Uwanja wa Ndege Dar: Mapokezi ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu - Julai 27, 2020
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣

2467864_Ed7nRNcWkAAkZDF.jpg
wabongo siwawezi hakiamungu😛😛
 
Ondoa muwasho wako hapa Lisu hakuhusu wewe mla matembele
Hiyo story imeanza kuchosha na hiyo excitement ya leo kadri siku zitakavyoenda watu wakishamzoea atabaki Lissu wa kawaida.

Lissu hana hoja nyingine zaidi ya kusimulia mkasa wake campaign zimeingiliwa na msiba tu kwa upande wa pili lakini si mtu tishio kwao if anything Magufuli alikuwa ashinde kirahisi sana ujio wa Lissu ni blessing in disguise unawapa picha walau kuna upinzani maana kama ulikuwa umepoteza mvuto.

Muache Lissu achukue 15 minutes of fame sio muda mrefu excitement ya watu kumuona itaisha.

Hana quality za kuwa raisi wa Tanzania ni siku chache tu ataanza pinga pinga yake kuonyesha jinsi gani alivyo mweupe, maana hana hoja zaidi ra risasi 16 story ambayo imeanza kutuchosha.
 
Ukimwi umeua ndugu zangu wa karibu kabisa kuanzia mwaka 1992.

Na hata sasa ninao ambao ni waathirika.

Kuna mmoja ni mwathirika tokea 1988! Miaka 32 sasa.

Kuna wanachama wengi tu wa JF ambao walikuwa hawajazaliwa hiyo 88....

Pole sana Mkuu.
Swali langu ni je wakati wanazikwa, wakati wa kutoa historia fupi ya marehemu, umma uliambiwa kuwa kafa kwa Ukimwi? Au ilitumiwa euphemism ili kuepuka kutaja neno Ukimwi?
Hata mimi nimefiwa na wengi tu kutokana na Ukimwi. Na wote tulijua kuwa marehemu ni muathirika lakini makaburini tulikuwa tunaambiwa amekufa kwa pneumonia, presha au matatizo ya afya ya muda mrefu. Never Ukimwi. Ndio hivyo hivyo na hii Corona.

Amandla...
 
Toka saa 6 maelfu tulikuwepo JKNIA Ila hadi sasa tupo UFIPA na tumetembea kwa mguu huko njiani full shangwe na hatujachoka hakika huyu ni mbeba maono
 
Tuacheni masikhara TUNDU LISSU ANAPENDWA KUPITA MAELEZO
Hakika! Anapendwa haswa haswa mpaka jiwe linaona wivu!

Hakukuwa na uhamasishaji wowote badala yake kulikuwa na matishio kutoka polifisiem juu ya kuthubutu kusogelea eneo la JNIA lakini matokeo yake imetokea crowd kubwa sana!

Viva Lissu, viva mkombozi, Mungu mbariki Lissu, bariki wafuasi wake, ibariki Tz
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Yaani Magufuli anamzidi hoja Lissu? Hoja zenyewe Watanzania sitowaangusha na kupiga pushup!!

Wewe jamaa unachekesha sana,huyo Magufuli mpaka sasa anachotegemea ni vyombo vya ulinzi na usalama,na Tume ya Taifa ya Uchaguzi basi.

Magufuli alisukumiwa kwenye Uraisi akajikuta yupo Ikulu anashangaa shangaa tu hajui aanzie wapi ndiyo akaenda kuanzia kupiga deki kule feri na kufuta sherehe za Uhuru.
Hizo ndio akili zenu

Wazazi sasa hivi wanajivunia sio tu hakuna hada shule zinajengwa na kukaratibiwa nchi nzima.

Unaambiwa sasa hivi vimemo aviishi wizarani wazazi waliokuwa wanaona private dili sekondari leo wanapigania watoto zao waende shule Kongwe.

Huu mtiti sasa umeshuka primary hakuna mtoto kukaa chini wala madarasa kujazana.

Hakina Mbowe et al waliokuwepo washachoka na Magufuli kila wanapochungulia kuna kazi; Lissu ndio kaingia ngoja aione Tanzania mpya atachoka tu ata mwezi aufiki.

Sitegemei kingine kwa Lissu kwenye hoja zaidi ya risasi 16 vipi watanzania atawafanyia nini hana, next atarudi kuwa Lissu yule yule mzee wa kupinga tu.
 
