Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Mbarawa azungumza kuhusu uwekezaji wa Bandari

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Mbarawa azungumza kuhusu uwekezaji wa Bandari

Ndugu Hamza acha upotoshaji, kwenye IGA ardhi imetajwa itagawiwa kwa mwekezaji, je ardhi si mali asili unaposema hakuna mali asili atakayo pewa? Bandari ina simama hewani? Maji ya bahati si mali asili? Msitumie upotoshaji.

Kama hamtaruhusu ardhi kumilikiwa basi ondoeni article 8 yote kwenye IGA
Hamza ni mzanzibar anadhana na wabara ni kama wazanzibar ni wavivu kusoma
 


Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa anazungumza na Waandishi wa Habari, Jijini Dar es Salaam muda huu kuhusu uwekezaji wa Bandari.

Mbarawa:
Pamoja na Serikali kuendeleza juhudi za maboresho ya Bandari zetu, bado ufanisi katika utoaji huduma wa Bandari haujafikia viwango vinavyotakiwa kimataifa.

Hali ya ufanisi wa Bandari ya Dar es Salaam na nyingine nyingi zinazoendeshwa na Mamlaka ya Bandari Tanzania upo chini sana, udhaifu huo unaonekana katika utendaji wa kila siku wa Bandari zetu pamoja na ukusanyaji wa mapato

Bandari ya Dar imeendelea kuwa nyuma dhidi ya Bandari shindani katika Kanda, mfano wastani wa meli kusubiri nangani ni siku 5 sawa na Saa 120 ikilinganishwa na siku 1 na saa 6 kwa bandari ya Mombasa.

Meli kutumia muda mrefu kupakia shehena kantini kwa wastani wa siku tano wakati kimataifa ni siku moja inayokubalika kimataifa.

Ufanisi mdogo wa Bandari ya Dar es Salaam umetokana na changamoto mbalimbali ikiwemo kukosekana mifumo ya kisasia ya TEHAMA, kutokuwepo kwa maeneo ya kutosha ndani na nje ya Bandari ya kuhifadhia shehena za mizigo pamoja na maegesho ya kutosha ya kuegeshea meli.

Changamoto nyingine ni kukosekana kwa mitambo ya kutosha na ya kisasa inayobadilika mara kwa mara kutokana na teknolojia na hivyo kuwa na gharama kubwa.

Athari za kutokuwa na ufanisi katika Bandari ya Dar es Salaam ni meli kusubiri muda mrefu nangani, mfano gharama ya meli kusubiri nangani kwa siku moja ni takribani Dola 25,000 (Tsh. Milioni 58).

Meli kutumia wastani wa siku tano kupakia na kupakua shehena ukilinganisha na siku 1 inayokubalika kimataifa.

Meli kubwa kutokuja katika Bandari ya Dar es Salaam kutokana na kuchukua muda mrefu kuhudumiwa, hivyo kusababisha bandari yetu kuwa inayolishwa na Bandari nyingine.

Uwezo mdogo wa Bandari ya Dar unaikosesha Nchi mapato makubwa ambayo yangeweza kusaidia katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayoendelea kutekelezwa Nchini.

Ili kutoendelea na hali hiyo, Serikali iliingia makubaliano 2000 Serikali ya Awamu ya Tatu iliingia mkataba wa upangaji na uendeshaji na Kampuni ya TICTS, mkataba ambao ulidumu kwa miaka 22 na kuipa haki za kipekee TICTS kuendesha shughuli za gati namba 8 hadi 11 za Bandari ya Dar es Salaam huku maeneo mengine yakihudumiwa na TPA.

Desemba 2022, Serikali ya Awamu ya 6 baada ya kuona mkataba hauendani na maslahi mapana ya Nchi yetu iliamua kusitisha mkataba huo.

Serikali kupitia Mamlaka ya Bandari Tanzania ilipokea mapendekezo ya wawekezaji mbalimbali Duniani, lengo kuu likiwa ni kufungua masoko ya kimkakati katika kufungua eneo la bidhaa na usafirishaji ndani ya Nchi na maeneo yanayotuzunguka.

Baada ya uchambuzi wa kina Serikali ilianzisha majadiliano na Kampuni ya DP World kwa sababu zifuatazo:

Uwezo mkubwa wa uendeshaji wa shughuli za Bandari Afrika, Asia, Ulaya, Marekani ya Kaskazini na Kusini na Australia.

DP World ina uwezo na kuchagiza mnyororo mzima wa usafirishaji kutoka maeneo ambapo bidhaa zinatoka hadi kwa walaji wa bidhaa.

DP World inamiliki zaidi ya meli 400 za mizigo, ina uzoefu wa uendeshaji wa Bandari 6 Afrika na zaidi ya Bandari 30 Duniani kote.

