Pre GE2025 Wizi na ufisadi wa fedha za serikali uliokithiri katika awamu hii, suluhisho haliko ndani ya CCM wala upinzani kuwa mbadala wa CCM

Pre GE2025 Wizi na ufisadi wa fedha za serikali uliokithiri katika awamu hii, suluhisho haliko ndani ya CCM wala upinzani kuwa mbadala wa CCM

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ila nadhani wanaotisha kwa ujambazi bila aibu. Unakuta polisi trafiki kapaki prado yupo hapo barabarani, hahahaha unajiuliza ila ene way kila mtu urefu wa rope
Hapa kuna ukweli. Kwa mshahara wa laki sita utawezaje kununua Prado? Wanasingizia tumekopa saccos, lakini utakuta mtu mwenyewe ana miaka 5 kazini, kwa kiwango hicho na muda huo hawezi kukopa pesa inayotosha kununua Prado. Kamba yao wameikita barabarani na ina urefu wa kutosha.
 
Tumefikia mahali ambapo hali ya wizi na ufisadi wa fedha za serikali inatisha. Si Tamisemi tu, bali hata vyombo vya usalama na taasisi za serikali ugonjwa ni huo huo. Udanganyifu katika mifumo ya malipo imekuwa ndio habari ya mjini, kuanzia tozo za kupaki magari, fine za trafiki, miamara ya serikali za mitaa na serikali kuu, mashirika ya umma nk, ni wizi, wizi, wizi tu!

Watu siku hizi hawana uoga tena. Kwa wale waliompenda Magufuli na ambao hawakumpenda, wote lazima tukiri kwamba katika uongozi wake watu waliogopa kufanya wizi kama huu unaofanyika sasa.

Sasa tujiulize, kwa nini watu hawana uoga tena wa kufanya ufisadi na wizi hadi kufikia kiwango hiki?

Bila aibu wala upendeleo, twapaswa kukiri kwamba kuongezeka sana kwa wizi na ufisadi chini ya Raisi Samia kunachangiwa na watu kuona kwamba (perception) kuanzia ofisi ya Raisi mwenyewe, mawaziri nk, kumekuwa na viongozi na hata mawaziri wapigaji wengi tu. Kama hatutaoneana aibu, basi lazima tuseme uongozi wa Raisi Samia ndio tatizo na ndio unafanya watumishi wa serikali, mashirika na hata vyombo vya usalama kuwa na udiriki wa kuiba kwa kiwango hiki, jambo ambalo tunakiri wasingethubutu kufanya wakati wa Magufuli.

Wengi wetu tunaona kwamba Raisi Samia mwenyewe alihalalisha wizi wa fedha za serikali pale alipotoa kauli kwamba kila mtu atakula kwa urefu wa kamba yake, kauli ambayo japo anajua imeleta utata, hajawahi kuirekebisha. Raisi Samia anapaswa aelewe kichocheo kikubwa cha wizi uliopo ni perception kwamba kama Raisi amekuwa akitoa fursa nyingi za kutajirisha ndugu zake wa karibu na mbali (nepotism), na sasa hata mawaziri wake na watu wengine kwenye mashirika na serikali kuu na za mitaa wanaona ni halai kujitajirisha kwa kuiba fedha za serikali. Hivi inafikia wakati wowote Raisi Samia anajiuliza utajiri wa kasi wa mtoto wake Abdul unavyotazamwa na Watanzania, kuanzia mawaziri hadi watu wa serikali za mitaa na kwingineko, na unakuwa na athari gani kwa uaminifu wa viongozi na watu walio na fursa za kuiba fedha za serikali? Kwa nini watu wawe waaminifu wakiwa na perception kwamba hata Ofisi ya Raisi nchini haya mambo yanafanyika?

Watanzania wote wamesikia juu ya yale Makonda aliyofunua kule Arusha, na Watanzania wote wanatambua aliyofunua Makonda ni tone dogo sana katika bahari ya wizi wa fedha za serikali unaofanyika nchini kwa sasa. Leo mpeleke Makonda Morogoro, Mbeya, Iringa, Tanga nk, atakutana na yale yale anayoibua Arusha - wizi, wizi, wizi!

