Pre GE2025 Wizi na ufisadi wa fedha za serikali uliokithiri katika awamu hii, suluhisho haliko ndani ya CCM wala upinzani kuwa mbadala wa CCM

Pre GE2025 Wizi na ufisadi wa fedha za serikali uliokithiri katika awamu hii, suluhisho haliko ndani ya CCM wala upinzani kuwa mbadala wa CCM

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Basi unarudi kwenye kichwa cha thread hii - si CCM wala chama mbadala wa CCM wanaweza kututoa kwenye tope tulipo, tunahitaji uongozi wa mseto kama transition ya kipindi kisichopungua miaka mitano ili turekebishe mambo
Uongozi wa mseto kwa kutumia Katiba gani?
 
Transition period. Zanzibar walipoanza uongozi wa mseto walitumia katiba gani? Kenya je? Huhitaji ku-complicate haya mambo.
Tz is a failed state, kwa hiyo siyo nchi nzuri au Bora ya kuitolea mifano kwenye masuala ya utawala Bora.
Je, hauoni kwamba Mgogoro wa Kiutawala bado haujamalizika au bado upo pale pale huko Zanzibar???Je, Ni kweli kwamba haujui uwepo wa tatizo hili huko Zanzibar?????
 
Tz is a failed state, kwa hiyo siyo nchi nzuri au Bora ya kuitolea mifano kwenye masuala ya utawala Bora.
Je, hauoni kwamba Mgogoro wa Kiutawala bado haujamalizika au bado upo pale pale huko Zanzibar???Je, Ni kweli kwamba haujui uwepo wa tatizo hili huko Zanzibar?????
Najua uwepo wa tatizo Zanzibar, ambalo sio tatizo lililopo serikali ya muungano,lakini tatizo la serikali ya muungano linaweza kuwa linachangia tatizo lililopo Zanzibar!
 
Najua uwepo wa tatizo Zanzibar, ambalo sio tatizo lililopo serikali ya muungano,lakini tatizo la serikali ya muungano linaweza kuwa linachangia tatizo lililopo Zanzibar!
Mbona Serikali ya mseto ipo Zanzibar, Sasa kwa Nini tatizo bado lipo huko ikiwa Serikali ya mseto ndio suluhisho kwa matatizo ya Kiutawala kama hayo??
 
Mbona Serikali ya mseto ipo Zanzibar, Sasa kwa Nini tatizo bado lipo huko ikiwa Serikali ya mseto ndio suluhisho kwa matatizo ya Kiutawala kama hayo??
Tatizo ni objectives za serikali ya mseto unayounda. Serikali ya mseto ya Zanzibar ipo kwa ajili ya kunyamazisha na kutuliza upinzani sio kutafuta way forward ya kudumu. Wapinzani wameridhika na kupewa nafasi fulani ili wanyamaze. Ile ya mseto ya Tanzania itakuwa ya muda lengo kubwa ikiwa ni kuleta katiba mpya na Tume huru ya uchaguzi. Baada ya hapo haihitajiki tena.

Angalia hii thread

 
Nadhani ubora wa mifumo pekee hauwezi kutatua. Kumbuka, mfumo wa kulipa fedha za serikali kupitia control number ulijikita pia kwenye kupunguza rushwa, na kama mfumo ni jambo zuri tu. Tatizo ni tabia za watu ambao wamejenga katika akili yao kwamba ni halali kuiba fedha za serikali. Sasa tumefikia mahali hata jeshi la polisi, sehemu usikotarajia mambo haya kufanyika, hawaridhiki na rushwa wanazotoza watu wanaona nao pia wana fursa ya kuiba kupitia mfumo wa malipo wa serikali.

Angalia kampuni binafsi za parking. Wanaiba kwa kutengezeza parking fee hewa kupitia mfumo wa malipo uliorahisishwa ili watu walipe kwa wakati wao bila kufukuzana na parking attendants. Halamashauri huko ndiko usiseme.

