Waziri Jafo abadili gia angani, afuta maamuzi yote ya wasimamizi wa uchaguzi kuwaengua wagombea. Wagombea wote ruksa kushiriki uchaguzi

Waziri Jafo abadili gia angani, afuta maamuzi yote ya wasimamizi wa uchaguzi kuwaengua wagombea. Wagombea wote ruksa kushiriki uchaguzi

Chadema nawakubali wanamwenyekiti mwenye akili sana na hazina ya Taifa hataki kutengeneza mazingira yavifo vyawaTanzania ,kisa uchanguzi
Waziri wa Nchi ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo ametangaza kuwaruhusu wagombea wote waliochukuwa fomu na kuzirejesha kwa ajili ya kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika nchini Tanzania Novemba 24, 2019 wanaruhusiwa kushiriki uchaguzi huo na amefuta maamuzi yote yaliyofanywa na wasimamizi wa uchaguzi Nchini kote ya kuwaengua wagombea wa vyama mbalimbali. Waziri Jafo ametoa uamuzi huu jijini Dodoma alipokuwa akizungumza na wanahabari leo.

Chanzo: Ukurasa wa OR-Tamisemi Facebook

 
Njama zao zimeshindwa vibaya sana,

Waendelee na Chaguzi zao ,wanajitoa ufahamu kila hatua wanapokea maagizo toka juu aibu sana kwa demokrasia ya vyama vingi.
 
Siasa za ulaghai zimefika mwisho Wananchi hatudanganyiki tena

Mimi nilijua huu ni mchezo wa upinzani kuepuka aibu ya kushindwa

Wamenusa harufu ya uchapakazi wa Magufuli anavyokubalika kwa Wananchi wakaona njia ya kuepuka aibu ni kujitoa kwenye Uchaguzi

Ila kwa kuwa Serkali inamkono mrefu ikawa imenasa huo mtego

Wengine walikosea kujaza fomu makusudi ili wasipitishwe

Ningeomba serkali iwarudishe wote hata wale wasio jua kusoma na kuandika
Nikusifu propaganda za kipumbavu unaziweza. Nahisi ulikuwa upinzani kabla na sasa unajipendekeza kuonesha umwenzetu.
Wote wakongwe wa siasa za kidemokrasia za CCM hawakubaliani na huu ubeberu magufuli alioupanga. Ma AT na WEO wamefanya kama alivyowataka wafanye.
 
Chadema nawakubali wanamwenyekiti mwenye akili sana na hazina ya Taifa hataki kutengeneza mazingira yavifo vyawaTanzania ,kisa uchanguzi
Craaaaap chadema act na chauma msirudi nyuma kwani lengo lao lilikuwa Nini? Mnavunja Sheria makusudi umma ukiamka ndio mnajirudi endeleeni na uchaguzi wenu maana tayari mna plan B baada ya plan A kushindwa mnatengeneza fitina kwenye taifa halafu mpaka tupige kelele pumbavu tungekaa kimya jeeee?

Mbowe na wenzako kamatia gia walishatingisha kiberiti acha tuone mwisho wake utabiri utimie tulijenja nyumba moja wakati wa kikwete sasahivi magufuli anatugombanisha tugombee fito go on
 
Tukutane kwenye kampeni sasa

Mkitoka hapo Hakuna kisingizio hata mkishindwa

Mchezo wa kitoto! Uchaguzi huu ikiwa ni pamoja na wasimamizi umeshakosa credibility. Nitashangaa sana hao waliojitoa wakitangaza kushiriki. Hili ni taifà; not a fiefdom. It is now crystal clear that there are very serious problems to be sorted out before this country can hold any credible elections. If the powers that be are not ready for consultations to restore credibility of the election process then let them run the show for as long as they wish. But for sure they will do untold damage to this once great country; Nyerere's country.
 
Kweli. Hapo ni danganya toto kwa pipi.

1. UPINZANI USIJARIBU KUENDELEA NA ZOEZI HILI.

2. ZOEZI LA UCHAGUZI LIBATILISHWE.

3. WATENDAJI WOTE WAFUKUZWE KAZI.

4. JAFO AJIUZULU MARA MOJA NA KAMA AMEHUSIKA KWENYE JINAI ASHTAKIWE.

5. UFANYIKE UANDIKISHAJI UPYA WA MAJINA.

6. USIMAMIZI WA UCHAGUZI KATIKA HATUA ZOTE UWE SHIRIKISHI. (Vyama vyote viweze kuhusika katika kuhakiki wanaojiandikisha).

Haya masharti yawekwe mezani!

Mbowe sio fala,wataweka haya masharti!

Upinzania wanajua kabisa sasa wana leverage kubwa mno!

Hakuna kuingia kwenye sanduku bila haya masharti kukubalika!
 
Pambana na maisha ya wananchi, CCM na Chadema hamfiki hata asilimia 11 ya watanzania

Sasa waziri Jafo jamii inakutazama kama kituko ambae hujui hatma ya maisha ya siasa zako za moto
Pole yake naona wajanja wamemuingiza mkenge, asipo angalia ndio atakuwa mbuzi wa kafara labda kama anapendwa kama kama DBA. Angesimamia haki toka mwanzo yasingemkuta, haipendezi mtu mzima kula matapishi ya chama chake.
 
Back
Top Bottom