Pre GE2025 Wizi na ufisadi wa fedha za serikali uliokithiri katika awamu hii, suluhisho haliko ndani ya CCM wala upinzani kuwa mbadala wa CCM

Pre GE2025 Wizi na ufisadi wa fedha za serikali uliokithiri katika awamu hii, suluhisho haliko ndani ya CCM wala upinzani kuwa mbadala wa CCM

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Tumefikia mahali ambapo hali ya wizi na ufisadi wa fedha za serikali inatisha. Si Tamisemi tu, bali hata vyombo vya usalama na taasisi za serikali ugonjwa ni huo huo. Udanganyifu katika mifumo ya malipo imekuwa ndio habari ya mjini, kuanzia tozo za kupaki magari, fine za trafiki, miamara ya serikali za mitaa na serikali kuu, mashirika ya umma nk, ni wizi, wizi, wizi tu!

Watu siku hizi hawana uoga tena. Kwa wale waliompenda Magufuli na ambao hawakumpenda, wote lazima tukiri kwamba katika uongozi wake watu waliogopa kufanya wizi kama huu unaofanyika sasa.

Sasa tujiulize, kwa nini watu hawana uoga tena wa kufanya ufisadi na wizi hadi kufikia kiwango hiki?

Bila aibu wala upendeleo, twapaswa kukiri kwamba kuongezeka sana kwa wizi na ufisadi chini ya Raisi Samia kunachangiwa na watu kuona kwamba (perception) kuanzia ofisi ya Raisi mwenyewe, mawaziri nk, kumekuwa na viongozi na hata mawaziri wapigaji wengi tu. Kama hatutaoneana aibu, basi lazima tuseme uongozi wa Raisi Samia ndio tatizo na ndio unafanya watumishi wa serikali, mashirika na hata vyombo vya usalama kuwa na udiriki wa kuiba kwa kiwango hiki, jambo ambalo tunakiri wasingethubutu kufanya wakati wa Magufuli.

Wengi wetu tunaona kwamba Raisi Samia mwenyewe alihalalisha wizi wa fedha za serikali pale alipotoa kauli kwamba kila mtu atakula kwa urefu wa kamba yake, kauli ambayo japo anajua imeleta utata, hajawahi kuirekebisha. Raisi Samia anapaswa aelewe kichocheo kikubwa cha wizi uliopo ni perception kwamba kama Raisi amekuwa akitoa fursa nyingi za kutajirisha ndugu zake wa karibu na mbali (nepotism), na sasa hata mawaziri wake na watu wengine kwenye mashirika na serikali kuu na za mitaa wanaona ni halai kujitajirisha kwa kuiba fedha za serikali. Hivi inafikia wakati wowote Raisi Samia anajiuliza utajiri wa kasi wa mtoto wake Abdul unavyotazamwa na Watanzania, kuanzia mawaziri hadi watu wa serikali za mitaa na kwingineko, na unakuwa na athari gani kwa uaminifu wa viongozi na watu walio na fursa za kuiba fedha za serikali? Kwa nini watu wawe waaminifu wakiwa na perception kwamba hata Ofisi ya Raisi nchini haya mambo yanafanyika?

Watanzania wote wamesikia juu ya yale Makonda aliyofunua kule Arusha, na Watanzania wote wanatambua aliyofunua Makonda ni tone dogo sana katika bahari ya wizi wa fedha za serikali unaofanyika nchini kwa sasa. Leo mpeleke Makonda Morogoro, Mbeya, Iringa, Tanga nk, atakutana na yale yale anayoibua Arusha - wizi, wizi, wizi!

Sasa ni wakati wa kikiri kwamba tatizo la wizi nchini ni tatizo linalotokana na udhaifuu wa Ofisi ya Raisi katika kusimamia nidhamu ya fedha na uongozi nchini, na imefikia mahali hakuna mtu anaemuogopa Raisi Samia katika kufanya ufisadi na kuiba. Jambo mojawapo la kisaikolojia, ni kwamba inawezekana watu hawana uoga na kuiba chini ya uongozi wa Raisi Samia kwa sababu hawamwogopi raisi mwanamke, au labda wameona hana ukali au weupe wa kukemea wizi wa fedha za serikali, au kwa sababu tu ya perception kwamba hata Ofisi ya Raisi kuna hizi tabia za kujinufaisha kibinafsi na fedha za serikali.

