Watu 12 wakamatwa kwa kula hadharani mchana Zanzibar
Mfahamu hapa inatumika hekima ya tamaduni sio dini.

Mfano kule ulaya kuna tamaduni matamasha ya LGBT jee hapa Tanzania wakisema waje wafanye mtakubali kwa tamaduni zenu?.
LGBQT imeharamishwa na katiba ya Tanzania, kula hadharani wakati wowote hakujaharamishwa na katiba au sheria yoyote.
 
Zanzibar ina utaratibu wake iliyojiwekea kwakuwa asilimia kubwa ya wakazi wa kule waislamu,,,,haitakiwi kula hadharani period.

Je tunashindwa kuheshimu hilo kwa mwezi mmoja tu? Tatizo letu sisi tunaingiza udini hapa ukristo vs uislamu.

Lakini tukitoa hiyo kutu akilini kwetu tutaona kwamba hiyo sheria na lazima ifuatwe period.


Tuache kila siku kulialia Zanzibar zanzibar pumbavu!
Kwani hao wanaoukala hadharani wewe wanakuwasha nini wewe ambaye huli?? Si uendelee na mambo yako au unatamani na kumezea mate ukiona mtu anakula hadharani.
 
Ndio maana nimesema kama mtatazama kwa mlengo huo mtalialia kila siku
Na ukifuatilia hizi thread zinazoashiria udini udini zikianzishwa utaona zinapata wachangiaji wengi haraka sana kuliko zile thread zinazohusu wizi wa mali za Nchi au kuhusu maendeleo ya Nchi hii !

Ni ajabu na kweli Nchi hii ina chuki za kidini za chini kwa chini !

Na tabia hii ni faida kubwa kwa Chama tawala kwa sababu wakiona kuna mijadala ambayo inawaumiza wao basi chap chap watu wanaanzisha thread za udini udini biashara inaishia hapo 😅😅😅😂😂😂 !

Na muelewe kwamba ili muweze kuitoa madarakani CCM ni lazima Watu wa dini hizi mbili kubwa waheshimiane na kuwa kitu kimoja !
Lakini kwa bahati nzuri hayo maelewano hayatakuja kupatikana hivi karibuni kwa sababu bado watu wanadhani eti kula au kutokula hadharani nayo ni issue kubwa katika Nchi 😂😂🙄🙄

Kwakweli CCM mbele kwa mbele for another 100 years !! 😱
 
Usitufanye wajinga

jifunze kutofautisha kati ya sheria za dini na sheria za kiserikali.
hilo swala limekuwepo tokea utawala wa karume,

je karume alipitisha amri hiyo akiwa kama kiongozi wa kiislamu au kama kiongozi wa serikali ya mapinduzi.

Mjinga kama wewe unatakiwa ujiulize swali kama hilo
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja linawashikilia watu kumi na mbili kwa tuhuma za kukutwa wakila mchana hadharani kipindi hiki cha Mwezi mtukufu wa Ramadhan ambao wanaifanya kuwa idadi ya watu waliokamatwa kwa tuhuma za kutenda makosa mbalimbali kufikia sitini na mbili

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini magharibi Unguja Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Abubakar Khamis Ally amesema kufuatia video iliyosambaa mitandaoni ikiwaonesha baadhi ya watu katika eneo la viwanja vya mnazi mmoja Zanzibar wakila hadharani wakati wa mchana wa Ramadhani, Jeshi hilo lilifanya msako na kuwakamata watu wapatao kumi na mbili wakiwa na vielelezo ambapo amesema wanaendelea na taratibu nyengine ili kuwafikisha Mahakamani.

Aidha ameyataja makosa mengine ni pamoja na unyang’anyi, Madawa ya kulevya na makosa mengine ambapo watuhumiwa wanashikiliwa na Polisi na wengine tayari wameshahukumiwa Mahakamani.
Serikali ya Zanzibar na kadhi na balaza lake wanawahadaa waisilamu wajinga wasio jitambua hili wadhani serikali yao ni ya kidini kumbe uongo mtupu ndio maana baadhi ya watu hata wakimfahamu jirani yao anapika na kula mchana nyumbani kwake wanapiga simu hali yakuwa hakuna katazo hilo kwenye dini bali ni siasa tu

Tangu lini serikali ya Mapinduzi ikawa na dini

Mbona kuna wazungu wanatembea matako nje na chupa za maji mikononi mchana kweupe

Mbona kuna mabenki ya kukopesha kwa riba

Mbana kuna wateule wa rais na wabunge wanawake

Mbona pombe inayweke mahotelini nk

Mbona wakusanya kodi wanawapinga penapiga wafaidi wafanya biashara wanao chelewa kulipa kodi