Sasa ni wakati wa kikiri kwamba tatizo la wizi nchini ni tatizo linalotokana na udhaifuu wa Ofisi ya Raisi katika kusimamia nidhamu ya fedha na uongozi nchini, na imefikia mahali hakuna mtu anaemuogopa Raisi Samia katika kufanya ufisadi na kuiba. Jambo mojawapo la kisaikolojia, ni kwamba inawezekana watu hawana uoga na kuiba chini ya uongozi wa Raisi Samia kwa sababu hawamwogopi raisi mwanamke, au labda wameona hana ukali au weupe wa kukemea wizi wa fedha za serikali, au kwa sababu tu ya perception kwamba hata Ofisi ya Raisi kuna hizi tabia za kujinufaisha kibinafsi na fedha za serikali.

Sasa je, suluhisho ni nini? Je, suluhisho liko ndani ya CCM au labda chama cha upinzani kuiondoa CCM madarakani?

Ukiniuliza maoni yangu binafsi, nitakuambia sioni ndani ya CCM kiongozi ambae anaweza kuwa mbadala wa Raisi Samia na kuweza kurudisha nidhamu ya fedha za serikali. Niambie, nani? Wale wote wanaotamani kushika nafasi ya uraisi, wote ukiwaangalia unaona kabisa huyu hawezi, na wala yule hawezi. Sioni mtu ndani ya CCM mwenye uwezo wa kurekebisha hali tuliyofikia Tanzania. Nani, Mpango? Makamba? Mwigulu? Majaliwa? Biteko? Jafo? Bashungwa? Hakuna hata mmoja, wote wameshaambukizwa kirusi cha kutoweza na kuweka maslahi ya chama na ukada mbele ya maslahi ya Tanzania.

Basi je, suluhisho liko nje ya CCM kwenye vyama vya upinzani? Tundu Lissu? Zitto Kabwe nk? Inawezekana, lakini ni jambo ambalo haliwezekani kusema Lissu au Ziito kwa mfano, wachukue nafasi ya Uraisi na nchi iwe chini ya uongozi wa vyama vyao. Hilo halitatupeleka popote.

Maoni yangu ni kwamba imefikia wakati tufikirie kuuna serikali ya mseto ambayo itajumuisha vyama vyote vya upinzani, ili tujipange upya. CCM peke yake, au Chadema peke yake, au ACT wazalendo peke yake, hawezi kututoa hapa tulipo. Lazima tutafute namna ya uwajibikaji wa serikali kwa kuwa na serikali ya mseto ambayo hivi vyama vya siasa nchini vitalazimika kufanya kazi pamoja kwa maslahi ya Tanzania, hapo tunaweza kufanikiwa.
Mtazunguka sana kutafuta wa kumsukumia jumba bovu hili

Lakini ukweli unabaki ni mmoja tu ni lazima apatikane mtu mwenye elements za Udikteta na alindwe sana na atawale kwa muda usiopungua miaka 20 🙄👁

Hapo ndipo Nchi itakaa kwenye mstari ulionyooka 🙄👁

Magufuli alishaonyesha kuwa Inawezekana 😳🙄🙄👁
 
Nijaribu uone. Ila kama nilivyosema, hakuna uongozi wa Chama kimoja nchini utatatua hili. Hata mie nikiwa ndio raisi chini ya uongozi wa chama fulani, CCM au Chadema au ACT, sintaweza, hata kama nina nia nzuri na ukali wa ajabu wa mafisadi. Kuna ufisadi mwingi tu ulifanyika hata wakati wa Magufuli mkali, japo si kwa kiwango cha wakati huu wa Raisi Samia
. Kuzuia kitu kinachoitwa Rushwa inahitajika mlolongo mrefu sana ulio na sheria kali za nchi... Kuanzia wananchi wenyewe mpaka serikali kwa ujumla.

. Wizi wa mali za umma hauji hivi hivi, lazima huwa kuna chazo.
1. Gape la ajira kwa wananchi
2. Sheria mbovu
3. Nchi kukosa plan ya maendeleo
 
Naona wale waliokuwa wanasema "lile dikteta katili, limeuwa watu" na kadhalika naona siku hizi hawapost tena huo upuuzi.

Ama kweli mwisho wa ubaya ni aibu. So haya ndio maisha ambayo wanafiki mnayataka tuishi mbwa nyie popote mlipo mle samaki mifupa iwakabe mbwa nyie mlimlaani sana mzee wa watu na kumbe alikuwa akitetea taifa, sasa tunateseka sote matako yenu.
Punguza unafiki. Nani ana muda wakumuongelea marehemu. Mtu kafa miaka mitatu iliyopita, wewe unailaumu kwanini haongelewi
 
Naona wale waliokuwa wanasema "lile dikteta katili, limeuwa watu" na kadhalika naona siku hizi hawapost tena huo upuuzi.