Sasa je, suluhisho ni nini? Je, suluhisho liko ndani ya CCM au labda chama cha upinzani kuiondoa CCM madarakani?

Ukiniuliza maoni yangu binafsi, nitakuambia sioni ndani ya CCM kiongozi ambae anaweza kuwa mbadala wa Raisi Samia na kuweza kurudisha nidhamu ya fedha za serikali. Niambie, nani? Wale wote wanaotamani kushika nafasi ya uraisi, wote ukiwaangalia unaona kabisa huyu hawezi, na wala yule hawezi. Sioni mtu ndani ya CCM mwenye uwezo wa kurekebisha hali tuliyofikia Tanzania. Nani, Mpango? Makamba? Mwigulu? Majaliwa? Biteko? Jafo? Bashungwa? Hakuna hata mmoja, wote wameshaambukizwa kirusi cha kutoweza na kuweka maslahi ya chama na ukada mbele ya maslahi ya Tanzania.

Basi je, suluhisho liko nje ya CCM kwenye vyama vya upinzani? Tundu Lissu? Zitto Kabwe nk? Inawezekana, lakini ni jambo ambalo haliwezekani kusema Lissu au Ziito kwa mfano, wachukue nafasi ya Uraisi na nchi iwe chini ya uongozi wa vyama vyao. Hilo halitatupeleka popote.

Maoni yangu ni kwamba imefikia wakati tufikirie kuuna serikali ya mseto ambayo itajumuisha vyama vyote vya upinzani, ili tujipange upya. CCM peke yake, au Chadema peke yake, au ACT wazalendo peke yake, hawezi kututoa hapa tulipo. Lazima tutafute namna ya uwajibikaji wa serikali kwa kuwa na serikali ya mseto ambayo hivi vyama vya siasa nchini vitalazimika kufanya kazi pamoja kwa maslahi ya Tanzania, hapo tunaweza kufanikiwa.
 
Naona wale waliokuwa wanasema "lile dikteta katili, limeuwa watu" na kadhalika naona siku hizi hawapost tena huo upuuzi.

Ama kweli mwisho wa ubaya ni aibu. So haya ndio maisha ambayo wanafiki mnayataka tuishi mbwa nyie popote mlipo mle samaki mifupa iwakabe mbwa nyie mlimlaani sana mzee wa watu na kumbe alikuwa akitetea taifa, sasa tunateseka sote matako yenu.
 
Naona wale waliokuwa wanasema "lile dikteta katili, limeuwa watu" na kadhalika naona siku hizi hawapost tena huo upuuzi.

Ama kweli mwisho wa ubaya ni aibu. So haya ndio maisha ambayo wanafiki mnayataka tuishi mbwa nyie popote mlipo mle samaki mifupa iwakabe mbwa nyie mlimlaani sana mzee wa watu na kumbe alikuwa akitetea taifa, sasa tunateseka sote matako yenu.
Mimi binafsi nilimheshimu sana Magufuli kwa uzalendo aliokuwa nao, na nilisema wazi, nitakubaliana na Magufuli kwa yote anayofanya kwa ajili ya nchi yetu, isipokuwa kuonea watu na hata kuwapoteza. Hilo niliona likimchafua sana na nilisema hakuna excuse ya kuondoa haki ya kuishi ya mtu kwa sababu tu ya uzalendo wako kwa nchi
 
Hata wewe pia, ukiwekwa kwenye buyu la Asali utakuwa mwinzi vile vile..
Nijaribu uone. Ila kama nilivyosema, hakuna uongozi wa Chama kimoja nchini utatatua hili. Hata mie nikiwa ndio raisi chini ya uongozi wa chama fulani, CCM au Chadema au ACT, sintaweza, hata kama nina nia nzuri na ukali wa ajabu wa mafisadi. Kuna ufisadi mwingi tu ulifanyika hata wakati wa Magufuli mkali, japo si kwa kiwango cha wakati huu wa Raisi Samia
 
Andiko lako lina hoja kiasi fulani,,,lkn siamini kuwa na serikali mseto ndio suluhisho la matatizo,,hata hao wakianza kulamba asali watalegea

Tunahitaji mtu ambaye kwa kauli yake,na mtazamo wake awe kweli anachukizwa na haya yanayotokea hapa nchini kwetu
 
Ila nadhani wanaotisha kwa ujambazi bila aibu. Unakuta polisi trafiki kapaki prado yupo hapo barabarani, hahahaha unajiuliza ila ene way kila mtu urefu wa rope
 
