Baba mkwe hataki nimrudishe mwanae anasema atamkanya kwa mara ya nyingine

Inategemea. Kupigana ni mambo flani hivi ya kishamba. Kama kakushindwa afungashe aende
Ni kweli huwa ni Kama ushamba flan hivi ila mtu analazimishwa kufanya huu ushamba....maonyo yanakuwa mengi sana hadi inashindikana kuonya kawaida.
 
Ni kweli huwa ni Kama ushamba flan hivi ila mtu analazimishwa kufanya huu ushamba....maonyo yanakuwa mengi sana hadi inashindikana kuonya kawaida.
Mkuu mimi hii kwangu naamini ni udhaifu mkubwa sana kupiga mke.
 
Labda unaweza niorodheshea huenda nikawa nimepungukiwa na nini?


Akili tu Mkuu hicho ndicho mke anadai kutoka kwa mme wake na vyote vipo NDANI ya Akili


Akili ni uwepo wa MUNGU NDANI ya mtu,


akili inaongoza haiongozwi,


KAZI ya Akili kwa mme ni kuimarisha mahusiano ya NDOA, KAZI ya akili kwa mke ni kukuza na kufisha


itafute akili wewe kama mume na uipe uhuru ifanye KAZI yake utakuja kunishukuru hapa
 
Mkuu, amka usingizini.
Kwa replies zake inaonekana mbishi mbishi sana, andhan ndoa inataka ubishi na u much know..mwanamke asha ona kaolewa na mwenzie anakoswa ile kuiona Man hood ndani kwake (kuongozwa), hivyo kaona amdharau tu yaishe. Ila kwa vile mbishi ngoja tumtonye kidogo kuna mwenzako anaheshimiwa sana mahali hajaongea huyo demu wako asha amka na kutekeleza.
Yupo mahalai mtafute utampata
 
Ni kweli kabisa ila Sasa hasikii maonyo yako na ba mkwe hataki umrudishe unafanyaje mzee.
wanasema tutumie busara katika maamuzi ila hapa namvutia tu siku chache atapanda pipa iwapo hatobadilika
 
Mpeleke kwao akatulize mawazo...swala la kumpiga sio busara lakini pia kuna wanawake wanawatwanga waumwe zao...nimewahi shuhudia jirani yangu wa kiume saa saba usiku anapiga kalele za msaada wa kichapo cha mke wake huku kavaa boxa...sijui wewe kama mke wako anaihiyo tabia.
 
Mkuu sio kweli niliwai ishi na binti mmoja tukiwa chuo miaka 3 alikua mtiiifu sana sikutaka kumuoa sababu alinizidi mwaka mmoja. hadi Leo sijapata ile haiba nadhani ni malezi huko walikotoka
 
Bado upo too general mkuu jaribu kuja with clear examples
 
Hapana mkuu hakuna kitu kama icho
 
HIvi upo kwenye ndoa?

Mpaka awaambie Wakwe (Wazazi wa mke) inamaana Jamaa ameshamwonya haonyeki au habadiliki

Then Jamaa amefanya vizuri kuwaambia wazazi wa binti kuliko kuwaambia ndugu zake jamaa...ingekuwa ni kumdhalilisha

Lastly, Mwanamke ambaye HANA UTII huwa havumiliki na mwishowe ataachika tu

Ingekuwa labda ana UTII lakini tatizo ni Uchafu tu, au Umbea, au Ufupi hivyo vinavumilika
 
Chunguza mkuu
Kama anakuvunjia heshima, fahamu kuna anayepswa heshima zote. Jitahidi umpate anayekwapua heshima yako kisha mruhusu wakaoane waishi maana mwanamke akishagawa papuchi nje ya ndoa fahamu huyo si wako tena.

Kwao hawatompokea. Just mruhusu aende anakokutaka yeye utakuwa umeshinda game
 
aisee
 
.......ndoa ni kuvumiliana.....sanaa....kama hana mambo machafuuuuu...
 
Wanasema bora shetani unayemjua kuliko malaika usiye mjua. Maisha ya ndoa ni ushirika fulani hivi ambao mke na mme PLUS wazazi wa pande 2 wameridhia. Kinacho waweka sawa ni vile kila mmoja anamchukulia mwenzie kama ni yeye, yaani chako changu changu chako. Je wewe unamchukuliaje mwezio, kwa nini unadhani hakutii, wewe unamtii? Matatizo ya mke na mme humalizwa na wawili hao tu. Kaeni chini muongee wenyewe, ikishindikana manake ushirika wenu unavunjika au mtaishi bila furaha.
 
huenda ukawa sahihi mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…