Waziri Jafo abadili gia angani, afuta maamuzi yote ya wasimamizi wa uchaguzi kuwaengua wagombea. Wagombea wote ruksa kushiriki uchaguzi

Waziri Jafo abadili gia angani, afuta maamuzi yote ya wasimamizi wa uchaguzi kuwaengua wagombea. Wagombea wote ruksa kushiriki uchaguzi

Wapinzani msikubali ya Jafo huu ni mtego wa panya kula punje ya karanga maana hawa wasimamizi walio wakata ndio hao hao wasimamizi wa kutangaza mshindi.
Labda kuwe na maridhiano ya tume huru bila hivyo acha Serikali icheze kivyake.
Hongera wapinzani huu ni ushindi wa awali kwenu kazeni buti.
 
Washenzi huwezi kuwaamini hata siku moja. Kwaroho mbaya kabisa wanajifanya wamefuta maamuzi yao nia yao ni kuwasubiri mbele ya safari ya mchakato huu wawafanyie ile mbaya kabisa. Wasimamizi ni hao hao waliotuambia kuwa wapinzani hawafai. Mimi naona CCM iende mbele na vile vyama 11 wajuane wenyewe mbele kwa mbele. Bado dhamira yao ya kushinda kwa kishindo hata ikibidi kufunga goli la mkono iko palepale.
Watakao rubuniwa shauri yao hiyo 24.11.2019 mimi sifiki huko kwani sina uhakika na kura yangu kuthaminiwa.
 
Lile swali dogo ambalo sijajua limeenda wapi sasa limekuwa swali la msingi.

Je, Chadema watarudisha udhamini kwa wanachama wao waliorejeshwa kwenye uchaguzi?

Maendeleo hayana vyama!
kama wasimamizi wa uchaguzi waliwaengua wapinzani na waziri kapindua maamuzi kama kusukuma mlevi.... jee, waziri huyo huyo hawezi kupindua matokeo dhidi ya wapinzani watakapotangazwa na wasimamizi wale wale?
 
Viongozi wa dini ni wanafiki..
NO. HAWA NI WATU MAKINI. FUNGUA MACHO dada. soon tutapata suruhisho kupitia UTENDAJI WA HUYU BWANA MKUBWA WA IKULU ALIYEWEKWA NA MUNGU ILI MPANGO WAKE UTIMIE. VIONGOZI WA DINI HAWANA UBAVU WA KUPINGA MPANGO WA MUNGU.
 
Kinachotaka kufanyika ni kama kile kilichofanyika zanzibar Maalim Seif anajua walichomfanyia.

Wapiga kura walikuwa wachache lakini zilijalizwa vilivyo.

Kama mnakumbuka uandikishaji ulivyokuwa na idadi ikapaa ndani ya siku 3 yaani toka waliojiandikisha mil 3 hadi milioni 19 hapo kila mtu na akili yakeya kuelewa.

Jumlisha maagizo na semina elekezi iliyofanyika ikulu walipewa maagizo, ikaja Ras, Ded, Rc na Dc walitoa maagizo yao.

Kinachotaka kufanyika ni kuihadaa dunia kuwa walishiriki na walishindwa na sio kingine. Walicheza rough mwisho wa siku wamejikuta wako wenyewe aibu ikawajaa ndio maana wamekuja na jibu hilo.
2208717_tapatalk_1573287976466.jpeg
 
Eti anasema kama jina lilikatwa alafu ukaenda kushtaki eti jibu likitoka kuwa umeshinda basi jina lako litakuwa kwenye form ya wagombea..
Sasa najiuliza mtu ameshakatwa alafu chama chake kishajivua alafu jina mkaliweke kwenye form ya wagombea ina maana huyo mgombea atakuwa binafsi au??
Atakua ni mgombea wa kulipwa kama ilivyo kwenye mpira kuna mchezaji wa kulipwa
 
Hawajui siasa.. chuo cha kivukoni kirudi.

