Freeman Mbowe: Rais leta maridhiano ya Kitaifa, sisi CHADEMA tuko tayari
Siku ya kuapishwa rais Magufuli Chadema walisusa Zitto alihudhuria na akampongeza, leo Zitto kasusa Chadema wamehudhuria, ndiyo siasa zilivyo.

Ni kweli, lakini sikumpongeza pia huyo Zito kwa kuhudhuria hafla ile. Hao cdm hawajajifunza tu kuwa hata ukihudhuriwa hafla za rais hana muda wa maridhiano?
 
Utamu WA Siasa ni kusahau matatizo yako Kwa kaulimbiu vya "Yanga Mbele kurudi nyuma mwiko" ukiangalia Siasa ya Tanzania utagundua kunatatizo la umoja wa kitaifa katika kutatua matatizo na hii inasababishwa na Sifa (Ndiyo maana ni Bora ungekuwa Uhuru wa BINTI MARINGO" kuliko Uchumi:.

Moja ya maandiko ya mwalimu Nyerere alikataza kitu kimoja Tu ambacho hata VIPI hakutakuwa na umoja wa kitaifa "Vyumba vya kupanga havitakiwi" mwisho wa kunukuu Mambo mengine yote "tumetaka wenyewe"

Ni rahisi kusikia "your finding first president fuki" watu wakaanza kutafutà raisi wa kwanza badala fuki ya para ya "hakutakiwi vyumba vya kupanga"

👉👉👉👉 people majibu yote yapo kwenu wenyewe

 
Asingehudhuria angepelekaje ujumbe wake? Kama walimwalika kumtega huku wakijua atasusa basi wamejiharibia maana hawakutegemea Kama angeenda! Na hata aliyempa nafasi ya kutoa salami alitegemea kusifiwa lakini kapewa ukweli na sura yake ilisomeka vyema kwa maneno aliyoambiwa na Mbowe! Mbowe kaitumia fursa ya kumsema hadharani ambalo mashahidi wameshangilia uwanjani hapa!

Huyo aliyeambiwa ana aibu? Sana sana alitumia uwepo wa Mbowe kujipatia point za mezani na kufuta mwenendo wake mbovu katika demokrasia. Kwa maneno marahisi aliyefaidika na uwepo wa Mbowe ni rais kuliko huyo Mbowe.
 
Chadema wawashauri wachaga kuwa Wawe na maridhiano na makabila mengine wasijione superior au kuonea watu wasio kabila yao au kujipendelea kwenye maeneo yenye watu wa makabila tofauti iwe maeneo ya kazi,iwe kwenye siasa ndani ya chadema au popote.

Wachaga wanahitaji maridhiano na makabila mengine ndani ya chadema yenyewe ili chadema isionekane Chama Cha wachaga

Sasa hapo Ndo unazidi kuwapaisha!wenyewe wametulia tulii!
 
Fununu zilizopo ni kuwa mishale ya saa kumi jioni watakuwa na kikao Cha maridhiano kitakachoshirikisha cdm's crew, baadhi ya maaskofu, mawaziri wakuu wastaafu na aliyepo, Marais wastaafu na mkulu mwenyewe hapo ikulu ndogo jijini mwanza. Sio kikao Cha kitoto!

Nasema hivi, hamna lolote bali ni utapeli wa mchana kweupe.
 
Watanzania wangeunga mukono hotuba ya maridhiano badala yakuendelea kuyasuta maridhiano.Kuna faida kubwa katika maridhiano.Ushirikiano wa ndani na nje ya nchi utaongezeka.Kuendelea kusema hatuitaji misaada,ela tunayo haitoshi kuzuihiya kuzorota kwa uchumi,kupanda kwa tozo,ushuru mbali mbali kwa wananchi.Prof Kabudi umeona Kenya wanafanya hivyo ebu onyesha mfano
 
Kuna watu wanahoji, kwanini Kamati Kuu Chadema imeamua kuhudhuria sherehe za Uhuru leo baada ya kususia kwa miaka kadhaa.

Kuna fununu zinasikika zikifanywa na viongozi wa dini na wazee wastaafu kuhakikisha maridhiano yanapatikana baina ya serikali na vyama vya upinzani hasa Chadema, kama ni kweli basi hatuna budi kuipongeza serikali inayoongozwa na Rais John Magufuli na kamati kuu ya Chadema kwa uamuzi wake huo. Najua Chadema italaumiwa na wengi hasa wahafidhina wasiopenda mabadiliko, lkn kama imeamua kwa misingi ya kujenga umoja wa kitaifa basi tuipe ushirikiano kwa manufaa ya nchi.

