Afisa Elimu Jiji La Tanga, wazazi tunaomba ufafanuzi wa hii michango ya fedha

Afisa Elimu Jiji La Tanga, wazazi tunaomba ufafanuzi wa hii michango ya fedha

Najiulizaga sana juu ya elimu ya siku hizi...!!!? Yani Kuna Nini kipya!!? Watoto wakomae kiasi hicho...
 
Kwa mwendo huu shule za private zitaendelea kuwa juu. Kuba shule inaitwa Kings secondari ipo Goba, saa kumi na moja napita kwenda job mwalimu yupo class na madogo wanapambana, ww umeambiwa mtoto akafanye pepa jumamosi unalalamika kama mwl anahusika na toto lako. Kama vp kataza bonto lako lisiende af jaribu ujinga

Sent from my Nokia C1 using JamiiForums mobile app
 
Walimu ndo wanafundisha wanaelewa changamoto za watoto wanapojifunza kama hutaki mtoto wako afundishwe muda wa ziada wasiliana nao watamruhusu mapema arudi nyumbani apumzike kama unavyotaka usitafute justification kuharibu mipango mizuri ya walimu kwa hawa watoto.
We need a timetable to be followed upuuzi huu zamani haukuwepo and all was well!
 
Kipi bora kwa mtazamo wako!
Ni bora hilo darasa lenye watoto 200 lenye uangalizi wa huyo mwalimu mmoja kuliko atoke mapema ili akalindwe na shamba boy.
Tunasema tunayo yaona , huwezi kuwa na uangalizi wa watoto 200 darasani, never . How can you control them and make learning take place effectively? Unajua maana ya learning ad how it is effected?
 
SHULE NI SOCIAL ORGANIZATION KUBWA AMBAPO KILA KITU KWA MTOTO ANAKIPATA kwani hata michezo ipo na inakuwa na uangalizi bora kutoka kwa walimu.
unajua kinachoendelea shuleni? Shule ya watot elfu 2 kwa walimu kumi kuna uangalizi gani? Think deep!
 
Pamoja na mambo yote lakini mtoto anatakiwa apate muda wa kupumzisha mwili na akili. Ashiriki kufanya kazi za nyumbani hata kwakiasi kidogo sana.

Ukitazama hao wanao wasaidia wanafunzi muda wa ziada(WENGI WAO) wanalenga hela kwahiyo kama hamna hela huduma haipo.

Maisha yanataka kwenda kwa kazi na kupumzika. Mtatia watoto uwendawazimu
Ulitaka wafanye bure?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hili jambo huwa naliwaza na kulisema kila siku. Nimesoma msingi miaka ya 90. Tuliingia shule saa 2 mpaka saa 8 na hii ilikuwa ni Jumatatu mpaka Ijumaa, darasa la kwanza mpaka la saba.

Sasa najiuliza leo wanafundishwa nini cha ziada kiasi kuwekwa mashule mpaka saa 1 usiku, Jumapili wanakwenda shule pia. Matokeo yakitoka na uoza ule ule.
zamani hakukua na shinikizo la kufaulisha, hata likifeli darasa zima poa Tu. Sasa hiv tamisemi wamekuja na Key performing Indicators, shule zimepewa malengo zifikie, kila mwalim, kila shule, kila wilaya na kila mkoa wanatakiwa kuwa na mpango kazi kufikia malengo.

Heb tuwape ushirikiano walimu maana wanaosaidiwa ni watoto wetu, tusitafute vikwazo tu, Kwanza zamani tulikua tunachelewa Sana kuanza shule, wengi wetu tulianza na miaka 9 ama 10, Sasa hiv miaka hiyo ni la 4 au 5 hivyo hawajielew hata wamefata nini shule. Sisi zamani tulikua tunaulizana maeneo kwenye Atlas, miji mikuu, tuna madaftari tunaandika viongozi wa serikali, mawaziri, wakuu wa wilaya na mikoa, Tulikua na vitabu vya JIANDAE VEMA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI. Kwa kiasi kikubwa tulikua tunajiongoza wenyewe.

Hawa watoto wa sasa hawajakomaa kisawasawa hawana self determination kama tulivyokua Sisi, Siri moja kubwa wanatumia Sana seminary na shule binafsi na kumkeep mtoto busy Kwa kumpa mazoez ya kutosha.Idle brain is a source of evils ndo maana hata private mtoto akirud jioni anakuja homework akifunga shule anakuja na home package anapambana na maswali mpaka shule zinafunguliwa. Kama unataka mtoto acheze mpeleke shule yenye sports academy.
 
Watoto wa saiv wanatakiwa kufundishwa kwa vitendo kuliko kukaririshwa na tatizo waalimu sio wabunifu. Na mitaala imebakia kukaririsha masuala ya vita vya maji maji badala ya kwenda na wakati wa technology. Yanayofundishwa veta yangepelekwa shule ya msingi ingependeza sana
sasa hapo shida ni walimu au wizara?
 