Ama kweli mwisho wa ubaya ni aibu. So haya ndio maisha ambayo wanafiki mnayataka tuishi mbwa nyie popote mlipo mle samaki mifupa iwakabe mbwa nyie mlimlaani sana mzee wa watu na kumbe alikuwa akitetea taifa, sasa tunateseka sote matako yenu.
Tunamshukuru Mungu kwa kutuondolea yule kiongozi muovu bila damu kumwagika. Uchu wake wa madaraka ndio uliochangia kwa kiasi kikubwa kuua checks and balances ndani ya nchi hii. Kama sio yeye aliua demokrasia ya watu kuhoji, Leo hii wenye nguvu ya kuhoji Bado wangekuwepo. Ametuwekea bunge la chama kimoja ili alitumie kuiweka madarakani zaidi ya miaka 10. Alikuja kuparalize mifumo na kutuletea habari za one man show.
 
CCM peke yake, au Chadema peke yake, au ACT wazalendo peke yake, hawezi kututoa hapa tulipo. Lazima tutafute namna ya uwajibikaji wa serikali kwa kuwa na serikali ya mseto ambayo hivi vyama vya siasa nchini vitalazimika kufanya kazi pamoja kwa maslahi ya Tanzania, hapo tunaweza kufanikiwa.
Chumvi ikiharibika haina dawa.
Huwezi kuinusuru nchi kwa kuendelea kuikumbatia hiyo ccm iliyokwisha haribika. Matendo ya ccm ndiyo yametufikisha kwenye mkwamo sugu. Lazima tutafute na kukubali mbadala
 
Ccm lazima iondoke kwanza ili nchi ianze upya.Lakini pia ili tutoke hapo kwenye mkwamo lazima tuondokane na tabia yakutegemea mtu mmoja kama mwamuzi wa kila kitu.Wenzetu walishaondoka uko wako kwenye kujenga mifumo thabiti inayojisimamia ndo maana wanaendelea ila sisi bado tunawaza mtu mmoja sahihi ambaye ata ukimpata anaweza kufa au kubadilika muda wowote.
 
Chumvi ikiharibika haina dawa.
Huwezi kuinusuru nchi kwa kuendelea kuikumbatia hiyo ccm iliyokwisha haribika. Matendo ya ccm ndiyo yametufikisha kwenye mkwamo sugu. Lazima tutafute na kukubali mbadala
Mbadala bila CCM maana yake ni muungano wa vyama au chama cha upinzani kimoja, na kuondoa(purging) wale wote walio tainted na CCM. Tunaweza kuharibu hata zaidi, kwa sababu ukifanya hivyo kunakuwa na tendency ya kuleta watendaji wapya wasio na uzoefu katika mifumo ya serikali. Kosa hili walifanya Zimbawe na South Africa na kuharibu sana uimara wa serikali na hata uchumi. Ndio maana nikasema suluhisho ni serikali ya mseto
 
Serekali ya majimbo. MTU akivuruga jimboni kwake anapambana na watu wake. Na hii italeta ushindani katika maendeleo.
Hii nayo ni point nzuri sana, ila tatizo ni kwamba kutakuwa na majimbo ambayo yana nafasi kidogo sana za kiuchumi, kwa mfano kusini mwa Tanzania nk. Itabidi umakini ufanyike kusawazisha. Lakini kubadili mfumo uliopo na wa central government kuingia mfumo wa majimbo, decentralization, inarahisisha sana kusimamia serikali katika dimension ndogo kwa ufanisi zaidi.
 
Umeongea vitu vya maana sana. Serekali imemshinda huyu mama. Apumzike TU!
Nadhani kuna tatizo kubwa zaidi ya huyu mama; serikali imewashinda CCM, hawana la kufanya tena kwa sababu ya cancer iliyo ndani yao katika mazingira ambayo wananchi wasio na upevu wa kisiasa wanaona hakuna mbadala wa CCM. Leo CCM hata wakiuza Mlima Kilimanjaro kwa Kenya, bado kuna watu watasifia huo uamuzi na wanaweza kushinda uchaguzi mkuu.
 
Mkuu, kama hatutaenda upande wa serikali ya mseto, hali zitazidi kuharibika, na inaweza kufikia wakati ambapo mbadala inaweza kuwa kuiondoa serikali iliyopo madarakani kwa nguvu, na hili tayari limeanza kuongelewa hadi Bungeni kwamba kuna wakati inafikia hali zinahalalisha kuiondoa serikali iliyopo madarakani kwa nguvu. Sidhani kama tungependa kuona hilo likifanyika nchini.