Tatizo sio mifumo - ni uongozi thabiti ambao watu wanajua uko serious katika kuchukia wizi. Hatuna huo uongozi kwa sasa.
Mfumo aliozungumzia mchangiaji ni tofauti na wewe unachokizungumzia. Wewe unazungumzia Financial Software au Financial Applications yeye anazungumzia Administrative and Management Systems ambazo zinahusisha vyote ulivyovitaja. Ila nakubaliana na wewe kuhusu kutokuwepo na uongozi thabiti wa kusimamia hayo kwa pamoja ili vyote vilete matunda tunayotarajia. Hii ni changamoto ya kuwa na uongozi wa mtu mmoja ambaye kila mtu anamuogopa badala ya kuogopa sheria na taratibu za kazi. Hata mifumo ya kuwajibisha watumishi wezi imekuwa corrupted!
 
JPM hakufa kwa sababu alikua serious, labda kama una taarifa iliyo tofauti na kile tunachoambiwa kilimuua
Wewe umeelewa vibaya kaka. Maana yangu ni kuwa hata uwe SERIOUS kiasi gani kwa kuwa unakuwa peke yako ukiondoka kila kitu ulichokisimamia kinakwama. Kinachotakiwa ni Taasisi imara siyo mtu mmoja SERIOUS peke yake.
 
Mfumo aliozungumzia mchangiaji ni tofauti na wewe unachokizungumzia. Wewe unazungumzia Financial Software au Financial Applications yeye anazungumzia Administrative and Management Systems ambazo zinahusisha vyote ulivyovitaja. Ila nakubaliana na wewe kuhusu kutokuwepo na uongozi thabiti wa kusimamia hayo kwa pamoja ili vyote vilete matunda tunayotarajia. Hii ni changamoto ya kuwa na uongozi wa mtu mmoja ambaye kila mtu anamuogopa badala ya kuogopa sheria na taratibu za kazi. Hata mifumo ya kuwajibisha watumishi wezi imekuwa corrupted!
Okay, shukurani kwa ufafanuzi. Hivi tatizo ni uoga au kulinda maslahi? Maana ingekuwa ni uoga watu wasingekuwa wanaiba. Tatizo ni kwamba watu wanaona uozo na wanajua ni uozo, lakini hawasemi ili wasiondolewe katika nafasi zao na wengine wakapewa ikiwa watasema ukweli. Watu waoga ni kama wale wa Putin, wanamwogopa Putin japo hawafaidiki na nafasi walizonazo. Hawa wa hapa kwetu sio uoga wa nanma hiyo, ni suala la wao kujifanya hawaoni uozo ili waendelee kukaa katika neema walizonazo. Si ulimsikia yule aliyesema nilipoona Magufuli atanitumbua na mie nasomesha watoto niliamua kupendekeza tubadili awamu za uongozi ziwe za miaka saba badala ya mitano ili kumfurahisha!
 
Wewe umeelewa vibaya kaka. Maana yangu ni kuwa hata uwe SERIOUS kiasi gani kwa kuwa unakuwa peke yako ukiondoka kila kitu ulichokisimamia kinakwama. Kinachotakiwa ni Taasisi imara siyo mtu mmoja SERIOUS peke yake.
Nadhani tuko pamoja. Taasisi imara bila mtu imara haitasaidia kama vile tu kuwa na mtu imara bila taasisi imara
 
Tumefikia mahali ambapo hali ya wizi na ufisadi wa fedha za serikali inatisha. Si Tamisemi tu, bali hata vyombo vya usalama na taasisi za serikali ugonjwa ni huo huo. Udanganyifu katika mifumo ya malipo imekuwa ndio habari ya mjini, kuanzia tozo za kupaki magari, fine za trafiki, miamara ya serikali za mitaa na serikali kuu, mashirika ya umma nk, ni wizi, wizi, wizi tu!

Watu siku hizi hawana uoga tena. Kwa wale waliompenda Magufuli na ambao hawakumpenda, wote lazima tukiri kwamba katika uongozi wake watu waliogopa kufanya wizi kama huu unaofanyika sasa.

Sasa tujiulize, kwa nini watu hawana uoga tena wa kufanya ufisadi na wizi hadi kufikia kiwango hiki?