Mabavu siasa za kizamani sana.
Siasa za ulaghai zimefika mwisho Wananchi hatudanganyiki tena

Mimi nilijua huu ni mchezo wa upinzani kuepuka aibu ya kushindwa

Wamenusa harufu ya uchapakazi wa Magufuli anavyokubalika kwa Wananchi wakaona njia ya kuepuka aibu ni kujitoa kwenye Uchaguzi

Ila kwa kuwa Serkali inamkono mrefu ikawa imenasa huo mtego

Wengine walikosea kujaza fomu makusudi ili wasipitishwe

Ningeomba serkali iwarudishe wote hata wale wasio jua kusoma na kuandika
 
Siasa za ulaghai zimefika mwisho Wananchi hatudanganyiki tena

Mimi nilijua huu ni mchezo wa upinzani kuepuka aibu ya kushindwa

Wamenusa harufu ya uchapakazi wa Magufuli anavyokubalika kwa Wananchi wakaona njia ya kuepuka aibu ni kujitoa kwenye Uchaguzi

Ila kwa kuwa Serkali inamkono mrefu ikawa imenasa huo mtego

Wengine walikosea kujaza fomu makusudi ili wasipitishwe

Ningeomba serkali iwarudishe wote hata wale wasio jua kusoma na kuandika

sawa mama.
 
Siasa za ulaghai zimefika mwisho Wananchi hatudanganyiki tena

Mimi nilijua huu ni mchezo wa upinzani kuepuka aibu ya kushindwa

Wamenusa harufu ya uchapakazi wa Magufuli anavyokubalika kwa Wananchi wakaona njia ya kuepuka aibu ni kujitoa kwenye Uchaguzi

Ila kwa kuwa Serkali inamkono mrefu ikawa imenasa huo mtego

Wengine walikosea kujaza fomu makusudi ili wasipitishwe

Ningeomba serkali iwarudishe wote hata wale wasio jua kusoma na kuandika
Mmekwisha achiwa mshinde kwa kishindo, sasa mbona mnageuka kula matapishi yenu? Kama unafikiri kuna mtu anaamini uchaguzi utakuwa huru chini ya wasimamizi wale wale waliofurunda basi huyo mtu akapimwe akili yake. Mimi Masiya simo kabisa.
 
Kwa Mara Ya Kwanza Naona Serikali inatetereka Baada ya Vyama Pinzani kufanya Maamuzi! Safi sanaa Sasa Tusimamieee Wagombea wote kujitoa! Naipenda CCM ila kwa Walichofanya kwenye Huu uchaguzi hapana
Kila siku huwa nawaza kuwa ipo siku watawala watajichanganya na tutayashuudia yanayotokea nchi jirani, nao walianza hivihivi, yaani kukiuka miiko ya uongozi sababubza uroho tuu.
 
Jaffo siku chache kabla alitoa tamko akisema kukatwa kwa wagombea wa upinzabi ni rafu za kawaida ktk siasa. Na akadai wagombea wa upinzani wengi hawakufuata taratibu. Sasa nini leo kimemsukuma kuwarejesha? Wapinzani msikubali kamwe!!!!
 
Lile swali dogo ambalo sijajua limeenda wapi sasa limekuwa swali la msingi.

Je, Chadema watarudisha udhamini kwa wanachama wao waliorejeshwa kwenye uchaguzi?

Maendeleo hayana vyama!

..majina YOTE yanarudishwa?

..hakuna atakayepita bila kupingwa?

..vipi kuhusu zoezi la kuhesabu kura?

..nashauri uwekwe utaratibu unaokubaliwa na kila chama wa kukampeni, kupiga kura, kuhesabu kura,na kutangaza matokeo.
 
Lile swali dogo ambalo sijajua limeenda wapi sasa limekuwa swali la msingi.

Je, Chadema watarudisha udhamini kwa wanachama wao waliorejeshwa kwenye uchaguzi?

Maendeleo hayana vyama!
Wasifanye huo ujinga maana walio wakata ndio hao hao wasimamizi wa kutangaza mshindi.
 
Back
Top Bottom