Pole sana Mkuu.
Swali langu ni je wakati wanazikwa, wakati wa kutoa historia fupi ya marehemu, umma uliambiwa kuwa kafa kwa Ukimwi? Au ilitumiwa euphemism ili kuepuka kutaja neno Ukimwi?
Hata mimi nimefiwa na wengi tu kutokana na Ukimwi. Na wote tulijua kuwa marehemu ni muathirika lakini makaburini tulikuwa tunaambiwa amekufa kwa pneumonia, presha au matatizo ya afya ya muda mrefu. Never Ukimwi. Ndio hivyo hivyo na hii Corona.

Amandla...
Well, kwa upande wetu haikuwa siri. Vifo vyao havikuwa vya ghafla.

Hakuna ambacho kingewezekana kufichwa.

Dalili zote walikuwa nazo. Achilia mbali uthibitisho wa kisayansi.

Kwa vile hakuna ugonjwa unaoitwa UKIMWI, kilichowaua ni yale magonjwa nyemelezi yanayomnyemelea mtu kutokana na huo ukosefu au upungufu wa kinga.

Hivyo, hao ndugu waliugua kwa muda mrefu.

Haikuwa siri. Wote wawazungukao walijua.

Sababu za vifo zilikuwa ni ‘ugonjwa wa kisasa’.
 
Mbowe anaongea sasa hivi anasema tutumie dakika moja kumuombea Mkapa watu wanakataa waanza minong'ono
 
Tuombe mdahalo wa Lissu na Magufuli tafadhali. Tuone ni nani ataingia mitini!
Lissu ana hadhi ya kufanya mdahalo na Magufuli. Akitaka Mdahalo atapewa Mwigulu tu akampe hiyo entertainment; Magufuli has better thing to do kuliko kusikiliza story ambayo tushaisikia ya kupiga risasi 16 get over it Lissu tushasikia.
 
Binafsi sikuwa na matarajio ya kwenda uwanja wa taifa kwenye sherehe za kumuaga mpendwa wetu mkapa.

Na hii sio kwamba sikuona uthamani wake kama Rais mstaafu La hasha, Mkapa kafanya mengi mazuri na namuombea anakoenda Alazwe mahala pema.

Lakini kwa Lissu Kama atakuwa na Ratiba ya kwenda na Mimi lazima niwepo na hapa tayari Niko kwenye basi natoka mkoani nakuja Dar.

Mwaka 2015 nilimpa kura yangu namba one anayeongoza Sasa, mwaka huu sikutegemea kupiga kura lakini Kama Lissu akigombea nitasafiri kwenda nilikojiandikishia nikapige kura.

Naombeni kujua ratiba ya Lissu kesho kama atakuwepo kwenye uwanja wa Mkapa
 
Tukio la Kifo cha Mkapa limeleta Wageni wengi Wakubwa na Vyombo vingi vya Habari vya Kimataifa vinaangazia Tanzania hivyo Wanaliogopa hilo.

Kwahiyo kumbe si kweli kuwa cdm wanaoleta fujo, bali vyombo vya dola ndio huwa wanawafanyia ukamongo kisa wivu wa kisiasa?
 
Lissu amekaribishwa watu wanashangilia kaambiwa aongee muda anaotaka
 
Ukiangalia ule umati wa watu unajiuliza ikiwa barua za kuomba kibali zingekubaliwa Daresalam leo ingekuwaje.!
Ni wengi hawajafika kumpokea lissu kutokana na uoga wao.
Kinachosikitisha ni kuwa kumbe ni watanzania wengi sana wanaugulia maumivu moyoni.
Tulizoea kusema wanaoumia ni wale waliokuwa mafisadi enzi zile, lakini umri ulioonekana kwenye video mbalimbali za mapokezi ya lissu ni umri wa vijana ambao nadhani wengi wao hata hawajawahi kuwa kwenye ajira rasmi.- hii ni moja ya ajenda inayotakiwa kupewa kipaumbele na uongozi wa vyama vyote.
Hata waliokatwa na wajumbe majuzi wanamaumivu makali mno......... Km kawaida ya maccm kila mmoja ametoa rushwa lkn watu wamekula ZERO yaani Bashite kabisa au wamekula makonda
 
Back
Top Bottom