Inawezekana ni udhaifu fulani Chadema imeonyesha, lkn kwa jicho jingine inawezekana pia ni ukomavu wa kisiasa na ni mwanzo mzuri kwa umoja wa kitaifa. Kwanini tuumizane kwa kugombea fito.

Nchi jirani ya Kenya kwa kipindi kirefu kumekuwa na mvutano baina ya Serikali ikiongozwa na Mhe. Uhuru Kenyata dhidi ya Kiongozi Mkuu wa Upinzani Raila Odinga. Lakini baada ya uchaguzi mkuu wa 2017 tumeona juhudi kubwa za wazi za upatanishi zikiongozwa na rais Uhuru mwenyewe, kwa kiasi fulani zimeanza kuzaa matunda na nchi inasonga, ila kwa kufanya hivyo Uhuru amempoteza marafiki wake wengi akiwepo rafiki wake wa karibu Ruto.

Wasiopenda Maridhiano watabeza, wasiotaka amani hawatapenda tukio hili lifanikiwe.

Maendeleo hayana chama.
Sisi ambao tumeona hali halisi ya madikiteita, Idd Amin, Mbowe ametimiza wajibu wake lakini SAHAU any positive move from a dictator
 
Kikwete aliwaita sana lakini hwapi ,wapinzani wa bongo ni pasua kichwa

Wapinzania watafungwa kwa ishu ya akwilina mambo ya kuomba maridhiano sio time yake


USSR

Wawafunge hata leo, kwani kuna jipya lipi hawajawafanyia hao wapinzani useme kuwafunga sasa ndio itakuwa jipya? Huyo Lissu amepishana na iziraili itakuwa kufungwa? Huyo anayeagiza hayo sasa huu ni muda wake wa kutamba, hata akina Elbashir walitamba muda wao, saa hii wao ndio wanasafisha vyoo huko gerezani.
 
Unaenda kumpigia magoti mtu aliyemtandika risasi 38 nduguyo utadhani anaua CHATU na kama haitoshi akaendelea kumshughulikia vivyo hivyo huku akiwa hoi kitandani.

CHADEMA hakuna kitu
Yesu alisema samehe saba Mara sabini. Siku zote kisasi ni cha Mungu mwenyewe.
 
Nadhani Mbowe kafanya kile ambacho Kamati kuu iliyokaa juzi imeridhia! Let us wait and see!
 
Saccos Tanzania
IMG_20191209_160944.jpeg
 
Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe amemtaka Rais Magufuli kuleta maridhiano ya kitaifa na kwamba yeye na chama chake wamenyoosha mkono wa mapatano

Ifuatayo ni Hotuba Fupi ya Kiongozi Mkuu wa Upinzani nchini Tanzania Freeman Aikael Mbowe mbele ya Watanzania katika kuadhimisha miaka 58 ya Uhuru:

Mheshimiwa Rais,
Waheshimiwa viongozi wote mlioko mahali hapa,
Waheshimiwa watanzania wenzangu!

Nimekuja kushiriki sherehe za miaka 58 ya Uhuru kama uthibitisho wa ulazima wa kuwepo maridhiano, kuwepo upendo, na kuwepo mshikamano katika Taifa letu.

Nawapongeza sana watanzania kwa siku hii ya leo na ninamuomba Mwenyezi Mungu siku ya leo ikafungue milango tuweze kuishi kama Taifa linalopendana, tuvumiliane, tukosoane, turuhusu demokrasia. Tukajenge Taifa lenye upendo na mshikamano.

Na Mheshimiwa Rais una nafasi ya kipekee kuweka historia ya maridhiano katika Taifa kwani kuna wengine wanalalamika, wengine wanaumia. Basi Mheshimiwa Rais tumia nafasi hiyo ukaliweke Taifa katika hali ya utengamano.

Nakushukuri sana. Asante sana.
_____________
Hotuba fupi ya Mwenyekiti wa CHADEMA na KUB, Mh *Freeman Mbowe* katika sherehe za maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru wa Tanganyika, zilizofanyika Jijini Mwanza leo 9 Disemba 2019
View attachment 1286525
UENYEKITIIII KWENU UMEKUWA WA UKOO KAMA MILA ZA KICHAGA NA KINA MANGI

MNASHINDWA KURIDHIANA HUKO KWENU NANI ARIDHIANE NA NYIE

MSHINDWEE NA MLEGEEEE MSAHAUU HUOO UPOOZI SIOO KWASASAAA ALLAH

MNATUTIA AIBU KAUCHAGUZI KADOGOOTU HAYO MARIDHIANO SI MTATUWEKEA SUMU KABISA TUFE

KIDUMU CHAMA TAWALA
 
Back
Top Bottom