Bila aibu wala upendeleo, twapaswa kukiri kwamba kuongezeka sana kwa wizi na ufisadi chini ya Raisi Samia kunachangiwa na watu kuona kwamba (perception) kuanzia ofisi ya Raisi mwenyewe, mawaziri nk, kumekuwa na viongozi na hata mawaziri wapigaji wengi tu. Kama hatutaoneana aibu, basi lazima tuseme uongozi wa Raisi Samia ndio tatizo na ndio unafanya watumishi wa serikali, mashirika na hata vyombo vya usalama kuwa na udiriki wa kuiba kwa kiwango hiki, jambo ambalo tunakiri wasingethubutu kufanya wakati wa Magufuli.

Wengi wetu tunaona kwamba Raisi Samia mwenyewe alihalalisha wizi wa fedha za serikali pale alipotoa kauli kwamba kila mtu atakula kwa urefu wa kamba yake, kauli ambayo japo anajua imeleta utata, hajawahi kuirekebisha. Raisi Samia anapaswa aelewe kichocheo kikubwa cha wizi uliopo ni perception kwamba kama Raisi amekuwa akitoa fursa nyingi za kutajirisha ndugu zake wa karibu na mbali (nepotism), na sasa hata mawaziri wake na watu wengine kwenye mashirika na serikali kuu na za mitaa wanaona ni halai kujitajirisha kwa kuiba fedha za serikali. Hivi inafikia wakati wowote Raisi Samia anajiuliza utajiri wa kasi wa mtoto wake Abdul unavyotazamwa na Watanzania, kuanzia mawaziri hadi watu wa serikali za mitaa na kwingineko, na unakuwa na athari gani kwa uaminifu wa viongozi na watu walio na fursa za kuiba fedha za serikali? Kwa nini watu wawe waaminifu wakiwa na perception kwamba hata Ofisi ya Raisi nchini haya mambo yanafanyika?

Watanzania wote wamesikia juu ya yale Makonda aliyofunua kule Arusha, na Watanzania wote wanatambua aliyofunua Makonda ni tone dogo sana katika bahari ya wizi wa fedha za serikali unaofanyika nchini kwa sasa. Leo mpeleke Makonda Morogoro, Mbeya, Iringa, Tanga nk, atakutana na yale yale anayoibua Arusha - wizi, wizi, wizi!

Sasa ni wakati wa kikiri kwamba tatizo la wizi nchini ni tatizo linalotokana na udhaifuu wa Ofisi ya Raisi katika kusimamia nidhamu ya fedha na uongozi nchini, na imefikia mahali hakuna mtu anaemuogopa Raisi Samia katika kufanya ufisadi na kuiba. Jambo mojawapo la kisaikolojia, ni kwamba inawezekana watu hawana uoga na kuiba chini ya uongozi wa Raisi Samia kwa sababu hawamwogopi raisi mwanamke, au labda wameona hana ukali au weupe wa kukemea wizi wa fedha za serikali, au kwa sababu tu ya perception kwamba hata Ofisi ya Raisi kuna hizi tabia za kujinufaisha kibinafsi na fedha za serikali.

Sasa je, suluhisho ni nini? Je, suluhisho liko ndani ya CCM au labda chama cha upinzani kuiondoa CCM madarakani?

Ukiniuliza maoni yangu binafsi, nitakuambia sioni ndani ya CCM kiongozi ambae anaweza kuwa mbadala wa Raisi Samia na kuweza kurudisha nidhamu ya fedha za serikali. Niambie, nani? Wale wote wanaotamani kushika nafasi ya uraisi, wote ukiwaangalia unaona kabisa huyu hawezi, na wala yule hawezi. Sioni mtu ndani ya CCM mwenye uwezo wa kurekebisha hali tuliyofikia Tanzania. Nani, Mpango? Makamba? Mwigulu? Majaliwa? Biteko? Jafo? Bashungwa? Hakuna hata mmoja, wote wameshaambukizwa kirusi cha kutoweza na kuweka maslahi ya chama na ukada mbele ya maslahi ya Tanzania.

Basi je, suluhisho liko nje ya CCM kwenye vyama vya upinzani? Tundu Lissu? Zitto Kabwe nk? Inawezekana, lakini ni jambo ambalo haliwezekani kusema Lissu au Ziito kwa mfano, wachukue nafasi ya Uraisi na nchi iwe chini ya uongozi wa vyama vyao. Hilo halitatupeleka popote.

