Waziri Jafo abadili gia angani, afuta maamuzi yote ya wasimamizi wa uchaguzi kuwaengua wagombea. Wagombea wote ruksa kushiriki uchaguzi

Watanzania tutabaki gizani hadi pale mwana wa Israel atakapokuja kutimiza wajibu wake,hainiingii akilini Watanzania wote tumeridhia uchaguzi usimamiwe na serikali iliyopo madarakani ambapo na wao ni sehemu ya washindani,hovyo kabisa
 

Waliowaengua wagombea wa vyama vingine ni Marais wa kata , Jaffo n wewe Urais?
 

Umesema point! Siasa za Tanzania zinadhaminiwa na chama na kama chama kimeshajitoa, mgombea hana tena udhamini wa chama cha siasa. Anaweza kuwa mgombea binafsi lakini si katika fomu ambazo zilishakataliwa.

Sasa ndio kuna sababu nzuri ya kugomea uchaguzi kwa vyama vya siasa. Kama kweli wagombea hawakukidhi vigezo halali - uhalali wa kuwarejesha kupitia tamko uko wapi? Sasa ni dhahiri maamuzi mengi yalifanywa kwa hila!
 
Uchaguzi umefanyika tayari? Kuna form za kujaza kukubali matokeo. Sio kaa uchaguzi wa monita wa darasa la pili.
 

Yap. This was serious miscalculation on the part of ccm. Bila shaka kitakachofuata kutoka kwa washindani ni kutoshiriki uchaguzi wowote utakaosimamia na watendaji wa kata/vijiji au Wakurugenzi waliokula kiapo.
 
Mimi sijaelewa hoja gani ya kisheria imefuatwa kuwarejesha waliokatwa kisheria kama sheria nankanuni zilivyotumika kuwaondoa hapo awali.
 
mbowe atupe ukweli chadema imesimamisha wagombea wangapi?
Mbowe anahusika vipi kwenye tamko la Jafo?

Unaweza ukawa unapenda kuigiza kuwa mtu mpumba.vu, lakini usichokijua, ukifanya mara nyingi baadaye utakuwa mpum.bavu halisia.

Hapa watu wanajadili hoja ya msingi maana ni suala kikatiba na sheria pia. Je, kisheria waziri ana uwezo wa kumvua mtu aliyetangazwa kuwa mshindi katika uchaguzi wa serikali za mitaa? Sheria inasemaje? Hii ni hoja nzito, na inaweka precedence kwa siku za mbeleni. Kama hujui, kaa kimya ili ueleweshwe na wenye ufahamu.

Usiwe mtu wa kuropoka ropoka. Upu.mbavu siyo kitu cha kukifanyia mazoezi. Ukijizoesha baadaye utakuja kushtuka tayari ukiwa mpumb.avu kamili.
 
Tatizo njaa ya jafo maana anachofanya anatekeleza agizo la anaemtuma anaemini ndege ni maendeleo GUSSIE,
 
Jafo na genge lake wanataka tu wasaidiwe kubariki haramu. Lazima sheria ichukue mkondo wake kuepuka similar unfortunate incidents happening again siku za usoni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…