Kuna baadhi ya wazazi wanaoelewa maana ya elimu bora wanaona kugharamika wao ili watoto wao wapate elimu bora japo elimu yetu ndio hivyoo ina changamoto nyingi
Mimi nilikua na mtoto st fransis mbeya, Mtoto akifunga shule anakuja na maswali mengi Sana, Yan akitoka chumbani ni kuja Kula na kurudi chumbani kufanya maswali mpaka wanafungua, mpaka namuonea huruma mtoto. Matokeo kutoka watoto wote one za Saba na nane chache, Nina mtoto mwingine lasaba mwaka huu wazaz tumetoa mil 1 Kwajil ya masomo ya ziada, ELIMU ni gharama, hakuna kizuri chabure
 
Hakika wewe ni fala sana.
Inaelekea huna elimu yoyote ktk bichwa lako.
Shule kama hiyo na zingine za namna hiyo hakuna elimu yoyote wanayopata watoto hapo. Ni mateso na kukonda tu.
Sana sana wanakaririshwa maswali tu. Baada ya miezi 2 au 3 Kila kitu hakuna kichwani.
Walioweka mapumziko ya likizo Kwa ajili ya mtoto walikuwa na akili sanaaaa .
heb ukipata muda fatilia shule binafsi zinazofanya vizuri, unaweza kuta hayo matus umeyapeleka kusiko sahihi
 
We need a timetable to be followed upuuzi huu zamani haukuwepo and all was well!
unaongelea zamani ipi, Kwanza zamani ilikua likizo lazima twende tution maana walimu walikua hawamaliz topics, kama hujaenda tution unakuja kuomba rafiki akufundishe. Zamani hakukua na shinikizo walimu wafaulishe, hivyo ilikua ukikaa kusubir ufundishwe kila kitu imekula kwako. O level nimesoma mpwapwa sec na advance Musoma
 
Mimi kitu ninachoshangaa sio mitihani ila mitihani inatungwa kwa mtaala wa zamani.mitihani ina makosa mengi sana.

Serikali inataka wanafunzi wafaulu wote kwa 100%.kwahyo walimu lazima wajiongeze kwa kila mbinu
mtaala wa zamani ukoje wenye makosa mengi?
 
Sikitai watoto kufanya mitahani hata kila siku. Ila napinga ni kwa nini iwe kila siku mitihani tena asubuhi alfajiri. Elimu anayopewa mtoto ni yakukariri na kufaulu mitahini na wala sidhani kama itamsadia sana mtoto hapo baadae endapo atakosa ajira.

Mtoto wa namna hii anaamini akifaulu mtihani na kupata daraja la kwanza basi atapata ajira nzuri na ndivyo anavyoambiwa na walimu wake. Ifike mahali tuwe wa kweli kuwa sera yetu ya elimu inanapungufu kiasi. Hili la kwenda kufanya mitihani asubuhi alfajiri na kwenda shule jumamosi mpaka jion mimi siliafiki.

Waliopanga ratiba ya masono walikuwa wanaakili timamu na kuna vigezo walizingatia ndio maana wakaweka muda wa kusoma ni kuanzia jumatatu hadi ijumaa tena saa kumi.

Watoto wetu wanahitaji muda wa ziada wa kutembelea ndugu na marafiki, kusaidia wazazi majukumu mbalimbali kama ya shamba na biashara na kurefresh pia. Sasa ukimchukua mtoto wiki nzima unamkaririsha notes kwa ajili ya kufaulu mtihani ni kweli anaweza kifaulu lakini akawa hana maarifa yeyote yatakayomsadia kupambana na maisha ya kwenye jamii maana hayuko familiar na jamii mda mwingi anautumia shule na waalimu wake.

Nakumbuka enzi sisi tunasoma tulikuwa tunamashamba ya shule tunalima, tulikuwa na stadi za kazi na zilitusaidia sana, sasa hivi ambapo dunia inasonga mbele kwenye sayansi na technolojia hii mitaala sina hakika kama bado ipo.

Nilitegemea wanafunzi wa shule zetu hizi watumie mda wa ziada baada ya masomo kufanya mambo ya ziada hasa yanayolenge kutambua vipaji vyao ambavyo vingekuwa ni ajira kwao na pia vingekuwa na msaada mkubwa wa kiuchumi kwa taifa hapo baadae.

Kwa dunia ya leo sanaa, michezo na technolojia ndio vyanzo vikubwa vya mapato kwa watu na nchi pia. Tumeona wanamichezo, wanamuziki, wanariadha waigizaji na wabunifu mbalimbali wanavyojipatia kipato na kuchangia kwenye uchumi wa nchi zao. Mfano mzuri ni wanageria hawa jamaa wamesoma sana lakini pia utawakuta wapo karibu kila ligi kuu ya ulaya wakisakata kabumbu na wanachangia mapato kwa taifa lao.

Utaratibu huu wa ufundishaji kama wa Tanga unaenda kuuwa vipaji vya baadhi ya watoto labda kama wangekuwa wanafundishwa na physical education.