Andiko lako lina hoja kiasi fulani,,,lkn siamini kuwa na serikali mseto ndio suluhisho la matatizo,,hata hao wakianza kulamba asali watalegea

Tunahitaji mtu ambaye kwa kauli yake,na mtazamo wake awe kweli anachukizwa na haya yanayotokea hapa nchini kwetu
Mkuu, kama hatutaenda upande wa serikali ya mseto, hali zitazidi kuharibika, na inaweza kufikia wakati ambapo mbadala inaweza kuwa kuiondoa serikali iliyopo madarakani kwa nguvu, na hili tayari limeanza kuongelewa hadi Bungeni kwamba kuna wakati inafikia hali zinahalalisha kuiondoa serikali iliyopo madarakani kwa nguvu. Sidhani kama tungependa kuona hilo likifanyika nchini.

Unasema tunahitaji mtu ambaye kwa kauli yake,na mtazamo wake awe kweli anachukizwa na haya yanayotokea hapa nchini kwetu, niambie katika waliopo wewe umemwona nani, mie sioni mtu wa namna hiyo.
 
Tumefikia mahali ambapo hali ya wizi na ufisadi wa fedha za serikali inatisha. Si Tamisemi tu, bali hata vyombo vya usalama na taasisi za serikali ugonjwa ni huo huo. Udanganyifu katika mifumo ya malipo imekuwa ndio habari ya mjini, kuanzia tozo za kupaki magari, fine za trafiki, miamara ya serikali za mitaa na serikali kuu, mashirika ya umma nk, ni wizi, wizi, wizi tu!

Watu siku hizi hawana uoga tena. Kwa wale waliompenda Magufuli na ambao hawakumpenda, wote lazima tukiri kwamba katika uongozi wake watu waliogopa kufanya wizi kama huu unaofanyika sasa.

Sasa tujiulize, kwa nini watu hawana uoga tena wa kufanya ufisadi na wizi hadi kufikia kiwango hiki?

Bila aibu wala upendeleo, twapaswa kukiri kwamba kuongezeka sana kwa wizi na ufisadi chini ya Raisi Samia kunachangiwa na watu kuona kwamba (perception) kuanzia ofisi ya Raisi mwenyewe, mawaziri nk, kumekuwa na viongozi na hata mawaziri wapigaji wengi tu. Kama hatutaoneana aibu, basi lazima tuseme uongozi wa Raisi Samia ndio tatizo na ndio unafanya watumishi wa serikali, mashirika na hata vyombo vya usalama kuwa na udiriki wa kuiba kwa kiwango hiki, jambo ambalo tunakiri wasingethubutu kufanya wakati wa Magufuli.

Wengi wetu tunaona kwamba Raisi Samia mwenyewe alihalalisha wizi wa fedha za serikali pale alipotoa kauli kwamba kila mtu atakula kwa urefu wa kamba yake, kauli ambayo japo anajua imeleta utata, hajawahi kuirekebisha. Raisi Samia anapaswa aelewe kichocheo kikubwa cha wizi uliopo ni perception kwamba kama Raisi amekuwa akitoa fursa nyingi za kutajirisha ndugu zake wa karibu na mbali (nepotism), na sasa hata mawaziri wake na watu wengine kwenye mashirika na serikali kuu na za mitaa wanaona ni halai kujitajirisha kwa kuiba fedha za serikali. Hivi inafikia wakati wowote Raisi Samia anajiuliza utajiri wa kasi wa mtoto wake Abdul unavyotazamwa na Watanzania, kuanzia mawaziri hadi watu wa serikali za mitaa na kwingineko, na unakuwa na athari gani kwa uaminifu wa viongozi na watu walio na fursa za kuiba fedha za serikali? Kwa nini watu wawe waaminifu wakiwa na perception kwamba hata Ofisi ya Raisi nchini haya mambo yanafanyika?

Watanzania wote wamesikia juu ya yale Makonda aliyofunua kule Arusha, na Watanzania wote wanatambua aliyofunua Makonda ni tone dogo sana katika bahari ya wizi wa fedha za serikali unaofanyika nchini kwa sasa. Leo mpeleke Makonda Morogoro, Mbeya, Iringa, Tanga nk, atakutana na yale yale anayoibua Arusha - wizi, wizi, wizi!

