabwe atawaelekeza kwenye uchumi, unajuwa ni serikali shirikishi, Wapinzani tunapiga mande dhidi ya CCM maharamia wa Taifa.
 
Lissu ndiye rais wa Tanzania ajaye baada ya uchaguzi wa October.
Mkuu kwani hao wanachi akili hizo za kufanya hayo kama Lisu angekamatwa hawakuwa nazo siku top ya viingizi wote wa chadema walipotiwa korokoroni?
 
Back
Top Bottom