Watanzania tujiulize Maswali muhimu ya Kibiashara kuhusu bandari zetu kwa dunia ya leo

Mkuu, hili la bandari si ni la kimuungano?
Ndio Bandari ni suala la muungano ila wao wanasema kila mmoja atasimamia Bandari zake ndio maana zanzibar wana ZPC na kama munavoiita wenyewe Tanganyika na yenyewe TPA sawa
 
Leo umeacha kushambulia wanaopinga mkataba? Maana Tangu awali wanaopinga kwako walikuwa Wahaini?
Wanaopinga mkataba usiokuwepo ni wehu, nanikaona na mimi nikishndana wehu ntakuwa mwenhu zaidi.

1) Sasa hivi nielewavyo mimi DP World wala Dubai hawaendeshi bandari yetu yoyote, kweli siyo kweli?
 
Hapa hakuna tutakalojadili watu wa nakuja na maneno tu oo bandari yetu isiuzwe mtu kama huyo unamjibu nini?
 
Hapo mimi kidogo nitakueleza kuhusu hizo Bandari za zanzibar kwa nini hazimo wanasema masula ya Bandari kila mmoja anasimamia bandari zake
 
Mkuu 'Proved':, nashukuru kwa kunialika hapa kwenye mada hii, ambayo mwanzilishi wake..., aaahaaa; acha nisiende huko.

Kaandika vizuri, sasa sijui kama kweli anatafuta ufumbuzi wa haya maswala mazito yanayotukabili sasa hivi kama taifa, au ni gheresha tu, kama aliyofanya kwenye ile mada nyingine inayofanana na hii.

Maoni yangu (mchango) wangu kwenye maswala ya namna hii ni rahisi kabisa na wala sina kusita juu yake.

DP World, au mwingine yeyote anayetafuta biashara ya kuja kufanya hapa kwetu, akipata faida halali ya kazi yake , nasi tukipata manufaa ya uwekezaji wake bila kuhatarisha mali zetu... anakaribishwa sana.

Sijui kama kuna mTanzania anayekataa jambo kama hilo.
Mzozo uliopo na unaokwepwa kama ukoma na hawa wenzetu wanaokomalia huyu DP World, ni kama kwamba ni huyo huyo pekee ndiye anayeweza kufanya kazi hiyo kwa ufanisi, na hakuna mwingine yeyote anayeweza kama yeye. Kuweka ushahidi juu ya hili, ni kuwa huyu DP World hakushindanishwanna mwingine yeyote katika kuwania kazi hiyo.

Mbaya zaidi, ni hapo waTanzania wanaposoma yanayoitwa "Makubaliano" yaliyofikiwa baina ya Tanzania na hiyo nchi nyingine, anakotoka huyo DP World.
"Makubaliano" ambayo wengi wanayatafsiri kama "Mkataba" yanayo 'demand' kwa Tanzania kufanya mambo ambayo haijawahi kuyafanya tokea nchi yetu iwe huru. Haya ndiyo yanayowastua watu wengi na kuhoji, na sasa kupiga kelele kabisa kwa hofu kuwa raslimali zetu zinauzwa kwa wageni bila ya uwepo wa ukomo, na kupitia katika hali hiyo, nasi raia tunaingizwa kwenye mpango wa kuwatumikia hawa wageni kama watumwa wao.

Acha nisiandike mengi, kwa sababu hapa ninatiririka tu bila kupumua.

Nimalize kwa hili ninalolichukulia kuwa la muhimu zaidi kuliko yote niliyoandika huko juu; nalo ni hili:

Nchi yetu tumepata uhuru tokea 1961, tuna umri zaidi ya miaka 60 sasa. Sisi kama binaadam ni watu wenye umri mkubwa sasa.
Ninasikitika sana kwa viongozi wetu kutoona maana ya umri wetu huu. Tutakuwa wategemezi wa kufanyiwa mambo yetu, hata madogomadogo kama haya ya kuendesha bandari hadi lini?
Ni lini sisi tutaanza kufikiria angalao kujijengea uwezo, hata kama ni taratibu ili lengo likiwa kufanya mambo yalliyomo katika uwezo wetu?

TICTS tumekaa naye hapo bandarini takribani zaidi ya miaka 20 hivi. Hatukujifunza chochote kutoka kwake katika muda wote huo? Hii kazi ya bandari inaugumu kiasi gani hicho?

Hapana. Ninafahamu wapo waTanzania wenye uwezo kabisa wa kufanya kazi pale bandarini, ni wao wanaofanya kazi zote hadi sasa.
Juzijuzi tumesikia sifa bandari yetu ikionyesha ufanisi katika kazi zao. Serikali ilizisikia hizi habari? Serikali ilifanya juhudi gani kuwatia moyo hawa wazalendo ili ufanisi zaidi uendelee kuwepo hapo bandarini?

Tunachosikia sasa ni "mifumohaisomani", ndiyo maana lazima tumlete DP World asomeshe mifumo..., kwa masharti gani? Kuuza raslimali za waTanzania na kuwapeleka utumwani?

