Uchaguzi 2020 Yaliyojiri kwenye kampeni za Mgombea Urais wa CHADEMA, Tundu Lissu kwenye Mikoa ya Manyara na Arusha

Uchaguzi 2020 Yaliyojiri kwenye kampeni za Mgombea Urais wa CHADEMA, Tundu Lissu kwenye Mikoa ya Manyara na Arusha

Ndugu Lissu, tupe majibu ya maswali haya kabla ya tarehe 28/10/2020.
====
Nawashukuru Jamiiforum.com kwa kutoa furusa hii ya kuuliza maswali. Nina imani mlengwa atayatendea haki maswali yetu kwa kuyajibu kwa ufasaha na kwa staha.

Maswali yangu ni haya kwa kuanzia.
1. Miaka kadhaa iliyopitia, Mtanzania mwenzetu ndugu Lissu, ukiwa bado mbunge ulinukuliwa ukiitakia mabaya Tanzania na watanzania wote hasa wale wenye uwezo mdogo kiuchumi. Ndugu Lissu ulinukuliwa ukisema kuwaunaitaka dunia/ ulimwengu iifungie/ iwekee vikwazo vya kiuchumi, kidiplomasia, kisiasa, kijamii na mengine kama hayo, yaani dunia itemee mate Tanzania. Kwa uhalisia vikwazo hivi vilipotumika kwenye nchi nyingine mfano Zimbabwe, Iran, hata Venezuela uathiri wananchi wenye vipato vya chini na kati, ambao kwa hapa Tanzania ndio walio walio wengi.

Je, Katika mazingira kama haya Watanzania hawa, sisi, tulio wengi tutapa sababu gani za kukuamini kuwa unaweza kuwa kiongozi wa nchi yetu na kujali maslahi ya nchi hii na watu wake wakati kwa vikwazo ulivyotuombea sisi vitupate vina lenga kukuimarisha wewe binafsi mbele ya wale ambao hawatutakii mema sisi watanzania na nchi yetu kwa ujumla wake!?

2. Siku kadhaa zilizopita ukiwa Mkoani Kilimanjaro, ulinukuliwa kupitia vyombo vya habari ikiwemo televisheni ya ITV ukisema kuwa utarudisha madaraka kwa wananchi kama ilivyokuwa wakati wa Ukoloni. Tulio wengi tunajua wakati wa ukoloni watanzani/wananchi walifanywa manamba na wengine kuuzwa nje kama watumwa.

Je, Kwa kauli hii sisi watanzania tutaachaje kuamini kuwa kipindi tu Ndugu Yetu Lissu utakapopata madaraka ya nchi hii utatuuza watanzania kwa mafungu kama bidhaa sawa na kipindi cha Ukoloni na hivyo ni halali tukunyime kura!?

3. Vyombo kadhaa vya kimataifa na baadhi vya humu nchini vimeandika habari kuwa unasimamiwa na mwansheria wa kimataifa ambaye si mtanzania. Pia wakati wamchakato wako wakupat nafasi ya kugombea inasemwa ulishawishi wajumbe wa mkutano kuvuruga wimbo wa Taifa kwa kuongeza maneno ambayo hayapo. Je, Kwa mambo yote mawili yaliyotajwa sisi watanzania tunakosaje haki ya kukunyima kura kwa kuonyesha unatudharau watanzania na pia unadharau mambo yanayotambulisha utanzania wetu!?

Karibu kwa majibu.

Source:Uchaguzi 2020 - EXCLUSIVE: Maswali kwa Mgombea Urais wa JMT, Tundu Lissu kutoka kwa Watanzania watumiao mitandao ya kijamii
====
Haya nitakujibu mimi tu , ni mepesi sana !
 
Endelea kuwakera Lissuuu.... Hadi waote nywele mwaka huu.
Huku siku zikiyoyoma kuelekea siku ya Uchaguzi Mkuu, mgombea Urais anayependwa na wengi na ambaye anatarajiwa kushinda kiti hicho kwa zaidi ya 70% Tundu Lissu leo anaendelea na kampeni za kuomba nafasi hiyo kubwa kwenye Mikoa ya Manyara na Arusha .

Kama kawaida mimi mtumishi wako nitakuletea kila kinachochijiri kutoka kote inakofanyika mikutano hii .

Endelea kubaki hapa hapa JF kwa taarifa za uhakika

" TANZANIA MPYA OYEEE , RAIS MPYA OYEEE "

View attachment 1603756

=======

Babati

[16:00, 10/18/2020] New Makene Tumaini Chadema: Mkutano mkubwa wa kampeni za uchaguzi kwenye viwanja vya kwa Raha, wilayani Babati, mkoani Manyara.

