Freeman Mbowe: Rais leta maridhiano ya Kitaifa, sisi CHADEMA tuko tayari
Kuna watu wanahoji, kwanini Kamati Kuu Chadema imeamua kuhudhuria sherehe za Uhuru leo baada ya kususia kwa miaka kadhaa.

Kuna fununu zinasikika zikifanywa na viongozi wa dini na wazee wastaafu kuhakikisha maridhiano yanapatikana baina ya serikali na vyama vya upinzani hasa Chadema, kama ni kweli basi hatuna budi kuipongeza serikali inayoongozwa na Rais John Magufuli na kamati kuu ya Chadema kwa uamuzi wake huo. Najua Chadema italaumiwa na wengi hasa wahafidhina wasiopenda mabadiliko, lkn kama imeamua kwa misingi ya kujenga umoja wa kitaifa basi tuipe ushirikiano kwa manufaa ya nchi.

Inawezekana ni udhaifu fulani Chadema imeonyesha, lkn kwa jicho jingine inawezekana pia ni ukomavu wa kisiasa na ni mwanzo mzuri kwa umoja wa kitaifa. Kwanini tuumizane kwa kugombea fito.

Nchi jirani ya Kenya kwa kipindi kirefu kumekuwa na mvutano baina ya Serikali ikiongozwa na Mhe. Uhuru Kenyata dhidi ya Kiongozi Mkuu wa Upinzani Raila Odinga. Lakini baada ya uchaguzi mkuu wa 2017 tumeona juhudi kubwa za wazi za upatanishi zikiongozwa na rais Uhuru mwenyewe, kwa kiasi fulani zimeanza kuzaa matunda na nchi inasonga, ila kwa kufanya hivyo Uhuru amempoteza marafiki wake wengi akiwepo rafiki wake wa karibu Ruto.

Wasiopenda Maridhiano watabeza, wasiotaka amani hawatapenda tukio hili lifanikiwe.

Maendeleo hayana chama.

MARIDHIANO NI MUHIMU SANA. ILI TAIFA LIWE NA MAFANIKIO NI LAZIMA MARIDHIANO YA DHATI YAPEWE UMUHIMU. HATA HIVYO MARIDHIANO YASIWE SABABU YA KUFUTA KESI ZA JINAI NA NYINGINE ZIMESABABISHA VIFO. KESI LAZIMA ZIENDELEE AMA SIVYO WATU WATAENDELEA KUFANYA JINAI NA BAADAYE KUDAI MARIDHIANO.
 
Kumuomba Jiwe maridhiano haimaanishi kuwa hayo maridhiano lazima uyashuhudie wewe au mimi, bali hata vizazi vijavyo vinahitaji uwanja sawa wa kufanya siasa.
Vizazi vijavyo vitakuja kushangaa tu ilikuwaje watu wakafanyiwa figisu za hatari kwny uchaguzi wa serikali za mitaa,wakapewa kesi za kutosha mahakamani,mwenzao mmoja mpk akapewa ulemavu wa kudumu na bado watu hao hao wakaenda kwny sherehe iliyoandaliwa na wababe wao na wakitoka hapo bado wataenda kwny hafla kule ikulu ndogo.

Ni maajabu kwa kweli.
 
Lini chadema walimtambua Magufuli Kama Raisi? Kuapishwa walisusa kuwa hawamtambui,bungeni alipoenda Kama Raisi walitoka kumkataa.

Watoe kwanaza tamko la kumtambua Magufuli Kama Raisi.

Wanataka maridhiano na Magufuli Kama Nani kwao ?
Lakini yule waliyemkataa, anawatambua uwepo wao ndio maana kawapa nafasi ya kusalimia Taifa. Tuwe wakomavu tu jamani, hii ni nchi yetu sote!
 
Haijalishi
Vizazi vijavyo vitakuja kushangaa tu ilikuwaje watu wakafanyiwa figisu za hatari kwny uchaguzi wa serikali za mitaa,wakapewa kesi za kutosha mahakamani,mwenzao mmoja mpk akapewa ulemavu wa kudumu na bado watu hao hao wakaenda kwny sherehe iliyoandaliwa na wababe wao na wakitoka hapo bado wataenda kwny hafla kule ikulu ndogo.

Ni maajabu kwa kweli.
 
Ngoja niandike kabisa nikichotaka kusema kabla sijasoma comments za mamluki,"Mbowe ni kichwa acha anendelee kukiongoza chama kwa namna itakavyondeza Mungu
 
Hahahaa kamanda umenichekesha sana..kumbe upo hapo?? Niko na delegation ya diplomats nakuja maeneo hayo

Viva Magufuli, Heko watanzania
Ndiyo muwe na adabu na akili ziwarudie muwache kuropoka hovyo
 
Lini chadema walimtambua Magufuli Kama Raisi? Kuapishwa walisusa kuwa hawamtambui,bungeni alipoenda Kama Raisi walitoka kumkataa.

Watoe kwanaza tamko la kumtambua Magufuli Kama Raisi.

Wanataka maridhiano na Magufuli Kama Nani kwao ?
Hiyo haijalishi. Kenya walikuwa na mtifuano mkubwa zaidi yetu.... Lakini Leo Uhuru na Laila wanakaa Meza moja.
 
