Waziri Jafo abadili gia angani, afuta maamuzi yote ya wasimamizi wa uchaguzi kuwaengua wagombea. Wagombea wote ruksa kushiriki uchaguzi

Waziri Jafo abadili gia angani, afuta maamuzi yote ya wasimamizi wa uchaguzi kuwaengua wagombea. Wagombea wote ruksa kushiriki uchaguzi

Waziri wa Nchi ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo ametangaza kuwaruhusu wagombea wote waliochukuwa fomu na kuzirejesha kwa ajili ya kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika nchini Tanzania Novemba 24, 2019 wanaruhusiwa kushiriki uchaguzi huo na amefuta maamuzi yote yaliyofanywa na wasimamizi wa uchaguzi Nchini kote ya kuwaengua wagombea wa vyama mbalimbali. Waziri Jafo ametoa uamuzi huu jijini Dodoma alipokuwa akizungumza na wanahabari leo.

Chanzo: Ukurasa wa OR-Tamisemi Facebook


Hata hivyo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa nchini Tanzania (Tamisemi), Selemani Jafo ametangaza wenyeviti wa vijiji 6,248, wa mitaa 1169 na vitongoji 37,505 wanaotokana na CCM wamepita bila kupingwa baada ya kutojitokeza kwa wagombea kutoka vyama vya upinzani.


“Kwa upande wa vitongoji Chama cha Mapinduzi kimepita bila kupingwa katika vitongoji 37,505 kati ya vitongoji 64,384 sawa na asilimia 58,”

Amesema katika wajumbe wa kundi la wanawake jumla ya wajumbe 64,085 wamepita bila kupingwa na wajumbe kundi la mchanganyiko jumla ya wajumbe 75,560 wamepita bila kupingwa.

Swali muhimu: Je waziri ana haki kubatilisha maamuzi ya wasimamizi na kamati za rufaa za chaguzi hizi za serikali za mitaa? Ni kanuni zipi zinampa haki ya maamuzi aliyoyafanya? Au wanataka tu kuhalalisha batili? Unawezaje kuhakikisha wagombea kuwa waliowaengua watawatendea haki katika uchaguzi huo? CCM wanaonekana kukosa busara ya kimkakati waliyojisifia na 'kusifiwa' kuwa nayo hiko nyuma
 
Waziri wa Nchi ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo ametangaza kuwaruhusu wagombea wote waliochukuwa fomu na kuzirejesha kwa ajili ya kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika nchini Tanzania Novemba 24, 2019 wanaruhusiwa kushiriki uchaguzi huo na amefuta maamuzi yote yaliyofanywa na wasimamizi wa uchaguzi Nchini kote ya kuwaengua wagombea wa vyama mbalimbali. Waziri Jafo ametoa uamuzi huu jijini Dodoma alipokuwa akizungumza na wanahabari leo.

Chanzo: Ukurasa wa OR-Tamisemi Facebook


Hata hivyo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa nchini Tanzania (Tamisemi), Selemani Jafo ametangaza wenyeviti wa vijiji 6,248, wa mitaa 1169 na vitongoji 37,505 wanaotokana na CCM wamepita bila kupingwa baada ya kutojitokeza kwa wagombea kutoka vyama vya upinzani.


“Kwa upande wa vitongoji Chama cha Mapinduzi kimepita bila kupingwa katika vitongoji 37,505 kati ya vitongoji 64,384 sawa na asilimia 58,”

Amesema katika wajumbe wa kundi la wanawake jumla ya wajumbe 64,085 wamepita bila kupingwa na wajumbe kundi la mchanganyiko jumla ya wajumbe 75,560 wamepita bila kupingwa.

Safi sana.Jambo hili lilitukarahisha sana hata sisi wanachama wa CCM.People must be ruled by consent,not by force.
 
Mnaomlaumu Jafo mnamuonea tu. Ifike pahala tuyajue mawaziri mashenzi kama akina Lugola au Mwigulu (enzi zake). Jafo ana hekima sana hata kwa kumtazama lakini bwana yuleee ndiyo remote control.
Hekima ni pamoja na kudimamia unayoyaamini. Ukishindwa hayo una matatizo kama walivyo unaowasema.
 
We have lost sense and wisdom. We need to start afresh.
You are correct.That is why I admire our President,he has realized that we need to start afresh,and he is tying to do just that despite the resistance.
 
You are correct.That is why I admire our President,he has realized that we need to start afresh,and he is tying to do just that despite the resistance.
He probably is not doing it right. Those decisions are being done under his watch and with his concert. He should take responsibility and own both bad and good concequencies of the decidions taken and carrief out by his government. Nyerere did so when his ujamaa vilkage undertaking did not bear the expected results.
 