Mheshimiwa Tundu Lissu akiongea na wananchi wa Babati.

Ahsanteni sana watu wa Babati kwa mapokezi na wingi wenu hapa leo. Lakini nawapa pole kwa kuumizwa kwenye hii miaka mitano. Miaka hii mitano iliyopita ni miaka ya ajabu, nalakusikitisha zaidi kwa mara ya kwanza kwenye majimbo ambayo tumeshinda mwaka huu hatuna wagombea kwa sababu ya serikali na tume ya uchaguzi wanataka CCM isitoke madarakani. Mwaka huu wagombea 35 Chadema wameenguliwa kwasabau binafsi za tume.

Watu wa Babati zimebaki siku 10, tutapiga kura Kwenye mazingira haya Haya magumu na tutashinda uchaguzi. Kitu pekee walichobaki Nacho MaCCM ni Tume ya uchaguzi. CCM wamekosa kibali cha wananchi, mikutano yao sasahivi wanakodisha wasanii. Mwaka 2015 Magufuli alikuwa anapiga push-up Ila mwaka huu anapiga magoti. Babati tarehe 28 twende tukapige kura ya ukombozi na tumshinde Magufuli na washirika wake.

Magufuli ni mtu wa ovyo, amejenga kiwanja cha ndege Kwao, lakini wananchi hawana maji. Amejenga kanisa kubwa akaliita St. Joseph akawaambia wakatoliki mje msali hapa, akaambiwa sisi hatujengewi makanisa. Magufuli amekuwa raisi wa ovyo.

Babati kwenye hii miaka mitano tumeumizwa,........


Babati zimebaki siku 10 kuelekea uchaguzi mkuu, sasa nataka niwaambie kuhusu hatari..

- Hatari ya kwanza nikuapishwa kwa Mawakala. Sheria inataka mawakala lazma waapishwe. Sasa CCM watataka mawakala wetu wasiapishwe. Tume na Wakurugenzi wanawajibu wakuwaapisha mawakala na wasipo waapisha wanataka ugomvi. Hakikisheni Mawakala wanaapishwa na wasipowaapisha wanataka ugomvi wapeni ugomvi.

- Hatari ya pili ni mawakala kuingia kwenye vituo. Tume itataka mawakala wetu wasiingie kwenye vituo. Sheria inasema tunahaki kuwa na mawakala, sasa tume wakitaka kuwazuia ni wanataka ugomvi na tuwape ugomvi.

- Hatari ya Tatu ni mawakala kunyimwa formu ya matokeo, kila wakala ana haki kupata nakala za matokeo. Formu ya matokeo ni ushahidi wa Matokeo kwenye kituo husika. Nakupewa matokeo ni muhimu.

Hatari ya nne ni CCM watatengeneza vituo hewa. Kila mahali kuna orodha ya vituo, hakikisheni mnakuwa na orodha Ili wasije wakaingizie. Hakikisheni hamuendi kwenye majumuisho ya kura.

- Hatari ya Tano ni kwenye kutangaza matokeo. Dawa yakuwazuia wasitangaze mtu ambaye hajashinda, ikifika saa sita hakikisheni mna formu za matokeo mmejumlisha matokeo na mkiona mmeshinda ingieni mtaani ijulisheni dunia. Sio kosa la jinai ukijua umeshinda na ushahidi unao ukajitangaza. Lazima tuache uoga ili tusikubali kuibiwa.

Babati tutashinda uchaguzi huu sababu watanzania wameshaamua na watafanya maamuzi, tutangazwa kwa heri au kwa shari. Jana mpwa wake Magufuli yule Kheri James wamesema hawatatumia risasi ila watatumia sindano za sumu, sasa sasa kama wanataka kufanya mchezo kuchezea uchaguzi huu wataishia thé Hegue. Wataishia kuwa wafungwa wahalifu wa Kimataifa wafanye hayo wanayoyasema.

Mwisho Babati nawaomba mtupe serikali, tupeni mamlaka tulinde haki yako na maslahi yako. Chadema tutatengeneza serikali itakayojali uhuru, haki na maendeleo ya watu.

Ahsanteni Babati na Mungu awabariki sana.