Watu wanasema hatuna pesa za kuwekeza pale, sawa; lakini mbona tumekopa WB ili kupapendezesha kabla hatujagawa chee kwa DP World?

Viongozi na watu vipofu wa akili wanasema waTanzania hawawezi kufanya chochote cha maana, ndiyo maana ni lazima tulete DP World afanye kazi.

Na mimi ninasema hivi, kwa mantiki hiyo hiyo, tunahitaji kuwaondoa akina Samia na serikali yake yote, tulete wenye uwezo wa kuendesha serikali kwa ufanisi zaidi.

Ukiona makosa humo ndani, fahamu kwamba nilikuwa ni kama nakimbia marathon wakati nikiyaandika haya.

Mkuu 'Proved', yangu ndiyo hayo. nakushukuru tena kwa kunialika hapa.
 
Bandari za tanganyika hatuwezi kukubali ziuzwe au zikodishwe na wazanzibar!
 
 
Sasa tumegeuka taifa la wajinga tusio na mwelekeo, kila mmoja anajitazama binafsi hajali jirani yake ana shida gani, wabunge wamegeuka walafi licha ya mishahara mikubwa na posho, lakini bado wanadanganyika kwa rushwa, tena mbaya zaidi, rushwa inayozitoa sadaka rasilimali za nchi yetu, hii kwangu ni laana.
 
Hizo unazoleta ni "assumptions" au Kiswahili "dhana". Mkataba wa awali ni wa mashirikiano ya maendeleo. Ikiwa kufayika mikataba ktokana na makubaliano hayo basi hiyo ni "guideline" a,bayo kuwa nayo hiyo unapata ulinzi wa mkataba wakp automatically kutokea Umoja wa Mayaifa inapotokea hitilafu yoyote ya nchi na nchi.

Ni njema kuwa nayo hiyo kuliko kuwawacha wafanya biashara wakaingie mkataba na wagfanya biashara wengine wa nje bila kuwa na "guoidelines" kama zilivyo hizpo kwenye makubaliano.


Tusifanye ujinga tulioufanya kwnye kuingia mkataba na TICYS, zimeingizwa nchi mule na wafanya biashara amabazo Tanzania ilikuwa haina makubaliano nazo ya mambo ya bandari. Mfano ilikuwemo mdani TICTS shirika la biashara la Wachina ambao na wao wna mkataba na kampuni ya kunedehsa bandanri ya Abu Dhabi, halafu wakaingizwa wengine wanaitwa Adabi, hata haieleweki wametokea, waoi, wewe uanwaelewa? Wana mkataba uliopitishwa kwa makubaliano yepi?


Miparaganyiko kama hiyo ndiyo huondolewa na haya makubaliano ya awali,

Hayo makubaliano yetu hayajaanzia hapo kwenye IGA, yalianzia kwenye MOU baina ya Dubai na Tanzania wakati Magufuli yupo hai, mama kayapeleka mbele zaidi yamefikia hatua ya IGA, sasa ni sisi kufayanya HGA kama Dubai wapo tayari. Ikisha HGA kuna mikataba sasa ya utebdaji baina ya mashirika au kampuni zitazoteuliwa na Yanzania na Dubai.

Ikiwa kuna shughuli zozote inazobidi zianze kabla ya HGA na Business Contracts basi kuna kitu kinaitwa MOY-U ambayo nadhani DR World na TPA wamekubaliana mambo ya kuboresha YEHAMA yaanze mradi pesa zipo, na nia ni kusubiri na kujadilianina mikataba mengine.


Natumai nimeeleweka.
 
Mimi FM NAUNGA MKONO BANDARI ZETU KUBINAFUSISHWA. The bottom line is watumishi wa umma kwa mujibu wa Labour laws za utumishi wa umma hawawezi na wameshindwa kuziendesha bandari zetu kibiashara na kwa ufanisi. Na hayo yamekuwa malalamiko ya muda mrefu. These guys are underperfoming. That is the fact. Biashara waachiwe private sector. DP W waje wawekeze na waendeshe biashara ya bandari kisasa. Sisi tumeshindwa.
 
Mimi FM NAUNGA MKONO BANDARI ZETU KUBINAFUSSHWA. The bottom line is watumishi wa umma kwa mujibu wa Labour laws za utumishi wa umma hawawezi na wameshindwa kuziendesha bandari zetu kibiashara na kwa ufanisi. Na hayo yamekuwa malalamiko ya muda mrefu. These guys are underperfoming. That is the fact. Biashara waachiwe private sector. DP W waje wawekeze na waendeshe biashara ya bandari kisasa. Sisi tumeshindwa.
 
Waulize wao serikali wameshindwa nn kuiboresha hii bandari kama Mombasa wameweza?.
 
Hayo ni mawazo yako na sina sababu ya kuyapinga kwa sababu pengine unayaelewa nisiyoyaelewa. Sasa turudi kwenye moja la kwanza:

1) Sasa hivi nielewavyo mimi DP World wala Dubai hawaendeshi bandari yetu yoyote, kweli siyo kweli?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…