Hapa patamu sana sasa, mbowe, zitto, maalim seif leteni sera hawa jamaa wamesoma alama za nyakati
 
sasa wakati watendaji wanakata mbuga , hawakai ofisini ulifikiri walipewa likizo?.
wakati wanaandamana kutaka kujua kwa wakurugenzi watachukua hatua gani ilikuwa ni maigizo? ..
wakati waliotoa form zao copy na kisha ile original kukutwa imebadilishwa , sivyo ilivyoandikwa ilikuwa maigizo?
.... wakati TV zote zinaeleza sakata hili la watendaji kukimbia ofisi , wengine ni ndugu zetu wanavunjika na miguu kuwakimbia chadema ilikuwa ni maigizo?......

biblia yangu inaniambia ..mithali 25:21 ... adui yako akiwa na njaa mpe chakula ; tena akiwa na kiu mpe ,mpe maji ya kunywa.

chadema ni kusudi la Mungu , wametekeleza mapenzi ya Mungu ... kwa kuwapa chakula chao ccm , ambao wao wanaona wanastahili kushinda tu .wengine hawastahili.

zaburi 51:17 ....dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika .Moyo uliyovunjika na kupondeka eeh Mungu hutaudharau.

chadema sasa hivi mioyo imevunjika na kupondeka kwa ajili ya amani ya tanzania ... Mungu hawezi kuwaacha , maono haya lazima yatimie tu.. kikubwa kwa chadema ni kutulia . kwa sababu , biblia imesema ni laazima chadema mtulie ndiyo mnapopata nguvu msiyumbushe na wanachama wenu wakorofi .....isaya 30:15.

Mungu ni mwema sana kwa upande wa chadema .
 
He probably is not doing it right. Those decisions are being done under his watch and with his concert. He should take responsibility and own both bad and good concequencies of the decidions taken and carrief out by his government. Nyerere did so when his ujamaa vilkage undertaking did not bear the expected results.
I concur with you.There is obvious hesitation on the part of the President in taking prompt and right decisions.Jafos' decision is however the right step in the right direction,inspite of the fact that damage to the image of the government and CCM has already been done.
 
Hao unaowashauri wadai Tume huru ni Wabunge ambao walishinda mwaka 2015 na kutangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa Wabunge. Unachokizungumza kinakinzana na hali halisi ya mambo. Kama Tume sio huru wao walipataje nafasi zao?
Swali la kijinga sana, sasa embu niambie mwaka 2015 mikutano ya siasa ilikuwa imezuiwa? Na wabunge walikuwa wanafutwa na wengine kupigwa risasi mchana kweupe. ..
Au unazungumzia Tume hii hii yenye maelekezo yote kutoka kwa Chair wa CCM
 
Waziri wa Nchi ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo ametangaza kuwaruhusu wagombea wote waliochukuwa fomu na kuzirejesha kwa ajili ya kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika nchini Tanzania Novemba 24, 2019 wanaruhusiwa kushiriki uchaguzi huo na amefuta maamuzi yote yaliyofanywa na wasimamizi wa uchaguzi Nchini kote ya kuwaengua wagombea wa vyama mbalimbali. Waziri Jafo ametoa uamuzi huu jijini Dodoma alipokuwa akizungumza na wanahabari leo.

Chanzo: Ukurasa wa OR-Tamisemi Facebook


Hata hivyo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa nchini Tanzania (Tamisemi), Selemani Jafo ametangaza wenyeviti wa vijiji 6,248, wa mitaa 1169 na vitongoji 37,505 wanaotokana na CCM wamepita bila kupingwa baada ya kutojitokeza kwa wagombea kutoka vyama vya upinzani.


“Kwa upande wa vitongoji Chama cha Mapinduzi kimepita bila kupingwa katika vitongoji 37,505 kati ya vitongoji 64,384 sawa na asilimia 58,”

Amesema katika wajumbe wa kundi la wanawake jumla ya wajumbe 64,085 wamepita bila kupingwa na wajumbe kundi la mchanganyiko jumla ya wajumbe 75,560 wamepita bila kupingwa.



-----


Jafo awaruhusu wagombea wote nchini waliochukua fomu na kuzirejesha kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
View attachment 1260310
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo wagombea wote waliochukua na kurejesha fomu za kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa serikali za mitaa bila kujali kama walienguliwa isipokuwa kwa wale wasio raia wa Tanzania, hawakujiandikisha au wamejiandikisha mara mbili.

