Nilisema ni vilaza hajui kujaza fomu. Sasa tumeamua kuwaruhusu muendelee kugombea na ukilaza wenu tuone kama mtakubalika na wananchi mkuu. Tuko nyinyi tu mpaka kieleweke hakuna kukimbia kwa kisingizio cha kitoto. Pesa za wabunge wenu mmekula sasa mnaleta kisingizio sasa tuone sasa sijui kwenye kampeni mtatumia pesa gani wakati pesa za wabunge mlishakula nyinyi mafisadi.
Bado hutaki? Sasa utatoa kisingizio gani tena mkuu!!?
Basi wabadirishe katiba, wagombea huru iwe ruksa.Jaffo anapelekeshwa,remote ipo Magogoni
Chadema haina pesa za kampein ,vyovyote vile chadema kinakwenda kufa kifo cha kibudu
State agent
Basi mnyamaze! Tulijua tu mlikuwa mnatafuta kiki kwa mabeberu yenu tukagundua janja yenu!
Jafo na magufuli wake wanatapatapa tu.mimi huwa najiuliza kama magufuli pamoja na kwenda shule bado anatabia hizi zisizo za kistaarabu katika dunia ya watu waliostarabika,je asingekwenda shule angekuwaje ? Si ndo angekuwa kiongozi wa mashetani hapa duniani?Serikali ilikata rufaa ushindi wa marehemu Christopher Mtikila kuhusu wagombea huru, na ikashinda, ikasema wagombea ni mali ya chama, chama kikijitoa maana yake hakuna mgombea.
Lakini inaonekana Jafo, anatamani wagombea huru, kutokana na tamko lake kwamba " Hakuna kujitoa, kila aliyejaza form atashiriki uchaguzi bila kujali matamko ya vyama vyao kujitoa"
Nami namshauri, akashauriane na mwanasheria mkuu na waziri wa sheria na katiba, wapeleke bungeni mabadiriko ya katiba kuruhusu wagombea huru.
Matamanio yake ni mazuri lakini chama chake hakiwezi kuruhusu na hakiwezi kukubaliana naye.
Wenzangu mnasemaje, tumuunge mkono Jafo, tuwe na wagombea huru, au tukubali vyama ujitoe na wagombea wao?!
Wewe unatumika na nani?Chadema na ACT mnatumika na mabeberu.
Alafu mwishoni atatoswaJaffo anapelekeshwa,remote ipo Magogoni