View attachment 1603956

View attachment 1603756
View attachment 1603942
View attachment 1603956View attachment 1604113View attachment 1604114View attachment 1604115View attachment 1604116View attachment 1604117View attachment 1604118View attachment 1603756
View attachment 1603942
View attachment 1603956View attachment 1604113View attachment 1604114View attachment 1604115View attachment 1604116View attachment 1604117View attachment 1604118View attachment 1604119View attachment 1604120View attachment 1604121View attachment 1604122View attachment 1604123
 
Maendeleo ya watu-Uwekezaji kwa rasilimali watu (mfano bima ya afya kupitia SWF ya gesi). Maana haina maana ya kuwekeza zaidi ya trillion 6 kwenye mradi ilihali vijana wanalia hawana mitaji ya biashara au wakulima wanalia hawana masoko au pesa za kuwekeza kilimo cha umwagiliaji.

Haki- Utawala wa sheria na siku 100 za kwanza anaanza na kuleta katiba mpya. Ataanzisha taxpayer bill of rights ili kuguarantee haki za mjasiriliamali kwenye masuala ya kodi na mifumo inayohusika.

Uhuru- Kuleta soko huria haswaa ambalo serikali haiingilii utendaji kazi wake ila inakua regulator tu. Vyombo vya habari kutoingiliwa uhuru. Wafanyabiashara kufanya kwa uhuri bila hofu ya TRA kuwalimbikizia makodi makubwa.

Karibu tujadili mapungufu au faida ya hizi sera zake.
Wewe ni moja kati ya watu ambao wanahitaji kusaidiwa juu ya matumizi yako ya akili! Ili kukusaidia, itabidi tukuamulie nani awe kiongozi was nchi yako, upige au usipige kura, tutakuamulia!
Nisamehe bure kama nimejukwaza ila ukweli ndio huo, no way out! Ahsante, waambie na wenzio!
 
IMG_20201017_221108_276.jpg

Maendeleo ya vitu sio kabisa makamanda. Maendeleo ya watu ndio kila kitu.
 
Wewe ni moja kati ya watu ambao wanahitaji kusaidiwa juu ya matumizi yako ya akili! Ili kukusaidia, itabidi tukuamulie nani awe kiongozi was nchi yako, upige au usipige kura, tutakuamulia!
Nisamehe bure kama nimejukwaza ila ukweli ndio huo, no way out! Ahsante, waambie na wenzio!
Nmeleta sera yake umeshindwa ichambua unaanza kuleta propaganda.

Mtaji wa CCM ni watu wenye IQ ndogo kma ww. Nina uhakika hta ilani ya CCM hujasoma ila unashabikia tu bila reasoning!!

Hvi nkikuhoji Ajira million mbili mlizoahidi 2015 ziko wapi utajibu nni? Viwanda je? Embu tusivurugiane usiku
 
View attachment 1604230
Maendeleo ya vitu sio kabisa makamanda. Maendeleo ya watu ndio kila kitu.
Wanaposema ndege sio kipaumbele hawamaanishi watu binafsi wasiwekeze kwenye aviation la hasha bali hela ya kodi ambayo inapaswa iwe reallocated kwa wote ielekezwe eneo ambalo linagusa maisha ya watu moja kwa moja.

Mfano viwanda au kutoa mitaji ya biashara, bima ya afya kwa wote ama kilimo cha umwagiliaji n.k.

Tatizo hamuelewi context ndio maana mkisimama utaskia hawatako barabara!! Hvi nani hajui umuhimu wa ndege? Ila je ndio eneo ambalo serikali ilipaswa kuwekeza kwa sasa? Unafahamu ooprtunity cost kma wangewekeza kwenye kilimo cha umwagiliaji? Unadhani kuna mpinzani angeinua mdomo?
 
angekuwa anahangaika sidhani kama angekuwa kapiga kampeni sehem zote alizotembelea.....kama huna hoja funga domo au cheki cartoon maybe ndio saiz yako na wana lumumba wenzako
Mbowe anafuja pesa za hilo genge, nyie washabiki mwatoa povu na kichangishwa kizwazwa kabisa. Hiyo saccos ya Mbowe, ni 100% mali yake mwenyewe. Watanzania makini hatuwezi chagua upuuzi, Lissu hawezi kuwa Rais wa Watanzania milele.
 
1. Sijaona swali la kisera zaidi ya speculations. 2. Sasa kweli tuuzwe kma manamba kweli? 3.Kuna nchi inakubali human slavery karne hii?

4. Vikwazo hta Mandela na Nyerere waliomba sauzi na Rhodesia ziwekewe vikwazo ili kupressure serikali zilizokua madarakani 5. je Nyerere hakujua waathirika watakua wale waafrika maskini?

