Waziri Jafo abadili gia angani, afuta maamuzi yote ya wasimamizi wa uchaguzi kuwaengua wagombea. Wagombea wote ruksa kushiriki uchaguzi

Waziri Jafo abadili gia angani, afuta maamuzi yote ya wasimamizi wa uchaguzi kuwaengua wagombea. Wagombea wote ruksa kushiriki uchaguzi

Hii ndiyo tanzania, nchi ambayo inasadikiwa kuwa ilikuwa kitovu cha demokrasia afrika. Sasa ni nchi ambayo pia inadhaniwa kuwa demokrasia katika nchii hii umekufa
Na sababu kuu ni kuwa chama tawala CCM ambacho zamani kilijinasibu kuwa, kina mbinu 1000 za kushida uchaguzi. Sasa kimebanwa kiasi kuwa kinaitumia serikali yake kulazimisha mambo. Na bahati mbaya hata mawaziri nao wamekoswa mbinu. Wamebaki kutamka kile wao wanadhani ni jawabu kumbe si jawabu mbali ni jibu. na wamekoswa hata aibu leo wanalopoka hili kesho lile. NILIMSIKIA JOFO ANADAI KUWA, WAGOMBEA WA UPINZANI WAO NDIO WALIKOSEA KUJAZA FOMU
. NA KANUNI ZIMEWAONDOA MTU ALIYE JAZA FOMU VIBAYA. SWALI ANAWARUDISHA KWA KANUNI HIPI, VIPI KAMA AMEWEZA KUWARUDISHA KUPITIA MAMLAKA ALIYO PEWA VIPI AWEZI PIA KUAMURU KUWATANGAZA CCM KUWA NDIYO WASHINDI. Vyama vya upinzani kwa umoja wenu, uchaguzi huu uwafundishe kudai tume huru
Mkiingia kichwa kichwa mkakubali kushiriki uchaguzi huu, hakika yatawakuta na kamwe msifikirie kuwa wagombea wenu wakishinda watatangazwa. KUMBUKA WAHENGA WALISEMA, AKUMULIKAYE USIKU, MCHANA ATAKUCHOMA.
Hao unaowashauri wadai Tume huru ni Wabunge ambao walishinda mwaka 2015 na kutangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa Wabunge. Unachokizungumza kinakinzana na hali halisi ya mambo. Kama Tume sio huru wao walipataje nafasi zao?
 
Hatua muhimu kuliko zote

1. Tume huru ya uchaguzi
2. Siasa ziruhusiwe majukwaani kwa mujibu wa katiba
3. Katiba ya Jaji Warioba

Wasikubali kushiriki uchaguzi wowote bila hayo mambo matatu.
 
Kila anayekuja speed na kuonekana anaweza kuwa "fursa" kujijenga lazima abomolewe na adharaulike...
Mwisho wa siku tubaki na msifiwa mmoja tu asiyekosea...
 
Hao unaowashauri wadai Tume huru ni Wabunge ambao walishinda mwaka 2015 na kutangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa Wabunge. Unachokizungumza kinakinzana na hali halisi ya mambo. Kama Tume sio huru wao walipataje nafasi zao?
Wachache kupata siyo kwamba tume ndio huru. Hivi ni kuulize kuna tume huru?
 
😂 mpaka hapa Kama vyama pinzani vitakuwa imara kwa maslahi ya Demokrasia ninategemea kusikia wataingia katka uchaguzi huu pale tu Kuna tume huru ya uchaguzi hata ya mpito!!! Jaffo na watendaji wake warudi mtaani kunadi wagombea wao.

Vinginevyo hakuna uchaguzi na Dunia imeshajua Kuna uchafuzi tu.
 
Hao unaowashauri wadai Tume huru ni Wabunge ambao walishinda mwaka 2015 na kutangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa Wabunge. Unachokizungumza kinakinzana na hali halisi ya mambo. Kama Tume sio huru wao walipataje nafasi zao?
Narudia kusema wabunge walioko bungeni walipelekwa na nguvu ya Umma . Muda huo demokrasia bado ilikuwepo kabla hajaja Farao asiye mjua Yusufu. Kwa farao huyu, ambaye watu wamepotea wameuliwa, wanatekwa, wanabambikiziwa kesi, tena serikali yake ikawapa wahalifu jina WASIO JULIKANA.

Wadhubuti kama kwa tume hii kuna mbunge toka upinzani hataingi bunge ni, labda wa CUF NA TLP.

Tunapo badili masuala yake kitaifa MASHAULI tuyajadili kwa lengo la kusaidia na kuleta mustakakali wa taifa.
 
Hao unaowashauri wadai Tume huru ni Wabunge ambao walishinda mwaka 2015 na kutangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa Wabunge. Unachokizungumza kinakinzana na hali halisi ya mambo. Kama Tume sio huru wao walipataje nafasi zao?

Wakati huo Magufuli hakuwa rais na wakati huo demokrasia ilikuwa ina nafuu kwa mbali.
 
Tarehe 24 wananchi wanachagua wagombea ....yaani ile asilimia 32.
badala ya kuwahamasisha wapige kampeni nyie mko mtandaoni
Kweli JINGALAO 😂 ccm ilishapita bila kupingwa kampeni za Nini kawaapisheni tu.

Hatupigi kura bila tume huru ya uchaguzi.
 
Awamu hii viongozi hawafuati sheria wala katiba,wanafanya vyovyote watakavyo!! wapi Ben Saa8? Wapi Azory?
 
Huyu kijana hana ''future'' tena. Hana kingine cha ku-prove kwamba hafai hata kutajwa
 
Kwenda Unafiki tu huna lolote nyuz zako nyingi ni kujikomba komba tu
Siasa za ulaghai zimefika mwisho Wananchi hatudanganyiki tena

Mimi nilijua huu ni mchezo wa upinzani kuepuka aibu ya kushindwa

Wamenusa harufu ya uchapakazi wa Magufuli anavyokubalika kwa Wananchi wakaona njia ya kuepuka aibu ni kujitoa kwenye Uchaguzi

Ila kwa kuwa Serkali inamkono mrefu ikawa imenasa huo mtego

Wengine walikosea kujaza fomu makusudi ili wasipitishwe

Ningeomba serkali iwarudishe wote hata wale wasio jua kusoma na kuandika
Hovyo
 
Hili la watendaji kufunga ofisi kuwazuia wa gombea wa upinzani kuchukua fomu na wagombea wa upinzani kukamatwa na kuswekwa gerezani wakati wanakwenda kuchukua fomu na kuwafanya wagombea wengi kushindwa kuchukua fomu, haya yote hayaoni? au anataka kusema kuwa hata wale ambao walikuwa ni wagombea lakini wakashindwa kuchukua fomu kutokana na ofisi kufungwa nao wanahesabiwa kama wagombea watakaopigiwa kura?.
 
Mnaomlaumu Jafo mnamuonea tu. Ifike pahala tuyajue mawaziri mashenzi kama akina Lugola au Mwigulu (enzi zake). Jafo ana hekima sana hata kwa kumtazama lakini bwana yuleee ndiyo remote control.
 
Back
Top Bottom