Waziri Jafo abadili gia angani, afuta maamuzi yote ya wasimamizi wa uchaguzi kuwaengua wagombea. Wagombea wote ruksa kushiriki uchaguzi

Wapinzani hawawezi kuingia kwenye uchaguzi kwa wasimamizi walewale wasiokuwa na ufahamu na demokrasia wanaopokea maelekezo bila ya kutafakari athari za hayo maelekezo kwa jamii inayowazunguka. Wasimamizi hawawezi aminika tena kwa jamii kwa haya waliyoyafanya.Upinzani unatakiwa ushikirie hapo wateuliwe wasimamizi wengine watakao malizia zoezi lilolobakia
 
Anaongea kwa kubabaika sana,hakutulia kabisa kitini...utadhani sio Yule chiriku tuliyemzoea..hahahahh
Hakuna kuweka mpira kwapani, hakuna kuweka mpira kwapani, hakuna kuweka mpira kwani....
 
Kwenye huu uchaguzi nilichogundua ni kuwa Chama kinachotaka kuwa mbadala wa CCM viongozi wake hawana hata uwezo wa kujaza fomu.
 
Wapinzani waliona watashindwa vibaya ikabidi wakimbie

Ila janja yao imestukiwa,hakuna kujitoa
Daaaa!! Yaaani mkuu wewe akili yako imeshikiliwa na watu wengine!! Yaani ni kufuata upepo tu!!! Toka juzi ulikuwa vingine leo baada ya jafo kuja kivingine na wewe tena umebadirisha gia angani!!
 
Jafo aeleze ni KIFUNGU kipi amekitumia katika kuwarudisha watu walio ondolewa kisheria. Vinginevyo aseme watu alio wateua kusimamia uchaguzi wameshindwa kuteleza majukumu yao ,wameonyesha udhaifu katika kusimamia sheria, miongozo na kanuni za uchaguzi. Hivyo akiri wamemwangusha,akisema hivyo wapinzani watamwelewa na watarudi
 
Serikali ilikata rufaa ushindi wa marehemu Christopher Mtikila kuhusu wagombea huru, na ikashinda, ikasema wagombea ni mali ya chama, chama kikijitoa maana yake hakuna mgombea.

Lakini inaonekana Jafo, anatamani wagombea huru, kutokana na tamko lake kwamba " Hakuna kujitoa, kila aliyejaza form atashiriki uchaguzi bila kujali matamko ya vyama vyao kujitoa"

Nami namshauri, akashauriane na mwanasheria mkuu na waziri wa sheria na katiba, wapeleke bungeni mabadiriko ya katiba kuruhusu wagombea huru.

Matamanio yake ni mazuri lakini chama chake hakiwezi kuruhusu na hakiwezi kukubaliana naye.

Wenzangu mnasemaje, tumuunge mkono Jafo, tuwe na wagombea huru, au tukubali vyama vijitoe na wagombea wao?!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…