Wenye familia na watoto mnawezaje kutazama Runinga nyumbani?

Wenye familia na watoto mnawezaje kutazama Runinga nyumbani?

Baba kama Baba ukifika ndani watoto rimoti wanapaswa wakukabidhi wewe

Unaangalia unachokitaka hiyo ndo maana ya mtawala

Shida uzungu unawasumbua

Ukiwa haupo tv ni yao ila ukifika tv ni ya kwako
Ushamba tu. Watoto watakuchukia bure.

Kwanza jitu zima unaangalia tv ya nini? Kama ni mpira kaangalie vibandani na wenzako!

Waache watoto wajimwaye mwaye waangalie tv wanavyotaka!
 
Hawa ni wababa wa enzi za ukoloni. Ni washamba na wanavaa MAYENU.

Kwanini usiwaache watoto wakaangalia katuni zao wewe uende chumbani ukasali hata rozari?

Watoto hawana raha, libaba linabadilisha tu chaneli! Khaaa!!!

Hili nalo mkalitazame!

cc Lamomy cocastic fundi bishoo Extrovert
waite upendavyo lakini kwangu mimi sio washamba

washamba ni wababa wa siku hizi ndio maana mashoga wameongezeka
 
B
Eti?

Unarudi nyumbani unakuta watoto wanatazama katuni zao kwa raha zao, au tamthilia pendwa za kike..... unawezaje kubadili chaneli bila kuonekana katili?

Tuseme muda wa Taarifa ya Habari, au hata mechi pendwa za soka..... ukibadili channeli watoto hao wanakukimbia sebuleni unabaki mwenyewe.

Hujisikii vibaya?

Hapa ndo umuhimu wa kupitia maeneo fulani kabla ya kurudi nyumbani, wenzetu mnawezaje?
kazi niliyobakia nayo ni kuwalipia vifurushi tuu ila kutumia TV yao nimekwisha Acha. Tamthilia zao zinagongana na musa wa vipindi muhimu kwangu. Acha wale jasho la baba.
 
Mimi ilikuwa ikifika saambili usiku namwachia Mama rimoti ili apitie ITV

Personally nyumabani taarifa ya habari ilikuwa lazima itazamwe doesn't matter mama yupo au hayupo.

Then watoto wajengee library room TV wawe wanaangalia kila jumapili tu
""Then watoto wajengee library room TV wawe wanaangalia kila jumapili tu"""
Dr mbona utakua kauzu sana 😂😂😂
 
TV siyo ya kuwaachia watoto,nakumbuka miaka ya 90 mwanzoni tukitizama wazungu videoni wakinyonyana ndimi tuliona uchafu,lakini Leo kila mtu analilia denda,mavazi ya mabinti leo tv Zina ushawishi mkubwa,namna tunavyojamiiana Leo ni matokeo ya tv,tv ni shule ovu isiyo rasmi,usiiache iwe mwalimu wa wanao
Uwez kuwaazuia,waachi wacheze ma game yao uko
 
We jamaa,weka muda wa watoto kukaa kwenye tv,saa mbili usiku baada ya kula ni kujisomea walau kwa saa moja unusu,Kisha kulala,siyo ajaze akina sharka na scoob doo kichwani


Ninacho fahamu mimi akitoka kwenye tv atakuwa anafikiria alichotoka kuangalia tena wakati wa kusoma ndio muda mzuri wakuwaza kuhusu tamthilia tena kama iliishia sehemu nzuri basi hapo ndioo kabsaa 😂😂 ila inategemea na mtoto mwenyew nikikumbuka mimi mwenyewe huwa nilikuwa siwezi soma nikitoka kuangalia movie ilikuwa nikulala tu
 
Kama mimi ndo mtoto huwa najiskia vibaya sana..
Mfano father yeye akija tuu
""Weka TV iman hapo mnaangalia angalia miziki ndo mnajifunza nini ""

Mda huo mtakaa ndani kimya
Wakati tunakua hatukuwa na tv ila radio ilikuwepo ilikuwa tunafuatilia sana vipindi vyote vya radio za kimataifa bila hata kujua kinaongelewa nini kipindi hicho ndiyo kwanza hata kiswahili hujui.

Ila ukiwepo Mpira mzee atawaelewa ataweka mpira miaka hiyo TBC walikuwa wanatangaza mechi za Simba na Yanga tu.

Nilipoanza kujitambua kitu cha kwanza kununua ilikuwa ni radio ili nisikilize ninachotaka mimi bila kumuona mzee miyeyusho na DW na VOA zake
 
Ushamba tu. Watoto watakuchukia bure.

Kwanza jitu zima unaangalia tv ya nini? Kama ni mpira kaangalie vibandani na wenzako!

Waache watoto wajimwaye mwaye waangalie tv wanavyotaka!
kitendo cha kuacha watoto wajimwaye mwaye ndio ushamba wenyewe

mwisho wa siku kauli ya 'watoto wa siku hizi hawana maadili'

kumbe maadili tunayaharibu wenyewe
 
Eti?

Unarudi nyumbani unakuta watoto wanatazama katuni zao kwa raha zao, au tamthilia pendwa za kike..... unawezaje kubadili chaneli bila kuonekana katili?

Tuseme muda wa Taarifa ya Habari, au hata mechi pendwa za soka..... ukibadili channeli watoto hao wanakukimbia sebuleni unabaki mwenyewe.

Hujisikii vibaya?

Hapa ndo umuhimu wa kupitia maeneo fulani kabla ya kurudi nyumbani, wenzetu mnawezaje?
Nunua Tv weka chumbani kwako
 
Ninacho fahamu mimi akitoka kwenye tv atakuwa anafikiria alichotoka kuangalia tena wakati wa kusoma ndio muda mzuri wakuwaza kuhusu tamthilia tena kama iliishia sehemu nzuri basi hapo ndioo kabsaa 😂😂 ila inategemea na mtoto mwenyew nikikumbuka mimi mwenyewe huwa nilikuwa siwezi soma nikitoka kuangalia movie ilikuwa nikulala tu
Yaani TV mwisho saa Tano asubuhi,jioni kusaidia mapishi,wa kiume akacheze mpira,saa moja unusu kula,saa mbili Hadi nne kusoma,na nauliza maswali walichosoma
 
Baba kama Baba ukifika ndani watoto rimoti wanapaswa wakukabidhi wewe

Unaangalia unachokitaka hiyo ndo maana ya mtawala

Shida uzungu unawasumbua

Ukiwa haupo tv ni yao ila ukifika tv ni ya kwako
Hapana inabidi kuwe Na Tv mbili moja weka chumbani hiyo utaangalia utakacho sebulen ya wageni Na watoto
 
Nikishakubali matokeo kuwa kwangu Tv ya sebuleni sio mali yangu.

Nashukuru Mungu niliweka TV chumbani. Ninachotaka kuangalia nakiangalia chumbani kwangu. Huko sebuleni ni Nickelodeon na Cartoon Network.

Ningeweza kutumia ubabe wa ubaba lakini sioni faida yake. Ikiwa nipo hai acha wanangu wa enjoy nyumbani kwa baba yao.
Hongera Sana ndo imavitakiwa
 
Back
Top Bottom