Sasa ni wakati wa kikiri kwamba tatizo la wizi nchini ni tatizo linalotokana na udhaifuu wa Ofisi ya Raisi katika kusimamia nidhamu ya fedha na uongozi nchini, na imefikia mahali hakuna mtu anaemuogopa Raisi Samia katika kufanya ufisadi na kuiba. Jambo mojawapo la kisaikolojia, ni kwamba inawezekana watu hawana uoga na kuiba chini ya uongozi wa Raisi Samia kwa sababu hawamwogopi raisi mwanamke, au labda wameona hana ukali au weupe wa kukemea wizi wa fedha za serikali, au kwa sababu tu ya perception kwamba hata Ofisi ya Raisi kuna hizi tabia za kujinufaisha kibinafsi na fedha za serikali.

Sasa je, suluhisho ni nini? Je, suluhisho liko ndani ya CCM au labda chama cha upinzani kuiondoa CCM madarakani?

Ukiniuliza maoni yangu binafsi, nitakuambia sioni ndani ya CCM kiongozi ambae anaweza kuwa mbadala wa Raisi Samia na kuweza kurudisha nidhamu ya fedha za serikali. Niambie, nani? Wale wote wanaotamani kushika nafasi ya uraisi, wote ukiwaangalia unaona kabisa huyu hawezi, na wala yule hawezi. Sioni mtu ndani ya CCM mwenye uwezo wa kurekebisha hali tuliyofikia Tanzania. Nani, Mpango? Makamba? Mwigulu? Majaliwa? Biteko? Jafo? Bashungwa? Hakuna hata mmoja, wote wameshaambukizwa kirusi cha kutoweza na kuweka maslahi ya chama na ukada mbele ya maslahi ya Tanzania.

Basi je, suluhisho liko nje ya CCM kwenye vyama vya upinzani? Tundu Lissu? Zitto Kabwe nk? Inawezekana, lakini ni jambo ambalo haliwezekani kusema Lissu au Ziito kwa mfano, wachukue nafasi ya Uraisi na nchi iwe chini ya uongozi wa vyama vyao. Hilo halitatupeleka popote.

Maoni yangu ni kwamba imefikia wakati tufikirie kuuna serikali ya mseto ambayo itajumuisha vyama vyote vya upinzani, ili tujipange upya. CCM peke yake, au Chadema peke yake, au ACT wazalendo peke yake, hawezi kututoa hapa tulipo. Lazima tutafute namna ya uwajibikaji wa serikali kwa kuwa na serikali ya mseto ambayo hivi vyama vya siasa nchini vitalazimika kufanya kazi pamoja kwa maslahi ya Tanzania, hapo tunaweza kufanikiwa.
Nitashakushangaa ukiwa mtu wa kusifu na kuabudu watawala

Upigaji unaanzia kwa raisiwenyewe tu
Na chama chake usimungunye maneno

Tuandike katiba mpya au yatokee Mapondizi ya kijeshi. hizo ndo soln
 
Mimi binafsi nilimheshimu sana Magufuli kwa uzalendo aliokuwa nao, na nilisema wazi, nitakubaliana na Magufuli kwa yote anayofanya kwa ajili ya nchi yetu, isipokuwa kuonea watu na hata kuwapoteza. Hilo niliona likimchafua sana na nilisema hakuna excuse ya kuondoa haki ya kuishi ya mtu kwa sababu tu ya uzalendo wako kwa nchi
Hoja y'ako hii inakwenda sambamba na hoja ya Mtibeli bwana RH,kasha wahi andika hapa JF,kwamba hata ufanye makubwa kiasi gani lakini ukicheza na uhai jua hivyo vitu ni hamna,sababu ya uhai ni johari ambayo haipaswi kuchezewa hata kidogo.

Hata Mungu alimpa Shetani ruhusa ya kumjaribu Ayubu,kwa kiasi atakacho,Lakini Mungu alimpa onyo Kali asicheze na uhai wake.Hii ni fundisho kwetu uhai ni jambo la Mungu mwenyewe sio mwanadamu.
 
Hoja y'ako hii inakwenda sambamba na hoja ya Mtibeli bwana RH,kasha wahi andika hapa JF,kwamba hata ufanye makubwa kiasi gani lakini ukicheza na uhai jua hivyo vitu ni hamna,sababu ya uhai ni johari ambayo haipaswi kuchezewa hata kidogo.