Unasema tunahitaji mtu ambaye kwa kauli yake,na mtazamo wake awe kweli anachukizwa na haya yanayotokea hapa nchini kwetu, niambie katika waliopo wewe umemwona nani, mie sioni mtu wa namna hiyo.
Watu wapo ila wamemezwa na mfumo wa kishetani. Huwezi kuwa kwenye kundi la mafisadi 20 halafu ukaanza kuleta ideology za kizalendo watakumaliza mapema mno.

Ratio ya wazalendo versus wasaka tonge tunaweza weka assumption ya 10:90 na ukiangalia hapo nguvu ya hao 90 iko kwa wenye madaraka. Unafanyaje mwisho wa siku, hata hao 10% wataishi maisha ambayo nafsi zinawauma ila hawana jinsi.
 
Tumefikia mahali ambapo hali ya wizi na ufisadi wa fedha za serikali inatisha. Si Tamisemi tu, bali hata vyombo vya usalama na taasisi za serikali ugonjwa ni huo huo. Udanganyifu katika mifumo ya malipo imekuwa ndio habari ya mjini, kuanzia tozo za kupaki magari, fine za trafiki, miamara ya serikali za mitaa na serikali kuu, mashirika ya umma nk, ni wizi, wizi, wizi tu!

Watu siku hizi hawana uoga tena. Kwa wale waliompenda Magufuli na ambao hawakumpenda, wote lazima tukiri kwamba katika uongozi wake watu waliogopa kufanya wizi kama huu unaofanyika sasa.

Sasa tujiulize, kwa nini watu hawana uoga tena wa kufanya ufisadi na wizi hadi kufikia kiwango hiki?

Bila aibu wala upendeleo, twapaswa kukiri kwamba kuongezeka sana kwa wizi na ufisadi chini ya Raisi Samia kunachangiwa na watu kuona kwamba (perception) kuanzia ofisi ya Raisi mwenyewe, mawaziri nk, kumekuwa na viongozi na hata mawaziri wapigaji wengi tu. Kama hatutaoneana aibu, basi lazima tuseme uongozi wa Raisi Samia ndio tatizo na ndio unafanya watumishi wa serikali, mashirika na hata vyombo vya usalama kuwa na udiriki wa kuiba kwa kiwango hiki, jambo ambalo tunakiri wasingethubutu kufanya wakati wa Magufuli.

Wengi wetu tunaona kwamba Raisi Samia mwenyewe alihalalisha wizi wa fedha za serikali pale alipotoa kauli kwamba kila mtu atakula kwa urefu wa kamba yake, kauli ambayo japo anajua imeleta utata, hajawahi kuirekebisha. Raisi Samia anapaswa aelewe kichocheo kikubwa cha wizi uliopo ni perception kwamba kama Raisi amekuwa akitoa fursa nyingi za kutajirisha ndugu zake wa karibu na mbali (nepotism), na sasa hata mawaziri wake na watu wengine kwenye mashirika na serikali kuu na za mitaa wanaona ni halai kujitajirisha kwa kuiba fedha za serikali. Hivi inafikia wakati wowote Raisi Samia anajiuliza utajiri wa kasi wa mtoto wake Abdul unavyotazamwa na Watanzania, kuanzia mawaziri hadi watu wa serikali za mitaa na kwingineko, na unakuwa na athari gani kwa uaminifu wa viongozi na watu walio na fursa za kuiba fedha za serikali? Kwa nini watu wawe waaminifu wakiwa na perception kwamba hata Ofisi ya Raisi nchini haya mambo yanafanyika?

Watanzania wote wamesikia juu ya yale Makonda aliyofunua kule Arusha, na Watanzania wote wanatambua aliyofunua Makonda ni tone dogo sana katika bahari ya wizi wa fedha za serikali unaofanyika nchini kwa sasa. Leo mpeleke Makonda Morogoro, Mbeya, Iringa, Tanga nk, atakutana na yale yale anayoibua Arusha - wizi, wizi, wizi!

Sasa ni wakati wa kikiri kwamba tatizo la wizi nchini ni tatizo linalotokana na udhaifuu wa Ofisi ya Raisi katika kusimamia nidhamu ya fedha na uongozi nchini, na imefikia mahali hakuna mtu anaemuogopa Raisi Samia katika kufanya ufisadi na kuiba. Jambo mojawapo la kisaikolojia, ni kwamba inawezekana watu hawana uoga na kuiba chini ya uongozi wa Raisi Samia kwa sababu hawamwogopi raisi mwanamke, au labda wameona hana ukali au weupe wa kukemea wizi wa fedha za serikali, au kwa sababu tu ya perception kwamba hata Ofisi ya Raisi kuna hizi tabia za kujinufaisha kibinafsi na fedha za serikali.