6.Inaonekana uelewa wako ni mdogo wa kutofautisha nchi na serikali. 7.Yaani Lissu akipambana na magufuli mnadai anapambana na wananchi!!! 8.Hvi hamfundishwi masomo ya uraia huko mashuleni?
Bora umejaribu kujitutumua kuokoa jahazi...maana wana Sumbawanga (Taja kabila), wamekula kona!!! Ha ha haaa! Turudi kwenye hoja zako.
===
1. Aisee, ebu nipe shule kwanza. Maswali ya kisera yakoje!? Unasema umeona speculations, katika maswali karibu yote nimetoa chanzo ama msingi wa swali tena kwa ushahidi! Iweje utwambie kuwa maswali yale ni speculations!? Ama unataka kutengeneza "definition " mpya ya speculations!

2. Kuuzwa kupo, Mkuu, dunia hii! Hivi unajua kwa nini kuna sheria kali za kuzuia " human trafficking" karibu kila nchi duniani!? Mkuu, kuna bilionea wa fedha za dola za Marekani, inasemekana alijiua kiwa mahabusu huko huko US!! Bilionea huyu inasadikika alikuwa nabiashara haramu ya kuwa'uwauza' watoto kwa matajiri wenzake na watu wengine mashuhuri kwa mambo ya 'starehe' haramu! Taarifa zilizopo huyo bilionea alikuwa anawanunua !! Wahathirika wakubwa biashara ya bilionea huyo ni Thailand na Indonesia na nchi nyingine za Latin Amerika!

3. Hakuna nchi inakubali slaverly karne hii wazi wazi, lakini kuna baadhi ya nchi za Mashariki ya Kati, zinatuhumiwa kuruhusu mfumo wa kupata wafanyakazi na ufanyakazi nchini humo kuwa na chembechembe za " u- slaverly "! Najua utauliza nitoe mfano! Sawa, Mkuu, Unajua namna wapiganaji wa vikundi vya kigaidi wanavyopatikana!!? Ukiuchimba mfumo wa upatikanaji wa wapiganaji hawa hasa huko Mashariki ya kati na Afrika Ya kati na hata kule kwa Durtete bara Asia utagundua, kwa namna moja ama nyingine zipo nchi karne hii zinafanya Slaverly! Maelezo haya, yanadhibitisha uwepo wa " utumwa mambo leo".

4.Mkuu, sasa nimeelewa kweli Lissu amewanyesha sumu za uongo kuwa wakati wa ukoloni, Madaraka yalikuwa kwa wananchi!!! Mnatia aibu sana!! Yaani unafikiria Rhodesia chini ya Smith wananchi wakati nuo walikuwa na hali nzuri ya maisha kiasi kwamba kwa Serikali dhalimu za Rhodesia kuwekewa vikwazo, wananchi/ waafrika wenzetu walikuwa waathirika wakubwa !?

Duh!! Umenishangaza sana!! Hata hivyo, kama kweli ulielewa vyema nia ya Mwalimu Nyerere na wenzake wakati huo, ebu uwaambie umma wa wanaJF, ni vikwazo vya aina gani Nyerere na wenzake walitaka ziwekewe serikali za kikoloni za Rhodesia!! Pia ujiulize kama Vikwazo ambavyo alitaka serikali ya Tanzania na wananch wake wawekewe viko sawa na vya Mwalimu Nyerere na wenzake!!!

5. Rejea point namba 4 hapo juu.

6.Naam kwa uelewa wako mkubwa ebu tupe ufafanuzi wa hoja yako hii na uioanishe na maelezo niliyotoa kwa maswali niliyomuuliza mgombea Ndugu Lissu!

7.Hii hoja nimeshindwa kuihusanisha na maswali niliyomuuliza ndugu Lissu, ebu dadavua zaidi ulimaanisha nini!

8. Katika hatua nilizopitia za kujifunza nimefanikiwa kufundishwa somo la uraia( basic). Lakini nikiri wazi bila kificho, elimu kubwa zaidi ya uraia ( applied) nimekutana nayo hapa JF. Kuna uwezekano mkubwa, hata wewe Mkuu,Zitto junior, unaweza kuwa mwalimu wangu wa somo la uraia hapa hapa JF.
===
Karibu kuzichaka pointi nane nilizoibua kutokana na bandiko lako hapa jamvini.
 
Nmeleta sera yake umeshindwa ichambua unaanza kuleta propaganda.