Ameyasema hayo leo wakati akiongea na waandishi wa Habari ofisini kwake Jijini Dodoma kuhusiana na mapingamizi na rufaa mbalimbali zilizotolewa wakati wa urejeshaji wa fomu katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Mhe. Jafo amesema kuwa hatua hiyo imetokana na kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambapo Waziri mwenye dhamana ya uchaguzi ana nafasi ya kutoa mwongozo wa jambo lolote kuhusu uchaguzi huo.

“ Kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019 Tangazo la Serikali Na. 371, Kanuni ya 49, Tangazao Na. 372 la mwaka 2019 Kanuni ya 51, Tangaza la Serikali Na. 373 la mwaka 2019 la mwaka 2019 Kanuni ya 52 na Tangazo la Serikali Na. 374 la mwaka 2019 kanuni ya 52 ninaotoa mwongozo kwamba wagombea wote ambao waliteuliwa na kudhaminiwa na vyama vyao na kufanikiwa kurejesha fomu zao za uteuzi kwa wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi katika kipindi kilichokuwa kimepangwa cha kuchukua na kurejesha fomu wanapewa sifa ya kupigiwa kura na wananchi.”

Amezitaja sababu ambazo hazitamruhusu mtu kugombea nafasi ya uongozi kuwa ni wale ambao watabainika kuwa wamejidhamini wenyewe, kutodhaminiwa na chama chake cha siasa, wagombea wawili wa chama kimoja kurejesha fomu katika nafasi moja na kama atakuwa amejitoa kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

“Nadhani ni habari njema kwa wale waliokuwa na madukuduku, mapingamizi sasa mambo yote yale tumeyaondoa ili mradi wamerejesha fomu zao lakini hawana pingamizi za uraia na mambo mengine niliyoyaeleza basi naelekeza wasimamizi na wasimamizi wasaidizi wawajumuishe kwa kuwa wamepewa sifa” amesema Mhe, Jafo.

Mhe. Jafo amesema hakuna kuweka mpira kwapani, hakuna kukimbia hapa mpaka kieleweke, kama mtu alirejesha fomu na hana makandokando niliyoyabainisha wote wamepewa sifa na watajumuisha kwenye wangombea wa uchaguzi.

Kuhusu Vyama vilivyojitoa Mhe. Jafo amesema kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi zinatambua kujitoa kwa mgombea na si Chama kujitoa hivyo mpaka sasa wagombea ambao walijaza fomu na kuzirejesha zikiwa zimedhaminiwa na vyama vya siasa wagombea hao wanatambulika kushiriki uchaguzi huo.

“Kama kuna chama kinataka kutoshiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa havikatazwi kuendelea kugoma kwani huwenda hiyo ndiyo aina ya demokrasia yao.”amefafanua Mhe. Jafo

Ameendelea kusema kuwa utaratibu wa uchukuaji na urejeshaji fomu, jumla ya wananchi 555,036 kutoka vyama vyenye usajili wa kudumu walifanikiwa kuchukua fomu za kugombea na kati ya hao wananchi 539,993 sawa na wasilimia 97.3 walifanikiwa kurejesha fomu zao.

Mhe. Jafo amesema wananchi walichukua fomu kutoka Chama cha Mapinduzi walikuwa ni 412,872 ikiwa ni asilimia 74 ya watu wote waliochukua fomu wakati Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) walikuwa ni 105,937 ambayo ni sawa na asilimia 19.

Amesema Chama cha Wananchi (CUF) walikuwa ni 24,592 ambao ni sawa na asilimia 4, ACT- Wazalendo walikuwa ni 8,526 ambao ni sawa na aslimia 1.5, NCCR-Mageuzi walikuwa ni 2,244 ambao ni asilimi 0.4 huku vyama vingine vyenye usajili wa kudumu walikuwa chini ya asilimi 0.1 kwa kila chama.

Hata hivyo Mhe. Jafo amesema mapingamizi na rufaa mbalimbali zipatazo 15,380 ziliwasilishwa katika kamati za rufaa kote nchini na kuwa baada ya uamuzi kutolewa rufaa 4,921 ambazo ni sawa na asilimi 32 ya rufaa zote zilitishwa.
“Baada ya maamuzi ya kamati, asilimia 32 ya rufaa hizo zilipitishwa lakini asilimi 68 ya rufaa zilikosa sifa kwa sababu mbalimbali kulingana na kanuni za uchaguzi.”amesema Mhe. Jafo

Mhe Jafo amefafanua kuwa katika machakto wa kuchukua na kurudisha fomu CCM iliweza kupita bila kupingwa katika maeneo mbalimbali kwa kuwa hapakuwa na mgombea yeyote kutoka vyama vingine vya siasa.

