Chozi la Jenerali Mabeyo akisimulia siku za mwisho za Hayati Magufuli linaashiria nini?

Chozi la Jenerali Mabeyo akisimulia siku za mwisho za Hayati Magufuli linaashiria nini?

Machi 17, mwaka huu Tanzania itaadhimisha miaka mitatu tangu kifo cha Rais John Magufuli.

Rais wa Kwanza kufariki Dunia akiwa madarakani katika historia ya Tanzania. Timu ya Daily News Dijital imefanya mazungumzo na aliyekuwa Mkuu wa Majeshi nchini Jenerali Mstaafu Venance Mabeyo ambaye amezungumzia saa 24 kabla ya Magufuli kuaga Dunia na saa 40 kabla ya Rais Samia Suluhu Hassan kuapishwa kuwa Rais wa awamu ya Sita katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mahojiano haya ni ya Kwanza kwa kiongozi huyu tangu astaafu wadhifa wake Juni 2022.

View: https://youtu.be/9Hyg_T0yb-8?si=t7iYDCsji_BLAk13
 
Nyinyi ndio mlitaka kupindua meza hamkutaka mama kizimkazi asiwe raisi, ndio nakuuliza mlitaka raisi awe nani?

View: https://www.instagram.com/p/C4mZR-bqprr/?igsh=MWgwcnc0MDF3Znh0Nw==
20221125_193026.jpg
 
Yes ilikuwa interview nzuri sana kwa bahati mbaya sana walioendesha interview hawakuwa na weledi.
Laiti wangalikuwa nao tungejua mambo mengi sana

1. Wakati hali ya Mh Rais ikiwa mbaya kwanini Makamu wa Rais na Waziri mkuu hawakuitwa warudi Dar ?
Kwanini Makamu wa Rais na Waziri mkuu hawakuwepo kusimamia matibabu ya Rais. kwanini walikuwa ziarani?
Ilipofikia mahali Kadinali na Paroko wanaitwa, je, hiyo haikutosha kuwaita viongozi wakuu

2. Kwanini wakuu wa vyombo vya usalama walisimamia jambo hili bila kuwa na support ya Serikali

3. Kwanini Jenerali Mabeyo atafute taratibu ndani ya katiba wakati Mwanasheria mkuu wa serikali yupo?

4. Jenerali Mabeyo ametueleza mambo muhimu sana kuhusu Katiba. Kwamba nchi inaendeshwa bila muongo ndiyo maana kila jambo lilionekana kama ''novelty' na kwamba hakuna anayejua
a. Rais akiwa mahututi nani awepo nani aongoze nini
b. Rais akifariki taratibu gani zifuatwe kutangaza kifo, nani afanye hilo
c. Makamu wa Rais anaapishwaje na vitu kama bendera vinakuwaje

Ukimsikiliza Jenerali ni kama vile tuliongozwa na ''busara' na siyo taratibu ndiyo maana kuna wale waliotaka iwe tofauti kwasababu kulikuwa na mwanya huo. Tunatakiwa tukae chini hili halipaswi kuwa jambo la kubahatisha au kusema 'hatukuwa na experience'' hapana.

JokaKuu
Yaani ni as if tunaongozaa na utashi wa kundi la watu badala ya legal frame ya nchi...So saaad!
 
Usiseme kama vile unaimiliki kesho na Tanzania. Tanzania ni mali ya Mwenyezi Mungu.
Ina maajabu mengi sana hii nchi. Tujifunze kuwa na kiasi
Sasa kama unalijua Hilo,Kwa nini uone Magufuli as if hakustahili Kufa? Yeye alikuwa anaimiliki kesho? Muwe mnajifunza sio kusingizia wasiohisika na vifo.

Mtu mgonjwa wa Moyo miaka Mingi still was living a stressful life unategemea nini?
 
..inaweza kuwa anaigiza kulia.

..pia habari yote inaweza kuwa ya kutunga.

..hujasikia kwamba Jiwe aliuwawa na genge la Msoga baada ya kuwadukua?

..pia hujasikia kwamba Jiwe alifia nchi jirani ktk hospitali iliyookoa maisha ya jamaa aliyemtumia watu wamuue?
Mkuu please ongezea nyama.
 
Sasa kama unalijua Hilo,Kwa nini uone Magufuli as if hakustahili Kufa? Yeye alikuwa anaimiliki kesho? Muwe mnajifunza sio kusingizia wasiohisika na vifo.

Mtu mgonjwa wa Moyo miaka Mingi still was living a stressful life unategemea nini?
Kifo ni haki ya kila mwanadamu kwann nyinyi mlikuwa na raisi wenu (mfukoni) baada ya Magufuli kufa. Na kwann hamkutaka kufuata katiba
 
Yaani ni as if tunaongozaa na utashi wa kundi la watu badala ya legal frame ya nchi...So saaad!
Tuliongozwa na 'Busara' za Jenerali Mabeyo, kungeweza kutokea matatizo makubwa sana.

AG (Mwanasheria Mkuu) alitakiwa asimame kutafsiri na kuelekeza Katiba inatamka nini na kama haitamki kisheria kipi kinafanyika.

Makamu wa Rais alipaswa kuapishwa usiku saa 6 na si kusubiri siku 3 au kujiuliza viongozi watapokewaje.

Rais yupo mahututi yupo na CDF, IGP na DGIS , Makamu na Waziri mkuu wanahanja hanja! ni hatari sana.

Jamani tuacheni ubishi, tukaeni chini na kutengeneza katiba ili tupate sheria zenye miongozo
Kusema eti hatuna uzoefu kama Marekani si kweli. Tulitakiwa tutumie uzoefu wa Marekani kufanya vizuri

Ni kama vile 'tunajitahidi kutengeneza kompyuta yetu from the scratch ' badala ya kutumia zilizopo kupiga hatua

Hii interview imeeleza mambo mengi sana
 
Kifo ni haki ya kila mwanadamu kwann nyinyi mlikuwa na raisi wenu (mfukoni) baada ya Magufuli kufa. Na kwann hamkutaka kufuata katiba
Hivi wewe unajielewa lakini? Katiba ipi ambayo haikufuatwa? Samia si ndio Rais Kwa mujibu wa Katiba au? Hao wenye Rais wa mfukoni ni kina nani?
 
Back
Top Bottom