Maoni yangu ni kwamba imefikia wakati tufikirie kuuna serikali ya mseto ambayo itajumuisha vyama vyote vya upinzani, ili tujipange upya. CCM peke yake, au Chadema peke yake, au ACT wazalendo peke yake, hawezi kututoa hapa tulipo. Lazima tutafute namna ya uwajibikaji wa serikali kwa kuwa na serikali ya mseto ambayo hivi vyama vya siasa nchini vitalazimika kufanya kazi pamoja kwa maslahi ya Tanzania, hapo tunaweza kufanikiwa.
Kipindi cha jpm ndo wizi ikithiri ukiongozwa na jpm mwenyewe ila hakuna chombo cha habari chochote kilichokuwa na ubavu wa kulipoti kama sas ambapo mengine ni uonvo lla vimeachwa vyote vikue bwana mwenye shamba atakuja kuchambua magugu na ngano. Viva samia kupro.otd freedom of speech
 
Alisema mtanikumbuka na kauli yake inaakisi ukweli

Raisi alifeli aliposema kila mtu atakula kwa urefu wa kamba yake,,,shida ilianzia pale

..kwa ubaguzi na ukatili.

..ni mhuni tu ndiye anayeweza kuwaambia walipakodi sitawaletea barabara kwasababu mmechagua mpinzani.
 
Tumefikia mahali ambapo hali ya wizi na ufisadi wa fedha za serikali inatisha. Si Tamisemi tu, bali hata vyombo vya usalama na taasisi za serikali ugonjwa ni huo huo. Udanganyifu katika mifumo ya malipo imekuwa ndio habari ya mjini, kuanzia tozo za kupaki magari, fine za trafiki, miamara ya serikali za mitaa na serikali kuu, mashirika ya umma nk, ni wizi, wizi, wizi tu!

Watu siku hizi hawana uoga tena. Kwa wale waliompenda Magufuli na ambao hawakumpenda, wote lazima tukiri kwamba katika uongozi wake watu waliogopa kufanya wizi kama huu unaofanyika sasa.

Sasa tujiulize, kwa nini watu hawana uoga tena wa kufanya ufisadi na wizi hadi kufikia kiwango hiki?

Bila aibu wala upendeleo, twapaswa kukiri kwamba kuongezeka sana kwa wizi na ufisadi chini ya Raisi Samia kunachangiwa na watu kuona kwamba (perception) kuanzia ofisi ya Raisi mwenyewe, mawaziri nk, kumekuwa na viongozi na hata mawaziri wapigaji wengi tu. Kama hatutaoneana aibu, basi lazima tuseme uongozi wa Raisi Samia ndio tatizo na ndio unafanya watumishi wa serikali, mashirika na hata vyombo vya usalama kuwa na udiriki wa kuiba kwa kiwango hiki, jambo ambalo tunakiri wasingethubutu kufanya wakati wa Magufuli.

Wengi wetu tunaona kwamba Raisi Samia mwenyewe alihalalisha wizi wa fedha za serikali pale alipotoa kauli kwamba kila mtu atakula kwa urefu wa kamba yake, kauli ambayo japo anajua imeleta utata, hajawahi kuirekebisha. Raisi Samia anapaswa aelewe kichocheo kikubwa cha wizi uliopo ni perception kwamba kama Raisi amekuwa akitoa fursa nyingi za kutajirisha ndugu zake wa karibu na mbali (nepotism), na sasa hata mawaziri wake na watu wengine kwenye mashirika na serikali kuu na za mitaa wanaona ni halai kujitajirisha kwa kuiba fedha za serikali. Hivi inafikia wakati wowote Raisi Samia anajiuliza utajiri wa kasi wa mtoto wake Abdul unavyotazamwa na Watanzania, kuanzia mawaziri hadi watu wa serikali za mitaa na kwingineko, na unakuwa na athari gani kwa uaminifu wa viongozi na watu walio na fursa za kuiba fedha za serikali? Kwa nini watu wawe waaminifu wakiwa na perception kwamba hata Ofisi ya Raisi nchini haya mambo yanafanyika?

