Chozi la Jenerali Mabeyo akisimulia siku za mwisho za Hayati Magufuli linaashiria nini?

Chozi la Jenerali Mabeyo akisimulia siku za mwisho za Hayati Magufuli linaashiria nini?


View: https://m.youtube.com/watch?v=9Hyg_T0yb-8

Katika dunia hii mtu wa mwisho ambae unaweza kuona chozi lake hadharani ni senior army officer na army general ndio kabisa awezi kuonyesha weakness hiyo hadharani.

Sasa cha kushangaza Mabeyo pamoja na kujitahidi kutabasamu ila chozi lilimshinda nguvu kwa sekundę kadhaa ameonekana akibubijikwa machozi ya hudhuni mbele ya camera. Kumbuka ata alipofiwa na mtoto wake rubani, general akutoa chozi alipofika eneo la tukio.

Je anajutia kutosikiliza maamuzi ya watu waliomshauri wapindue męża ya katiba huyo mama hiyo nafasi sio size yake na kinachoendelea leo Tanzania.

Huyu jamaa hakufaa kuwa mwanajeshi. Jianaume zima linaliaje mbele ya kamera? Ovyo kabisa
 
Imagine Leo akiulizwa katika hali Ile, why wengine waliendelea kama vile nothing urgent was there?

Kwanini VP hakuambiwa kama msaidizi wa kwanza wa Rais kuhusu hali ya mgonjwa?

Kwakweli hii inezua maswali mengi na pengine wanazidi kutuzulia maswali zaidi kuliko majibu.
Unataka kusema VP alikuwa hajui kabisa hali ya rais
Kiongozi wa nchi inajulikana anaumwa unataka shughuli zote zisimame kwamba VP WM nk waache majukumu yao wabaki kumwangalia mgonjwa
 
Mwenzako analilia cheo,alitegemea aendelee nacho lakini akaliwa kichwa 😁😁

Saizi anasema labda tungepindua meza ningebaki nacho 🤣🤣🤣🤣🤣

Ila wewe maskini Sasa ndio unaacha kazi zako na kumsikiliza kabisa

Shida ya wanasiasa. Retired CDF anataka cheo gani?🤣🤣🤣🤣

Unafikiri kila mtu ana kiherehere kama mlivyo? Hata baada ya retirement mnataka kuendelea kuongoza.

Ujumbe umefika, pengine uko coded....
 
..Mwamunyange ilikuwa aastaafu mwaka 2016 maana yake huo ndio mwaka aliotimiza miaka 60. Hivyo basi ni sahihi kusema Mwamunyange alizaliwa mwaka 1956.

..Taarifa za kwenye mitandao zinasema Mabeyo amezaliwa mwaka 1956. Yaani mwaka mmoja na Mwamunyange.

..Hoja yangu bado inasimama kwamba kulikuwa na walakini ktk uteuzi wa Mabeyo.

Hata 1956 haiwezekani sababu itamaanisha kwamba JWTZ walimpa nyota Mwamunyange akiwa na umri wa miaka 17 kuweka rekodi sawa JWTZ ukiwahi sana kupata nyota katika umri mdogo ni ukiwa na umri wa miaka 21 hapa unakuwa umejitahidi sana kuwahi kupata nyota
 
Shida ya wanasiasa. Retired CDF anataka cheo gani?🤣🤣🤣🤣

Unafikiri kila mtu ana kiherehere kama mlivyo? Hata baada ya retirement mnataka kuendelea kuongoza.

Ujumbe umefika, pengine uko coded....
Kuna mtu Huwa hataki cheo akiwa mzima na Afya timamu? 😁😁

Watu wajinga Huwa mnatekwa akili sana na machozi Kwa sababu hamjui sayansi na saikolojia 🤣🤣🤣🤣🤣
 
This was a great interview!

Very informative even though the general appeared to be holding back some
information.

Understandably so!
Yes ilikuwa interview nzuri sana kwa bahati mbaya sana walioendesha interview hawakuwa na weledi.
Laiti wangalikuwa nao tungejua mambo mengi sana

1. Wakati hali ya Mh Rais ikiwa mbaya kwanini Makamu wa Rais na Waziri mkuu hawakuitwa warudi Dar ?
Kwanini Makamu wa Rais na Waziri mkuu hawakuwepo kusimamia matibabu ya Rais. kwanini walikuwa ziarani?
Ilipofikia mahali Kadinali na Paroko wanaitwa, je, hiyo haikutosha kuwaita viongozi wakuu

2. Kwanini wakuu wa vyombo vya usalama walisimamia jambo hili bila kuwa na support ya Serikali

3. Kwanini Jenerali Mabeyo atafute taratibu ndani ya katiba wakati Mwanasheria mkuu wa serikali yupo?

4. Jenerali Mabeyo ametueleza mambo muhimu sana kuhusu Katiba. Kwamba nchi inaendeshwa bila muongo ndiyo maana kila jambo lilionekana kama ''novelty' na kwamba hakuna anayejua
a. Rais akiwa mahututi nani awepo nani aongoze nini
b. Rais akifariki taratibu gani zifuatwe kutangaza kifo, nani afanye hilo
c. Makamu wa Rais anaapishwaje na vitu kama bendera vinakuwaje

Ukimsikiliza Jenerali ni kama vile tuliongozwa na ''busara' na siyo taratibu ndiyo maana kuna wale waliotaka iwe tofauti kwasababu kulikuwa na mwanya huo. Tunatakiwa tukae chini hili halipaswi kuwa jambo la kubahatisha au kusema 'hatukuwa na experience'' hapana.

JokaKuu
 
Unataka kusema VP alikuwa hajui kabisa hali ya rais
Kiongozi wa nchi inajulikana anaumwa unataka shughuli zote zisimame kwamba VP WM nk waache majukumu yao wabaki kumwangalia mgonjwa
Nafuatilia Clip Mimi...Angejua hali asingeendelea na yake mpaka mwenzake anakata roho...Kama Kuna mambo ya muhimu kumkabidhi ambayo hayakuwa documented je? Kwani Katiba inasemaje? Nani anakuwa Rais kama aliyepo hawezi majukumu? Kwanini basi hakuwepo hapo wakati huyu ameshindwa majukumu?
 
Back
Top Bottom