Hata Mungu alimpa Shetani ruhusa ya kumjaribu Ayubu,kwa kiasi atakacho,Lakini Mungu alimpa onyo Kali asicheze na uhai wake.Hii ni fundisho kwetu uhai ni jambo la Mungu mwenyewe sio mwanadamu.
Sawa kabisa. Ndio maana nilishasema humu ndani, kwamba japo makubwa aliyofanya Hitler kwa nchi yake ya Germany, anakumbukwa zaidi kwa mabaya na mauaji aliyofanya
 
Tumefikia mahali ambapo hali ya wizi na ufisadi wa fedha za serikali inatisha. Si Tamisemi tu, bali hata vyombo vya usalama na taasisi za serikali ugonjwa ni huo huo. Udanganyifu katika mifumo ya malipo imekuwa ndio habari ya mjini, kuanzia tozo za kupaki magari, fine za trafiki, miamara ya serikali za mitaa na serikali kuu, mashirika ya umma nk, ni wizi, wizi, wizi tu!

Watu siku hizi hawana uoga tena. Kwa wale waliompenda Magufuli na ambao hawakumpenda, wote lazima tukiri kwamba katika uongozi wake watu waliogopa kufanya wizi kama huu unaofanyika sasa.

Sasa tujiulize, kwa nini watu hawana uoga tena wa kufanya ufisadi na wizi hadi kufikia kiwango hiki?

Bila aibu wala upendeleo, twapaswa kukiri kwamba kuongezeka sana kwa wizi na ufisadi chini ya Raisi Samia kunachangiwa na watu kuona kwamba (perception) kuanzia ofisi ya Raisi mwenyewe, mawaziri nk, kumekuwa na viongozi na hata mawaziri wapigaji wengi tu. Kama hatutaoneana aibu, basi lazima tuseme uongozi wa Raisi Samia ndio tatizo na ndio unafanya watumishi wa serikali, mashirika na hata vyombo vya usalama kuwa na udiriki wa kuiba kwa kiwango hiki, jambo ambalo tunakiri wasingethubutu kufanya wakati wa Magufuli.

Wengi wetu tunaona kwamba Raisi Samia mwenyewe alihalalisha wizi wa fedha za serikali pale alipotoa kauli kwamba kila mtu atakula kwa urefu wa kamba yake, kauli ambayo japo anajua imeleta utata, hajawahi kuirekebisha. Raisi Samia anapaswa aelewe kichocheo kikubwa cha wizi uliopo ni perception kwamba kama Raisi amekuwa akitoa fursa nyingi za kutajirisha ndugu zake wa karibu na mbali (nepotism), na sasa hata mawaziri wake na watu wengine kwenye mashirika na serikali kuu na za mitaa wanaona ni halai kujitajirisha kwa kuiba fedha za serikali. Hivi inafikia wakati wowote Raisi Samia anajiuliza utajiri wa kasi wa mtoto wake Abdul unavyotazamwa na Watanzania, kuanzia mawaziri hadi watu wa serikali za mitaa na kwingineko, na unakuwa na athari gani kwa uaminifu wa viongozi na watu walio na fursa za kuiba fedha za serikali? Kwa nini watu wawe waaminifu wakiwa na perception kwamba hata Ofisi ya Raisi nchini haya mambo yanafanyika?

Watanzania wote wamesikia juu ya yale Makonda aliyofunua kule Arusha, na Watanzania wote wanatambua aliyofunua Makonda ni tone dogo sana katika bahari ya wizi wa fedha za serikali unaofanyika nchini kwa sasa. Leo mpeleke Makonda Morogoro, Mbeya, Iringa, Tanga nk, atakutana na yale yale anayoibua Arusha - wizi, wizi, wizi!

Sasa ni wakati wa kikiri kwamba tatizo la wizi nchini ni tatizo linalotokana na udhaifuu wa Ofisi ya Raisi katika kusimamia nidhamu ya fedha na uongozi nchini, na imefikia mahali hakuna mtu anaemuogopa Raisi Samia katika kufanya ufisadi na kuiba. Jambo mojawapo la kisaikolojia, ni kwamba inawezekana watu hawana uoga na kuiba chini ya uongozi wa Raisi Samia kwa sababu hawamwogopi raisi mwanamke, au labda wameona hana ukali au weupe wa kukemea wizi wa fedha za serikali, au kwa sababu tu ya perception kwamba hata Ofisi ya Raisi kuna hizi tabia za kujinufaisha kibinafsi na fedha za serikali.