Watanzania wote wamesikia juu ya yale Makonda aliyofunua kule Arusha, na Watanzania wote wanatambua aliyofunua Makonda ni tone dogo sana katika bahari ya wizi wa fedha za serikali unaofanyika nchini kwa sasa. Leo mpeleke Makonda Morogoro, Mbeya, Iringa, Tanga nk, atakutana na yale yale anayoibua Arusha - wizi, wizi, wizi!

Sasa ni wakati wa kikiri kwamba tatizo la wizi nchini ni tatizo linalotokana na udhaifuu wa Ofisi ya Raisi katika kusimamia nidhamu ya fedha na uongozi nchini, na imefikia mahali hakuna mtu anaemuogopa Raisi Samia katika kufanya ufisadi na kuiba. Jambo mojawapo la kisaikolojia, ni kwamba inawezekana watu hawana uoga na kuiba chini ya uongozi wa Raisi Samia kwa sababu hawamwogopi raisi mwanamke, au labda wameona hana ukali au weupe wa kukemea wizi wa fedha za serikali, au kwa sababu tu ya perception kwamba hata Ofisi ya Raisi kuna hizi tabia za kujinufaisha kibinafsi na fedha za serikali.

Sasa je, suluhisho ni nini? Je, suluhisho liko ndani ya CCM au labda chama cha upinzani kuiondoa CCM madarakani?

Ukiniuliza maoni yangu binafsi, nitakuambia sioni ndani ya CCM kiongozi ambae anaweza kuwa mbadala wa Raisi Samia na kuweza kurudisha nidhamu ya fedha za serikali. Niambie, nani? Wale wote wanaotamani kushika nafasi ya uraisi, wote ukiwaangalia unaona kabisa huyu hawezi, na wala yule hawezi. Sioni mtu ndani ya CCM mwenye uwezo wa kurekebisha hali tuliyofikia Tanzania. Nani, Mpango? Makamba? Mwigulu? Majaliwa? Biteko? Jafo? Bashungwa? Hakuna hata mmoja, wote wameshaambukizwa kirusi cha kutoweza na kuweka maslahi ya chama na ukada mbele ya maslahi ya Tanzania.

Basi je, suluhisho liko nje ya CCM kwenye vyama vya upinzani? Tundu Lissu? Zitto Kabwe nk? Inawezekana, lakini ni jambo ambalo haliwezekani kusema Lissu au Ziito kwa mfano, wachukue nafasi ya Uraisi na nchi iwe chini ya uongozi wa vyama vyao. Hilo halitatupeleka popote.

Maoni yangu ni kwamba imefikia wakati tufikirie kuuna serikali ya mseto ambayo itajumuisha vyama vyote vya upinzani, ili tujipange upya. CCM peke yake, au Chadema peke yake, au ACT wazalendo peke yake, hawezi kututoa hapa tulipo. Lazima tutafute namna ya uwajibikaji wa serikali kwa kuwa na serikali ya mseto ambayo hivi vyama vya siasa nchini vitalazimika kufanya kazi pamoja kwa maslahi ya Tanzania, hapo tunaweza kufanikiwa.
Kwenye watu wengi huwezi kukomesha wizi unacho weza ni kudhibiti
 
Nadhani tuko pamoja. Taasisi imara bila mtu imara haitasaidia kama vile tu kuwa na mtu imara bila taasisi imara

..tumejaribu mambo mengi lakini bado hatujatengeneza taasisi na mifumo imara.

..hebu tujaribu kuandika Katiba Mpya bora itakayolinda maslahi ya wananchi, na vilevile kuwalinda wanaozingatia maadili na utawala bora.

..katiba ya sasa hivi imetengeneza Raisi-mungu-mtu. Na inalinda wezi wa rasilimali zetu.
 
Nadhani tuko pamoja. Taasisi imara bila mtu imara haitasaidia kama vile tu kuwa na mtu imara bila taasisi imara
Ukiwa na taasisi imara kila mtu anafanya kazi kulingana na taratibu za kazi. Hata taasisi za kusimamia nidhamu zinakuwa vibrant. Na ile kauli ya "Pengo lako haliwezi kuzibika" inakuwa haina uhalali wowote pindi mtu mmoja (imara) akiondoka.
 