Mtaji wa CCM ni watu wenye IQ ndogo kma ww. Nina uhakika hta ilani ya CCM hujasoma ila unashabikia tu bila reasoning!!

Hvi nkikuhoji Ajira million mbili mlizoahidi 2015 ziko wapi utajibu nni? Viwanda je? Embu tusivurugiane usiku
Kama utaendelea kuamini ya kwenye kampeni, lazima usiku wako uvurugike!
 
Sasa imefika patamu.

Katibu Mkuu CCM na yule zezeta Popole ukiwasikiliza wanayonena sasa hivi utajua mkanganyiko tayari umeingia ndani ya chama hicho.

Hata zile 'Fiesta' sasa zimekosa maana; haziongezi chochote kwenye kampeni za mgombea wa chama hicho.

Hapa jamvini, hali haina tofauti. Akina Paskali wenye Njaa na ayohani Mbatizaji na kundi zima wamekuwa wa kuokoteza vijimaneno, au hawaonekani kabisa.

Hakika kuna jambo kubwa linategemewa kutokea hivi karibuni.

Huyu Jamaa aliyebugia shaba zaidi ya 16, ndio kwanza anaonekana kama kaongezewa damu mpya na nguvu zisizoelezeka zinatoka wapi!
Na yule mwenzake, zile 'pushup, safari hii zimegeuka na kuwa kutambaa kwa magoti, akiwalilia aliokuwa akiwafokea kama watoto wasimtupe mkono.

Lakini wapiga kura wasisahau, kiongozi anayekuwa juu ya sheria na katiba iliyomweka madarakani, wakifanya makosa baada ya kushuhudia yaliyofanyika, wakumbuke yatakayofuata wakifanya makosa tena safari hii, hawataishi kuyasahau.
Akirudi hatutalimia meno,sijui tutalimia kitu gani,naona hali itakuwa ngumu zaidi ya hii miaka 5,kuminywa kwa haki kutaongezeka maradufu.
 
Ndugu Lissu, tupe majibu ya maswali haya kabla ya tarehe 28/10/2020.
====
Nawashukuru Jamiiforum.com kwa kutoa furusa hii ya kuuliza maswali. Nina imani mlengwa atayatendea haki maswali yetu kwa kuyajibu kwa ufasaha na kwa staha.

Maswali yangu ni haya kwa kuanzia.
1. Miaka kadhaa iliyopitia, Mtanzania mwenzetu ndugu Lissu, ukiwa bado mbunge ulinukuliwa ukiitakia mabaya Tanzania na watanzania wote hasa wale wenye uwezo mdogo kiuchumi. Ndugu Lissu ulinukuliwa ukisema kuwaunaitaka dunia/ ulimwengu iifungie/ iwekee vikwazo vya kiuchumi, kidiplomasia, kisiasa, kijamii na mengine kama hayo, yaani dunia itemee mate Tanzania. Kwa uhalisia vikwazo hivi vilipotumika kwenye nchi nyingine mfano Zimbabwe, Iran, hata Venezuela uathiri wananchi wenye vipato vya chini na kati, ambao kwa hapa Tanzania ndio walio walio wengi.

Je, Katika mazingira kama haya Watanzania hawa, sisi, tulio wengi tutapa sababu gani za kukuamini kuwa unaweza kuwa kiongozi wa nchi yetu na kujali maslahi ya nchi hii na watu wake wakati kwa vikwazo ulivyotuombea sisi vitupate vina lenga kukuimarisha wewe binafsi mbele ya wale ambao hawatutakii mema sisi watanzania na nchi yetu kwa ujumla wake!?

2. Siku kadhaa zilizopita ukiwa Mkoani Kilimanjaro, ulinukuliwa kupitia vyombo vya habari ikiwemo televisheni ya ITV ukisema kuwa utarudisha madaraka kwa wananchi kama ilivyokuwa wakati wa Ukoloni. Tulio wengi tunajua wakati wa ukoloni watanzani/wananchi walifanywa manamba na wengine kuuzwa nje kama watumwa.

Je, Kwa kauli hii sisi watanzania tutaachaje kuamini kuwa kipindi tu Ndugu Yetu Lissu utakapopata madaraka ya nchi hii utatuuza watanzania kwa mafungu kama bidhaa sawa na kipindi cha Ukoloni na hivyo ni halali tukunyime kura!?