Wawekezaji wengine waliowasilisha mapendekezo yao hayakukidhi sifa kwa mwekezaji ambaye alihitajika.
Tatizo haliko kwenye mwekezaji, tatizo liko kwenye utata wa mkataba. Kwa muda gani? Bandari zote Tanganyika,au baadhi ya bandari? Kwa Nini iwe bandari za Tanganyika tu na kuziengua za Zanzibar? Waziri afafanue utata wa mkataba, wawekezaji tunawataka.
 
Hamza:Mkataba haukupelekwa kimwendokasi,ulifuata utaratibu
 
Hamza:Serikali inaamini Mkataba/makubaliano yapo sahihi,
 
Lugha ya Kiswahili inatupa ukakasi kwani haitoi tafsiri sahihi ya huu Mkataba/makubaliano
Treaty v Contract!?
 
Watu wamegoma kuwaachia,,Watz wamekuwa ruba,,,Wamekuwa wakali na vya kwao na si dhambi wanastahili sana kuvipagania kwa nguvu na kwa juhudi zote,,,,Viongozi wetu ni vizuri wangekuwa wanasoma alama za nyakati,,Kuishi kwa kujali na kuthamini nyakati ni jambo moja Bora Sana na la msingi mnoo katika kuishi na kuyajenga maisha Yaliyo Bora!!
 
Uharaka kwa kukimbilia bungeni ili Bunge kutoa Azimio tarehe 10 June 2023 bila kutoa nafasi wananchi na wadau kujadili suala la bandari

Ibara 63 (3) (e) ya Katiba ya Tanzania mikataba ya kimataifa ya inatamka hatua gani ifuatwe. Na inatakiwa Mchakato wa ndani ufikishwe baraza la mawaziri halafu inakwenda bungeni na bunge linatakiwa kuomba maoni kutoka kwa wananchi kabla ya kutoa Azimio la Kuunga mkono


TOKA MAKTABA barua ya Mwaliko kwa wadau

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
BUNGE LA TANZANIA
Simu: +255 026 23222761-5
Fax No. +255 026 2322624
E-mail: cna@bunge.go.tz
TAARIFA KWA UMMA
Ofisi ya Bunge,
S.L.P. 941,
DODOMA.

Kamati ya Pamoja (Joint Committee) ya Bunge ya Miundombinu na ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) inawaalika wadau kutoa maoni kuhusu Azimio la Bunge kuhusu Mapendekezo ya Kuridhia Makubaliano kati ya Serikali
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Dubai
kuhusu Ushirikiano wa Kiuchumi na Kijamii kwa ajili ya Uendelezaji na Uboreshaji wa Utendaji Kazi wa Bandari Tanzania la Mwaka 2023(Intergovernmental Agreement – IGA , between the United Republic of Tanzania and the Emirate of Dubai concerning Economic and Social Partnership for the Development and Improving Performance of Ports in Tanzania).

Mkutano wa kupokea na kusikiliza maoni ya wadau (Public Hearing) utafanyika siku ya Jumanne tarehe 06, Juni saa 7:30 mchana katika Ukumbi wa Msekwa ‘D’, Ofisi ya Bunge, Jijini Dodoma.

Kamati inawaalika watu wote wenye maoni kuhusu Azimio hilo kufika na kuwasilisha maoni yao kabla haujapelekwa katika hatua nyingine.

Vilevile Kamati itapokea maoni kwa njia ya Posta au Barua pepe kwa anuani ifuatayo:-

Katibu wa Bunge, Ofisi ya Bunge,
10 Barabara ya Morogoro
S.L.P. 941,
40490 Tambukareli
DODOMA.
Baruapepe: cna@bunge.go.tz na kamati@bunge.go.tz

Azimio hilo linaweza pia kupakuliwa katika tovuti ya Bunge,
www.bunge.go.tz. Aidha, unashauriwa kuwasilisha jina lako kupitia barua pepe tajwa endapo utapenda kuwasilisha maoni yako kwa kuzungumza kwa ajili ya
hatua za kiutawala.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa,
Ofisi ya Bunge,
S.L.P 941,
DODOMA
 
Watu wamegoma kuwaachia,,Watz wamekuwa ruba,,,Wamekuwa wakali na vya kwao na si dhambi wanastahili sana kuvipagania kwa nguvu na kwa juhudi zote,,,,Viongozi wetu ni vizuri wangekuwa wanasoma alama za nyakati,,Kuishi kwa kujali na kuthamini nyakati ni jambo moja Bora Sana na la msingi mnoo katika kuishi na kuyajenga maisha Yaliyo Bora!!
Watanzania wamechafukwa
 
Back
Top Bottom