Sasa je, suluhisho ni nini? Je, suluhisho liko ndani ya CCM au labda chama cha upinzani kuiondoa CCM madarakani?

Ukiniuliza maoni yangu binafsi, nitakuambia sioni ndani ya CCM kiongozi ambae anaweza kuwa mbadala wa Raisi Samia na kuweza kurudisha nidhamu ya fedha za serikali. Niambie, nani? Wale wote wanaotamani kushika nafasi ya uraisi, wote ukiwaangalia unaona kabisa huyu hawezi, na wala yule hawezi. Sioni mtu ndani ya CCM mwenye uwezo wa kurekebisha hali tuliyofikia Tanzania. Nani, Mpango? Makamba? Mwigulu? Majaliwa? Biteko? Jafo? Bashungwa? Hakuna hata mmoja, wote wameshaambukizwa kirusi cha kutoweza na kuweka maslahi ya chama na ukada mbele ya maslahi ya Tanzania.

Basi je, suluhisho liko nje ya CCM kwenye vyama vya upinzani? Tundu Lissu? Zitto Kabwe nk? Inawezekana, lakini ni jambo ambalo haliwezekani kusema Lissu au Ziito kwa mfano, wachukue nafasi ya Uraisi na nchi iwe chini ya uongozi wa vyama vyao. Hilo halitatupeleka popote.

Maoni yangu ni kwamba imefikia wakati tufikirie kuuna serikali ya mseto ambayo itajumuisha vyama vyote vya upinzani, ili tujipange upya. CCM peke yake, au Chadema peke yake, au ACT wazalendo peke yake, hawezi kututoa hapa tulipo. Lazima tutafute namna ya uwajibikaji wa serikali kwa kuwa na serikali ya mseto ambayo hivi vyama vya siasa nchini vitalazimika kufanya kazi pamoja kwa maslahi ya Tanzania, hapo tunaweza kufanikiwa.
Andiko lina ukweli mwingi! Suluhisho ndilo bado la kufikiria!
Anko Magu ninaamini aliharibiwa na haya majambazi ama kwa uchawi au kifitina tu! Ninaungana na chalamila kuwa msaidizi namba moja wa Anko magu alihusika kwenye kifo chake!
Hayo ni dhahiri haiwezekani mtu aseme anaponya nchi huku akiiuza na kuifisidi kwa kasi ya ndege!
Suluhisho ni moja!
Tunahitaji Ibrahim Traore mmoja tu ayashughulikie haya majambazi kwa nguvu zote na kujenga hofu na nidhamu! Baasi Utawala wa kiraia uje baadaye! basi kwa sababu hata anko magu mbona aliipeleka nchi kijeshi kabla hayo majizi hayajafitinisha?
 
Andiko lina ukweli mwingi! Suluhisho ndilo bado la kufikiria!
Anko Magu ninaamini aliharibiwa na haya majambazi ama kwa uchawi au kifitina tu! Ninaungana na chalamila kuwa msaidizi namba moja wa Anko magu alihusika kwenye kifo chake!
Hayo ni dhahiri haiwezekani mtu aseme anaponya nchi huku akiiuza na kuifisidi kwa kasi ya ndege!
Suluhisho ni moja!
Tunahitaji Ibrahim Traore mmoja tu ayashughulikie haya majambazi kwa nguvu zote na kujenga hofu na nidhamu! Baasi Utawala wa kiraia uje baadaye! basi kwa sababu hata anko magu mbona aliipeleka nchi kijeshi kabla hayo majizi hayajafitinisha?
Kwa kweli Tanzania inahitaji Traole wake, huo ni ukweli usiopingika. Huenda yupo tu huko kwa wajeda, anaangalia tu kinachoendelea
 
Watu wapo ila wamemezwa na mfumo wa kishetani. Huwezi kuwa kwenye kundi la mafisadi 20 halafu ukaanza kuleta ideology za kizalendo watakumaliza mapema mno.

Ratio ya wazalendo versus wasaka tonge tunaweza weka assumption ya 10:90 na ukiangalia hapo nguvu ya hao 90 iko kwa wenye madaraka. Unafanyaje mwisho wa siku, hata hao 10% wataishi maisha ambayo nafsi zinawauma ila hawana jinsi.
Hao wau wako wapi, lazima wapatikane katika mfumo unaoonekana, la sivyo hawawezi kutusaidia
 
Back
Top Bottom