Huyo raisi na mawaziri mbona mishahara yao mikubwa huku wananchi wanashindia mihogo na dagaa mchele

Mbona serikali ya Mapinduzi inakopa kwa riba

Mbona serikali ya Zanzibar inaongozwa na katiba ilio tungwa na bunge badala ya kuongozwa na qur,aan na Sunnah

Wazinifu awapigwi mawe na wengine kuchapwa bakora [emoji817]

Waisilamu wa Zanzibar muamke kutoka usingizini serikali yenu sio ya dini wala aiongozwi na dini bali katiba tu

Huyo kadhi wenu na masheikh wa mitaa ni waongo tu wanasiasa hao wanacho dhambi wanayo iyona ni ya mtu kula hadharani tu mbona haya mengine hawa yaoni waisilamu wa Zanzibar zinduka
 
kwa zanzibari wacheni walinde mila na desturi zao.
kinachotakiwa hapo ni kuheshimu utaratibu wao walio jiwekea ktk kipindi hiki cha mwezi mtukufu, kama unajiona huwezi kufuata utaratibu wao usiend au ondoka kwa muda huu.
 
acha ujinga wewe, kwani tanganyika haina waislam, iweje chakula kiliwe mchana kweupe kwenye migahawa iliyopo misikitini na walaji hawakamatwi? Zanzibar ina udini mwingi sana inapaswa kukemewa kwa hilo
Hicho kijamaa kijinga sana kinaonekana hakijielewi
 
Ishu ni kwamba zanzibar si nchi ya kiislam, kama vipi basi iwe ya kiislam, iwe kama Nigeria kaskazini palipo na sharia za kiislam. Sehemu hiyo ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iwe na sharia za kiislam na ijulikane hivyo kuliko kujifanya ni nchi ya kisekula huku inakumbatia udini/uislam. Udini ulikemewa sana Tanzania na hautakiwi kumea na kukua katika nchi isiyoongozwa kwa itikadi za kidini
 
jifunze kutofautisha kati ya sheria za dini na sheria za kiserikali.
hilo swala limekuwepo tokea utawala wa karume,

je karume alipitisha amri hiyo akiwa kama kiongozi wa kiislamu au kama kiongozi wa serikali ya mapinduzi.

Mjinga kama wewe unatakiwa ujiulize swali kama hilo
Amri ni Sheria? Hiyo siyo nchi ya kifalme kwamba asemalo Rais limeshapita,either wekeni hiyo Sheria Kwenye maandishi au kaeni kimya..
Punguani ww
 
Watanganyika waingie kwa wingi zanzibar wakakomeshe utamaduni wa kuzuia watu kula mchana kipindi hichi wanachodai wamefunga. Sheria na tamaduni za kipuuzi hazipaswi kuendelezwa
 
Adhana inamaana kubwa sana chief,,, ukiacha kuwaita watu Katika swala lkn ni ulingano ambao unamlingani mwanadamu amtambue Mola wake

Inatangaza ukubwa wa Mwenyezi Mungu, inatangaza hakuna mola mwingine apasae kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mungu mmoja tu wa kweli, hapa hakuna baba, mwana wala roho

Na inamtangaza Mtume ambaye ni wa mwisho na hatokuja mwingine naye ni muhammad, ambaye Mimi na wewe tunatakiwa kumfuata iii tuongoke.

Kwahiyo adhana ni ibada

Hilo unadhani mkiambiana misikitini kwenu haieleweki mpaka mpaze sauti kuubwa, isitoshe katika lugha ambayo watu wa eneo hilo hawaitambui? Hamuoni mnawakera wengine jambo ambalo linapoteza maana ya ibada?
Wewe kumpigia mtu makelele alfajiri kwa maneno ya kurudia rudia yasiyo eleweka kwa wengi unafikiri ni sawa?

Rwanda 🇷🇼 nasikia hakuna kero ya aina hiyo. Thanks to that government.
 
kwa zanzibari wacheni walinde mila na desturi zao.
kinachotakiwa hapo ni kuheshimu utaratibu wao walio jiwekea ktk kipindi hiki cha mwezi mtukufu, kama unajiona huwezi kufuata utaratibu wao usiend au ondoka kwa muda huu.
Kwani dhambi inayofanyika Zanzibar ni kula mchana wa ramadhani tu hizi nyingine wanamuachia nani?riba pombe uzinzi ushoga ufisadi?kama wameamua kama serikali imeamua kusimamia dini isichague dhambi zinazo tendwa na wanyonge tu
 
Back
Top Bottom