Waziri Jafo abadili gia angani, afuta maamuzi yote ya wasimamizi wa uchaguzi kuwaengua wagombea. Wagombea wote ruksa kushiriki uchaguzi

Hivi wewe unaishi wapi? unachokiandika huwa unakisoma kabla ya kupost? umejaa kutu ya ujinga usio na kifani
 

Sasa wale mlikuwa mnasema sheria inafiatwa ni sababu gani tena inafanya mbadilike. Uchaguzi huu mfumo mzima sio mzuri kiwekwe tume huru
 
Sinema zinazidi kushika hatamu
 
Wamejadiriana,wameona aibu inayokuja kwa hiyo wameona wawambie tu wagombee,hata kama umeshinda mpinzani atakaetangazwa ni kijani kama kawaida yao. Maoni yangu vyama wala visihangaike na uchaguzi huo kwa sasa. Waendelee tu mambo yao mengine,hili limeshapita. Hapo ujue inatafutwa damu.
 
Haitatokea CCM kususia uchaguzi...

Kuna kada kinda kinda nilikua napiga nae story leo...

Hata yeye mwenyewe amekua anasikitishwa sana kwa yanayoendelea...


Cc: mahondaw
 
Kelele zote zile kumbe waliochukua form kugombea kupitia Chadema ni asilimia 19% tu
.....hii ina maana ilikuwa haina upinzani kwa asilimia zaidi ya 80
Sasa data za fake news mbona uongozi wa chadema usema tofauti. Acha uongo😂
 
Pole pole ajitokeze alaani kitendo cha Jafo kujimwambafay na kurejesha wagombea ambao walikataliwa.

Jafo must go!
 
Taasisi za haki za binadamu za kimataifa na pia mahakama ya uhalifu wa kimataifa wamemwandikia barua waziri Jafu wakimuonya ajiandae kukabiliwa na kesi kwenye mahakama ya The Hague endapo kutatokea uvunjifu wa Amani.
 
Naona watu wanasahau kwamba wanarudishwa majina yao baada ya kulalamika kwamba tumewaonea, sasa na sisi imetuuma wagombea wetu tuliowapitisha bila kupingwa wanalazimika kupigania kura.

Kwa taarifa yenu mtatukuta tu huku kwenye kura, sisi ndio wasimamizi, mtarudi tu kwenye mdomo wa simba,hatujachoka kuwala.

Sasa mnadhani wasimamizi wa uchaguzi ni akina Nani zaidi ya sisi tuliowakata majina yenu?
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji16]Chinekeeeeeee
 
Uchaguzi wa serikali za mitaa umenajisiwa,hausafishiki kwa matangazo ya kwenye vyombo vya habari.
Ufutwe kabisa,Serikali ikae na vyama vya siasa kuona njia sahihi ya kufanya chaguzi hizi,lakini hii ya kusema wagombea waliofutwa wamerejeshwa si kweli,chaguzi hizi haziwezi kuwa huru asilani
 
Hujuma uchakachuaji vurugu za CCM bado vipo chini chini kwa msaada wa polisi lakini angalau sasa wananchi wachague hata mtu akiiba kura anakuwa akijua kichwani ndani ya nafsi kuwa siyo chaguo la wananchi, atakuwa akijishitukia na kutenda haki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…