Watu 12 wakamatwa kwa kula hadharani mchana Zanzibar
Sawa sawa ... Kwanza mkuu mi kiufupi na ndugu zangu tunaogopa sana maji..
Tutabaki huku huku aiseeee huko hapana ๐Ÿ™Œ๐Ÿ™Œ๐Ÿ™Œ๐Ÿ™Œ๐Ÿ™Œ๐Ÿ™Œ
Mi naenda mara kadhaa huko ila mwisho mwezi wa tano, wajinga wale wabaguzi sana
 
Mfahamu hapa inatumika hekima ya tamaduni sio dini.

Mfano kule ulaya kuna tamaduni matamasha ya LGBT jee hapa Tanzania wakisema waje wafanye mtakubali kwa tamaduni zenu?.
Mkuu, issue hapa ni uroho. Acheni uroho mkifunga, wwe umefunga kula alafu hutaki kuona watu wanakula eti wanakutamanisha sasa hapa si bora usifunge tu tena mnakamata mpaka mama ntilie wanaopikia ndani kwao
Alafu umetoa mfano hauna maana, ushoga sio utamaduni wa ulaya ni tabia imeanza recently kuleta vikundi kabla ya hapo haukukubalika na hata sasa wazungu sio wote wanaukubali, tamaduni ni tabia na mwenendo ambao umekubalika na jamii fulani kwa kipindi cha miaka mingi, vizazi na vizazi
 
Chukulia uko ofisini kwako karibia staff wenzako wengi wamefunga,,,je unaweza kula mbele yao? Busara tu ya kawaida itakuelekeza nini?
Kwani shida ipo wapi ? Mtu aliefunga kwa imani hata ukila mbele yake wala si tatizo, kafunga kwa imani sio kwamba kashinda njaa kama mtu anaefanya diet.
 
Zanzibar ina utaratibu wake iliyojiwekea kwakuwa asilimia kubwa ya wakazi wa kule waislamu,,,,haitakiwi kula hadharani period.

Je tunashindwa kuheshimu hilo kwa mwezi mmoja tu? Tatizo letu sisi tunaingiza udini hapa ukristo vs uislamu.

Lakini tukitoa hiyo kutu akilini kwetu tutaona kwamba hiyo sheria na lazima ifuatwe period.


Tuache kila siku kulialia Zanzibar zanzibar pumbavu!
Pumbavu mama yako..Udini tu
 
Zanzibar ni dola la kiislam?

serikali ya Zanzibar inaongozwa na katiba ya kiraia au Quran?

mahakama zinashtaki waliokamatwa wanakula wakiwemo wakristo kwa sheria za kiislam?


Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja Zanzibar ACP Abubakar Khamis Ally amesema Jeshi hilo litaendelea kuwakamata wale wote wataoonekana au kukutwa wakila chakula mchana hadharani katika mwezi huu mtukufu kwa waislam ramadhani.

ACP Abubakar Khamis Ally amenukuliwa na AyoTV akisema โ€œKwa mwezi huu kwa ramadhani kwa tamaduni ya Nchi hii hata sehemu za vyakula utakuta zimefungwa kwahiyo sio vyema wakakaa maeneo wakala hadharani hilo ni kosa na ndio maana tunawakamata na tutaendelea kuwakamata kwani inaleta kero kwa wengineโ€

Hadi sasa ni Watu 12 wamekamatwa kwa kosa hilo

MY TAKE:

Suala la mfungo wa Ramadhan ni la kidini sio utamaduni, kusema kwamba kwavile Zanzibar imejaa waislam ni utamaduni au utaratibu wao hivyo kila mtu afuate hata wasio waislam sio sawa, huu ni ubaguzi wa kidini, hivi kwakuwa bara wamejaa wakristo tukisema adhana zipigwe marufuku kwavile sio utaratibu wetu, hiki ni nini kama sio udini ? kitekelezwe kwakuwa ni utamaduni / utaratibu ? NO !!

huu ni mwezi mtukufu wa Ramadan kwa waumini lakini kuna wasio waumini huu mwezi kwao ni wa kawaida waachwe waendelee na maisha yao ya kawaida

Tanzania (bara na visiwani) ni nchi huru kila mtu ana uhuru wa kufanya anachotaka maadam havunji sheria za nchi (sio za dini), kila mtanzania ana haki ya kula hadharani .

Ile ni serikali ya mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) au serikali ya Kiislamu ya Zanzibar (SKZ)?
 
Kwani mi nikila wao imani yao inathirika na nini? Unafunga kumfurahisha mtu au Mungu wako?
Kuna utofuti wa kufunga na kufanya diet kwa kujifosi kushinda njaa, anaefunga hababaiki lakini anaefanya diet mnamuingiza tamaa ana haki ya kulalamika.
 
Si ijulikane tu kuwa serikali ya zanzibar ni ya kislam, sasa kama polisi inakamata watu wanaokula mchana huo ni uvunjifu wa haki za binadam

Wakiwapeleka mahakamani watawahukumu kwa sheria gani?
 
Mfahamu hapa inatumika hekima ya tamaduni sio dini.
Mfungo wa ramadhani ni suala la Dini sio tamaduni,ni jambo la ajabu sana kwa baadhi ya wazanzibari kujimilikisha suala hili la dini na wakadai eti ni utamaduni wao.
 
Chukulia uko ofisini kwako karibia staff wenzako wengi wamefunga,,,je unaweza kula mbele yao? Busara tu ya kawaida itakuelekeza nini?
Sasa ukajifiche wapi na upo ofisini ndani ?

Au utoke ukale nje ambako utaambiwa unakula hadharani mkuu ?

Katika uisilamu sio dhambi kula mbele ya mtu aliyefunga,bali dhambi ni kwa anayekula kama kaamua asifunge na sio atapata dhambi kwa kula mbele yako
 
Chukulia uko ofisini kwako karibia staff wenzako wengi wamefunga,,,je unaweza kula mbele yao? Busara tu ya kawaida itakuelekeza nini?
kwanini nishindwe kula mbele yao, kufunga wafunge wao tupateshida wote huu upuuzi wa wapi??

hii dini ya kiisilamu imekua tatizo kila sehemu duniani, hivi wa buddha wa hindu wa kristo nao wakianza vitu kama hivi hii dunia itakalika kweli??
 
Mfungo wa ramadhani ni suala la Dini sio tamaduni,ni jambo la ajabu sana kwa baadhi ya wazanzibari kujimilikisha suala hili la dini na wakadai eti ni utamaduni wao.
tatizo vichwa vyao vimejazwa elimu ahela tu
 
Back
Top Bottom