Mbowe hiyo nafasi hakuitumia vizuri angeanza hivi sisi Kama chadema tuna makosa mengi tumeifanyia Serikali ya CCM na Raisi hatuwezi sema sisi hatuna makosa sababu sisi sio miungu.Pia CCM yaweza kuwa imetukosea upinzani kwa kujua au kutojua kwani CCM sio miungu kwa muktadha huo tunaomba maridhiano na kusameheana kuwa kitu kimoja tujenge nchi moja.
Lakini Mbowe alivyoongea ninkana kwamba wao Ni malaika na CCM na Magufuli ndio mashetani wanaotakiwa walete maridhiano ya kitaifa!!!! Wao chadema Ni akina malaika Gabriel na mikael
Hebu punguza jazba
 
Hakika nachukua nafasi hii kuupongeza Uongozi wa juu wa Chadema kuamua kwanza kushiriki Maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru wa Tanganyika nchi yetu sote.Pili naupongeza kwa dhati Uongozi wa Chadema kutaka uwepo wa maridhiano mbele ya Watanzania zaidi ya milioni 25 walioshiriki Sherehe hizo ktk Uwanja wa CCM Kirumba Mkoani Mwanza.Naamini Rais Magufuli na Chama cha CCM,Marais Wastaafu,Mawaziri Wakuu wastaafu ,Marais Wastaafu wa Zanzibar na Viongozi mbalimbali wa Dini zetu wote kwa pamoja watakubaliana na mawazo ya viongozi wa Chadema ili Tanzania ya Amani na Demokrasia izaliwe upya na tupige hatua kujiletea maendeleo chini ya Rais Magufuli.
Screenshot_20191110-220655_Google.jpeg
 
Matokeo ya kuhudhuria kwa Mbowe na kamati kuu yanategemea maamuza ya rais Magufuli kwa 99%.
 
Hiyo haijalishi. Kenya walikuwa na mtifuano mkubwa zaidi yetu.... Lakini Leo Uhuru na Laila wanakaa Meza moja.
Huwezi kutaka maridhiano na mtu anaye kuchukulia poa,anaye kuzidi nguvu na kila kitu na anajua hamna kitu utamfanya.

Wanaridhiana watu wanaokaribiana nguvu,kwamba usiporidhia nna uwezo wa kuzingua lkn mtu anajua hamna kitu CDM itafanya unadhani amesikiliza chochote.
 
Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe amemtaka Rais Magufuli kuleta maridhiano ya kitaifa na kwamba yeye na chama chake wamenyoosha mkono wa mapatano

Ifuatayo ni Hotuba Fupi ya Kiongozi Mkuu wa Upinzani nchini Tanzania Freeman Aikael Mbowe mbele ya Watanzania katika kuadhimisha miaka 58 ya Uhuru:

Mheshimiwa Rais,
Waheshimiwa viongozi wote mlioko mahali hapa,
Waheshimiwa watanzania wenzangu!

Nimekuja kushiriki sherehe za miaka 58 ya Uhuru kama uthibitisho wa ulazima wa kuwepo maridhiano, kuwepo upendo, na kuwepo mshikamano katika Taifa letu.

Nawapongeza sana watanzania kwa siku hii ya leo na ninamuomba Mwenyezi Mungu siku ya leo ikafungue milango tuweze kuishi kama Taifa linalopendana, tuvumiliane, tukosoane, turuhusu demokrasia. Tukajenge Taifa lenye upendo na mshikamano.

Na Mheshimiwa Rais una nafasi ya kipekee kuweka historia ya maridhiano katika Taifa kwani kuna wengine wanalalamika, wengine wanaumia. Basi Mheshimiwa Rais tumia nafasi hiyo ukaliweke Taifa katika hali ya utengamano.

Nakushukuri sana. Asante sana.
_____________
Hotuba fupi ya Mwenyekiti wa CHADEMA na KUB, Mh *Freeman Mbowe* katika sherehe za maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru wa Tanganyika, zilizofanyika Jijini Mwanza leo 9 Disemba 2019
View attachment 1286525
Maridhiano wanafanya watu walio more or less kwenye level moja.
Mtu aliyeiba uchaguzi na kupata 99.9 percent huwezi kufanya naye maridhiano.
 
Mbowe atimue washauri wote, wanamptosha

Wamemshauri kususia Uchaguzi sasa wanataka maridhiano ya nini
 
Hawa CHADEMA wame kwenda Mwanza kutafuta huruma ya kufutiwa kesi na wengine kuachiwa kugombea ubunge kwa usawa mwaka 2020 bila figisu kama wakati wa uchaguzi wa mitaa.
 
Magufuli aliyepinda na anaye endelea kupindisha Katiba ya Tanzania ndiye anastahili KUNYOOSHWA…!
Umenena kweli tupu. Mimi Ni mmoja ninayemwona Rais Magufuli kama mtawala anayetumia si ushawishi kwa watu wa nchi bali mabavu kufanya anachokifanya. Na mbaya kuliko yote, amekuwa ni adui mkubwa wa demokrasia na haki za binadamu changanya na kupata uungwaji mkono wa wazee wasiojielewa kama Mwinyi na Malecela.
 
Back
Top Bottom