Najua kuna watu humu mtakuja kunipinga bila kuweka ushahidi wenye kueleweka. Kunabaadhi ya ajira zinazotoka na michezo tumeanza kuzipoteza kwa wageni na hii inachangiwa na vijana wetu kubanwa huku mashuleni muda wote bila kuzingatia ratiba hasa za michezo, talent show na sanaa. Tumeona hata kwenye ligi yetu ya sasa tumetawaliwa na wakongomani kila sehemu kuanzia mabeki hadi forward, hatufahamu hizi ni ajira tena zenye mapato makubwa tu. Wachezaji kama Joseph Kaniki Kumbakumba, Emanueli Gabrieli, Sekilojo Chambua, Bonifas Pawasa, Lunyamila, Nteze John Lungu, Ally Mayai Tembele, wazawa hawa waliotawala ligi yetu kipindi mpira haulipi kwa sasa hawapo tena.

Kipindi sisi tunasoma tulikuwa na break yaani mapunziko saa nne asabuhi hadi saa nne na nusu na saa tisa na nusu hadi saa kumi kila siku. Muda huo tuliutumia kucheza mpira, uzwiji, korosho, arita bao au kwenda kudokoa miwa kwenye mashamba ya wahindi au kwenda kuogelea tena kwenye mito yenye vina virefu kwa sisi wanaume na wasichana waliutumia kucheza rede, mdako au kukaa kwenye vikundi vikundi na kujadili mambo yao au ya watu wengine huku wengine wakibaki kuwa watazamaji wa hii michezo. Na hii haikuathiri uwezo wetu wa kitaaluma yaani unamkuta mtu darasani wa moto, kwenye mpira wa moto akipelekwe shamba wa moto na siku za weekend unamkuta kasimamia biashara ya baba yake kama duka au mashine ya kusaga na kule pia ni wa moto. Na hapo bado kunasiku mzee anaweza kukuzuia usinde shule akuchunge ng'ombe au ukang'olee mpunga au ukalinde ngedera mashambani na ukapoteza vipindi vya siku mbili tatu ila ukirudi shule akaandika notes na msela wako akakubrash kidogo unakuwa wa moto.

Baada ya mwanafunzi kujua kusoma na kuandika elimu yetu ilipaswa kumjenga huyo mwanafunzi kuwa mbobezi katika kada fulani, kama ni kilimo, mifugo, uvuvi, michezo ubunifu, biashara siasa n.k la sivyo tutaendelea kuwa na vijana wenye vyeti na ufaulu mzuri ila maarifa madogo, hii itapelekea kila wakati serikali kulalamikiwa kuwa haitoi ajira kwa vijana na ukweli ni kuwa srikali inaajiri kwa vipaumbele, hakuna serikali inayoweza kuajiri graduates wa vyuo vyote na fani zote kila mwaka.
 
1. Kila asubuhi watoto eti wanafanya mitihani. Mtoto anawajibika kuripoti shuleni saa 12 asubuhi na kuanza mtihani saa 12.30 asubuhi.
hiyo mitihani ya alfajiri ni kwa madarasa yote au yale yanayojitayarisha na mitihani mwisho wa mwaka huu?

Halafu mitihani ya kila siku ya nini? Wakifundisha vizuri tu weekdays haina haja ya kuwapa stress wanafunzi kila siku. Weekend tests zinatosha
 
Kuna shule inaitwa Diamond na mwenzie Olympio. Hawa jamaa mpaka jumapili watoto wa darasa la saba wanakwenda shule na wasipoenda walimu wanapiga kama wanapiga mwizi. Ukihoji kama mzazi unaambiwa ndio tushapanga kama shule.

Serikali kuna haja wakaja na kauli moja kuhusu swala la elimu na masaa ya masomo. Tunakoelekea watoto watakuwa hawapati hata muda wa kulala.
Kwa uwingi wa watoto kwa darasa moja pale Olympio na level ya ufaulu wanayopata ni sahihi kabisa njia wanayotumia.Niliangalia matokeo darasa la saba Olympio darasa lina wahitimu zaidi ya 600.Ndiyo maana wazazi wengi wanapeleka watoto wao hapo maana ni nafuu na bado inashindana na shule nyingi za Private zenye ada kubwa.

Walau Wazazi tu appreciate juhudi za walimu kuwapatia elimu watoto wetu.
 
Binafsi sioni tatizo kama lengo ni kumsaidia mtoto afaulu vizuri na pia wazazi punguzeni lawama zisizokuwa na kichwa wala miguu hizo senti za sh 200 ndo zinakufanya upige kelele sidhani kama ujinga utaisha kirahisi Tanzania kama tuna wazazi vichwa maji kama wewe.
 
Waalimu wengi vichwa maji, mtoto unamfundisha saa 11 jioni ana njaa ataelewa nini

Ndo maana watu wanazarau waalimu
Wewe ndio kichwa maji,unafikiri kazi ni kufundisha mda wote!
Njaa ya mwanao unamweleza nani mwenye jukumu la kumlisha?
Mlipie mwanao chakula na stationaries acha kujibebisha.
Wenzio wanasomesha Private na wanalipa pesa nyingi husikii walalamika.
We elfu tatu kwa wiki ushatukana walimu!
 
Back
Top Bottom