Aibu kubwa kwa Taifa taa za uwanja wa Benjamini Mkapa kuzimika mechi ikiwa inaendelea
Kwa hili hata waandaji wa video show mitaani urahumiwa sana na watazamaji na ni aibu sana kwa muandaaji. Ivyo ni aibu kwa nchi ya Tanzania, meneja wa kiwanja. Inatakiwa waadhibiwe wanao sababisha usumbufu huu hasa waziri anayehusika, meneja wa uwanja na watu wa nishati kama ili linawahusu
 
Nashangaa sana katika hili taifa mwanzo walisema Kuna mtu/kibaka alifanya hujuma akakamatwa Sasa leo Tena ni Nini???

Halafu tunaomba kuandaa afcon kwa hali hii tutakubaliwa kuandaa mashindano ya afcon??


Ni aibu kubwa kwa KWELI/tunaaibika kimataifa.
Tuliwaambia meneja wa uwanja hafai aondolewe haraka,wakasingizia kibaka.Inawezekana huyo mtu aliyesingiziwa amehukumiwa tayari,lakini Mungu anawaonesha kuwa haikuwa sahihi kwani mwenye makosa yupo bado kwenye nafasi

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Hii ni mara ya pili baada ya ile mechi ya Taifa stars na Uganda, shida ni nini?

Tukienda tu kwa kubembelezana kama ilivyo kwa Waziri wa Nishati! Iko siku tutapata bonge la Aibu zaidi ya hili la umeme kuwa mdogo kwenye uwanja wa Mkapa mechi ya kimataifa inayohusisha Timu za Tanga na Rivers!

Halafu sijui ni kwa nini huwa inakuwa hivi!

Kila mtu aliyewahi kulalamikiwa sana na wananchi kwenye tawala hizi, mtu huyo huja kuwa sababu ya serikali kufeli vibaya na kuwa ya hovyo hovyo tu

Nchi nzima kwani imekosa watu makini hadi iwe yuleyule tu aliyefeli hata kabla ya kuanza?

Hivi majuzi kwenye ziara ya Rais kabisa kule Arusha! Umeme ulikatika mbele yake na bado mh Januar Makamba bado aliendelea kuwa waziri

Mfano

Makonda!
Magufuli alikuwa hafanyi maintenance ya vifaa vya umeme
 
Mechi ya marudiano kati ya Taifa Stars na Uganda, mambo yalikuwa hivi hivi! Mwisho wa siku tukaishia kufungwa.

Hivi ni kwa nini huu uwanja unakosa standby generator? Mapato ya huu uwanja yanaishia kwenye mikono ya nani? Huu uwanja una usimamizi makini kweli?
Generator linahitaji winchi kubwa Sana ili kulinyanyua kwa ajili ya kulisafiriaha. Hivyo serikali imemlipa mkandarasi wa kutengeneza winchi mpk mwaka 2035 kitakuwa limekamilika
 
Ilitokea mechi baina ya Tanzania na Uganda taa zilizimika na kupelekea mechi kusimama kwa muda na baadae mechi ikaendelea mwanga wa taa ukiwa hafifu, likapita kimya kimya!
Imetokea tena sasa taa zimezimika kabisa uwanja umetanda giza mechi imesimama! Hii aibu inafichwa wapi hii?
Caf bila shaka waliwapa Tff maagizo ya kurekebisha dosari zilizopo kwenye huo uwanja, na waziri mkuu akakazia, sasa hivi ni maboresho ya vyoo na mabenchi ya ufundi ndiyo waliyofanya hawakuona tatizo la mfumo wa taa?
Simba kwenye mapato hivi majuzi tuliona walikatwa mamilioni ya fedha kwa ajili ya uwanja, hivi hizo fedha zinatumikaje?
Uwanja unaingiza mamilioni ya pesa, taa zinagharimu kiasi gani ama kama shida ni mfumo wa umeme marekebisho yake yanagharimu kiasi gani….?!

Halafu kwa masihara haya ndio wanaomba kuhost Afcon really….!!!!??


Kwa hizi aibu ni vyema meneja wa uwanja na wote wanaohusika wakatumbuliwa tu! Hili halistahili kupita aiseeh!
 
Generator linahitaji winchi kubwa Sana ili kulinyanyua kwa ajili ya kulisafiriaha. Hivyo serikali imemlipa mkandarasi wa kutengeneza winchi mpk mwaka 2035 kitakuwa limekamilika
😂😂😂😂😂😂
 
Hii ni mara ya pili baada ya ile mechi ya Taifa stars na Uganda, shida ni nini?

Tukienda tu kwa kubembelezana kama ilivyo kwa Waziri wa Nishati! Iko siku tutapata bonge la Aibu zaidi ya hili la umeme kuwa mdogo kwenye uwanja wa Mkapa mechi ya kimataifa inayohusisha Timu za Tanga na Rivers!

Halafu sijui ni kwa nini huwa inakuwa hivi!

Kila mtu aliyewahi kulalamikiwa sana na wananchi kwenye tawala hizi, mtu huyo huja kuwa sababu ya serikali kufeli vibaya na kuwa ya hovyo hovyo tu

Nchi nzima kwani imekosa watu makini hadi iwe yuleyule tu aliyefeli hata kabla ya kuanza?

Hivi majuzi kwenye ziara ya Rais kabisa kule Arusha! Umeme ulikatika mbele yake na bado mh Januar Makamba bado aliendelea kuwa waziri

Mfano

Makonda!
Tangu umeme ulipokatika pale Ukumbi wa Kuringe Rais Samia akiwa anahutubia nilijua hii Tanesco ni majanga sana
 
Mechi ya marudiano kati ya Taifa Stars na Uganda, mambo yalikuwa hivi hivi! Mwisho wa siku tukaishia kufungwa.

Hivi ni kwa nini huu uwanja unakosa standby generator? Mapato ya huu uwanja yanaishia kwenye mikono ya nani? Huu uwanja una usimamizi makini kweli?
Uwanja uliogharimu bilioni 40 unakosa standby genereta ya milioni 100 !! Tena zipo pale mikocheni STENDI ya daladala Chama 😅😅🙏🙏
 
Back
Top Bottom