..tumejaribu mambo mengi lakini bado hatujatengeneza taasisi na mifumo imara.

..hebu tujaribu kuandika Katiba Mpya bora itakayolinda maslahi ya wananchi, na vilevile kuwalinda wanaozingatia maadili na utawala bora.

..katiba ya sasa hivi imetengeneza Raisi-mungu-mtu. Na inalinda wezi wa rasilimali zetu.
Sahihi kabisa.
 
Tumefikia mahali ambapo hali ya wizi na ufisadi wa fedha za serikali inatisha. Si Tamisemi tu, bali hata vyombo vya usalama na taasisi za serikali ugonjwa ni huo huo. Udanganyifu katika mifumo ya malipo imekuwa ndio habari ya mjini, kuanzia tozo za kupaki magari, fine za trafiki, miamara ya serikali za mitaa na serikali kuu, mashirika ya umma nk, ni wizi, wizi, wizi tu!

Watu siku hizi hawana uoga tena. Kwa wale waliompenda Magufuli na ambao hawakumpenda, wote lazima tukiri kwamba katika uongozi wake watu waliogopa kufanya wizi kama huu unaofanyika sasa.

Sasa tujiulize, kwa nini watu hawana uoga tena wa kufanya ufisadi na wizi hadi kufikia kiwango hiki?

Bila aibu wala upendeleo, twapaswa kukiri kwamba kuongezeka sana kwa wizi na ufisadi chini ya Raisi Samia kunachangiwa na watu kuona kwamba (perception) kuanzia ofisi ya Raisi mwenyewe, mawaziri nk, kumekuwa na viongozi na hata mawaziri wapigaji wengi tu. Kama hatutaoneana aibu, basi lazima tuseme uongozi wa Raisi Samia ndio tatizo na ndio unafanya watumishi wa serikali, mashirika na hata vyombo vya usalama kuwa na udiriki wa kuiba kwa kiwango hiki, jambo ambalo tunakiri wasingethubutu kufanya wakati wa Magufuli.

Wengi wetu tunaona kwamba Raisi Samia mwenyewe alihalalisha wizi wa fedha za serikali pale alipotoa kauli kwamba kila mtu atakula kwa urefu wa kamba yake, kauli ambayo japo anajua imeleta utata, hajawahi kuirekebisha. Raisi Samia anapaswa aelewe kichocheo kikubwa cha wizi uliopo ni perception kwamba kama Raisi amekuwa akitoa fursa nyingi za kutajirisha ndugu zake wa karibu na mbali (nepotism), na sasa hata mawaziri wake na watu wengine kwenye mashirika na serikali kuu na za mitaa wanaona ni halai kujitajirisha kwa kuiba fedha za serikali. Hivi inafikia wakati wowote Raisi Samia anajiuliza utajiri wa kasi wa mtoto wake Abdul unavyotazamwa na Watanzania, kuanzia mawaziri hadi watu wa serikali za mitaa na kwingineko, na unakuwa na athari gani kwa uaminifu wa viongozi na watu walio na fursa za kuiba fedha za serikali? Kwa nini watu wawe waaminifu wakiwa na perception kwamba hata Ofisi ya Raisi nchini haya mambo yanafanyika?

Watanzania wote wamesikia juu ya yale Makonda aliyofunua kule Arusha, na Watanzania wote wanatambua aliyofunua Makonda ni tone dogo sana katika bahari ya wizi wa fedha za serikali unaofanyika nchini kwa sasa. Leo mpeleke Makonda Morogoro, Mbeya, Iringa, Tanga nk, atakutana na yale yale anayoibua Arusha - wizi, wizi, wizi!

Sasa ni wakati wa kikiri kwamba tatizo la wizi nchini ni tatizo linalotokana na udhaifuu wa Ofisi ya Raisi katika kusimamia nidhamu ya fedha na uongozi nchini, na imefikia mahali hakuna mtu anaemuogopa Raisi Samia katika kufanya ufisadi na kuiba. Jambo mojawapo la kisaikolojia, ni kwamba inawezekana watu hawana uoga na kuiba chini ya uongozi wa Raisi Samia kwa sababu hawamwogopi raisi mwanamke, au labda wameona hana ukali au weupe wa kukemea wizi wa fedha za serikali, au kwa sababu tu ya perception kwamba hata Ofisi ya Raisi kuna hizi tabia za kujinufaisha kibinafsi na fedha za serikali.

