Video: Tundu Lissu atoa ufafanuzi wa hoja aliyoitoa Babati Aprili 26, 2024 kumjibu Fatma Karume kuhusu 'Ubaguzi na Muungano wetu'

Wangefunika kombe mwanaharamu apite, huu muungano wa kihuni kabisa, kumbe walishajinyofoa kwenye Muungano sasa wamerudi kutuuza
Halafu wanatuuza bila ya aibu kabisa!
Tundu Lissu kafunua kombe lote. Natumaini watu wataanza kuelewa tulipofikishwa na CCM hii.

Unajuwa tumefikafikaje huku?
CCM Bara (Tanganyika) imezidiwa ujanja na CCM Zanziba.
Viongozi wa CCM Bara, wengi ni wachumia tumbo; hakuna mmoja kati yao anayeweza kusimama na kutetea hoja inayokinzana na matakwa ya CCM Zanzibar. Matatizo yetu yanatoka huko.
 
Huyu dogo lisu watnzania hatumpendi ka nini. Arudi kwa hub wake mzungu man
 
Tatizo la ma ccm. Mkiona watu wanafundishwa kutumia akili zao vizuri, mnawatisha na vita. Kwani miungano mingapi imevunjwa hapa duniani? Mtaendelea kutawala kwa sababu ya mapungufu ya vyama vya upinzani, lakini hamuwezi zuia watu kuelimika na kutumia elimu zao kuwang'oa madarakani. Ni swala la muda tu
 
Hahaha, jilaumu mwenyewe kwa kuzaliwa na wazazi mbumbumbu, wenye uwezo mdogo kiakili, ukaenda shule badala ya kusoma ukakalia ujinga mwisho wa siku garbage in garbage out.
Ni akili yake tu mbovu. Wazazi hawahusiki hapo.
 
Wameamua kutufanyizia
Ni siku nyingi kidogo" wanatufanyizia."
Walipoamua kuwa na Bendera ya nchi yao na Katiba yao, nilijuwa tumeanza kufanyiziwa. Wakatangaza kabisa na mipaka ya nchi yao; kwamba chochote kitakachopatikana ndani ya mipaka hiyo, kama gesi au mafuta, hakuna mTanzania yeyote atakayedai utajiri huo unamhusu! Kuna kufanyiziwa zaidi ya hapo?
Labda kilichoshindikana ni kule kujiunga na Jumuia ya nchi za Kiislam. Hii nayo isingeshindikana kama si kelele nyingi toka nje ya CCM yenyewe.
 
Jibu hoja acha kuweweseka
 
Kwani hawataki nini? Tanganyika +Zanzibar=Tanzania.
Dr.Mwinyi rais wa Zanzibar
Samia S.Hassan Rais wa Tanzania.
Rais wa Tanganyika ni nani?
Tuungane tuvunje Zanzibar tu baki na Tanzania. Nchi moja Rais mmoja, au Nchi Tatu marais watatu.

Wanataka tupendane lakini hawataki tuongee mambo ya msingi.
 
Dah sijui nani kawafunua CDM!

Kama kuna hoja ambayo chama Kuu wanaiogopa na hawataki iongelewe ni Muungano.

Ukianisha kwa makini vipengere vya katiba ya zanzibar vinavyoonyesha namna Baraa inavyonywa katika mambo mtambuka kama mgawano wa mapato ya muungano, composition ya wabunge, uteuzi wa viongozi, ardhi, uraia n.k kuna jambo lisilo tarajiwa linaweza likatokea nchini.

Ili kuonyesha ukubwa wa tatizo na athari zake chama komavu kinapaswa kuainisha takwimu na facts kadhaa ikiwemo idadi za Wakuu wa mikoa, Wakuu wa wilaya, Mawaziri, wabunge, Majaji, Makatibu wakuu, RAS, DAS, DED, Wakuu wa Taasisi, na Mabalozi kutoka Zanzibar ambao wapo katika Serikali ya Jamuhuri. pia deni la serikali, mgawanyo wa fedha za mikopo, kugharamia muungano, mauzo ya umeme, mgawanyo makusanyo ya traa n.k. Ukianisha hizi takwimu na kuwaelewesha Wananchi kwa ufasaa, panaweza kuchimbika.

Kuna mwaka Mtikilaa aliitisha mkutano viwanja vya mnazi mmoja, akainisha facts za namna wahindi wanavyoinyonya bongo isivyo stahili. Umati uliokuwepo mnazi mmoja ulipandwa na ghadhabu na kuvamia maduka ya wahindi na kuanzisha ghasia isiyo ya kawaida.

Huyu bwana akiendelea kuanisha facts za dosari za muungano akijikita kwenye muungano tu, anaweza kusababisha jambo la jambo nchini. Cha msingi asichochee chuki na vurugu. Amani inapaswa kulindwa kwa gharama yoyote, hivyo kama kwa kuwasanua wananchi amani itatoweka basi ni bora tukaendelea kuwa kama tulivyo na tulivyokuwa.

Mungu atupiganie ili bongo nayo itoboe
 
Mheshimiwa Tundu Lissu ni ligi ingine kabisa.🙌🏿 Korido za Lumumba sasa hivi wanakaa wima, na kama wanalala mumo humo makazini, wanalala wima vilevile.
 
Lissu na Fatuma Karume kujibizana ni sawa kabisa. Wote ni pungufu wa akili.
 
Mh Lissu amefafanua mambo mengi ya msingi ambayo tulikuwa hatujui.

Kumbe mtanganyika ukiwa unaishi Zanzibar huruhusiwi kumiliki ardhi?

Sasa mbona hapa Kakonko nipo na wapemba wengi sana wanalima maharage na mazao mengine bila kubughuziwa?

Ebu tumsikilize MH Lissu.
Your browser is not able to display this video.
 
Zanzibar lazima ilindwe, otherwise Wazanzibar watamezwa.

Ukiamuwa kuwa mkweli wa nafsi yako kero za muungano usizijadili kwa mihemko, mimi kwanza ningependa Wazanzibar tuwape uhuru wao tunadumaza maendeleo yao.

Zanzibar nje ya muungano hata Dubai tutakuwa hatuendi tunamaliza mambo yetu Zanziba.

Machogo tunawafukarisha Wazanzibar kwa manufaa ya ccm.
 
mko soo petty ninyi watu, Zanzibar ina square meter > 2000 elfu mbili sasa mlitaka watu zaidi ya milioni 50 wakamiliki ardhi Zanzibar? hivi hamna matatizo mengine tangagiza zaidi ya obsession na Zanzibar? kwa mfano hata umeme au maji ya kunywa ambapo mmezungukwa na maziwa lkn hakuna maji?

kama mnataka ardhi kisiwani kwa nini hamuendi Mafia au Mafia siyo kisiwa? Kiko tanganyika 100% au sijui kilwa au hata ziwa viktoria lina visiwa pia? Mmemkosa hoja za kuongea kwenye nchi yenye kila aina ya shida?

too law kwa opposition party kuwa so petty …
 
Ulikua hujui peke yako , si uko bize na mangekimambi utajulia wapi
 
Mimi naona tofauti kidogo. Kilichopo sasa ni kutaka kuitawala Zanzibar na inapokuwa ngumu tunaanza kulialia. Inatafutwa gia ya kuenda kwenye serilkali moja, jambo ambalo WAZANZIBARI wengi hawalikubali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…