“Hii inamaana katika nafasi zilizoombwa katika baadhi ya maeneo, aliyechukua fomu na kurudisha fomu ni mgombea kutoka Chama cha Mapinduzi pekee na hakukuwa na mgombea yeyote kutoka vyama vingine vya siasa,” amesema Mhe. Jafo.

Akifafanua zaidi, Mhe Jafo amesema kwa upande wa nafasi ya wenyeviti wa vijiji CCM imepitwa bila kupingwa katika vijiji 6,248 kati ya vijiji 12,319 vilivyopo nchini ambayo ni sawa na asilimia 51.

Ameendelea kusema kuwa kwa upande wa wenyeviti wa mitaa, CCM imepita bila kupingwa katika mitaa 1,169 kati ya mitaa 4,263 iliyopo nchini ambayo ni sawa na asilimi 27 na kwa upande wa vitongoji CCM imepita bila kupingwa kwenye vitongoji 37,505 kati ya vitongozji 64,384 sawa na asilimia 58.

Mhe Jafo amesema kwa upande wa wajumbe wa kundi la wanawake jumla ya wajumbe 64,085 wamepita bila kupingwa na wajumbe kundi la mchanganyiko jumla ya wajumbe 75,560 wamepita bila kupingwa.

Aidha, Mhe.Jafo amevitaka vyama vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi huo kuhakikisha wanawasilisha ratiba za kampeni kwa wasimamizi wa uchaguzi

Kuna haja gani ya kuwa na sheria za uchaguzi kama mtu mmoja anayejiita Waziri wa TAMISEMI anaamua kubadili mambo jinsi anavyotaka?
 
Kuhusu Vyama vilivyojitoa Mhe. Jafo amesema kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi zinatambua kujitoa kwa mgombea na si Chama kujitoa hivyo mpaka sasa wagombea ambao walijaza fomu na kuzirejesha zikiwa zimedhaminiwa na vyama vya siasa wagombea hao wanatambulika kushiriki uchaguzi huo.
Hata kama mtu ameshachaguliwa, chama kilichomdhamini kikimfutia udhamini, anapoteza sifa ya kuwa kiongozi na hivyo hufanyika uchaguzi mpya kujaza nafasi hiyo; Je mheshimiwa huoni kuwa vyama vilivyotangaza kujitoa si vimefuta udhamini kwa wagombea wao? Mimi naona kama chama kimejitoa na hata baada ya kauli yako hii ya kuwarudisha wote, bado wanaendelea kujtoa, wasilazimishwe maana tukifanya hivyo wananchi wanaweza kuwachagua watu wasio na udhamini wa vyama na baadae tukalazimika kuingia kwenye gharama kubwa za uchaguzi mwingine
 
I concur with you.There is obvious hesitation on the part of the President in taking prompt and right decisions.Jafos' decision is however the right step in the right direction,inspite of the fact that damage to the image of the government and CCM has already been done.
Unafikiri Jafo kafanya hayo kwa maamuzi yake yeye binafsi au kaelekezwa baada ya kuona mambo si sahihi? Kinachotafutwa hapa ni kuhalalisha najisi...kisha tutaona maajabu zaidi kipindi kinachofuata. Very unfortunate.
 
Hata kama mtu ameshachaguliwa, chama kilichomdhamini kikimfutia udhamini, anapoteza sifa ya kuwa kiongozi na hivyo hufanyika uchaguzi mpya kujaza nafasi hiyo; Je mheshimiwa huoni kuwa vyama vilivyotangaza kujitoa si vimefuta udhamini kwa wagombea wao? Mimi naona kama chama kimejitoa na hata baada ya kauli yako hii ya kuwarudisha wote, bado wanaendelea kujtoa, wasilazimishwe maana tukifanya hivyo wananchi wanaweza kuwachagua watu wasio na udhamini wa vyama na baadae tukalazimika kuingia kwenye gharama kubwa za uchaguzi mwingine
Kinachotafutwa si uchaguzi bali kuhalalisha matokeo yaliyokwishapangwa. Msikilize Jafo kwa makini utagundua hili.
 
Wakati wa kurudisha fomu hawako ofisini kama ilivyotakiwa na maamuzi yao mmeyabariki kwa kuwapitisha wenzenu bila kupingwa

wale waliobahatika kurudisha mmewakata sasa hivi mnajifanya kuwarudisha kwenye gemu kuficha aibu yenu

Watanzania siyo wajinga na endeleeni kuwabagua wazungu wengine mkiwaita mabeberu na wengine mkiwaita marafiki zenu

Kwa maoni yangu sasa ifike wakati wa mtu kutopitishwa bila kupinga ili chama kimoja kikimpitisha mpumbavu asiwe kiongozi wa wananchi kwa lazima
 
Back
Top Bottom