Sasa je, suluhisho ni nini? Je, suluhisho liko ndani ya CCM au labda chama cha upinzani kuiondoa CCM madarakani?

Ukiniuliza maoni yangu binafsi, nitakuambia sioni ndani ya CCM kiongozi ambae anaweza kuwa mbadala wa Raisi Samia na kuweza kurudisha nidhamu ya fedha za serikali. Niambie, nani? Wale wote wanaotamani kushika nafasi ya uraisi, wote ukiwaangalia unaona kabisa huyu hawezi, na wala yule hawezi. Sioni mtu ndani ya CCM mwenye uwezo wa kurekebisha hali tuliyofikia Tanzania. Nani, Mpango? Makamba? Mwigulu? Majaliwa? Biteko? Jafo? Bashungwa? Hakuna hata mmoja, wote wameshaambukizwa kirusi cha kutoweza na kuweka maslahi ya chama na ukada mbele ya maslahi ya Tanzania.

Basi je, suluhisho liko nje ya CCM kwenye vyama vya upinzani? Tundu Lissu? Zitto Kabwe nk? Inawezekana, lakini ni jambo ambalo haliwezekani kusema Lissu au Ziito kwa mfano, wachukue nafasi ya Uraisi na nchi iwe chini ya uongozi wa vyama vyao. Hilo halitatupeleka popote.

Maoni yangu ni kwamba imefikia wakati tufikirie kuuna serikali ya mseto ambayo itajumuisha vyama vyote vya upinzani, ili tujipange upya. CCM peke yake, au Chadema peke yake, au ACT wazalendo peke yake, hawezi kututoa hapa tulipo. Lazima tutafute namna ya uwajibikaji wa serikali kwa kuwa na serikali ya mseto ambayo hivi vyama vya siasa nchini vitalazimika kufanya kazi pamoja kwa maslahi ya Tanzania, hapo tunaweza kufanikiwa.
Umeongea vitu vya maana sana. Serekali imemshinda huyu mama. Apumzike TU!
 
Naunga mkono hoja, inabidi somo la uadilifu, uaminifu na kusimamia haki lianze kufundishwa kwanzia chekechea ili tutengeneze vizazi vijavyo.
Sio bure kuna mahali tumekosa kama jamii!.
Naam mkuu, ila kwa kizazi cha sasa hakuna mwenye unafuu kwenye upande wa rushwa.. Kwa sababu tayari umesota mtaani kwa mda mrefu bila kumiliki kibunda, hivyo ukikabidhiwa kitengo lazima utalipiza kisasi kwa speed ya hali ya juu.
 
Naam mkuu, ila kwa kizazi cha sasa hakuna mwenye unafuu kwenye upande wa rushwa.. Kwa sababu tayari umesota mtaani kwa mda mrefu bila kumiliki kibunda, hivyo ukikabidhiwa kitengo lazima utalipiza kisasi kwa speed ya hali ya juu.
Ukiajiriwa ukakuta boss wako siyo mwizi lazima na wewe utakuwa msafi, wizi unaanzia juu kushuka chini
 
Hoja y'ako hii inakwenda sambamba na hoja ya Mtibeli bwana RH,kasha wahi andika hapa JF,kwamba hata ufanye makubwa kiasi gani lakini ukicheza na uhai jua hivyo vitu ni hamna,sababu ya uhai ni johari ambayo haipaswi kuchezewa hata kidogo.

Hata Mungu alimpa Shetani ruhusa ya kumjaribu Ayubu,kwa kiasi atakacho,Lakini Mungu alimpa onyo Kali asicheze na uhai wake.Hii ni fundisho kwetu uhai ni jambo la Mungu mwenyewe sio mwanadamu.
Sure dikteta alikuwa mtu hatari sn
 
Mimi binafsi nilimheshimu sana Magufuli kwa uzalendo aliokuwa nao, na nilisema wazi, nitakubaliana na Magufuli kwa yote anayofanya kwa ajili ya nchi yetu, isipokuwa kuonea watu na hata kuwapoteza. Hilo niliona likimchafua sana na nilisema hakuna excuse ya kuondoa haki ya kuishi ya mtu kwa sababu tu ya uzalendo wako kwa nchi
Yaani uua watu kisa uzalendo? alitukosea sn
 
Back
Top Bottom