Sasa je, suluhisho ni nini? Je, suluhisho liko ndani ya CCM au labda chama cha upinzani kuiondoa CCM madarakani?

Ukiniuliza maoni yangu binafsi, nitakuambia sioni ndani ya CCM kiongozi ambae anaweza kuwa mbadala wa Raisi Samia na kuweza kurudisha nidhamu ya fedha za serikali. Niambie, nani? Wale wote wanaotamani kushika nafasi ya uraisi, wote ukiwaangalia unaona kabisa huyu hawezi, na wala yule hawezi. Sioni mtu ndani ya CCM mwenye uwezo wa kurekebisha hali tuliyofikia Tanzania. Nani, Mpango? Makamba? Mwigulu? Majaliwa? Biteko? Jafo? Bashungwa? Hakuna hata mmoja, wote wameshaambukizwa kirusi cha kutoweza na kuweka maslahi ya chama na ukada mbele ya maslahi ya Tanzania.

Basi je, suluhisho liko nje ya CCM kwenye vyama vya upinzani? Tundu Lissu? Zitto Kabwe nk? Inawezekana, lakini ni jambo ambalo haliwezekani kusema Lissu au Ziito kwa mfano, wachukue nafasi ya Uraisi na nchi iwe chini ya uongozi wa vyama vyao. Hilo halitatupeleka popote.

Maoni yangu ni kwamba imefikia wakati tufikirie kuuna serikali ya mseto ambayo itajumuisha vyama vyote vya upinzani, ili tujipange upya. CCM peke yake, au Chadema peke yake, au ACT wazalendo peke yake, hawezi kututoa hapa tulipo. Lazima tutafute namna ya uwajibikaji wa serikali kwa kuwa na serikali ya mseto ambayo hivi vyama vya siasa nchini vitalazimika kufanya kazi pamoja kwa maslahi ya Tanzania, hapo tunaweza kufanikiwa.
Leo naapa kueleza ukweli.Unataka nieleze ukweli?
 
Kipindi cha jpm ndo wizi ikithiri ukiongozwa na jpm mwenyewe ila hakuna chombo cha habari chochote kilichokuwa na ubavu wa kulipoti kama sas ambapo mengine ni uonvo lla vimeachwa vyote vikue bwana mwenye shamba atakuja kuchambua magugu na ngano. Viva samia kupro.otd freedom of speech
Unajua JPM hakuwa mwizi wa kiasili. JPM alitaka kuwa na fedha ambazo angezitumia anavyotaka yeye bila mambo ya bajeti ya Bunge. Kwa hiyo alikuwa anachukua fedha kutoka taasisi mbalimbali kama Bandari, na kuziweka ambako haijulikani. Ndio zile trilioni 15 CAG alisema hajui zilienda wapi.

Kuna wakati hata alitoa maagizo barabara zijengwe bila bajeti ya Bunge, akisema fedha nitatoa, kwa sababu alikuwa nazo. Hata kitengo cha wasiojulikana kiliendeshwa kwa hizo fedha ambazo zilikuwa hazina hata accountability.

Ndio maana alipokufa, watu wachache waliojua ziko wapi walianza kuzihamishia account zao, Samia akatoa amri kwa benki zote wasimamishe transaction kubwa zote za ndani kwa miezi mitatu. Walikuwa wakizitafuta hizo fedha, na sijui kama walizipata.

Sasa huo ndio ulikuwa wizi wa Magufuli
Ukiwa na taasisi imara kila mtu anafanya kazi kulingana na taratibu za kazi. Hata taasisi za kusimamia nidhamu zinakuwa vibrant. Na ile kauli ya "Pengo lako haliwezi kuzibika" inakuwa haina uhalali wowote pindi mtu mmoja (imara) akiondoka.
Nchi kama South Africa, Zimbabwe, wana utaratibu mzuri sana wa kitaasisi. Lakini unaona madudu yanayofanyika?
 
Back
Top Bottom