3. Vyombo kadhaa vya kimataifa na baadhi vya humu nchini vimeandika habari kuwa unasimamiwa na mwansheria wa kimataifa ambaye si mtanzania. Pia wakati wamchakato wako wakupat nafasi ya kugombea inasemwa ulishawishi wajumbe wa mkutano kuvuruga wimbo wa Taifa kwa kuongeza maneno ambayo hayapo. Je, Kwa mambo yote mawili yaliyotajwa sisi watanzania tunakosaje haki ya kukunyima kura kwa kuonyesha unatudharau watanzania na pia unadharau mambo yanayotambulisha utanzania wetu!?

Karibu kwa majibu.

Source:Uchaguzi 2020 - EXCLUSIVE: Maswali kwa Mgombea Urais wa JMT, Tundu Lissu kutoka kwa Watanzania watumiao mitandao ya kijamii
====
Najibu original post yako maana naona unatanua mjadala kwa irrelevant issues.

1. Vikwazo alivyotaka nyerere vilikua vya kiuchumi huko Sauzi na Rhodesia, mpaka kushiriki masuala ya kimataifa walifungiwa je ina maana Mandela na Nyerere walisaliti watu weusi kwa kulilia vikwazo?
Jibu ni kwamba Serikali na Nchi ni vitu viwili tofauti ndio maana Nyerere alipeleka majeshi kupigana na Idd Amin lakini sote tunajua wananchi waliathirika sana na ile vita na hizo ndio cost za kudai uhuru. Serikali ikiminywa itasurrender otherwise itapinduliwa na wananchi kupitia sanduku la Kura maana ndio imewaingiza kwenye shida.
Kwahiyo Lissu anapambana na serikali sio wananchi otherwise unionyeshe kivp Mandela na Nyerere kuomba vikwazo vya uchumi haifanani na Lissu. Weka hapa hizo tofauti.

2. Kurudisha uongozi kwa wananchi kma enzi za ukoloni. Sasa mtu akisema tujenge reli kma ilivyokua enzi za ukoloni ina maana anaongelea biashara ya utumwa? Au kaongelea specifically reli.

Usilete speculation, yye kasema anaiga administration ambayo ni decentralized ssa wapi alisema ata replicate na mambo mengine ya hao wakoloni?

Kwanini unaleta speculation?

Bottom line sera ya majimbo ya CHADEMA ndio sera kuu ya chama na ndio Lissu anasimamia so usiende out of context. Afterall slave trade haina soko sahvi maana dunia inainvest kwenye AI hao wa biashara za watu ni mahousegirl na mabarmaid tena kwa black market ambayo inafanywa na mtu yeyote tu sio mpaka awe rais.

3. Speculation nyingine!! Ni wapi hapo alisema waongeze ubeti!! Hiyo ni idea za vijana wa hamasa kina Twaha Mwaipaya sasa Lissu anahusikaje na u-MC wa mikutano?
Hakuna sheria inakataza kuwa na wanasheria wa kimataifa ndio maana hta CCM mmeafiki sheria ya permanent sovereignty ikubali suala la arbitration kufanyika nje ya nchi!! Otherwise unaleta double standard.

Una jingine?
 
Kama utaendelea kuamini ya kwenye kampeni, lazima usiku wako uvurugike!
Kipi cha kwenye kampeni? Mliahidi kwenye ilani hivyo iliwekwa kwenye mpango wa maendeleo wa miaka 5!!

Shida hamsomi mnakimbilia kucomment tu mitandaoni. Na nyie ndio mtaji wa CCM, elimu ndogo hta kuchambua ilani na bajeti hamuwezi!!

Huyo JPM toka aingie madarakani hakuna bajeti imetekelezwa kwa hta 70% ila wanaCCM wangapi wanajua?

Endeleeni tu kushabikia ujinga
 
Kipi cha kwenye kampeni? Mliahidi kwenye ilani hivyo iliwekwa kwenye mpango wa maendeleo wa miaka 5!!

Shida hamsomi mnakimbilia kucomment tu mitandaoni. Na nyie ndio mtaji wa CCM, elimu ndogo hta kuchambua ilani na bajeti hamuwezi!!

Huyo JPM toka aingie madarakani hakuna bajeti imetekelezwa kwa hta 70% ila wanaCCM wangapi wanajua?

Endeleeni tu kushabikia ujinga
Kwa ujinga huo, tutakuamulia tena safari hii!
 
Naomba mawakara watafutiwe usafiri wa uhakika la sivyo wataporwa fomu za matokeo na watu wasiojulikana alafu iwe imetoka hiyo.
 
Back
Top Bottom